Friday, January 15, 2010

BENITEZ HAONDOKI LIVERPOOL

Nafasi ya kocha Rafael Benitez siyo swala la kujadili licha klabu ya Liverpool kuondoshwa katika FA Cup baada ya kuchapwa na Reading, taarifa hiyo ni kwa mujibu wa kiongozi wa michezo wa klabu hiyo Christian Purslow.
Benitez anakabiliwa na msukumo mkubwa toka kwa mashabiki hasa baada ya kupteza nafasi kwa klabu hiyo iliyoshuka daraja, kuondolewa mapema katika ligi ya mabingwa na kufanya vibaya katika ligi kuu ya England.
Licha ya matatizo yake, Mhispania huyo bado anaendelea kupambana kubaki katika dimba la Anfield.
hata hvyo katika mahojiano Purslow amesema Benitez anaungwa mkono na uongozi wa bodi ya klabu hiyo.
Kapteni wa zamani wa Liverpoll, Ronnie Whelan jana alikaririwa akisema anaamini kocha Benitez sasa nafasi yake inalazimika kuchukuliwa na kocha mwingine.

No comments:

Post a Comment