Monday, February 8, 2010

MATUMLA APIGWA UJERUMANI NA BENJAMIN SIMON

Bondia wa ngumi za kulipwa anayeshikilia mkanda wa Dunia unaotambulika na Shirikisho la ngumi la IBF Benjamin Simon wa Ujerumani amemdunda bondia wa Tanzania Rashidi Matumla kwa pointi pambano lililofanyika jana usiku nchini Ujerumani.
Mwamuzi namba moja pawel kandyn ametoa pointi 118 kwa 110 mwamuzi namba mbili claus greysel pointi na 119 kwa 109 mwamuzi namba tatu Ben decrosy ametoa pointi 119 kwa 109.
Akizungumzia pambano hilo kocha wa Rashidi Matumla ambaye ndiye mwandaji wa safari hiyo Ally bakari Champion amesema kwamba mchezo huo kwa bondia wake ulikuwa mgumu lakini amecheza mchezo mzuri na amemtumia salam Bondia Franciss Cheka wa Morogoro.

No comments:

Post a Comment