Wednesday, November 11, 2009

UCHAGUZI TBF WASUASUA

Uchaguzi wa Shirikisho la mpira wa kikapu uliopangwa kufanyika Novemba 28 mwaka huu unaweza usifanyike kutokana na sikukuu ya Idd Alhaj.
Uchaguzi huo uliosogezwa mbele mara tatu mfululizo unaonekana kusuasua kutokana na ukata wa kifedha.
Hadi hii leo wagombea waliojitokeza ni 25, baadhi yao ni Nafasi ya Urais, Richard Kasesela, Mussa Mziya, Jakson Kalikumtima na Phaes Magesa, katika Nafasi ya Makam wa Rais Ahmed Rajab Ahmed, Alijua Mwakalinga ma Alexander Msoffe.
Wengine nafasi ya katibu Msaidizi ni Robert Manyerere, John Nash, Oden Mmbaga, Prosper Mushi na Selemani Semunyu anayewania nafasi ya kamisheni ya watoto.

No comments:

Post a Comment