Monday, February 6, 2012
JERUSALEM GROUP YAZINDUA KATIBA YAKE
AUT EZEKIEL NA KAJALA WAGOMBEA BWANA..!!
Baadhi ya watu wa karibu na mastaa hao, walifunguka na kusema kuwa dalili hizo mbaya zimejitokeza hivi karibuni ambapo nyota hao walionekana wakipigiana simu za kutukanana.
Kajala na Aunty hivi karibuni urafiki wao ulikuwa ni wa hali ya juu ambapo hata hivyo baadhi ya watu walitabiri kuwa hawawezi kufika mbali kwani wote ni wanawake ambao wanapenda kujirusha.
Mmoja wa wasanii ambae anafanya kazi na nyota hao, ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema kuwa siku ambayo Kajala anatoroka na mpenzi wa rafiki yake walikuwa sehemu moja wanakunywa, baada ya wote kulewa ndiyo mchezo huo ulipofanyika.
Alisema baada ya kufanya kitendo hicho alimtaarifu Aunty, kuwa asiwe na wasiwasi kwani mpenzi wake ameondoka naye na hawezi kurudi eneo la tukio kwani wako mbali.
“Unajua hawa walikuwa ni marafiki sana na naweza kusema awali walikuwa kama ndugu lakini baada ya kuchukuliana wanaume basi hali imekuwa mbaya na kwa sasa hawapeani hata salamu.” alisema msanii huyo.
Baada ya warembo hao kutafutwa, Kajala, alisema kuwa hana bifu na Aunty lakini tatizo ambalo lipo ni dogo na watalimaliza kwani mapenzi hayana mwisho katika hii dunia.
Alisema alimchukua mpenzi wa rafiki yake lakini siku hiyo alikuwa amelewa na hakujua kama anafanya makosa makubwa kama hayo.
“Unajua pombe zikiwa zimepanda kichwani unaweza kufanya kitu ambacho hukutegemea kukifanya, lakini kuhusu hilo naweza kusema kwamba yataisha kwa sababu sisi marafiki wa kushibana,” alisema Kajala.
Kwa upande wa Aunty alidai kuwa hawezi kurudiana tena na mpenzi wake huyo ambaye tayari amelala na Kajala kwani haitaji kutoka na mwanaume ambaye tayari ametembea na msanii.
Aliongeza kwa kusema kuwa endapo Kajala, anahitaji waendelea kuwa marafiki basi amuombe msamaha kupitia vyombo vya habari ili kila mtu aweze kujua kilichotokea kati yao.
Sunday, February 5, 2012
SUPER D BOXING COACH AJIDHATITI KUENDELEZA MCHEZO WA NGUMI 2012
klabu ya Bigrayt Mwananyamala yaendelea kuwanowa vijana
MASHINDANO YA KWANZA YA MCHUJO KUTAFUTA MABONDIA WATAKAOWAKILISHA TAIFA LA TANZANIA
Watakao husika katika mchujo huo ni mabondia ambao wapo mazoezi,katika vituo vilivyoainishwa na BFT kwa ajili ya mazoezi ya awali kwa wachezaji walioteuliwa kwa kuzingatia vigezo vya kuwa wamefanya vizuri sana katika mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa yaliyoandaliwa au kutambuliwa na BFT.
Vituo hivyo ni uwanja wa ndani wa Taifa,Magereza Ukonga,mwenge JWTZ,mgulani JKT na kituo kilichopo jijini Mwanza.
Kwa umuhimu na ubora wa mashindano BFT inawaomba wale wote ambao wanahitaji kucheza na kujima na wachezaji walioteuliwa awali waende kujiandikisha katika vituo hivyo kwa kuwa watakao ruhusiwa kucheza ni wale tu ambao watakuwa wamepitishwa na makocha wa timu ya taifa waliopo katika vituo hivyo.
Katika mashindano hayo tunategemea kupata ufadhiri kutoka katika mamlaka ya usajiri wa biashara na makampuni (BRELA)
Hali ya mazoezi katika kambi zote inaendelea vizur hadi kufikia leo hakuna majeruhi na katika kituo cha mwenge leo watakuwa na zoezi la kucheza wao kwa wao kwa nia ya kujiimalisha zaidi na kuzoea hali ya mashindano kwa maandalizi ya tarehe 15.
Mako.re Mashaga
KATIBU MKUU
Mob;0713588818
MCHEZO WA POOL UNAZIDI KUPANDA CHATI NCHINI
FRANCIS CHEKA MADA MAUGO KUGOMBEA UBINGWA WA IBF RAUNDI 12 APRIL 28 PTA SABASABA
GRAND MALT KUNOGESHA SAUTI ZA BUSARA.
Meneja wa Kinywaji cha Grand Malt Consolata Adama akizungumza na waandishi wa Habari hawapo pichani kuhusu udhamini wa kinywaji cha Grandmalt kwenye Tamasha la Sauti za Busara litakaloanza Jumatano 08/02/2012 hadi jumapili 12/02/2012 kwenye kiwanya cha Ngome Kongwe Zanzibar.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Toleo la Leo
GRAND MALT KUNOGESHA SAUTI ZA BUSARA.
Dar es Salaam, FEBRUARY 6, 2012:
Kinywaji maarufu cha Grand Malt leo kimethibitisha kukamilisha maandalizi ya kuliongezea raha tamasha la Sauti za Busara linalofanyika Zanzibar kuanzia tarehe 8 hadi tarehe 12 Februari.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa kinywaji cha Grand Malt; Bi Consolata Adam alisema; Sauti za Busara ni tamasha muhimu sana kwa nchi yetu, kwani linatangazwa ulimwengu mzima na hivyo kuvutia watu wa mataifa mbali mbali kuja kushuhudia tamasha hili, hii ni fursa kubwa kwa kutangaza vivutio vya utalii vya nchi yetu. Pia tamasha hili linaleta mapinduzi makubwa katika tasnia ya muziki hapa nchini, kwa kuwaalika wasanii mbalimbali toka kila kona ya bara la Afrika, hii pia ni fursa kwa wasanii wa nyumbani kujifunza mengi toka kwa wasanii hawa.
Kufuatia umuhimu wa tamasha hili, Grand Malt imekuwa mstari wa mbele kama mmoja wa wadhamini, kuhakikisha kuwa tamasha hili litakuwa na hamasa ya aina yake, tumeweka vikundi ya kutoa burudani katika maeneo mbalimbali ambapo maandamano ya Sauti za Busara yatapita siku ya tarehe 9, ikiwemo viwanja vya Kisonge, ambapo pia wakazi wa Zanzibar watapata nafasi ya kupata kinywaji chao cha Grand Malt bila wasiwasi. Hivyo tunawakaribisha wakazi wa Zanzibar na watu wote watakahudhuria tamasha hili kuja kuburudika na Grand Malt huku tukifurahia burudani za Tamasha la Sauti za Busara 2012. Alisema Consolata.
Aidha alisema Kinywaji cha Grand Malt kitakuwa katika eneo la Ngome kongwe kwa siku zote za tamasha ili kuongeza furusa kwa watu mbalimbali kupata nafasi ya kuburudika na kinywaji kisichokuwa na kilevi na kilichotengenezwa kwa kutumia virutubisho vilivyo bora kabisa cha Grand Malt.
-MWISHO-
Kwa Maelezo zaidi wasiliana na:
Consolata Adam – Grand Malt Brand Manager, +255767266766, consolata.adam@tz.sabmiller.
Editha Mushi, Communications & Media Manager, +255767266420, editha.mushi@tz.sabmiller.com
TANGAZO LA DAWA YENYE NGUVU

ALLY WA YANGA BOMBA UHURU NA MSIMBAZI 0787230551 AU 0652755838
,0652755838 UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM
BUGURUNI LOZANA STENDI YA TAX ULIZIA ADAMU KIBANDANI 0755875884
MWANANYAMALA FIKA JABA KLABU ULIZA MACHELLAH 0713470492
SHEREHE ZA MAULID YA KUZALIWA BWANA MTUME MUHAMMAD S.A.W
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kushoto) akiwa katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume S.A.W zilizofanyika jana katika viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Zanzibar,(kushoto) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabbi,(wa kwanza kulia) Jaji Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Othman Makungu,na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji. (05/02/2012) (PICHA NA RAMADHAN OTHMAN IKULU)
Ustadhi Salum Rashid wa Madrsa Qadiria ya Amani akisoma Maulid Barzanji Mlango wa nne,ambao Waislamu husimama na kumswalia Bwana Mtume,S.A.W,wakati wa sherehe za Maulid zilizofanyika jana katika Viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,( katikati wakiitikia Dua katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume S.A.W zilizofanyika jana katika viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Zanzibar,ikiombwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabbi,(wa pili kushoto)(wa kwanza kulia) Jaji Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Othman Makungu,na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,Wazri wa Katiba na Sheria Sheikh Abuu Bakar Khamis,(kushoto). (05/02/2012) Thursday, February 2, 2012
Abdalah Mohamed 'Prins Naseem KUTETEA UBINGWA WAKE NA Salehe Mkalekwa .Februari 24
BINGWA wa mkanda wa Shirikisho la ngumi za kulipwa Tanzania (PST) Abdalah Mohamed 'Prins Naseem' atapanda ulingoni kutetea mkanda wake wa PST Februari 24 mwaka huu dhidi ya Salehe Mkalekwa.
Pambano hilo la ubingwa wa PST litakuwa ni pambano la uzito wa kg 57 na litashirikisha mapambano mengine manne ya utangulizi.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa pambano hilo Shaban Adiosi 'Mwayamwaya' alisema pambano hilo litafanyika katika ukumbi wa New Kibeta uliopo mbagala kuu Dar es Salaam.
Alisema pambano hilo la ubingwa wa PST ni muendelezo wa shirikisho hilo kuendelea kuwainua mabondia chipkizi ambao hawajawa na majina makubwa ili nao waweze kufikia kiwango kizuri cha mchezo huo.
"Ubingwa huu wa PST ni maalum kwa ajili ya mabondia chipkizi na ndio maana mabondia wanaoshirikishwa wengi ni chipkizi na lengo ni kuendeleza vipaji vyao,"alisema Mwayamwaya.
Aliyataja mapambano ya utangulizi yatakayopamba pambano hilo yatakuwa kati ya Shaaban Zungu na Hasan Salehe watakaopigana uzito wa kg 55, Safari Mbeyu na Ibrahim Maokola watakaopigana uzito wa kg 67, Jofrey Pacho atakayetwangana na Seleman Shaaban na Abdalah Yusuph atakayepigana na Omari Kijepa.
Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones na wengine kibao ‘DVD’ hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha Rajabu Mhamila ‘Super ‘D’.
“Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika pambano kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi,” alisema Super ‘D’.
Rashidi MATUMLA VS MANENO OSWARD KUPAMBANA TENA Februar 25 UKUMBI WA PTA SABASABA DAR
BONDIA wa ngumi za kulipwa Rashid Matumla 'Snek man' amesema kukutana ulingoni mara kwa mara na bondia Maneno Osward 'Mtambo wa gongo' hawachezei njaa isipokuwa ni mapenzi ya ngumi aliyokuwa nayo.
Matumla na Maneno wanakutana ulingoni kwa mara ya tano sasa ambapo baadhi ya wadau wamekuwa wakihisi labda mabondia hao hupigana kwa sababu ya kutafuta fedha.
Akizungumza kwa njia ya simu Dar es Salaam jana, Matumla alisema yeye binafsi bado anauwezo wa kupigana katika mchezo huo na kama angetaka kustaafu angeweza kufanya hivyo ila bado anayo nafasi ya kufanya vizuri katika mapambano yake.
Alisema pambano lake dhidi ya Maneno litakalopigwa Februari 25 mwaka huu katika ukumbi wa PTA Sabasaba litakuwa ni pambano lake la tano kukutana na bondia huyo.
"Mimi na Maneno tumeshakutana mara nne ulingoni hadi sasa na hili litakuwa ni pambano letu la tano kupigana,"alisema Matumla na kuongeza kuwa.
"Katika mapambano hayo nimemshinda Maneno mapambano mawili, amenipiga pambano moja na tumetoka sare pambano moja lakini kama itawezekana nitamtwanga katika pambano lijalo,"alisema Matumla.
Alisema kwa sasa anajifua chini ya kocha wake Habibu Kinyogoli ambaye ameingia naye mkataba wa kumnoa na anainami atafanikiwa kumtwanga Maneno katika mchezo huo.
Pambano hilo la Februari 25 litakuwa ni pambano la marudiano kwa mabondia hao baada ya kutoka sare katika pambano la kwanza lililofanyika katika ukumbi wa Henken Mtoni Desemba 25 mwaka jana.
Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones na wengine kibao ‘DVD’ hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha Rajabu Mhamila ‘Super ‘D’.
“Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika pambano kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi,” alisema Super ‘D’.
TIGO YAONGOZA KUWA NA MASHABIKI WENGI FACEBOOK
BONGO MOVIES VS WANAMZIKI WA DANSI KUKIPIGA JUMAPILI KUCHANGIA WAATHILIKA WA MAFULIKO
BONGO MOVIES VS WANAMZIKI WA DANSI KUKIPIGA JUMAPILI KUCHANGIA WAATHILIKA WA MAFULIKO
ZANTEL MAKES NEW APPOINTMENTS
![]() |
| Ahmed Seif – Commercial Director PMO |
![]() |
| Sarah Mwigune – Customer Experience Director |
ONYESHO LA LADY IN READ 'RELOADED' 2012 KUCHANGISHA PESA KWA AJILI YA KUJENGA KITUO CHA KUSAIDIA WAATHIRIKA WA MADAWA YA KULEVYA.
Wednesday, February 1, 2012
FRANCIS CHEKA MADA MAUGO KUGOMBEA UBINGWA WA IBF RAUNDI 12 APRIL 28 PTA SABASABA
Bondia Fransic Cheka akizungumza na waandishi wa habari leo kupigania ubingwa IBF raundi 12 litakarofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba Aprilo 28.(picha na www.superdboxingcoach.

Makamu mwenyekiti wa Oganaizesheni ya ngumi za Kulipwa Nchini, Madaraka Nyerere (Kushoto) akiwaelekeza mabondia Fransc Cheka kulia na Mada Maugo jinsi ya kusaini mkataba wa makubaliano wa kupigania ubingwa IBF raundi 12 litakarofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba April 28.(picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Abdallah Mohamed 'Prince Nassime' kugombania ubingwa wa PST na Swaleh Mkalwekwa feb.24
Bondia Abdallah Mohamed 'Prince Nassime' kulia akifuliwa na kocha wake msaidizi Rajabu
Bondia Abdallah Mohamed 'Prince Nassime' (kulia) akioneshana ufundi wa kutupa makonde na Jofray Sadiq wakati wa mazoezi ya kujiandaa kugombania ubingwa wa taifa Kg.67 unaotambuliwa na shilikisho la kumi za kulipwa PST na Swaleh Mkalwekwa feb.24












