Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, August 26, 2015

BONDIA LULU KAYAGE ATIMKIA AFRIKA YA KUSINI KUKIPIGA TENA

Bondia Lulu Kayage akiwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya safari yake ya Afrika kusini kupigana mpambano mwingine agoust 28 picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Lulu Kayage akiwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya safari yake ya Afrika kusini kupigana mpambano mwingine agoust 28 picha na SUPER D BOXING NEWS

Mdau wa mchezo wa ngumi nchini Hamissi Berege kushoto akizungumza na George Sabuni ambaye anambatana na bondia lulu Kayage kulia kwenda kwenye mpambano wake mwingine utakaofanyika agous 28 Afrika ya kusini picha na SUPER D BOXING NEWS

Na Mwandishi Wetu
BONDIA wa Kike Lulu Kayage amenda tena nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya mpambano wake mwingine na bondia mwingine kutoka uko utakaofanyika agost 28 nchini Afrika ya kusini

akiongea kabla ya kupanda ndege bondia huyo alijingamba kuwa ataenda uko na atashinda kwa kuwa yupo fiti zaidi kwa sasa

hivyo nitaendeleza wimbi la ushindi aliongeza kwa kusema anaomba duwa kwa watanzania wamuombee ili aweze kumchakaza msauzi uyo tena kwa K,O mbaya kama alivyo mpiga 

mwenzake Lizbeth Sivhag bondia huyo aliyeambatana na bondia mkongwe wa siku nyingi George Sabuni kwa ajili ya kumbumbusha mambo mbalimbali awapo uringoni

amesema kwa sasa watanzania wategemee furaha kutoka kweke kwani mchezo anaocheza ni mgumu sana na yeye amejizatiti kuleta mafanikio kwa taifa nzima la Tanzania

Monday, August 24, 2015

ONESMO NGOWI AMPIGA TAFU YA VIFAA BONDIA LULU KAYAGE


Rais wa I.B.F Africa Onesmo Ngowi kulia akimkabidhi vifaa vya mchezo wa ndondi bondia Lulu Kayage baada ya kutembelea ofisi za rais huyo zilizopo posta Dar es salaam Lulu Kayage ataondoka nchini kuelekea Afrika ya kusini kwa ajili ya mchezo wake mwingine kabla ya kugombania ubingwa wa I.B.F Afrika mnamo Desemba 2 mwaka uhu
Rais wa I.B.F Africa Onesmo Ngowi wa pili kulia akiwa na bondia Lulu Kayage wa pili kushoto kulia ni George Sabuni na kushoto ni Hamisi Berege
BONDIA LULU KAYAGE AKIPOZI KATIKA OFISI ZA I.B.F AFRIKA
BONDIA LULU KAYAGE AKIPOZI KATIKA OFISI ZA I.B.F AFRIKA
BONDIA LULU KAYAGE AKIPOZI KATIKA OFISI ZA I.B.F AFRIKA

Saturday, August 22, 2015

BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' AMDUNDA ALLY MUHURO KWA T.K.O YA RAUNDI YA TATU


Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kulia akimshambulia kwa makonde mazito Ally Muhuro wakati wa mpambano wao ulifanyika siku ya jumamosi Class alishinda kwa T.K.O ya raund ya tatu Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kushoto akimtupia konde mpinzani wake Ally Muhuro wakati wa mpambano wao uliofanyika jumamos Class alishinda kwa T.K.O raundi ya tatu Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kushoto akimtupia konde mpinzani wake Ally Muhuro wakati wa mpambano wao uliofanyika jumamos Class alishinda kwa T.K.O raundi ya tatu Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Rojas Massamu kushoto akipambana na Subea Chube wakati wa mpambano wao Massamu alishinda kwa K,O ya raundi ya nne Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Awadhi Faraji kushoto akipambana na Shomari Mirundi wakati wa mpambano wao Mirundi alishinda kwa .K.O ya raundi ya pili Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Kelvin Majiba kushoto akipambana na Vicent Mbilinyi wakati wa mpambano wao uliofanyika katika viwanja vya shule ya Uhuru kariakoo Dar es salaa Mbilinyi alishinda kwa point Picha na SUPER D BOXING NEWS




Monday, August 17, 2015

IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' NA VICENTI MBILINYI KUWAKABILI WAPINZANI WAO AGOST 22

Bondia  bingwa wa Afrika wa mikanda miwili WPBF na UBO Afrika Ibrahimu Class 'King Class Mawe'anapanda tena uringoni kwa mara nyingine kukabiliana na Ally Muro katika mpambano wake  wa kumaliza ubishi nani zaidi kati ya mabondia hawo utakaofanyika katika viwanja vya basketball vilivyopo katikashule ya msingi Uhuru Wasichana Kariakoo Dar es salaam

bondia huyo mwenye historia ya kucheza machezo mzuri wa masumbwi misri ya mfalme wa ngumi duniani Mohamed Ali amekuwa kivutio kikubwa nchini ambapo mashabiki wengi wamekuwa wakimulizia kuwa anacheza lini hata hivyo jibu limepatikana kuwa anacheza agost 22 katika viwanja vya shule ya Uhuru wasichana

katika mpambano uho watasindikizwa na bondia machachali anaechipukia kwa sasa Vicent Mbilinyi atakayemenyana na Kelvin Majiba wakati Raymond Mbwago atacheza na Roger Masawe wakati Husein Pendeza atamalizana ubishi na Shomari Mirundi mipambano yote hiyo ni ya raundi sita
 lengo likiwa ni kuwashulisha mabondia wafanye kazi yao ya ngumi na kufanya mazoezi kila wakati ili mabondia hawo wapate chachu na changamoto za mchezo kila wakati ili waweze kupata mapambano makubwa ambaya yatawapeleka mbali zaidi kimchezo ambapo michezo yote itakayochezwa siku hiyo itawekwa katika madaraja mbalimbali ya viwango vya mabondia boxrec
Lengo  kubwa la mchezo huo ni kumpongeza Lulu Kayage bondia pekee wa kike katika ngumi za kulipwa aliyethubutu kuonesha uwezo wake akiwa ugenini na kumpiga kwa T.K.O ya raundi ya pili bondia wa Afrika ya kusini Lizbeth Sivhaga na ndie atakaekuwa mgeni wa heshima katika mapambano hayo
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile



Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi



pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

Thursday, August 13, 2015

FAINALI YA TMT KUFANYIKA AUGUST 22, MAKUMBUSHO YA TAIFA POSTA



WWW.BUKOBASPORTS.COM Shindano la kuibua na Kusaka Vipaji vya Kuigiza lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT) ambalo limedumu kwa takribani Miezi Minne hatimaye shindano hilo linakaribia kufika tamati mnamo tarehe 22 August 2015 huku Mshindi Mmoja Akiondoka Na Kitita Cha Shilingi Milioni Hamsini Za Kitanzania.

Na Washiriki waliofanikiwa kuingia Hatua ya Kumi bora watapata kifuta jasho huku wakiwa na mkataba mnono wa kufanya kazi na Kampuni namba moja ya Kutengeneza na Kusambaza filamu za Kitanzania ambao pia ndio waratibu wa Shindano Hilo la Tanzania Movie Talents (TMT) ya Proin Promotions Ltd.

Shindano la TMT lilianza mapema mwezi wa Nne kwa kutafuta vipaji katika Kanda ya Ziwa ambapo usaili ulifanyika Mkoani Mwanza na kuhitimishwa Kanda ya Pwani Mkoani Dar Es Salaam kwa kupatikana Jumla ya Washindi 20 kutoka Kanda sita za Tanzania
Washindi wa kanda sita walipata fursa ya kuingia ndani ya mjengo wa TMT huku wakipatiwa mafunzo ya sanaa kutoka kwa Walimu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam huku mchujo ukiendelea na kupelekea kila wiki Washiriki wawili kuaga shindano, takribani wiki tano jumla ya washiriki 10 waliweza kuaga shindano hili ambalo limefikia hatua ya kuwapata washiriki 10 waliofanikiwa kuingia hatua ya Kumi bora huku wakingojea fainali itakayotoa mshindi wa kitita cha shilingi milioni hamsini za kitanzania
Mpaka sasa washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya Kumi bora wanaendelea na kujifua Kwaajili ya fainali ambayo imebaki wiki moja tu kwa fainali hiyo kuliteka jiji la Dar huku hofu na presha zikiwapata Washiriki hao.
Fainali ya TMT itafanyika Siku ya Jumamosi ya tarehe 22 August 2015 katika ukumbi wa makumbusho ya taifa karibu na Chuo cha IFM kwa viingilio vya shilingi Elfu 50 kwa VIP na Elfu 30 kwa viti vya kawaida.
TMT 2015 inapigwa tafu na Precious Air, Cam gas, ITV na Radio One, Global Publishers, I-View Studio, Paisha na Hussein Pamba Kali

PETER MUHUNZI WA TEFA APETA RUFAA YAKE MUHIBU KANU AONDOLEWA



Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Advocate Rashid Saadallah (katikati) akiongea na wandishi wa habari kuhusu maamuzi ya rufaa za wagombea wa nafasi mbalimbali za uchaguzi wa Chama cha Soka Temeke (TEFA) jana kwenye ofisi za DRFA jijini Dar es Salaam. Kulia ni katibu wa kamati hiyo Fahad Katanga na kushoto ni msemaji wa DRFA, Omar Katanga. (Picha na Rahel Pallangyo)

MWENYEKITI wa TEFA, Peter Muhunzi na Sizza Chenja wameshinda rufaa baada ya kuwekewa pingamizi kwenye mchakato wa uchaguzi wa Chama cha Soka mkoa wa Temeke. (TEFA)
Akitoa maazimio ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA,Mwenyekiti wa Kamati, Advocate Rashid  Saadallah, alisema kamati yake ilipitia mapingamizi yake kwa makini na kina kwa kufuata katiba ya TEFA, DRFA na ya chama mama ambacho ni TFF na kutoka na maamuzi ambayo hata hivyo alikiri kama mgombea hataridhika anaweza kukata rufaa kwenye ngazi nyingine ambayo ni TFF.
“Peter Muhunzi ambaye anagombea nafasi ya mwenyekiti wa TEFA, ameshinda rufaa yake baada ya kuthibitisha kigezo cha elimu kwa maana ya kumaliza kidato cha nne na Sizza Chenja kamati imempitisha aendelee na mchakato wa uchaguzi baada ya kuthibitisha kuwa ana uzoefu wa kutosha katika uongozi wa mpira wa miguu kama katiba ya TEFA Ibara ya (31)(1)(j) inavyotaka”, alisema Saadallah
Pia alisema Rashid Salim, ambaye pia anagombea nafasi ya Mwenyekiti -ameshindwa kuleta vielelezo kuthibitisha uzoefu wake katika masuala ya mpira kama Ibara ya 31(1)(j) inavyosema pia Aziz Mohamed Khalfan, kamati imegundua kwamba alienda kwenye mchakato wa uchaguzi akiwa hana sifa kwa sababu alifungiwa na kamati ya nidhamu na usuluhishi ya kutokushiriki au kujihusisha na mpira kwa muda wa miezi kumi na mbili (12) na TEFA.
Saadallah alisema kwenye nafasi ya Makamu wa kwanza wa Mwenyekiti, Shufaa Jumanne amepitishwa aendelee na mchakato wa uchaguzi baada ya kuridhika na uthibitisho wa uzoefu wa zaidi ya miaka mitatu katika uongozi wa soka Daudi Mumbuli, kamati inaitupilia mbali rufani baada muweka pingamizi kushindwa kutokea mbele ya kamati kuthibitisha madai yake.
Naye Omary Kapilima ambaye anagombea makamu wa kwanza wa Mwenyekiti  ameondolewa baada ya kushindwa kuleta cheti cha kidato cha nne kinachotambulika na Baraza la Mitihani la Taifa yaani (NECTA) ili kukidhi kigezo cha elimu kama inavyotakiwa na Ibara ya 31(1)(b) ya katiba ya TEFA japo  kathibitisha uzoefu wa uongozi wa mpira na Salehe Mohamed kamati inamuengua katika mchakato wa uchaguzi kwa kushindwa kuthibitisha kiwango chake cha elimu kwa  kushindwa kuleta cheti cha kidato cha nne(Academic Certificate) kama inavyotakiwa na Ibara ya 31(1)(b) ya katiba ya TEFA pia Bakili Makele ambaye alikuwa anagombea makamu wa pili ameenguliwa kwa kigezo hicho cha elimu kwani amekiri kwamba elimu yake ni ya darasa la saba
 Amack Nabola ambaye anagomea Ujumbe wa soka la wanawake na vijana ameenguliwa katika mchakato kwa kukosa sifa ya elimu ya kidato cha nne kama ibara ya 31(1)(b) ya katiba ya TEFA inavyotaka lakini Fikiri Magoso ambaye anagombea mjumbe wa kamati ya Utendaji amepitishwa kugombea nafasi hii kwa sababu anakidhi vigezo kwa kuwa na cheti cha darasa la saba kama katiba ya TEFA anavyomtaka mgombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji kuwa na elimu isiyo chini ya darasa la saba.
Mgombea Muhibu Kanu ambaye alikuwa nagombea nafasi mbili, ya makamu Mwenyekiti na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji kamati imemuengua kwa sababu  ni kinyume cha kanuni za uchaguzi za TFF za mwaka Ibara 10(9) ambayo inakataza mgombea kugombea nafasi zaidi ya moja.
Pia Saadallah alisema kamati yake imefanyia kazi pingamizi la ambazo kikatiba na kanuni kwani zile za matumizi mabaya ya fedha na ubadhirifu, kamati haina mamlaka ya kuyatolea maamuzi hivyo yanapelekwa kwenye kamati ya maadili ya DRFA.

TANGAZO LA DAWA YENYE NGUVU





DAWA YA NGUVU ZA KIUME NA MSIMKO KWA WANAWAKE WASIO NA HAMU YA TENDO LA NDOA AMBAYO HULETA MSISIMKO KWA WANAUME NA WAKE WAKUTANAPO.KWA SASA INAPATIKANA KWA BEI NAFUU HAPA JIJINI DAR ES SALAAM MAKUTANO YA MTAA WA KIPATA NA BARABARA YA MSIMBAZI
ALLY WA YANGA BOMBA UHURU NA MSIMBAZI 0787230551 AU 0652755838, 0715406938


PIGA NO O713827689, 0755074505 , au 0719 541366
,0652755838 UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM



SHULE YA UHURU FIKA JENGO LA AZAM BAKHRESA ULIZA NGAEJA 0715110900

KARIAKOO SHULE YA UHURU STENDI YA MABASI YA TANDIKA ULIZIA ZUNGU MUHUZA TIKETI 0712743870

NA UKIWA ILALA SHARIF SHAMBA FIKA DSJ BANDA NAMBA 14 SIMU 0718718671

NA UKIWA KOTA ZA BANDARI KARIAKOO FIKA MKUNGUNI KIBANDANI KWA HUSEIN 0753893295

MWANANYAMALA FIKA JABA KLABU ULIZA MACHELLAH 0713470492

ENZOY INALETA HESHIMA

Uchaguzi Ubunge Jimbo la Handeni lawaka moto



“Kimsingi hakuna mgombea anayejua amepata kura ngapi na wapi amekosa, maana hata huyo Salu anayedaiwa ameshinda amepewa ushindi wa jumla na hakuna anayejua namna  gani mchakato huo umefanyika, ndio maana ofisi ya CCM wilaya iliamua kufanya  siri, huku kila mgombea akiambiwa jambo la kumpa moyo,” alisema Mbwana.

Naye Chifu Msopa alisema kwamba hawawezi kukubali mtu mmoja afanye mambo kwa maslahi yake, hivyo wagombea wote wa ubunge watasusia mchakato wa kampeni katika jimbo la Handeni, kama hali ya kubebana itaendelea dhidi ya Katibu na washindi wake aonao wanafaa kuliko wengine.

“Hatutaki kuendelea kuwa waoga huku wachache wakiendelea kuiharibu CCM yetu, uchaguzi huu urudiwe au kufuata maagizo ya Kamati ya Siasa ya wilaya na ile ya Maadili ambayo kwa bila kujua kwanini, Katibu aliyaweka kando mapendekezo hayo na kufanya anavyotaka mwenyewe,” alisema Msopa.

Kwa kipindi cha wiki moja sasa jimbo la Handeni limekuwa kwenye mgogoro mkubwa kati ya viongozi wa CCM wilaya ya Handeni na wagombea ubunge ambao kwa kiasi kikubwa wameonyesha kuchukizwa na mwenendo mbovu wa katibu wa CCM handeni, ambaye ameendelea kuwabeba wagombea, wakiwamo wale waliotajwa kwenye kashfa za rushwa.

SIKU YA KIMATAIFA YA VIJANA DUNIANI YAADHIMISHWA KWENYE VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR



Maandamano  yakiongozwa na bendi ya jeshi la polisi
 
Baadhi ya vijana kutoka shule mbalimbali wakiandamana kuingia katika viwanja vya mnazi mmoja wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishw  jijini Dar es Salaam. Mashirika mbalimbali  ya mataifa yanayofanya shughuli za vijana ni kamaUNFPA, IYF, UNIC, ILO, RESTLESS DEVELOPMENT, YUNA, AMREF, MARIE STOPES, pamoja na PSI.(Picha zote na Geofrey Adroph)
 
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na viongozi wengine wakipokea maandamano ya vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi na wapili kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bibi. Natalia Kanem.
 
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel pamoja viongozi wengine wakipokea maandamano ya vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
 Viongozi katika meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akizungumza na vijana wakati wa Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Katika hotuba yake aliweza kuzungumzia maswala ya watoto wa kike kubeba mimba wakiwa na umri mdogo ambao unapelekea kuacha masomo kutokana na ujauzito huo pia aliwasisitiza vijana kuwa na umoja kwani ndio nguvu kazi ya Taifa.
Mwendeshaji wa Sherehe hiyo Bi. Usia Nkhoma ambaye ni Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC)  akizungumza jambo na  vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi(wa nne kutoka kulia) akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza na vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.Wa tatu kutoka Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel, Wa kwanza kulia ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa pili kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
 Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akitoa shukrani kwa wawakilishi wa Umoja wa Mataifa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa pili kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwahutubia vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake aliwasisitiza vijana kujitokeza katika uchaguzi unaotegemea kufanyoka mwezi wa kumi mwaka huu ili kuchagua viongozi makini watakaoweza kutetea masuala ya vijana na pia aliwasisitiza vijana kufanya kazi za kujitolea.
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum akiwasalimia vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Bw. Hesein Melele(wa kwanza kuli) kijana ambaye ni mwakilishi wa asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA) akiwasilisha maazimio yaliyofikiwa na vijana wakati wa kongamano lililofanyika Agosti 10 mwaka huu kujadili ujumbe wa siku ya kimataifa ya vijana duniani na kuandaa maazimio yaliyowasilishwa kwa mgeni rasmi leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani.
 Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jangwani, Tatu Ahmed akitoa shukrani kwa wageni waalikwa waliofika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani.
Mratibu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutoka asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA), Rahim Nasser akiwatolea ufafanuzi vijana waliofika kwenye banda la Umoja wa Mataifa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani  Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akimsikiliza kwa makini Mratibu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutoka asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA), Rahim Nasser alipotembelea kwenye banda la Umoja wa Mataifa
 Mkufunzi wa Ujasiriamali/Biashara wa Program ya anzisha na imarisha biashara yako (SIYB) iliyochini ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. MacDonald Lanzi (wa pili kutoka kulia) akimfafanulia jambo Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel. Wa pili kushoto ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa kwanza kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
Mshauri na Mkufunzi wa Ujasiriamali/Biashara wa Program ya anzisha na imarisha biashara yako (SIYB) iliyochini ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. Lawrence Ambokile(mwenye koti jeusi) akitoa ufafanuzi kwa Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipotembelea banda ilo
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
Ofisa Habari wa Kituo cha Taarifa cha Umoja wa Mataifa Tanzania (UNIC), Stella Vuzo(wa kwanza kushoto), Meneja mradi wa ICS Bi. Imisa Masinjila(wa pili kutoka kushoto)Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara hiyo Prof. Hermas Mwansoko(wapili kutoka kulia) pamoja na Imisa Masinjila wakizungumza jambo maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum(wa kwanza kushoto) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem(katikati) wakizungumza jambo na  Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi  wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya vijana waliofika kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
  Bw. Hesein Melele(katikati) kijana ambaye ni mwanachama wa asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA) akiwa kwenye picha ya pamoja na vijana wenzake ambao ni Rehema Pascal(kushoto) pamoja na Felister
  
 
 
 
 
 
 
 

 Vijana kutoka vikundi mbalimbali wakitoa burudani wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 
 
 
Vijana wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali yaliyokua yakiendelea wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.