Friday, January 22, 2010

KARATE KUENZI MUUNGANO KWA MASHINDANO

Mashindano ya karate ya kuwania kombe la Muungano yataanza kuvurumishwa April 24 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Phlip Chikoko ni Mwenyekiti wa Chama cha mchezo wa karate Taifa, TASHOKA, amesema mashindano hayo yanafanyika kila mwaka na yanashirikisha wachezaji kutoka mikoa yote inayoshiriki mchezo huo.
Maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika ambapo washindi watajinyakulia zawadi mbali mbali vikombe medali.
Aidha amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kama wanavyojitokeza katika mashindano ya mpira wa miguu.

No comments:

Post a Comment