Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, July 31, 2014

NGUMI ZILIVYOPIGWA MANZESE SIKU YA IDDI PILI



Bondia Sadick Nuru kushoto akioneshana umwamba na Baraka Mchonge wakati wa mpambano wao ulifanyika Mazese Dar es salaam wakati wa sikukuu ya iddi pili Nuru alishinda kwa point mpambano huo Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Stevin Kobelo kushoto akirusha ngumi kumpiga Karim Ramadhani wakati wa mpambano wao uliofanyika siku ya iddi pili katika ukumbi wa Manyara park manzese Dar es salaam mpambano huo walitoka droo ya kufungana point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia Joseph Gili kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Ibrahimu Tamba wakati wa mpambano wao uliofanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa manyara park manzese Dar es salaam Tamba aklishinda kwa T.K.O  ya raundi ya nne Picha na www.superdboxingcoach .blogspot.com
Bondia Julius Kisalawe kushoto akipambana na Ramadhani Kumbele wajkati wa mpambano wao wa ubingwa wa TPBC uliofanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa Manyara Park Manzese Dar es salaam Kumbele alishinda kwa point na kufanikiwa kuchukua ubingwa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini Habibu Kinyogoli 'Masta' kulia akimvisha mkanda wa ubingwa bondia ramadhani Kumbele baada ya kumdunda Julius Kisalawe kwa point kushoto ni Refarii Ally Bakari picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Diamond Platnumz arejea nchini na tuzo yake



 
 Diamond Platnumz  akionesha tuzo yake aliyoshinda kwa baadhi ya vyombo vya habari  na mashabiki waliofika kumlaki,mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere leo asubuhi (30.7.2014) kutokea Marekani ambako alishinda zawadi ya Mwanamuziki bora wa kiume wa Afrika Mashariki 2014.
 Mwanamuziki nyota wa miondoko ya Bongo Fleva Diamond Platnumz akiwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere leo asubuhi (30.7.2014) kutokea Marekani ambako alishinda zawadi ya Mwanamuziki bora wa kiume wa Afrika Mashariki 2014.Pichani akilakiwa na Mama yake Mzazi na baadhi ya washabiki na wapenzi wa muziki huo.
 Diamond Platnumz akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere leo asubuhi (30.7.2014) kutokea Marekani ambako alishinda zawadi ya Mwanamuziki bora wa kiume wa Afrika Mashariki 2014. 

MATUKIO KATIKA PICHA MASHINDANO YA DANCE MIA MIA DON BOSCO OYSTERBAY WIKI ILIYOPITA



 Vijana wakionyesha umahiri wao wa kuchezea Baiskeli wakati wa mashindano ya Dance Mia mia, yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Don Bosco Oysterbay wiki iliyopita.
 Kundi kutoka TMK, likishamblia jukwaa.
 Kundi kutoka Kigamboni, likishambulia jukwaa.
 Kundi lililoonyesha kukonga vilivyo nyoyo za mashabiki waliokuwapo uwanjani hapo.
 Si Kung Fu bali ni Dance Mia mia......
 Michezo ya Baiskeli....

Tuesday, July 29, 2014

MPAMBANO WA NGUMI ULIVYOFANYIKA MBEZI SIKU YA IDDI



Bondia Nenge Juma kushoto akipambana na Said Mohamed wakati wa mpambano wao uliofanyika siku ya sikukuu ya iddi mosi mbezi mwisho juma alishinda kwa TKO ya raundi ya tatu picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Lugano Mwaikambo akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Michael Chinyama wakati wa mpambano wao uliofanyika siku ya sikukuu ya idi mosi mbezi mwisho jijini Dar es salaam Chinyama alishinda kwa point picha  na www.superdboxingcoach.blogspot.com

SIMANZI ZAENDELEA KUTAWALA NDANI YA NYUMBA YA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT)



Jaji Vyonne Cherry au Monalisa akitoa maoni kwa washiriki waliokuwa wameshiriki kwenye filamu fupi iliyochezwa na washiriki wa TMT
  Kundi la Kwanza la Washiriki wa TMT waliocheza filamu fupi iitwayo LUGHA GONGANA wakiwa mbele ya meza ya Pilato katika ukumbi wa makumbusho ya Taifa mwanzoni mwa wiki.
 Mshiriki wa TMT, Mwanaafa Mwinzago akifunika uso wake kwa kutoamini kuwa ameponea kwenye tundu la sindano kutokana na kuondolewa katika maumivu ya Jua la Utosi na kuendelea na mashindano hayo
 Mshiriki Wa TMT, Moses Obunde (Mwenye Suti) akimpongeza Mshiriki Mwenzie Mzee Kapalata Mtawa kwa kuweza kuondolewa Kwenye Jua la Utosi na Kupelekwa Kivulini katika Shindano la TMT linaloendelea.
 Washiriki walioingia kwenye Jua la Utosi wakiwa mbele ya Meza ya Pilato huku mshiriki mmoja kutoka kwa washiriki hao aliyaaga mashindano ya TMT.
 Simanzi Zikianzia hapo sasa mara baada ya Washiriki kupunguzwa ili apatikane mmoja wa kuondoka
 Wakabaki wawili na hatimaye mmoja kati ya hao aliweza kuondolewa katika mashindano hayo
Baadhi ya Washiriki wa TMT wakimuaga Mshiriki mwenzao Pendo Edward (Katikati) ambaye aliweza kutolewa kwenye mashindano kutokana na kura kuwa chache.Picha Zote na Josephat Lukaza
Na Josephat Lukaza - Proin Promotions Limited - Dar Es Salaam.
Hatua ya mchujo katika Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limeingia wiki ya tatu ya mchujo sasa mara baada ya mshiriki mmoja kuaga shindano hilo wiki hii. Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limekuwa shindano bora ambalo kadri siku zinavyozidi kwenda linazidi kuteka nyoyo za watanzania wengi waliopo ndani na nje ya Nchi kutokana na utofauti wake na uzuri wake pia.
Mshiriki mmoja ambaye ni Pendo Edward aliweza  kuchomwa na jua la utosi lililompelekea kutoka kwenye shindano hilo kubwa la Tanzania Movie Talents (TMT) ambapo mpaka sasa washiriki kumi na tano (15) ndio wamebaki katika nyumba ya TMT na hali ya simanzi bado inaendelea katika nyumba ya TMT kwa wiki hii ambapo mshiriki mwingine atatakiwa kutoka.
Shindao la TMT limekuwa likivuta hisia za watanzania wengi waliopo ndani na Nje ya Tanzania kutokana na Utofauti wake na ubora wake na kupelekea watanzania wengi sana kufuatilia shindano hilo kwa ukaribu na umakini zaidi.
Hatimaye wiki hii Tanzania Movie Talents iliamua kuzindua Zoezi la kuwapigia kura washiriki wake kupitia ukurasa wetu wa facebook ambapo sasa watanzania na wapenzi wa TMT ambao wanauwezo wa kupata na kutumia internet sasa wanaweza kuwapigia kura washiriki waliowavutia kupitia ukurasa wetu wa facebook na vilevile kuendelea kuwapigia kura washiriki kwa kutumia simu zao za mkononi.
Jinsi ya Kumpigia kura Mshiriki umpendae kwa Kutumia Simu ya Mkononi Andika Neno "TMT" ikifuatiwa na namba ya ushiriki halafu tuma kwenda 15678. Mfano TMT 00 tuma kwenda 15678
Na Jinsi ya Kumpigia kura mshiriki kupitia ukurasa wetu wa facebook BOFYA HAPA  kwa kupata maelezo.

WAZIRI WA UCHUKUZI DK.HARRISON MWAKYEMBE AFANYA ZIARA YA KIKAZI KATIKA MAKAO MAKUU YA OFISI ZA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA TANZANIA (TCAA)




Waziri wa Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe akisaini kitabu cha wageni wakati alipofanya  ziara ya kikazi katika Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA.Wapili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa bodi hiyo Mbwana Mbwana.Kulia ni makamu Mwenyekiti Weggoro Nyamajeje na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya TCAA ,Charles Chacha. Waziri Dk. Harrison Mwakyemba ndiyo waziri pekee  aliyetembelea ofisi hizo tangua kuanzishwa.
Waziri wa Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe (kulia)akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Ndege wa Mamlaka Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Nuis Kasambala alivyokuwa akimuelezea na kumuonyesha jinsi wanavyofanya mitihani kwa wanafunzi wa ndege  wakati alipofanya  ziara ya kikazi  Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA. Waliosimama nyuma ni Kamati ya bodi ya Mamlaka hiyo wakifuatilia kwa makini.              
Waziri wa Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe (kulia)akisisitiza jambo kwa  Mkurugenzi wa Ndege wa Mamlaka Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Nuis Kasambala alivyokuwa akimuelezea na kumuonyesha jinsi wanavyofanya mitihani kwa wanafunzi wa ndege  wakati alipofanya  ziara ya kikazi  Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wanafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA. Waliosimama nyuma ni Kamati ya bodi ya Mamlaka hiyo wakifuatilia kwa makini
Waziri wa  Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe (kulia) akikabidhiwa  na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Charles Chacha moja ya tuzo waliyotunukiwa Tanzania na Baraza la Usafiri wa Anga Duniani kwa kutambua mchango wa TCAA.anayeshuhudia katikati ni Makamu Mweneyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka hiyo Weggoro Nyamajeje,  wakati alipofanya  ziara ya kikazi  Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Mbwana Mbwana akitoa shukrani kwa niaba ya bodi na wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kwa Waziri wa  Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe, (wapilia kutoka kulia)wakati alipofanya  ziara ya kikazi  Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA. Wengine ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi Weggoro  Nyamajeje na Kaimu Mkurugenzi wa TCAA ,Charles Chacha.
Waziri wa  Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe (katikati) akisisitiza jambo wakati alipokuwa akijibu maswali ya wafanyakazi wa  Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)  wakati alipofanya  ziara ya kikazi  Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Mbwana Mbwana, wengine ni  Makamu Mwenyekiti Weggoro Nyamajeje na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Charles Chacha.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga wakimsikiliza kwa makini Waziri wa  Uchukuzi  Dk. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani)  wakati alipofanya  ziara ya kikazi  Makao Makuu ya Ofisi  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuongea na wafanyakazi na kuzindua bodi ya Wakurugenzi  ya TCAA.

Monday, July 28, 2014

MWANAMUZIKI ALI KIBA ATEMBELEA CHUMBA CHA HABARI CHA GAZETI LA JAMBO LEO DAR ES SALAAM LEO



 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni  ya Jambo Concepts (T), Limited, Juma Pinto (kushoto), akipokea CD yenye nyimbo mbili za Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba wakati alipotembelea ofisi za gazeti hili Dar es Salaam leo kutambulisha nyimbo hizo pamoja na kuelezea mikakati yake ya baadaye kimuziki.
 Ali Kiba alimkabidhi CD Mkurugenzi wa Kampuni ya Jambo Concepts (T), Limited, Benny Kisaka.
  Ali Kiba alimkabidhi CD, Mmiliki wa Blog ya Wananchi, William Malecela.
 Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Jambo Leo, Nyendo Mohamed (kulia), akimtambulisha Ali Kiba kwa waandishi wwenzake.
 Mpiga picha Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Richard Mwaikenda (kulia), akimueleza jambo Ali Kiba.
 Ali Kiba akisalimiana na Mhariri wa Makala wa Gazeti la Jambo Leo, Robert Hokororo.
 Ali Kiba akisalimiana na Mwandishi Mwandamizi wa Gazeti la Jambo Leo, Neema Mgonja.
 Ali Kiba akisalimiana na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jambo Leo, Anicetus Mwesa.
Ali Kiba akisalimiana na Msanifu kurasa Msaidizi wa Gazeti la Jambo Leo, Hamza Mussa.Imeandaliwa na www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062.

NAIPONGEZA SERIKALI KUSITISHA AJIRA UHAMIAJI


Mgombea Uraisi Tucta Dismas Lyassa akijadiliana jambo na wakili wake Jebra Kambole. Picha na Mpigapicha Wetu.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE



Ndugu zangu Watanzania


Asubuhi ya leo tarehe 28 Julai 2014 nilitoa taarifa maalumu kwa vyombo vya habari nikiitaka Serikali kutolea ufafanuzi malalamiko yaliyojaa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya habari. Asante Mungu kwamba Serikali imetolea majibu jambo hili kwa kusitiza ajira zote.

 Rejea taarifa yangu kwa vyombo vya habari niliyoitaka Serikali kutoa majibu katika suala hili asubuhi ya leo tarehe 28 Julai na nakala yake kutumwa katika ofisi mbalimbali za Serikali.


Nachukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa kuwa sikivu katika hili na huenda katika mengi yajayo, kama Rais Mtarajiwa wa Tucta baada ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Agosti 4-5 Dodoma, naahidi kushirikiana na Serikali hasa kama itakuwa sikivu.

Nahitaji kupatiwa majibu pia juu ya hatima ya mabaamedi wanaolazwa chumba kimoja zaidi ya kumi tena siyo katika vitanda, bali zaidi huwa wanalala chini; wanafanyakazi hadi usiku, wengine wanakoishi ni mbali na baa, hoteli nk.

Nahitaji kuona kero za walimu, wafanyakazi wa Serikali za Mitaa, madini, simu, kilimo, utafiti afya, mawasiliano, reli, bandari nk zinakomeshwa; Ni aibu hadi leo kuna walimu wanapoanza kazi  wanalala kwa walimu wakuu wakisubiri kupatiwa sehemu za kuishi, ni aibu hadi leo mwalimu anafanyakazi kazi miezi sita inapita hakuna mshahara anaolipwa…hatuwezi kwenda hivi, ni lazima majibu yapatikane.

Wafanyakazi wa Tanzania  tunapaswa kuimba nyimbo zingine, siyo za kero zile zile kila kukicha. Naamini yote yanawezekana, cha msingi ni kwa Serikali na waajiri kusimamia kwa haki mambo yote juu ya wafanyakazi. Hakuna lisilowezekana tukipigania haki.

Imetolewa leo Julai 28, 2014

                                   Na Dismas Lyassa                                  


(Mgombea Uraisi TUCTA) 
0754 49 8972/0712183282

VIONGOZI WA CHUO NA HOSPITALI YA IMTU WATINGA MAHAKAMANI, DPP AWAONDOLEA MASHTAKA


 Washtakiwa wakiwa katika gari la polisi 
 Wakipanda gari baada ya kusomewa mashitaka
 Wakitoka mahakamani baada ya kusomewa mashitaka
 
Washtakiwa wakisubiri kuingia mahakamani. Picha na Sultani Kipingo wa Globu ya Jamii

Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), aliwapandisha kizimbani vigogo wanne wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba (IMTU) na baadaye kuwaondolea mashitaka kupitia hati ya Nole ya kuwaondolea mashtaka ya kushindwa kufukia viungo vya binadamu na kupeleka hati ya kufukia viungo vilivyotumika kufundishia kwa Kampuni Coroner. 

 Vigogo hao ni, Venkat Subbaian (57), Appm Shankar (64), Prabhakar Rao (59) na Dinesh Kumar (27) ambao walisomewa mashtaka yao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo  saa 8:07  mchana.  Washtakiwa hao walisimama kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kwey Lusemwa. 

Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Magoma Magina alidai kuwa Julai 20, mwaka huu washtakiwa wakiwa na nyadhifa  tofauti, Profesa, Mtawala na wahadhiri, kwa makusudi walishindwa kufukia mifuko 83 iliyokuwa na viungo vya binadamu kinyume cha sheria ya 128 kifungu cha 8 na cha 9 cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA). 

 Magina alidai kuwa katika shitaka la pili, washtakiwa wote kwa pamoja walishindwa kupeleka hati ya kumtarifu kwamba wamefukia viungo hivyo baada ya kutumika kufundishia kama sheria inavyowataka.
Hakimu Lusemwa alisema washtakiwa watakuwa nje kwa dhamana kwa kuwa na wadhamini wawili raia wa Tanzania kila mmoja. 


Hata hivyo, kabla mahakama haijasikiliza kipengele cha dhamana, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Salum Ahmed aliwasilisha hati ya Nole kutoka kwa DPP akidai kuwa anawaondolea vigogo hao mashtaka na kwamba hana nia ya kuendelea kuwashitaki. 

 Ahmed alidai kuwa DPP anawaondolea washtakiwa mashitaka hayo chini ya kifungu cha 91 kidogo cha (1) cha CPA kwa kuwa hana nia ya kuendelea kuwashitaka. 

 Wakili wa washtakiwa Gaudiosus Ishengoma alisema kwamba inaonekana kuna mbinu kubwa dhidi ya washtakiwa.

Alisema anavyofahamu kwamba hati ya mashitaka ingekuwa na kasoro wateja wake wangepata dhamana na baadaye ingewezekana kubadilishwa. 
Alisema kutokana na sababu hiyo, ana wasiwasi kwamba inawezekana DPP ana nia ya kuwafungulia wateja wangu kesi yenye mashitaka yasiyokuwa na dhamana ili wakasote mahabusu. 

 Viwanja vya mahakama hiyo vilikuwa tulivu huku wanaodaiwa kuwa wafanyakazi wa IMTU wakiwa wamesimama katika makundi makundi wakijadiliana hili na lile. 

Kupitia magari ya Jeshi la Polisi, T 366 AVG aina ya Rav4 alipanda mshtakiwa wa tatu kwa madai kuwa ni mgonjwa na washtakiwa wengine waliondoka mahakamani hapo katika gari yenye namba za usajili KX06EFY aina ya Toyota Landcruiser na kurudishwa mahabusu ya jeshi hilo.

KATIBA MPYA YAWATOA JASHO AKINA WASSIRA, PROF LIPUMBA NA LISSU, WATUPIANA LAWAMA LIVE KATIKA MDAHALO JIJINI DAR ES SALAAM.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Stephen Wassira akizungumza kwenye mdahalo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema) Tundu Lissu na katikati ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba. Picha na Rafael Lubava.

Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Stephen Wassira akiwakilisha CCM, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, jana walitoana jasho katika mdahalo wa Katiba ulioandaliwa na East African Business and Media Institute.


Mdahalo huo uliohudhuriwa na watazamaji wapatao 500, ulikuwa na mada inayosema: ‘Nani anakwamisha Upatikanaji wa Katiba Mpya.’ Kila upande ulitumia fursa hiyo kutupa shutuma kwa mwingine huku jazba na kelele vikitawala miongoni mwa waliohudhuria.


Hata hivyo, suala la muundano wa serikali ndiyo uliochukua nafasi kubwa katika mdahalo huo huku Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ukiishutumu Serikali ya CCM kuwa ndiyo kikwazo cha upatikanaji wa Katiba Mpya nayo ikitupa mpira huo kwa Ukawa kwa kitendo chake cha kutoka katika Bunge Maalumu la Katiba.


Profesa Lipumba alisema wahafidhina wa CCM ndiyo waliomshauri Rais Jakaya Kikwete abadilike kimsimamo kuhusu upatikanaji wa Katiba Mpya.


“Rais Kikwete alikuwa na nia njema kabisa kuhusu Katiba Mpya lakini wahafidhina wa CCM wanaopenda madaraka walipoona muundo wa serikali tatu wakambana naye akabadilisha msimamo, tunamwomba abadilike, nchi hii ni yetu sote ili tupate katiba ya wananchi,” alisema.


Lissu aliongeza kwa kusema kuwa anayekwamisha upatikanaji wa Katiba Mpya ni CCM ambao wanaweka maoni yao badala ya kujadili rasimu iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo ndiyo maoni ya wananchi.


“Hatuwezi kurudi kwenye Bunge Maalumu la Katiba kwenda kujadili rasimu ya CCM kwa sababu wanaonyesha hawana nia ya Katiba Mpya, bali wanataka kuwadanganya Watanzania, watawadanganya wananchi kwa kuleta Katiba ileile ila ikiwa na rangi tofauti,” alisema huku akishangiliwa.


Alisema Ukawa hawawezi kushiriki katika udanganyifu wa aina hiyo na kwamba wameamua kuwaachia CCM ili wananchi waweze kuwahukumu kwa uovu watakaoufanya.


Alisema kati ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba katika Kundi la 201, wajumbe 166 ni wana CCM walioteuliwa ili kuongeza idadi ya watu.


“Humo kuna viongozi wa dini mashehe na maaskofu na waganga wa kienyeji ambao ni wana CCM ili wapitishe Katiba yenye masilahi yao binafsi,” alisema.


Hata hivyo, Wassira alisema hoja za Ukawa hazina mashiko na kumtaka Lissu kuwaomba radhi masheikh na maaskofu kwa kuwa hawakuteuliwa na Rais kutokana na kuwa wanachama wa CCM, bali ni mapendekezo ya taasisi wanazozitumikia.


“Namwomba Tundu Lissu akawaombe radhi masheikh na maaskofu kwa sababu kundi hili liliteuliwa kutokana na mapendekezo ya wahusika wenyewe pasipo shinikizo la Rais. Hapakuwa na uwezekano wa Rais kuwatambua wana CCM ili awateue wanaofaa. Kama ana ugomvi na Kingunge Ngombale Mwilu aseme.”


Alisema wanaokwamisha upatikanaji wa Katiba Mpya ni Ukawa... “Katiba Mpya haiwezi kupatikana mitaani, bali kwa majadiliano na maridhiano kwenye Bunge Maalumu la Katiba, nawashauri warudi bungeni ili tuweze kupata Katiba Mpya.”


Alisema Bunge Maalumu la Katiba lina mamlaka ya kubadilisha vifungu kwenye rasimu ya Katiba na kwamba halipo kwa ajili ya kupitisha tu vifungu vilivyowekwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.


Kauli hiyo ya Wassira ilifanya kila aliposimama kuzomewa na wananchi waliohudhuria mdahalo huo huku wafuasi wa Chadema na CCM wakitishiana kupigana hali iliyosababisha mabaunsa kuwatoa nje ya ukumbi baadhi yao walioshindwa kustahimiliana.


Wajumbe wawili waliokuwa katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole na Awadh Said, katika michango yao walitaka kuheshimiwa kwa maoni ya wananchi ili kupata katiba itakayowafaa kwa muda uliokusudiwa.


Polepole alisema tatizo la wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ni masilahi binafsi na ya makundi katika utafutaji wa Katiba Mpya.


“Wananchi wasimamie masilahi ya taifa na wasiwaachie mchakato mzima wanasiasa ambao wana masilahi binafsi pamoja na yale ya kikundi yenye shinikizo la masilahi binafsi,” alisema Polepole.


Awadh alisema maoni yalikusanywa kutoka katika mabaraza ya katiba 170 na 600 ya taasisi na vyama vya siasa kutoka katika wilaya zote 43 za Zanzibar.


“Kwa nini juhudi zote hii zibadilishwe na wajumbe 629 peke yao kwenye Bunge Maalumu la Katiba? Tufuate maoni ya wananchi kupitia tume ndipo tutakuwa tunawatendea haki Watanzania,” alisema.


Alielezea kusikitishwa na kitendo cha Serikali kufunga tovuti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba akisema kimewanyima wananchi haki ya kupata taarifa mbalimbali za tume hiyo.MWANANCHI

MWANAMUZIKI ALI KIBA ATEMBELEA CHUMBA CHA HABARI CHA GAZETI LA JAMBO LEO DAR ES SALAAM LEO


 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni  ya Jambo Concepts (T), Limited, Juma Pinto (kushoto), akipokea CD yenye nyimbo mbili za Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba wakati alipotembelea ofisi za gazeti hili Dar es Salaam leo kutambulisha nyimbo hizo pamoja na kuelezea mikakati yake ya baadaye kimuziki.
 Ali Kiba alimkabidhi CD Mkurugenzi wa Kampuni ya Jambo Concepts (T), Limited, Benny Kisaka.
  Ali Kiba alimkabidhi CD, Mmiliki wa Blog ya Wananchi, William Malecela.
 Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Jambo Leo, Nyendo Mohamed (kulia), akimtambulisha Ali Kiba kwa waandishi wwenzake.
 Mpiga picha Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Richard Mwaikenda (kulia), akimueleza jambo Ali Kiba.
 Ali Kiba akisalimiana na Mhariri wa Makala wa Gazeti la Jambo Leo, Robert Hokororo.
 Ali Kiba akisalimiana na Mwandishi Mwandamizi wa Gazeti la Jambo Leo, Neema Mgonja.
 Ali Kiba akisalimiana na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jambo Leo, Anicetus Mwesa.
Ali Kiba akisalimiana na Msanifu kurasa Msaidizi wa Gazeti la Jambo Leo, Hamza Mussa.Imeandaliwa na www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062.