Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, January 31, 2014

Promota jay msangi apigwa stop na serikali kuandaa mapambano ya ngumi




Shi....Shilole achia ngoma mpya iitwayo Chuna Buzi



Shilole
BAADA ya kutamba na kibao chake cha 'Nakomaa na Jiji', msanii Zuwena Mohammed 'Shilole' ameachia kazi mpya iitwayo 'Chuna Buzi' na kuwataka mashabiki wake kumuunga mkono kama walivyofanya katika kazi zake za nyuma kuanzia 'Lawama', 'Dume Dada' hadi 'Paka la Baa'.
Wimbo ni utunzi wa Barnaba Boy ambaye ameutendea haki kwa kum back-up mkali huyo anayekimbiza katika filamu pia.

AZAM kukipiga na Ferreviario de Beira Chamazi




* CAF yaruhusu uwanja wake wa Chamazi

chamazi_2
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika CAF leo tarehe 31 Januari 2014 limeupa kibali cha kuchezea mashindanoya kimataifa yanayoandaliwa na CAF uwanja wa Azam Complex Chamazi na kuufanya uwanja wa kwanzaunaomilikiwa na klabu Afrika Mashariki  kuruhusiwa kuandaa (ku-host) mashindano makubwa ya vilabu
Kwa mujibu wa barua pepe iliyotumwa leo na CAF kupitia kwa naibu mkurugenzi wa mashindano Bwana Khaled Nassar, Uwanja wa Azam Compex Chamazi umepita vigezo vyote vinavyohitajika na CAF kuchezewa mashindano ya kimataifa hivyo kuanzia tarehe ya leo, uwanja huu unaruhusiwa “kuchezewa mechi za CAF
Bwana Khaled ameandika katika taarifa yake ya barua pepe kwenda TFF na Azam FC kuwa CAF ilimtuma mkaguziwake toka nchini Zimbabwe Bwana Wilfried Mukuna kuja kukagua uwanja huu. Bwana Mukuna aliwasilisha ripoti CAF iliyopelekea shirikisho hilo kutoa kibali kwa Azam FC na TFF kuruhusiwa kuutumia uwanja huu kwa mechi zinazoandaliwa na CAF
Uongozi wa Azam FC umetoa shukrani kwa mkaguzi wa CAF Bwana Mukuna, Uongozi wa TFF chini ya Rais Jamal Malinzi, na uongozi wa CAF Cairo Misri hasa Bwana Khaled Nasser kwa kuwezesha zoezi hili kufanyika kwa uwazi na uweledi wa hali ya juu uliopelekea uwanja wetu kupata kibali cha kutumika kwenye michezo ya kimataifa.
Azam FC sasa imewatangazi
wapenzi wake kuwa kuanzia msimu huu mechi zake za  CAF zitachezwa Azam Complex Chamazi

BIBI KIZEE AKUTWA CHUMBANI KWA MTU NA KUHUSISHWA NA IMANI ZA KISHIRIKINA LEO HUKO HAMUGEMBE MJINI BUKOBA



 Bi. Kizee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70, ambaye jina lake halikuweza kufahamika kwa urahisi  amenusurika kifo baada ya polisi kumnusuru kwa kudaiwa kukutwa akiwa uchi chumbani kwa mtu  akifanya mambo yasiyoeleweka alfajiri ya leo  Ijumaa Januari 31,2014 
 Bi. Kizee akiwa kwenye gari la polisi baada ya kuokolewa na polisi kutoka kwa wananchi wenye asila kali mara tu ya kukutwa kwenye chumba. Mashuhuda wa mwanzo wanasema Bibi huyo amekutwa akitapatapa bila kujua la kufanya huku mwili wake ukiwa Uchi na nguo zake  zikiwa pembeni kitendo kinachopelekea kusadikiwa kwamba Bibi huyu ni  mchawi wakati wengine wakisema wasubili taarifa ya Polisi.
 
 Polisi wakiondoka eneo la tukio wakiwa na  Shuhuda mmoja aliyedai alikuwa miongoni mwa watu waliomkurupusha bibi huyo chumbani.
 Wakielekea kituo cha cha polisi cha Bukoba Mjini leo asubuhi.
 Bibi huyo akiwa kwenye ulinzi mkali baada ya kufikishwa kwenye kituo kikuu cha polisi mjini Bukoba
PICHA ZOTE NA BUKOBAWADAU BLOG

KINANA AWAZUSHIA NEEMA WAENDESHA BODABODA MBEYA



 Katibu Mkuuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akiwa abebwa na waendesha bodaboda alipofanya nao mkutano leo kwenye Ukumbi wa Mtenda, Sowto, jijini Mbeya, ambapo alizungumzia mambo mbalimbali likiwemo la kuinua kipato chao cha maisha.
Waendesha bodaboda Mkoa wa Mbeya, wakwa wamembeba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye baada ya kufurahishwa na hotuba yake.
Waendesha bodaboda wakishangilia baada ya Kinana kuwakuna kwa hotuba nzuri iliyolenga kuwasaidia kuboresha  maisha yao.

First Meeting of the African Ambassadors in the Africa House



 Balozi wa African Union nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali (kulia) akiongoza mkutano wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014
 Waheshimiwa Mabalozi waliohudhuria mkutano huo wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014
 Waheshimiwa mabalozi wakifuatilia mkutano wa kwanza wa Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye jengo jipya la ofisi ya African Union lililopo Georgetown, Washington, DC. siku ya Jumatano January 29, 2014

Thursday, January 30, 2014

SUPER D AMPONGEZA BONDIA MUSSA MCHOMANGA NA KUMZAWADIA



Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimkabidhi clip bandeji na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi kwa bondia Mussa Mchopanga baada ya kumdunda Anton Idoa kwa K,o ya raundi ya pili bondia huyo ndie bingwa kwa sasa wa mkoa wa Dar ers salaam na anajiandaa na mashindano ya Majiji yatakayofanyika katikati ya mwaka huu Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Anton Idoa akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Mussa mchopanga wakati wa mashindano ya Mkoa wa Dar es salaam yaliyofanyika katika ukumbi wa Panandi panandi Ilala Mchopanga alishinda raundi ya pili picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Anton Idoa kushoto akirusha konde ambalo alijareta madhala kwa mpinzani wake ambae anamwangalia Mussa Mchopanga wakati wa Mashindano ya Mkoa wa Dar es salaam Mchopanga alishinda kwa K,O ya raundi ya pili picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Kocha Mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini Habibu Kinyogoli kushoto akimwinua mkono juu bondia Mussa Mchopanga baada ya kumvalisha medali ya Dhaabu baada ya kuibuka mshindi wa mkoa wa Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimkabidhi clip bandeji na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi kwa bondia Mussa Mchopanga baada ya kumdunda Anton Idoa kwa K,o ya raundi ya pili bondia huyo ndie bingwa kwa sasa wa mkoa wa Dar ers salaam na anajiandaa na mashindano ya Majiji yatakayofanyika katikati ya mwaka huu Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com



Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimkabidhi cheti kwa bondia Mohamed Chibumbuli mara baada ya kuibuka mshindi wa mashindano ya mkoa wa Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimkabidhi cheti kwa bondia Mohamed Chibumbuli mara baada ya kuibuka mshindi wa mashindano ya mkoa wa Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimvisha medali ya dhaabu bondia Mohamed Chibumbuli mara baada ya kuibuka mshindi wa mashindano ya mkoa wa Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimvisha medali ya Fedha bondia Abdul Rashidi  mara baada ya kuibuka mshindi wa pili wa mashindano ya mkoa wa Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

KAMATI YA PAC YAFANYA UKAGUZI VITABU VYA CHENJI YA RADA DAR



Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, (CHADEMA), Zitto Kabwe, akiwa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam Jumatano Januari 29, 2014, akikagua vitabu vya ziada. Kamati ya bunge ya PAC, ilifanya ziara ya kushtukiza shuleni hapo ili kubaini kama vitabu vilivyonunuliwa kutokana na chenji ya rada vimekwishagawiwa kwenye shule mbalimbali kama ilivyoahidi serikali. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, kamati yake ilikuta vitabu hivyo vikitumiwa na wanafunzi.

Zitto akizungumza na wanafunzi
Wanafunzi wakipiga makofi, wakati mwenyekiti huyo akizungumza nao
Wanafunzi wakisikiliza maelezo ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC), ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe, kwenye shule ya msingi Bunge katikati ya jiji la Dar es Salaam Jumatano Januari 29, 2014.Picha na K-Vis Blog.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MAWAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, SAYANSI ELIMU IKULU DAR.



 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha-Rose Migiro, wakati alipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo kwa mazungumzo. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwakaribisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa (katikati) wakati walipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa (katikati) wakati walipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam

UNIC yaendelea kutoa mafunzo ya mateso ya kambi za wayahudi


DSC_0014
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond juu ya umuhimu wa kujifunza mauaji ya kimbari ya wayahudi ya mwaka 1933.
Na Mwandishi Wetu, MOblog Tanzania
Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) kimeendelea kutoa mafunzo na elimu juu ya umuhimu wa kukumbuka maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya ukombozi wa kambi za mateso ya Auschwitz kwa wanafunzi wa sekondari na shule za msingi nchini.
Akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond ya jijini Dar es Salaam leo asubuhi, Afisa habari wa kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama amesema kwamba ni muhimu kwa kizazi na kizazi kujifunza madhara ya mauaji na maangamizi ya moto dhidi ya wayahudi yaliofanywa na askari wa kinazi wa Ujerumani.
“Ni muhimu kutoa mafunzo kwa vijana wakitanzania wa shule za msingi na sekondari ili wajue kwamba tofauti za rangi na za kidini hazina nafasi ya kutugawa kama binadamu,” amesema Nkhoma.
DSC_0005
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Diamond na Mlezi wao wakimsikiliza Bi. Ledama (hayupo pichani).
DSC_0044
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama, akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataiafa katika siku ya kimataifa ya maadhimisho ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya maangamizi ya moto.
Alisisitiza kwamba mauaji na mateso ya Auschwitz yalipoteza mamilioni ya watu wasio na hatia na mafunzo haya yanaonyesha chuki na ubaguzi dhidi ya wayahudi na chuki za aina nyingine yoyote hazina nafasi katika ulimwengu wa leo.
Nkhoma amesema kwamba binadamu wote ni sawa na tofauti za kipato au dini au rangi haziwezi tena kujenga chuki dhidi ya binadamu wengine kwa sababu wote kama binadamu tuna haki sawa mbele za mungu.
DSC_0051
Wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond jijini Dar es Salaam, wakifuatilia sinema maalum ya mauaji ya kambi za mateso ya wayahudi mwaka 1933.
Wakati huo huo, ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika siku ya kimataifa ya maadhimisho ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya maangamizi ya moto amesema aliona makambi ambako wayahudi, waroma, wasinti, mashoga, wafungwa wa kivita na watu wenye ulemavu walitumia siku za mwisho katika hali ya kinyama.
“Umoja wa Mataifa ulianzishwa kuzuia kila aina hii ya fazaa kutokea tena, lakini bado misiba kuanzia Cambodia hadi Rwanda mpaka Srebrenica inaonyesha kuwa sumu ya mauaji ya kimbari bado inatiririka,” ilisema taarifa hiyo.
DSC_0082
Pichani juu na chini ni Wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond wakisoma baadhi ya machapisho ya Umoja wa Mataifa.

VYAMA VYA NGUMI ZA KULIPWA NCHINI VYAUNGANA KUWAKUTANISHA MABONDIA JUMAMOSI


Vyama vya ngumi za kulipwa nchini  vimekubali  kuungana na wenzao TPBO kushiriki mkutano wa mapromota wa ngumi na mabondia wote wa Tanzania. Mkutano huo unaotarajiwa  kufanyika katika ukumbi wa vijana Kinondoni, siku ya jumamosi tarehe 1/2/2014 kuanzia  saa nne asubuhi. Mkutano huo ulioitishwa na TPBO chini ya udhamini wa KITWE GENERAL TRADERS ukiwa na lengo la kuweka mikakati ya sasa na ya baadae kwa ajili ya kuinua ngumi za hapa nchini,sanjali na kutambulikana kwa mapromota na mabondia wenyewe kwa kutengenezewa vyeti maalum na vitambulisho, vitakavyowafanya watambulike katika jamii ya wanamasumbwi wa hapa Tanzania na hata nje ya mipaka ya nchi yetu,hizo ni sehemu ya mada zitakazozungumzwa.
Ibrahim kamwe akizungumza na vyombo vya habari ,alisema ‘Mkutano huo ambao utawahusisha mapromota wote ,pamoja na viongozi wa vyama vya ngumi za kulipwa,makocha na mabondia wote wa ngumi za kulipwa, haijalishi wewe ni nani ili mradi ni mwalimu wa ngumi, mratibu wa ngumi au bondia ni vema ukafika katika mkutano huo ambao ni mara ya kwanza kufanyika  katika historia ya ngumi za kulipwa kuwakutanisha kwa pamoja waratibu, viongozi na mabondia wa nchi nzima kwa pamoja, pia mkutano huo utaendana na mapromota kupewa vyeti  na kurekebisha usajili wa mabondia ambao usajili wao haujakaa sawa.

Wednesday, January 29, 2014

KING CLASS MAWE ASAINI MKATABA WA KUPAMBANA NA CHEKA FEB 8 PTA SABASABA




BONDIA bora wa mwaka 2013,2014 katika uzito wa  KG 63  Ibrahimu Class 'King Class Mawe' ame saini mkataba wa kupambana na Cosmas Cheka Feb 8 mwaka huu katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam
Mara baada ya kusaini mkataba huo wa kucheza raundi 10 za ubingwa wa Taifa kg,60 amesema atafanya mazoezi ya kutosha kuhakikisha ana msambalatisha mpinzani wake raundi za awali kwa kuwa alikuwa anachonga sana juu yake

mpambano huo uliodhaminiwa na Promota Maarufu nchini Jay Msangi utakuwa na msisimko wa aina yake kutokana na mabondia hawo kuwa gumzo katika ulimwengu wa masumbwi ndani na nje ya nchi ya tanzania

King Class aliongeza kwa kusema kuwa nipo fiti nimejiandaa na ninasubili tu kuvishwa ubingwa huo wa taifa kwani Cheka ana ujanja kwangu mbinu zake zote nimesha zikamata

King Class Mawe anae nolewa na jopo la makocha wanao ongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' Rajabu Mhamila 'Super D' Kondo Nasoro 

Bondio huyo amewashukulu wadau wa mchezo wa ngumi kwa kumuwezesha kuchaguliwa kuwa bondia bora wa mwaka katika uzito wake kwa kuwapita mabondia wengine wanne na yeye kuibuka kidedea katika kin'yan'gan'yiro hicho

LG yazindua aina ya OLED TV nchini Tanzania



Ofisa Mauzo wa Kampuni ya LG Bw, Valerian Banda akionesha mawani kwa ajili ya kuangalia TV ya Oled ambayo kwa mara ya kwanza imeingizwa nchini sasa zinapatikana katika maduka yote ya LG
Dar es Salaam, tarehe 29 January 2014 – LG imezindua TV ya kwanza ulimwenguni aina ya OLED ambayo ndiyo imeingia katika soko ya nchini Tanzania, TV aina ya OLED inayojikunja ni mwanzo wa burudani ndani ya nyumba. Aina yake ya kujikunja ambayo inaitwa IMAX inatupa uzoefu wa hali ya juu pamoja na kuangalia kwa starehe kubwa.
TV hii mpya aina ya OLED kutoka LG ikiwa na teknolojia ya rangi nne, ambayo kwa mujibu wa kampuni inaongeza pikseli nyeupe kwa rangi nyekundu, kijani na blu kwa mtazamo bora. Itakuwa na screen nyembamba aina ya OLED ambayo ukubwa wake ni 4.3mm. Pamoja na stendi yake ambayo ina vipimo ifuatavyo 1227x799x192mm na uzito wa kilo 17.2.  
 TV aina ya OLED LG namba 55EA9800 inakuja na idadi ya chaguo ya kuunganisha ambayo ni HDMI port (x4), port ya kusikiliza muziki ( 3.5mm), RF, AV ( composite), port ya muziki, USB 2.0 (x2), USB 3.0 na LAN port.”
TV hii pia ina kitako ambacho ni wazi kama kioo ambacho TV huwa haionekani kama imeungana nacho na TV huonekana kama inaning’inia hewani. Pia TV hii imewezeshwa kuwa na muonekano wa spika tano kwenye kitako chenye LG 55EA9800 zenye uwezo waku toa sauti ya watti 40.
Bwana Rajesh Darji, wa Garnet Star Ltd Distributor wa LG Home Entertainment Products amesema“ Hii TV aina ya OLED inapatikana katika maduka makubwa ya LG na wakala wake.
Hii itampa mteja  uonaji mzuri isiyokuwa na mwisho. Burudani ya nyumbani imejazwa na mabadiliko yanayo endelea kila siku na sisi kama kampuni ya LG ni kazi yetu kuwa letea bidhaa inayoendana na wakati huu”
Mtengenezaji kutoka Korea ya Kusini amekaririwa akisema kuwa utendaji waLG 55EA9800 una kasi mara mia zaidi ya TV zingine aina ya LED/LCD, ambayo inaweza kupunguza mwanga wa picha zinazo jionesha kwa kasi katika kioo cha TV
Kampuni ya LG imeongeza‘rimoti ya ajabu’yenye uwezo wa kupokea sauti na ishara na mchanganyiko wa mambo mbali mbali.

MASHINDANO YA NGUMI MKOA WA DAR ES SALAAM YAPAMBA MOTO


Bondia Cosmas Peter kushoto akipambana na Hfidhi Bamtula wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana kwenye mashindano ya Mkoa ambayo yanachagua bondia atakaewakilisha Mkoa wa Dar es salaam Bamtula alishinda kwa Point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Hafidhi Bamtula kushoto akitupa ngumi ambayo imenda hewani bila mafanikio alipokuwa akipambana na Cosmas Peter wakati wa Mashindano ya Mkoa wa Dar es salaa ambayo wanachagua mabondia wa mkoa huo Bamtula aklishinda kwa point mpambano huo Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Emillian  Patrick kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Hamad Furahisha wakati wa mashindano ya mkoa wa Dar es salaam Patrick alishinda kwa point mpambano huo picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Kasimu Mbutike kushoto akimtupia konde la mkono wa kushoto Yusufu Said wakati wa mashindano ya mkoa Wa Dar es salaam yaliyofanyika katika ukumbi wa panandi panandi Ilala Bungoni Said alishinda kwa point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

LG yazindua aina ya OLED TV nchini Tanzania









Dar es Salaam, tarehe 29 January 2014 – LG imezindua TV ya kwanza ulimwenguni aina ya OLED ambayo ndiyo imeingia katika soko ya nchini Tanzania, TV aina ya OLED inayojikunja ni mwanzo wa burudani ndani ya nyumba. Aina yake ya kujikunja ambayo inaitwa IMAX inatupa uzoefu wa hali ya juu pamoja na kuangalia kwa starehe kubwa.
TV hii mpya aina ya OLED kutoka LG ikiwa na teknolojia ya rangi nne, ambayo kwa mujibu wa kampuni inaongeza pikseli nyeupe kwa rangi nyekundu, kijani na blu kwa mtazamo bora. Itakuwa na screen nyembamba aina ya OLED ambayo ukubwa wake ni 4.3mm. Pamoja na stendi yake ambayo ina vipimo ifuatavyo 1227x799x192mm na uzito wa kilo 17.2.  
 TV aina ya OLED LG namba 55EA9800 inakuja na idadi ya chaguo ya kuunganisha ambayo ni HDMI port (x4), port ya kusikiliza muziki ( 3.5mm), RF, AV ( composite), port ya muziki, USB 2.0 (x2), USB 3.0 na LAN port.”
TV hii pia ina kitako ambacho ni wazi kama kioo ambacho TV huwa haionekani kama imeungana nacho na TV huonekana kama inaning’inia hewani. Pia TV hii imewezeshwa kuwa na muonekano wa spika tano kwenye kitako chenye LG 55EA9800 zenye uwezo waku toa sauti ya watti 40.
Bwana Rajesh Darji, wa Garnet Star Ltd Distributor wa LG Home Entertainment Products amesema“ Hii TV aina ya OLED inapatikana katika maduka makubwa ya LG na wakala wake.
Hii itampa mteja  uonaji mzuri isiyokuwa na mwisho. Burudani ya nyumbani imejazwa na mabadiliko yanayo endelea kila siku na sisi kama kampuni ya LG ni kazi yetu kuwa letea bidhaa inayoendana na wakati huu”
Mtengenezaji kutoka Korea ya Kusini amekaririwa akisema kuwa utendaji waLG 55EA9800 una kasi mara mia zaidi ya TV zingine aina ya LED/LCD, ambayo inaweza kupunguza mwanga wa picha zinazo jionesha kwa kasi katika kioo cha TV
Kampuni ya LG imeongeza‘rimoti ya ajabu’yenye uwezo wa kupokea sauti na ishara na mchanganyiko wa mambo mbali mbali.