Monday, January 18, 2010

MICHUANO YA WAZI TENIS KUANZA FEBRUARI

Mashindano ya wazi ya mchezo wa tenisi yataanza kuvurumishwa mwanzoni mwa February mwaka huu katika viwanja vya klabu ya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Nahodha wa mchezo huo Inger Njau amefahamisha kwamba mashindano hayo ni utaratibu wa mashindano ya kila mwaka na yanasimamiwa na chama cha tenisi Tanzania.
Aidha ameongeza kwamba washiriki wa mashindano hayo wanatoka kila pembe ya Tanzania pamoja na majirani zao Kenya na Uganda.
amesema maandalizi ya mashindano hayo yapo tayari ikiwemo zawadi kabambe kutoka kwa mdhamini wa mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment