Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 18, 2012

Washindi wa Tuzo za Zuku Kutangazwa ZIFF




Washindi wa  Tuzo tatus za Zuku zilitangazwa wakati wa kufungwa rasmi wa tamasha la ZIFF. Tuzo za Zuku ni jamii mpya za tuzo ambazo zimefanikishwa kwa mara ya kwanza katika Tamasha la ZIFF. Tuzo hizo zili wazawadia filamu zenye ubunif wa kuelezea hadithi za kiafrika,  zilizotengenezwa Afrika, na watengenezaji na wasanii  kutoka bara la afrika.
Akizungumza wakati wa kutoa tuzo, Wangeci Murage Zuku alisema, "Tunafurahia sana kuanzisha tuzo mpya katika tamasha la ZIFF  na lengo letu ni kukuza tuzo hizi hadi ziwe mojawapo wa tuzo za kifahari hapa Afrika”.
Mwaka huu, tuzo la Zuku Best African Film Award lilipewa filamu ya ‘Inside Story’ kutoka Rwanda iliyotayarishwa na Rolie Nikiwe. Tuzo la Zuku Best Actor Tuzo lilishindwa na mwigizaji Kevin Ndege Mambo ambaye alifanya kazi kama katika filamu ya ‘Inside Story’.  Tuzo la  Zuku Best Actress lilishindwa na waigizaji wanawake watatu yaani Thuli Khulamelo, Nomfundo Dunazana na Reona Ngiba ambaye waliigiza katika filamu ya ‘Uhlanga the mark’
Tuzo za Ousmene Sembene Award and Verona Award na Tuzo la ZIFF Golden Dhow Award zilishindwa na mfilmau ya ‘Uhlanga the mark’. Tuzo la ‘ZIFF Best Short Film’ lilishindwa na Filamu ‘Mocassin’ iliyotayarishwa na Denis M. Kimathi. Tuzo la ZIFF Best Documentary Award, lilishindwa na filamu ya “Mama Africa” iliyotayarishwa na Mika Kaurismaki. Tuzo la ZIFF Best Animation Award lilipewa “Ostora” iliyotayarishwa na Hani Kichi
Kwa upande wa filamu za Tanzania, ‘Zamora’ iliyotayarishwa na Shams Bhanji iliweza kutwa tuzo mbili za filamu bora afrika mashariki na filamu. Filamu ya “Chungu” iliyotayarishwa na Kiela Billa iliwea kutwaa tuzo ya filmau bora ya ZIFF.
Zuku ambayo ni kampuni ya TV ya kulipia ambayo inaendelea kukua kwa kasi inapatikana Tanzania, Uganda na Kenya, ina nia ya kudhamini ZiFF kwa kipindi cha miaka 10 kwa thamani ya jumla ya dola milioni moja. Udhamini huo unatarajiwa kutoa  utulivu na msaada ambayo kwa upande utachangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha sekta ya filamu, si tu nchini Tanzania lakini maeneo mengine ya Afrika.
Kingamuzi cha Zuku kinatoa wigo mpana wa uchaguzi wa burudani ka vile habari za michezo, sinema, makala na muziki. Hizi ni pamoja na chaneli tatu za  BBC World News, MTV Base, Setanta Sports, Fox Entertainment na E!. Zuku pia inatoa chanelli zingine kama Zuku AFrika, Zuku Life, Zuku Sports na Zuku Movies. Huduma hii patikana kupitia satellite mahali popote Tanzania

No comments :

Post a Comment