Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, August 31, 2012

MBUYU TWITE ATUA KUIMARISHA UTANI WA JADI YANGA NA SIMBA



 Beki wa kimataifa wa timu ya Yanga ya Dar es Salaam, Mbuyu Twite, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana wakati alipowasili akitokea Rwanda, tayari kwa kujiunga na timu yake ya Yanga baada ya gumzo la muda mrefu na mvutano wa hapa na pale wa Watani wa Jadi Yanga na Simba, ambao kila mmoja alikuwa kijinadi kuwa amemsajili mchezaji huyo huku mmoja akibaki kuambulia manyoya.

Akizungumza na mtandao huu kuhusu kutua nchini huku akiwa ametinga Jezi no 4, yenye jina la Mwenyekiti wa Simba Ismail Rage, beki huyo amesema kuwa yeye ni mchezaji kama walivyo wengine na anatambua kuwa ametua katika timu yenye upinzani mkubwa na mahasimu wao Simba, hivyo yeye ametua kuendeleza Utaji wa Jadi  baina ya timu hizo, na ndiyo maana ameamua kuvaa jezi yenye jina la Rage, ili kuonyesha maana halisi ya  utani huo pamoja na kutokea mtafaruku wa hapa na pale kati ya vilabu hivyo.

Aidha Twite, amesema kuwa ''Namuheshimu sana Rage, na namuomba aniache nifanye kazi niliyotumwa na Baba yangu kama alivyoniamini na kuniruhusu kuja kuitumikia Yanga na kuwarejeshea Faranga yao Simba'' alisema Twite kwa kiswahili kilichopindapinda.

Twite amewataka mashabiki wa Yanga kumuamini na kupuuza yanayoendelea kuenea juu yake kuwa huenda akikosa kuichezea timu hiyo kutokana na kuchanganya madawa na kusema kuwa yeye ni mchezaji halali wa Yanga timu ambayo imefuata taratibu zote zinazotakiwa.

''Ujue hata mimi nilikuwa na wasiwasi japo nilipokea faranga za Rage, kwani hatukufanya vile imefanya Yanga hadi kufikia jana nilipopokelewa na mashabiki wengi wengi wengi sana wa yanga pale kwa uwanja wa Ndege'' alisema Twite.
Mbuyu Twite, akilakiwa na mashabiki lukuki wa Yanga kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jana.

WA5 WATINGA FAINALI YA SHINDANO LA MISS KANDA YA MASHARIKI TALENT, KUUMANA KESHO MORO



 Warembo wa 5, waliofanikiwa kutinga katika hatua ya Fainali ya shindano la Miss Kanda ya Mashariki, baada ya kuchuana vikali katika shindano lao dogo la Redd's Miss Kanda ya Mashariki Talent, lililofanyika jana usiku kwenye Hoteli ya Usambara, mjini Morogoro. Kutoka (kushoto) ni Mrembo, Joyce Baluhi, Shakhila Hassan, Zuhura Gola, Irene Veda na Salvina Kibona, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutangazwa washindi.
 Mrembo, Rose Lucas, akionyesha umahiri wake kwa kushambulia jukwaa ipasavyo kujaribu bahati yake kwa kuwakomvis Majaji, wakati wa shindano hilo.
 Mrembo, Shakhila Hassan, akiimba wimbo wa dini, Ebeneza na kuwapagawisha Majaji na mashabiki waliohudhuria onyesho la mpambano huo jana usiku.
 Mrembo, Joyce Baluhi, akisebeneka na wimbo wa Demu Mwigizaji wa Tunda Man, na kuwakosha vilivyo, Majaji na mashabiki waliohudhuria shindano hilo.
 Mrembo, Irene Thomas, akishambulia jukwaa kwa kucheza Dancehall........
 Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga (wa pili kushoto) akiwa meza kuu na Miss Tanzania 2010, Geneviv Emmanuel (kulia) na Miss Morogoro 2010, Asha Saleh, wakifuatilia shindano hilo.
 Baadhi ya wadhamini wa shindano hilo, pia walikuwepo kuwakilisha, (kushoto) ni mmoja kati ya wadhamini wa shindano hilo, Kitwe General Traders, ambapo pia wadhamini wengine ni pamoja na mtandano huu wa www.sufianimafoto.blogspot.com, Kampuni ya SPM:- Sufiani Photo Magic, Redd'd, Dodoma Wine, Usambara Safari Lodge, Chilakale Resort, B-Ze Hotel, Clouds Fm, Endepa, Gazeti la Jambo Leo na Simple & Easy Car.
 Sehemu ya mashabiki waliohudhuria shindano hilo.
 Sehemu ya mashabiki waliohudhuria shindano hilo, 'kuona na kunywa kikali'.....
 Washiriki wakicheza wimbo wao wa ufunguzi wa shoo hiyo kwa pamoja.
 Majaji wakishauliana jambo wakati shindano hilo likiendelea..........
 Hapa ni mshiriki, Irene Veda, akijifua kwa kupuliza Sax phone kabla ya kuanza kwa shindano hilo...
 Hapa ni kabla ya kuanza shindano hilo, warembo wakipiga picha ya pamoja kushoo Love.
 Namba za Bahati zilizotinga Tano Bora ...............
Mrembo, Irene Veda, akiimba na kupuliza Sax Phone......
You might also like:

Friday, August 24, 2012

Rais Dk. Shein ahimiza wananchi wa Zanzibar kujitokeza kuhesabiwa, zoezi la Sensa keshokutwa




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akitoa taarifa maalum kwa wananchi kuhusu zoezi la kuhesabiwa la Sensa, litakalofanyika siku ya Jumapili, Agosti 26, mwaka huu, ambayo itawezesha na kufanikisha mipango ya
maendeleo kwa Taifa. (Picha ya Ramadhan Othman, Ikulu)


Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
 24.8.2012                                                                                          

RAIS  wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, ameeleza kuwa matokeo ya sensa ndio yanayoipa Serikali taarifa halisi na ya kitaalamu juu ya idadi ya watu na taarifa nyengine muhimu katika kutayarisha mipango ya maendeleo.
 Dk. Shein aliyasema hayo leo katika taarifa yake aliyoitoa kupitia vyommbo vya habari kwa wananchi kuhusu umuhimu wa wananchi katika kushiriki kikamilifu katika zoezi la sensa ya watu na makaazi itakayofanyika tarehe 26 Agosti, mwaka huu.

Kwa matiki hiyo, Dk. Shein alieleza kuwa kujua idadi ya watu katika eneo fulani kunaiwezesha Serikali kukadiria mahitaji ya huduma kwa wakaazi wake ambapo kinyume chake ni kutoa huduma pungufu kwa vile hakuna takwimu sahihi ya wakaazi hao.

Dk. Shein alisema kuwa si jambo la kufurahisha kusikia kuwa baadhi ya watu ambao wanawashawishi watu wengie wasishiriki katika zoezi hilo muhimu na kusisitiza kuwa wananchi wa Zanzibar sio wageni katika zoezi hilo kwani wameshashiriki kwa vipindi kadhaa na kupata mafanikio ambapo sensa ya mwanzo iliyowajumuisha watu wote ilifanyika mwaka 1948.

Alisema kuwa suala la kuzingatia ni kuwa sensa haina uhusiano wo wote na matakwa ya watu kibinafsi bali ina lenga kuleta mafanikio kwa watu wote kwani hilo ni jambo la msingi sana kwa lengo la kuiwezesha  Zanzibar kujua idadi halisi ya wananachi wake na kuwafikishia maendeleo.

“Sote lazima tuweke mbele mapenzi na uzalendo kwa nchi yetu tukielewa kuwa sisi ndio wapangaji, watekelezaji na wasimamzi wa mipango yetu ya maendeleo kwani bila ya kushiriki katika utekelezaji wa majukumu hayo nchi yetu itawachwa nyuma na mataifa mengine yatasonga mbele kwa kasi, jambo ambalo siyo vyema kuliruhusu”, ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kwa mara nyengine tena kuwasihi wananchi wote kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo muhimu hapa nchini.

Aidha, Dk. Shein alisema kuwa sensa zote ni muhimu, lakini sensa ya mwaka huu ina umhimu wa kipekee kwa kuwa taarifa zitakazokusanywa zitatumika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025 kwa Tanzania Bara na mwaka 2020 kwa Zanzibar pamoja na Mkakati wa Kukuza na Kupunguza Umasikini MKUKUTA na MKUZA.

Dk. Shein alieleza kuwa Zanzibar imepiga hatua kubwa katika nyanja mbali mbali za kiuchumi, kisiasa, utawala bora, haki za binaadamu na ustawi wa jamii licha ya kuwepo kwa baadhi ya changamoto kadhaa.

Dk. Shein alisema kuwa taarifa kutoka Ofisi ya Rais inayoshughulikia Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo zimebainisha mafanikio makubwa katika kukuza uchumi katika kipindi cha miaka miwili iyiliyopita.

Alieleza kuwa pato la jumla la mtu binafsi limeongezeka kutoka wastani wa Tsh. 782,000 mwaka 2010 hadi kufikia Tsh. 960,000 mwaka 2011. Aidha, taarifa za hivi karibuni zinaonesha kuwa uchumi wa Zanzibar umekuwa kwa asilimia 6.8 katika mwaka 2011 ikilinganishwa na asilimia 6.5 ya mwaka 2010.

Pamoja na hayo, Dk. Shein alieleza kuwa jitihada mbali mbali zimefanyika kupunguza tatizo la mfumko wa bei ambapo katika miezi ya mwanzo ya mwaka huu ilionekana hali  kuwa sio nzuri na kutokana na juhudi hizo mfumko wa bei umeweza kudhibitiwa hadi kufikia asilimia 9.4 kwa mwezi wa Juni kwani awali ya mwaka 2011 na 2012 ilifikia hadi asilimia 16.6.
Akiendelea kutaja mafanikio hayo, Dk. Shein alisema kuwa mafanikio yamejitokeza kwa upande wa ujenzi wa miundombinu, kuimarika kwa huduma za maji safi na salama na pia kuzidi kusambaa kwa huduma za umeme kwa wananchi wengi zaidi hasa wa vijijini.

Pia, Dk. Shein alisema kuwa Zanzibar imepiga hatua katika uimarishaji wa sekta ya kilimo baada ya Serikali kutekeleza ahadi yake ya kutoa  ruzuku kwa wakulima ambapo asilimia 75 ya gharama imebebwa na Serikali.

Alieleza kuwa hatua iliyofikiwa hivi karibuni ya kuwandolea wananchi mchango wa Tsh. 40,000 kwa waja wazito wanaojifungua kwa njia ya operesheni, imetokana na kuwa na takwimu sahihi zenye kuonesha idadi yao na kiasi cha fedha kinachopatikana.

Sambamba na hayo, Dk. Shein aliwashukuru viongozi wa ngazi mbali mbali katika jamii ambao muda wote wameendelea kuwahamasisha wananchi ili washiriki katika sensa ya mwaka huu, huku akiwashukuru wananchi wote kwa ushirikiano mkubwa walioutoa wakati wa maandalizi ya zoezi la sensa tangu lianze katika hatua mbali mbali.

Aidha, Dk. Shein alisisitiza kuwa kwa azma ya kuitakia mema Zanzibar, ni vyema kila mtu ashiriki katika kuhesabiwa na kufanikisha zoezi hilo “Hii ni dhamana yetu sote”,alisema Dk. Shein.
Mbali na hayo Dk. Shein aliwataka Maafisa wa sensa na wote watakaoshiriki katika zoezi hilo kuwa na bidii ya kazi yao, nidhamu, ustahamilivu na uchangamfu wakati wote na wawafahamishe na wawaelimishe watu yanayopaswa kufanywa na maelezo yanayohitajika.

HASHEEM THABEET NA NYOTA WENZAKE WA NBA WATOA MAFUNZO YA KIKAPU DAR



NYOTA wa mpira wa kikapu kutoka Marekani, Hasheem Thabeet Mtanzania anayehezea Oklahoma City, Luol Deng Muingereza mwenye asili ya Sudan Kusini, anayechezea Chicago Bulls leo wameendesha programu ya kliniki kusaka vipaji vya mpira wa kikapu kwa wanafunzi wa shule za sekondari za Dar es Salaam kwenye viwanja vyta Don Bosco, Upanga.
Kliniki hiyo ilihudhuria na nyota wengine wa NBA, akiwemo Adam Andre, Masai Ujiri, mmiliiki na Meneja wa timu ya Denver Nuggets, Amadaou Gall Fall na Kocha J.
Alikuwepo pia Mkurugenzi Msaidizi wa Michezo Tanzania, Juliana Yassoda, Balozi Mdogo wa Marekani, Robert K Scott, Rais wa Chama cha  Mpira wa Kikapu (TBF), Mussa Mziya na Makamu wake, Phares Magesa.
Zoezi lilianza saa nne asubuhi kwa hotuba ndefu, zilizowafanya watoto waungue juwa muda wa zaidi ya saa mbili, kabla ya kuanza kupewa mafunzo hayo. Pichani ni watoto waliohudhuria wakiteseka na jua kwa kusikiliaza hotuba ndefu.

Watoto juani

Magessa akizungumza na Scott

Mdau wa michezo,l Athumani Tippo 'Zizziu' kushoto akiwa ma Michael Maluwe wa TBF

Mziya kulia akizungumza na Mama Yassoda. Kushoto ni Magessa

Ona watoto walivyoteseka na jua

Watoto juani

Watoto juani

Meneja Bidhaa wa Coca Cola, akitoa hotuba 'fupi'

Kocha Everist Mapunda akiwa na wachezaji wa Vijana, Anthony Leikanga, Gidibo Tindwa, Sada Ilyas 

Mtoto Felix Tippo kulia akisikiliza hotuba

Mama Yassoda akienda kurusha mpira kuzindua kliniki hiyo

Balozi Scott akitoa maelekezo kwa watoto

Amadou Fall akimsaidia mtoto kurusha mpira kwenye kikapu

Kutoka kulia Hasheem, Masai na Luol 

Kutoka kulia Balozi Scott, Masai na Magesa

Kutoka kulia Luol, Hasheem, Scott, masai na Magessa

Magessa katikati akiwa na Luol kulia na Hasheem kushoto

Kliniki

Masai kushoto na Amadaou

Kliniki

YANGA YAIRARUA RAYON 2-0



Kiiza katika mechi ya leo. (Picha na Saleh Ally wa Championi)
MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Yanga SC ya Dar es Salaam, wameanza vyema ziara yao ya mechi za kujipima nguvu nchini Rwanda, baada ya kuichapa Rayon Sport mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Amahoro mjini Kigali.
Yanga ambao jana walitembelea Ikulu ya Rwanda, walipoalikwa na rais Paul Kagame kupeleka Kombe la Afrika Mashariki na Kati, ambalo tangu mwaka 2002 mfadhili wake mkuu na mlezi wake ni Rais Kagame, mabao yake yalitiwa kimiani na Hamisi Kiiza dakika ya pili na Simon Msuva dakika 12.
Katika mchezo huo, kikosi cha Yanga kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Nsajigwa Shadrack/Stefano Mwasyika, Oscar Joshua/Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’/Frank Damayo, Simon Msuva, Haruna Niyonzima/Omega Seme, Didier Kavumbangu, Hamisi Kiiza/Jerry Tegete na Nizar Khalfan/Shamte Ally.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb ameiambia BIN ZUBEIRY kwa simu kutoka Kigali kwamba, timu yao ilicheza vema na kuwazidi kabisa uwezo wenyeji wao.
Alisema Yanga ilikuwa ina uwezo wa kufunga mabao zaidi, kama washambuliaji wake wangetumia vema nafasi zote walizotengeneza.
Bin Kleb alisema kwamba Yanga itashuka tena dimbani kumenyana na Polisi Jumapili na kwa mujibu wa ratiba ya awali, wanatakiwa kurejea Dar es Salaam Jumatatu.
Awali, Yanga ilikuwa icheze pia na mabingwa wengine wa zamani wa Kombe la Kagame, APR, lakini kutokana na timu hiyo kukabiliwa na mgogoro hivi sasa uliosababisha kufukuzwa kwa kocha Mholanzi, Ernest Brandy na nafasi yake kupewa kocha mzalendo kwa muda, imeshindwa kucheza.
Katika ziara hiyo, Yanga haijaambatana na mfungaji bora wa Kombe la Kagame, Said Bahanuzi ambaye amebaki Dar es Salaam kwa matatizo ya kifamilia. Yanga imekwenda Rwanda na msafara wa watu 42, wakiwemo wachezaji 28, Maofisa watano wa benchi la Ufundi na viongozi wanane.
Viongozi walio na timu Kigali ni Mwenyekiti, Yussuf Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini Mama Fatma Karume, Francis Kifukwe na Seif Ahmed ‘Magari’ sambamba na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Abdallah Bin-Kleb na Salum Rupia.
Benchi la ufundi ni kocha mkuu; Tom Saintfiet, Kocha Msaidizi Fred Felix Minziro, Kocha wa makipa, Mfaume Athumani, Meneja Hafidh Saleh, Daktari, Sufiani Juma na Mtunza vifaa Mahmoud Omary ‘Mpogolo’, wakati wachezaji ni makipa: Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Said Mohamed. Mabeki Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, Stefano Mwasyika, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondan, Ibrahim Job, Ladisalus Mbogo; viungo Athumani Iddi ‘Chuji’, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela, Simon Msuva, Shamte Ally, Omega Seme, Idrisa Rashid, Nizar Khalfan, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Rashid Gumbo, Nurdin Bakari na washambuliaji; Hamis Kiiza ‘Diego’, Jerry Tegete na Didier Kavumbangu.
Yanga ilitwaa Kombe la Kagame kwa mara ya pili mfululizo wiki mbili zilizopita, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa kuifunga Azam FC mabao 2-0, ambayo yalitiwa kimiani na Hamisi Kiiza ‘Diego Milito’ na Said Bahanuzi ‘Spider Man’.
Hiyo kwa ujumla ilikuwa mara ya tano mfululizo, Yanga inatwaa Kombe hilo, baada ya awali kuchukua mwaka jana, wakiifunga Simba katika fainali bao 1-0, Uwanja wa Taifa mfungaji Kenneth Asamoah ambaye ametemwa, ingawa siku hiyo Kiiza pia alifunga bao safi, ambalo refa alilikataa.
Yanga ilichukua kwa mara ya kwanza Kombe hilo, mwaka 1975 ikiifunga tena Simba katika fainali, mabao 2-0 wafungaji Sunday Manara ‘Computer’ na Gibson Sembuli (sasa marehemu) Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Ikachukua tena mwaka 1993, Uwanja wa Nakivubo, Kampala, Uganda kwa kuifunga SC Villa mabao 2-1, yaliyotiwa kimiani na Said Nassor Mwamba ‘Kizota’ (sasa marehemu) na Edibily Jonas Lunyamila.
Ilichukua tena mwaka 1999, ikiifunga tena SC Villa, Uwanja wa Nakivubo, kwa penalti 5-3, kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120, Yanga ikisawazisha bao kupitia kwa Lunyamila, baada ya Hassan Mubiru kutangulia kuifungia Villa, siku hiyo Manyika Peter akicheza penalti mbili za Waganda.   
Aidha, kwa kutwaa Kombe hilo chini ya Mbelgiji huyo, Yanga imeendeleza rekodi yake ya kutwaa mataji ya michuano hiyo, chini ya makocha wa kigeni baada ya mwaka 1975 kuchukua chini ya Tambwe Leya aliyekuwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kabla ya kuchukua uraia wa Tanzania, (sasa marehemu), 1993 chini ya Nzoyisaba Tauzany aliyekuwa raia wa Burundi kabla ya kuchukua uraia wa Tanzania, mwaka 1999 chini ya Raoul Shungu wa DRC na mwaka jana chini ya Mganda, Sam Timbe.

HABARI: http://bongostaz.blogspot.com

MZEE ANTHONY MATONYA AFARIKI DUNIA KATIKA KIJIJI CHA BAHI SOKONI KITONGOJI CHA NGHUNGUNGU DODOMA.



 Mze Anton Matonya wakati wa uhai wake akiendelea na kazi yake iliyompatia umaarufu ya kuomba hapa akiwa Morogoro.

Ni Matonya aliyepata umaarufu zaidi baada ya mkuu wa zamani wa mkoa wa Dar es salaam, Yusuf Makamba kumtimua jijini na kuagiza mamlaka husika kuhakikisha haruhusiwi kuingia kwenye mipaka ya Dar es salaam.

Ni yule ambaye baada ya kutimuliwa Dar es salaam, aliibukia Morogoro ambako aliendeleza staili yake ya kuomba akiwa amelala chali huku mkono akiwa ameunyoosha juu kwa muda mredfu bila ya kutikisika hata kama jua ni kali kupita kiasi.

Kijijini, Matonya anaishi kwenye nyumba ya tembe ambayo ni mali  ya mtoto wake wa kike aitwaye Elizabeth Matonya. 


Nyumba hiyo ya asili ya watu wa Dodoma ipo kwenye Kijiji cha Bahi Sokoni katika Kitongoji cha Nghungugu, umbali wa kilomita 3 kutoka yalipo makao makuu ya wilaya ya Bahi.
Kwa hisani ya Juma Mtanda Morogoro.

Wanahabari 20 Lindi, Mtwara wanolewa matumizi ya Internet.




Waandishi wa habari wa Mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwa
kwenye Mafunzo ya matumizi ya Internet kwenye ukumbi wa chuo cha SAUT Mtwara leo.
 Mwandishi wa Blog ya Raha za Pwani Mkoani Lindi, Ahmed Abdullaziz naye akiwa kwenye mafunzo hayo yaliyofanyika leo Mkoani Mtwara.
 Waandishi wengine kutoka vyombo mbalimbali wakiperuzi mitandao wakati wa mafunzo hayo.
Hapa wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo.
WAANDISHI wa habari nchini wametakiwa kuachana na matumizi pekee ya
internet kuandika habari badala yake  kutafuta habari uhalisia wake.
Hayo yameelezwa na  waandishi wa habari wakati wa mafunzo ya matumizi ya internet
kwa waandishi wa mikoa na wilaya za Lindi na mtwara yaliyoandaliwa na
MISA TAN kwa ufadhili wa mfuko wa vyombo vya habari, Mawasiliano na
Maendeleo Finland yanayoendelea katika ukumbi wa chuo kikuu cha Stella
Maris mkoani Mtwara.
Licha ya kuwepo kwa njia rahisi ya upatikanaji wa habari kupitia
mitandao ya internet hapa nchini waandishi wametakiwa kufuatilia
habari halisia kuepukana na kuwepo na mitandao ya uongo inayopotosha
jamii.
Kwa upande wake mratibu wa mafunzo hayo Andrew Marawiti, kutoka Misa
Tanzania akieleza malengo ya mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo  wa
matumizi ya internet katika upatikanaji wa habari mbalimbali na
uhalisia wake ili kuepuka na mitandao inayolenga kupotosha jamii.
Jumla ya  waandishi wa habari 20 kutoka mikoa ya lindi na mtwara
wanapata mafunzo ya matumizi ya internet yanayotolewa  na Taasisi ya
maendeleo ya Habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania(MISA
TANZANIA)chini ya Ufadhili wa Mfuko wa vyombo vya Habari, Mawasiliano
na Maendeleo Nchini  Finland (VIKES FOUNNDATION)
Na Ahmed Abdullaziz-Lindi

Chama kipya Cha Siasa nchini ADC leo kimefanya uhakiki wa mwisho jijini Dar. Wanachama wajitokeza kwa wingi . Viongozi wafurahia ufanisi.




 Baadhi ya wanachama waliojitokeza kwenye zoezi la uhakiki wa Chama Kipya Cha Siasa nchini (ADC) wakisubiri zamu yao kuhakikiwa na maofisa wa Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa nchini jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya Wanachama waliojitokeza ambapo jijini Dar es Salaam pekee wamepata wanachama zaidi ya 400, ikiwa ni sehemu ya mwisho kufanyiwa uhakiki ili kupata usajili wa kudumu.
 Maofisaa wa Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa nchini wakihakiki kadi za wanachama na taarifa zao kwenye zoezi hilo jijini Dar es Salaam leo.
Afisa wa ofisi ya msajili (kushoto) akisoma majina ya watu wanaotakiwa kufanyiwa uhakiki leo jijini Dar es Salaam leo