Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, May 31, 2011

HABARIKA NA KATUNI



TIGO NA ROTARY KLAB WATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA MISEWE


Ofisa UHusiano wa Tigo Jackson Mmbando akiwaonesha wanafunzi moja ya kibao
Gavana Msaidizi wa Rotary Klab akimkabidhi kiti diwani wa kata ya segerea Bw.Azurdy Mwambagi leo

KAMATI YA SHEREHE ZA UBINGWA YAKUTANA LEO

Kamati itakayosimamia sherehe za ubingwa Tanzania Bara inatarajia kukutana leo kwa mara ya kwanza kwa ajili ya maandalizi ya sherehe hizo zitakazozinduliwa tarehe 18/6/2011.
Akizungumza na mtandao wa Klabu ya Yanga,Afisa wa habari wa Klabu ya Yanga,Louis Sendeu,amesema maandalizi hayo yanaanza hii leo kwa kushirikiana na wadhamini wao TBL,kupitia bia ya Kilimanjaro Lager.“Sherehe hizi zitahusisha baadhi ya Mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani kupitia wanachama wao waliopo katika matawi mbalimbali.”Sendeu.
Wajumbe watakaoshiriki katika kikao hicho ni pamoja na Stanley Kivella (Yono)ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Louis Sendeu Katibu.
Wajumbe ni Athumani Makaranga,Pelegrinius Rutta na Mohamed Bhinda.

NSA JOB SASA ATIMKIA ULAYA

Aliyekuwa mshambuliaji wa Klabu ya Yanga,Nsa Job, anatarajiwa kuondoka nchini kwenda nchini Sweden kwa ajili ya kufanya majaribio katika Klabu moja nchini humo inayoshiriki ligi daraja la kwanza.Akizungumza na mtandao wa Klabu ya Yanga,Job amesema tayari mipango yote imekamilika chini ya wakala wake Nyupi Mwakikosa ambaye anasimamia shughuli zote za kujiunga na Klabu hiyo.Hata hivyo Nsa Job amesema hadi sasa hajafahamishwa kikamilifu juu ya Klabu anayokwenda kufanya majaribio lakini tayari wakala wake amemhakikishia kuhusu majaribio hayo na ameeleza kuwa hata ikishindikana zipo Klabu mbili za America ya Kusini tayari amekwisha fanya mazungmzo nayoNsa amesema safari yake itakuwa ni ya tarehe 20/6/2011 anatarajia kuondoka na shirika la ndege la KLM.

NGAO YA MALKIA WA UINGEREZA YAPATIKANA YANGA

Ngao ya Malkia wa Uingereza iliyoshindaniwa Mwaka 1953

Uongozi wa Klabu ya Yanga umefanikiwa kupata Ngao mbili zenye hadhi ya kimataifa ikiwemo ngao ya Malkia Elizaberth wa Uingereza iliyopatikana Mwaka 1953 na nyingine iliyoshindaniwa katika miaka ya 1954.Taarifa hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga Celestine Mwesigwa ambaye Ngao hizo ni hazina ya Klabu ya Yanga katika kuweka kumbukumbu ya Yanga ikiwemo na vitu vingine.“Baada ya kupata Ngao hizi ipo haja ya kuwatafuta wazee waliowahi kuiongoza Klabu yetu ama waliocheza ili tuweze kupata uhakika na Ngao hizi tulizozipata.”Mwesigwa.

Katibu Mkuu ametoa wito kwa wanachama na wadau wote wa Yanga kujitokeza kwa wingi kama kuna mtu ana taarifa yoyote kuhusu Ngao hizo pamoja na zawadi mbalimbali ambazo watu wanazo majumbani kwao kuvirejesha mara moja katika Makao Makuu ya Klabu ya Yanga.

Hivi karibuni uongozi wa Yanga umeonyesha nia ya kuweka mikakati ya kuanzishwa eneo la kutunzia kumbukumbu mbalimbali za Klabu ya Yanga vikiwemo Vikombe mbalimbali,Ngao pamoja na tuzo za wachezaji na viongozi.

Sunday, May 29, 2011

SUPER D KUPAMBANISHA MAPAMBANO YA KLABU ZA NGUMI ILALA



MCHAKATO wa Kuendeleza mchezo wa ngumi za Ridhaa Katika MKoa wa KImichezo wa ILALA, unatarajiwa kuingia katika hatua nyingine Juni 4 kati ya klabu ya ngumi ya Amana na Matimbwa,

Mapambano hayo ya raundi nne, yanatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Panandi Panandi uliopo bungoni Wilaya ya ILala ambapo mabondia wanne kutoka katika kila klabu, watachapana makonde.

Mabondia wa Amana watakaopanda siku hiyo ni IBrahimu Class Kg.64, Khalfani Othumani Kg 57, Kassimu Sambo Kg 54, na Saidi Ally Kg 48. Klabu ya Matimbwa itawakilishwa na MOhamedi Matimbwa Kg 64, MOhamedi Muhani Kg 57, Edson Joviki Kg 54 na MOhamedi Kumbilambali Kg 48

Akizungumza Dar es SAlaam leo Mratibu wa mapambano hayo ambae pia ni kocha wa mchezo wa ngumi akishirikiana na Kinyogoli Foundition, RAjabu Mhamila Super D, Alisema mpango huo utaendelea mpaka wahakikishe wamefanikiwa kuibua vibaji na kuviendeleza

Alisema tangu waanze mpango wa kuandaa mapambano mkohani humo wamefanikiwa kurudisha hamasa ya mchezo huo mkoani humo na kuwataka wadau mbalimbali kutoa sapoti kwa mchezo huo ili upate kuendelea ambapo Super D alitoa mfano wa vitu wanavyoviitaji ikiwemo posho za nauli kwa wachezaji vifaa vya kuwatia moyo na zawadi mbalimbali kwa mabondia

MSONDO NGOMA YAENDELEA KUTESA VIWANJA VYA SIGARA


Mama Nzawisa akicheza sambamba na Amri SAidi Dongo
WAimbaji wa Msondo wakilishambulia Jukwaa
Hasani moshi kulia akiimba sambamba na Romani Mngande
Abdul Ridhiwani akiwa na Romani Mng'ande
Shabani Dede Kushoto na Hassani MOshi

KINONDONI YANYAKUA KOMBE LA MAJIMBO UVCCM


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Saidi Mtimizi akimkabidhi kombe nahoza wa timu ya Kinondoni Mahmudy Chikwela

Cecilia Jelemia akitoa baraka zake katika kombe hilo jana

Vodacom Miss Dar Indian Ocean ilivyofana



Vodacom Miss Dar Indian Ocean 2011, Stella Robert akipunga mkono kwa furaha baada ya usiku wa kuamkia leo kutawazwa kuwa Malkia wa Kitongoji hicho alipowashinda wanyane wengine 10 waliokuwa wakiwania taji lililokuwa likishikiliwa na Alice Luchiku Miss Kinondoni 2010.
Miss Dar Indian Ocean 2011, Stella Robert (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washindi wengine wanafasi ya pili Hamisa Hassan (kulia) na Renada Apoley baada ya kutangazwa washindi katika nafasi hizo.
Show ya ufunguzi ya warembo ilikuwaa kama hivi....
Vazi la ufukweni kila mrembo alipita kivyake, pichani ni Linda Joshua akijaribu bahati yake.
Catherine Frisch nae alijitosa...
Zahra Anonina hakubaki nyuma...
Georgina Saula alihakikisha nae anarusha kete yake.....
Renada Apoley ambaye aliibuaka Mshindi wa tatu huenda hivi aliwachengua majaji....
Sabrina Abllah akipiota na kivazi chake cha ufukweni....
huyu ni Fatma Pongwa akijinadi kwa majaji na mashabiki....
Sikama Judith Emmanuel alitishwa na kina cha maji la hasha ni mbwembwe tu za kuwastua majaji.
Geneveive Lucas nae alitaka kufuata nyayo za wajina wake aliyetwaa taji la Miss Tanzania mwaka 2010 lakini hakufurukuta.....
Hamisa Hassan alijaribu bahati yake na kuingia fainali na kupata tiketi ya kushiriki Miss Kinondoni 2011.
Kama ilivyo andikwa katika maandiko matakatifu kuwa Wamwisho atakuwa wa kwanza na Wakwanza atakuwa wa Mwisho ndivyo usemi huu ulijidhihirisha baada ya Mrembi huyu aliyekuwa wa mwisho kuibuka wa kwanza.
Miss Tanzania 2010 Genevieve Emmanuel Mopangala (kulia) pamoja na warembo wenginine walioingia fainali za Miss Tanzania nao walikuwepo kushuhudia tukio hilo.
Kikosi kazi cha Clouds FM kilikuwa katika viunga vyua Mbalamwezi kama hivi ...
Meza ya majaji ilikuwa makini katika kufanya kazi yao...
Clouds tena waliwakilisha....
Burudani toka kwa rais wa Wasafi na Diamond ilipatikana na alishambulia vyema...
wadau walikuwepo nao kujionea kimwana anaenyakua taji hilo na walifurahi pale mrembo waliompa maxi kushinda...
Kamati ya Miss Tanzania ilikuwepo ukumbi wa Mbalamwezi kujionea tukio...
Elihuruma Ngowi kutoka Vodacom Tanzania alikuwepo katika safu ya wadhamini.
Hawa ni Nouma ndo waleeee wadada wa Nganga moja Ndembe ndembe waliwasha moto na kuzua gumzo walahi ilikuwa nouma..
Millard Ayo na kikosi chake toka Clouds walikuwepo...

YALIYOJIRI KATIKA NUSU FAINALI YA KUMSAKA KIMWANA MANYWELE WA TWANGA PEPETA 20011 NDANI YA CLUB SUN CIRO


Mkurugenzi wa Kampuni ya The African Stars Entertainment (ASET),Asha Baraka akizungumza ndani ya Club SunCiro, katika shindano hilo la nusu fainali lililofana.

Kutoka kushoto ni MC Sauda Mwilima, Mratibu wa shindano hilo Maimatha Jesse (Mai), Asha Baraka na Khadija Kalili.
Washiriki wa shindano hilo wakiwa jukwaani katika shindano la kumsaka Kimwana wa Twanga 2011

Miondoko ikiendelea nyoka zikakatwa kila mmoja kwa umahiri wake aliojaaliwa.
Migongo ikapindwa basi ilimradi ilikuwa rahaaaaa.

Hapa kazi ikiendelea.


Majaji akiwamo Mtangazaji wa Kituo Cha Redio Clouds Gerald Hando wakiwatendea haki washiriki aliyeketi ni aliyekuwa mshindi wa pili wa shindano la Kimwana Manywele 2007 Husna Idd