Sunday, November 18, 2012

PICHA ZA KITOTO KICHANGA KILICHOOKOTWA JALALANI MKOANI SINGIDA.



Mtoto wa kiume anayekadiriwa kuwa na umri kati ya mwezi moja au mwezi mmoja nusu akiwa amebebwa na mama msamaria mwema baada ya kuokotwa akiwa ametelekezwa kwenye takataka ngumu nyuma ya nyumba ya kulala wageni ya Subira iliyopo mjini Singida.
Mama msamaria mwema akiwa anasindikizwa na askari polisi kumpeleka mtoto mchanga kituo kidogo cha polisi kilichopo kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida.Mtoto huyo wa kiume ameokotwa (16/11/2012) baada ya kutelekezwa kwenye lundo la takataka na mtu ambaye bado hajafahamika hadi sasa. (Picha na Nathaniel Limu).

No comments:

Post a Comment