Monday, July 13, 2009

WAOGELEAJI 6 KUSHIRIKI MASHINDANO YA DUNIA ITALIA

Chama cha mchezo wa kuogelea Tanzania kinatarajia kuondoka Julai 18 kwenda nchini Italia kwa ajili ya mashindano ya Dunia ya mchezo huo yatakayoanza Julai 21 mwaka huu.

Akizungumza na kipindi cha michezo na burudani Rais wa chama hicho Deogratius Vicent ametanabaisha kuwa safari hiyo itajumuisha watu sita yaani wachezaji wanne na viongozi wawili.

Vicent ameongeza kuwa lengo lao ni kwenda na wachezaji 12 lakini kutokana na matatizo yaliyokuwa nje ya uwezo wao basi hawana budi kwenda na idadi hiyo pungufu.

Hata hivyo amewaombna wadau wote wanaoupenda mchezo huo kujitokeza kwa wingi katika kuwapiga tafu ili waende kuiwakilisha vema Tanzania.

No comments:

Post a Comment