Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 11, 2012

UZINDUZI WA FILAMU MPYA YA SAYLA




 

Msimamizi wa kampuni ya Dynamic Minds, Angella Karashani akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa filamu mpya ya Salya iliyowashirikisha watu maarufu wakiwemo Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni msanii wa Filamu, Wema Sepetu na Wastara  Juma.

Na Khadija kalili

MSANII Wastara Juma akiwa na jopo la wasanii na watu maarufu kutoka katika kada mbalimbali nchini wanatarajia kuzindua filamu yao mpya itakayokwenda kwa jina la Sayla.

Filamu hiyo ambayo imepangwa kuzinduliwa katika mikoa mine ambayo ni Arusha, Morogoro, Dodoma na Dar es Salaam.

Aidha filamu hiyo itazinduliwa Mkoani Dodoma ambako inatarajiwa Wabunge wanaondelea na bunge la Bajeti nchini watahudhuria.

Wastara aliongeza kwa kuwataja baadhi ya wasanii na watu mashuhuri waliocheza filamu hiyo ni pamoja na msanii nyota nchini wa kike nchini Wema Sepetu, huku baadhi ya watu mashuhuri ni pamoja na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Shyrose Bhanji.

Wabunge wengine ni Ester Bulaya (Viti Maalum CCM), Halima Mdee na Zitto Kabwe (CHADEMA), watangazaji maarufu ni pamoja na Maimatha Jesse, Ephraim Kibonde na wengineo wengi.
Katika filamu hiyo Wastara nayeye amecheza huku mhusika mkuu ni Angela Karashani , filamu hiyo imeandaliwa na Kampuni ya Dynamic Minds.

Wastara ambaye ni mke wa muigizaji  Juma Kilowoko ‘Sajuki’ amewashkuru Watanzania kwa msaaada wao wa hali na mali na kuwataka wamuunge mkono katika  ununuzi wa filamu hiyo ambayo mapato yake yatakwenda katika kumsadia Sajuki na familia yake kwa ujumla

No comments :

Post a Comment