Na Mwandishi wetu, Renton, Washington
Timu
ya Seattle Sounders FC imetangaza ushirikiano na Tanzania, nchi ambayo
ni nchi kubwa kabisa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.Ushirikiano
huo ulitiwa saini na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Balozi
Hamis Kagasheki (Mbunge) na Mmiliki wa timu ya Seattle Sounders Joe
Roth katika hafla fupi iliyofanyika jana mjini Renton.
Mbali
ya Waziri Kagasheki, wengine walioshuhudia kutiwa saini kwa
ushirikiano huo ni Balozi wa Tanzania nchini
Marekani, Mheshimiwa Balozi Mwanaidi S. Maajar, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi
ya Utalii Tanzania Dr. Aloyce Nzuki na maofisa wengine kutoka Wizara
ya Utalii, Ubalozini na maofisa wa Seattle Sounders FC.
Mambo
muhimu katika ushirikiano huo ni uwekwaji wa alama za vivutio vya
utalii vya Tanzania katika maeneo mbali mbali kama CenturyLink Field na
Starfire Sports Complex, uwanja wa mazoezi wa Sounders FC uliopo eneo
la Tukwila.
"Ushirikiano
wetu na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) utasaidia kutangaza vivutio vya
Utalii vya Tanzania nje ya mipaka yake kwani kuna vivutio vya ajabu mno
na kuleta unafuu kwa watalii ,” alisema Mmiliki wa timu ya Sounders
FC, Joe Roth. Na kuongeza kuwa ushirikiano huo utatoa nafasi muhimu
kwa soko la Utalii wa Tanzania nchi ya mipaka yake.
Waziri
Kagasheki mbali ya kupongeza kwa kufanikisha hatua hiyo muhimu katika
sekta ya Utalii nchini alisema kuwa ushirikiano huo utatoa fursa nyingi
kwa Watanzania na Wamerekani kwani utahimarisha juhudi za Wizara ya
Utalii katika kukuza soko la Utalii wa Kimataifa na wa Ndani.
Mheshimiwa Kagasheki pia alisema kuwa ushirikiano huo utatoa fursa za kibiashara kwa nchi zote mbili na kuongeza uwekezaji.
Katika
kuhakikisha zoezi ujumbe wa kupromoti vivutio vya Utalii wa Tanzania
vinawafikia wengi, michoro mbali mbali ya ukutani itachorwa kwenye ndani
ya uwanja upande wa Kaskazini Magharibi na Kaskazini Mashariki na
itaonekana kwa mara ya kwanza kwenye televisheni nchini Marekani wakati
wa mechi ya Sounders FC dhidi ya timu ya Chelsea katika uwanja wa
Field CenturyLink Julai 18 (Tanzania Julai 19).
Pia
maofisi wa TTB watakuwa mbele wakati wa mkutano wa kabla ya mechi wa
mashabiki wa soka na kuzungumzia masuala mbali mbali ya utalii na
usafiri katika nchi yao.
Timu
ya Seattle Sounders FC ilianza majadiliano ya ushirikiano na Tanzania
mwaka 2010 ambapo kocha msaidizi wa timu hiyo Kurt Schmid alisafiri
kuja nchini katika mpango wa kutafuta vipaji vya wachezaji.
Mchezaji wa timu ya Taifa, Mrisho
Ngassa kutoka timu ya Azam FC alisafiri mpaka Marekani na kucheza
mechi ya kihistoria kati ya Seattle Sounders na timu ya Machester
United mwaka jana (2011).
No comments :
Post a Comment