Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, August 29, 2014

BONDIA THOMAS MASHALI KUMKABILA HENRY WANDERA WA KENYA OKTOBA 4 TANDALE




 Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya oktoba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam wanaoshudia kushoto ni Raisi wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ostadhi' na promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
 Rais wa TPBO Yassin Abdala akiandika mkataba wa bondia Thomas Mashali katikati atakaepambana na mkenya Henry Wandera oktoba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam kulia ni  promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya oktoba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam wanaoshudia kushoto ni Raisi wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ostadhi' na promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Na Mwandishi Wetu

BONDIA Thomas Mashali 'Simba asiyefugika' anatarajia kupanda uringoni tena  oktoba 4 mwaka huu kumvaa mkenya Henry Wandera mpambano utakaofanyika katika ukumbi wa New Madiba zamani Korini

Mashali anapigana uku akiwa na historia ya kupoteza mpambano wake wa mwisho zidi ya bondia Mada Maugo ambapo walicheza katika uwanja wa taifa na kupoteza kwa point mpambano huo

akizungumzia mpambano huo Mashali amesema atokubali kupoteza tena mchezo huuo ukizingatia anachezea nyumbani kwao alopozaliwa na ndipo alipoanzia ngumi maeneo ya Tandale hivyo sito kubali niaibike mbele ya ndugu zangu hivyo nawambia wapenzi waje kwa wingi kuangalia mashali anavyofanya kazi yake ya mchezo wa masumbwi

nae promota wa mpambano huo Khamis Ally amewahakikishia kuwa sehemu ya parkingi ni kubwa na ulinzi ni wa kutosha kifupi katika ulinzi tumejipanga vizuri pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine mazuri ya utangulizi ambapo mabondia wengi wamejitokeza kucheza siku hiyo

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa 
DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

MABONDIA CHEKA NA SHAURI KUZIPIGA AUGOST 30 JAMUHURI MOROGORO


Mabondia Ramadhani Shauri na Cosmas Cheka wakitunishiana misuli
  Na Mwandishi Wetu

Mabondia Ramadhani Shauri na Cosmas Cheka watazipiga tena mwishoni mwa mwezi huu Augost 30 katika uwanja wa Jamuhuri Morogoro akizungumzia mpambano huo bondia Shauri amesema kuwa yupo fiti ingawa katika mechi yake ya mwisho aliyocheza nje ya nchi alipa cuting katika jicho la kulia ata hivya ata hakikisha anafanya vizuri katika mpambano huo

utakaofanyika Morogoro nae mratibu wa mpambano huo Kaike Siraju amesema maandalizi yote ya mpambano huo yameshakamilika kinachosubiliwa ni siku tu ya mpambano huo tu aliongeza kuwa katika mpambano huo kutakuwa na mapambano ya utangulizi yatakayowakutanisha mabondia 

Twaha Kiduku atakaezipiga na Deo Njiku wakati Juma fundi atazipiga na Epson John na mapambano merngine ya utangulizi

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa 
DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

Thursday, August 28, 2014

Isere Sports yapokea mali mpya ya vifaa vya michezo


 Ofisa mauzo wa Isere Sports, Rasul Nkusa akionesha aina ya mpira na raba mpya zilizowasili nchini
Hizi ni baadhi ya truck Suits zilizowasili Isere Sports

Meneja Masoko wa Isere Sports, Abas Isere akionesha skafu na kofia za bendera ya taifa zilizowasili nchini
Hizi ni baadhi ya jezi zilizowasili kwa ajili ya kuusambaza kwa wadau wa michezo Tanzania na nje ya nchi kulia ni Ofisa Masoko Msaidizi, Ismail Bura.

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Isere Sports inayoagiza na kuuza vifaa vya michezo nchini imepokea shehena kubwa ya mali mpya ya vifaa vya michezo kutoka Dubai na China.

Mkurugenzi wa Michezo wa Isere Sports, Abas Isere alisema jana kuwa vifaa hivyo vyenye ubora unaokubalika vimewasili na tayari vimeanza kusambazwa kwenye ofisi zao zilizopo mtaa wa Mchikichi na Living Stone, Karikaoo na jingine la Dodoma.

Alisema vifaa vilivyowasili ni truck suits za rangi mbalimbali, jezi za mpira wa miguu, netiboli, wavu, basketi ambavyo vyote vinauzwa kwa bei nafuu na kutoa wito kwa maofisa kutoka taasisi mbalimbali za Serikali kutoa oda zao mapema.

Vifaa vingine vilivyowasili ni matufe, mikuki, visahani, vikombe, mipira ya michezo yote, raba za michezo, viatu vya mpira na vingine vingi ambavyo vinafaa kutumika kwenye mashindano mbalimbali nchini.

Monday, August 25, 2014

Mshindi kati ya Muddy matumla vs Nassibu Ramadhani atapambana na Francis miyeyusho kuwania ubingwa wa dunia WPBF

Bondia Mohamed Matumla kushoto akipambana na Nassibu Ramadhani   mpambano wao wa kwanza alishinda Matumla

MSHINDI wa mpambano wa September 27 kati ya Mohamed Matumla na Nassibu Ramadhani atamvaa bondia Mshindi kati ya Muddy matumla vs Nassibu Ramadhani atapambana na Francis miyeyusho kuwania ubingwa wa dunia WPBF

mpambano utakaofanyika nchini kwa ajili ya kugombania ubingwa uho baada ya mpambano wa Matumla na Nasibu kupatikana mshindi

BENDI YA MAPACHA WATATU WATOA BURUDANI NA KUPAGAWISHA WAKAZI WA ILALA


Wasanii wa bendi ya Mapacha watatu wakitoa burudani katika viwanja vya Garden Ilala bungoni Dar es salaam jana picha na www.burudan.blogspot.com
Wasanii wa bendi ya Mapacha Watatu wakitoa burudani kushoto ni Josephe Bivence na Jose Mara akikunguta Drams wakati wa onesho lao
Mwimbaji wa bendi ya Mapacha watatu Khalidi Chokolaa akiimba sambamba na mmoja ya mashabiki waliojitokeza katika onesho lao lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika viwanja vya Garden Ilala Picha na www.burudan.blogspot.com
Mwimbaji wa bendi ya Mapacha watatu Khalidi Chokolaa akiimba sambamba na mmoja ya mashabiki waliojitokeza katika onesho lao lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika viwanja vya Garden Ilala Picha na www.burudan.blogspot.com

KAMPUNI YA MSAMA PROMOTION NA JESHI LA POLISI WAKATAMA KAZI FEKI ZA WASANII



1
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari kwenye kituo cha polisi cha Urafiki wakati akitangaza kukatatwa kwa watuhumiwa 17 wanaorudufu kazi za wasanii kinyume na utaratibu yaani kazi feki katika jiji la Dar es salaam na baadhi ya mikoa ambapo kazi feki za wasanii zilizokamatwa thamani yake ni shilingi milioni 12, Kulia ni ASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho ambaye amesema amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa 17 ambao wanasubiri kupelekwa mahakamani.(PICHA NKIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
2
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na KAMASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho wakionyesha CD feki zilizokamatwa jijini Dar es salaam
3
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akionyesha mashine ya Photocopy inayotumiwa kurudufu CD hizo.
4
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na ASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho wakionyesha CD feki zilizokamatwa jijini Dar es salaam
5
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua zaidi kuhusu wizi huo wa kazi a wasanii unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara na kuwanyonya wasanii.
6
Kituo cha polisi cha Urafiki

DIAMOND ATANGAZA KUOA RASMI



Wema akiwa na Diamond
KUPITIA Gazeti la Mwanaspoti ambalo kwa mujibu wa takwimu za mauzo nchini ni wazi kwamba halina mpinzani, msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz ametangaza ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Wema Sepetu anayosema itafungwa hivi karibuni.Msanii huyo ghali zaidi nchini kwa sasa, ametamka hayo alipozungumza na Mwanaspoti nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam juzi Jumatano. Alisema kuna mambo mengi yaliyomchelewesha kufikia hatua hiyo, ikiwamo maandalizi kwani amepanga mashabiki wake wahudhurie harusi hiyo.
“Ndoa ni kitu cha heri na baraka, lakini kitu kinachofanya kidogo mambo yachelewe ni kwamba sisi au mimi ni mtu ninayefahamika, kwa hiyo hata ndoa yangu watu wengi wanatamani waihudhurie,” alisema Diamond.Pia amesisitiza kwamba ndoa si jambo la masihara kwani ni tendo la kiimani na ndio maana amekuwa makini katika mipango yake.
“Nataka kila kitu kishuhudiwe na mashabiki, ninaweza hata kuifanyia Uwanja wa Taifa,” aliongeza.“Unajua nilishindwa kufanya mambo haya haraka kwa sababu wengi nadhani wangeamini kwamba ninafanya hivyo ili kutafuta umaarufu zaidi, tunataka tufanye kiusahihi yasije tokea mambo kama ya Instagram tunataka tuje kuwa mfano wa kuigwa.”
Alipoulizwa tarehe ya ndoa hiyo Diamond alisema: “Nilishasema ni hivi karibuni, unajua siku zote vitu vya kheri waswahili wanasema lazima uvifiche, hata Mwenyezi Mungu naye anasema anampenda mtu aliye na siri, lazima vitu vingine uvifiche ili vipate kufanikiwa. Wakati mwingine kunakuwa na husda, hasidi kwa hiyo ukiviweka wazi sana vinaweza kutofanikiwa.”
Taarifa kwamba Diamond hataoa zilisambaa na kudaiwa kumchefua mchumba wake Wema Sepetu ambapo katika mahojiano mkali huyo wa wimbo ‘Mdogo Mdogo’ alisema: “Kwanza sikuwahi kusema siwezi kuoa, nilishtushwa na gazeti hilo, nilisikitika kwa kweli na iliniuma sana, lakini nikaona nikijibu nitaonekana kwamba sina adabu, kwa sababu siku zote anayeanza huwa haonekani lakini anayemaliza. Pia siwezi kubishana na vyombo vya habari, mwisho wa siku ni watu haohao nitawategemea wanifanyie kazi zangu,” alisema.
Hata hivyo Diamond alisema mchumba wake anaumizwa na vichwa vya habari ambavyo vimekuwa mwiba kwake.
“Hata hivyo magazeti yetu tumeshayazoea jinsi yanavyoandika, wakati mwingine inakuwa kama chachandu au kufurahisha baraza,” aliongeza.
Kuhusu taarifa kwamba ameachana na mchumba wake huyo, alisema: “Hatuna tatizo watu wengi wanasema tumeachana, lakini hatujaachana na hatuwezi kujibishana.
“Sijui nikujibu nini kwa sababu kila nitakachokujibu utaona namsifia kwa sababu yule ni mchumba wangu.

RAIS KIKWETE ATUNUKU KAMISHENI KWA MAOFISA WAPYA WA JESHI



Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi na kumpongeza luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe baada ya kuibuka mwanafunzi bora wakati wa hafla ya kuwatunuku kamisheni maafisa wapya 179 wa jeshi la Wananchi waliohitimu vyema mafunzo yao katika chuo cha Jeshi Monduli Mkoani Arusha jana.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitunuku kamisheni kwa maafisa wapya 179 wa jeshi waliohitimu vyema mafunzo yao ya muda mrefu katika chuo cha jeshi Monduli Mkoani Arusha jana.
Maofisa wapya wa Jeshi wakila kiapo mbele ya Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kuwatunuku kamisheni iliyofanyika katika chuo cha jeshi kilichopo Monduli Mkoani Arusha jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wapya wa jeshi baada ya kuwatunuku kamisheni katika sherehe zilizofanyika katika chuo cha jeshi Monduli mkoani Arusha jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe aliyeibuka mwanafunzi bora(Best Oficer Cadet Traineer Overall) wakati wa mafunzo ya muda mrefu ambapo maafisa 179 wa jeshi walihitimu vyema na kutunukiwa kamisheni katika chuocha jeshi Monduli jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mwanafunzi Bora katika kozi ya muda mrefu ya jeshi Luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe(watatu kushoto) pamoja na wazazi wake muda mfupi baada ya Rais Kuwatunuku kamisheni maofisa 179 wa jeshi katika chuo cha Monduli Mkoani Arusha jana.
Mtoto mdogo akimsalimia Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kumalizika kwa sherehe za kuwatunuku kamisheni Maofisa 179 wa jeshi katika chuo cha jeshi Monduli Mkoani Arusha jana. (picha na Freddy Maro)

INDIA BUSINESS FORUM 'IBF' KUJITANUA ZAIDI


Balozi wa India nchini Debnath Shaw akizungumza na wafanyabiashara mbalimbali kutoka India
Balozi wa India nchini Debnath Shaw kushoto akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara waliojitokeza wakati wa sherehe ya wafanyabiashara wa India wanaoishi nchini wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya toyota ,Vinod Rustagi,Mkurugenzi wa Kamal Steels, Satyama Gupta na Mwenyekiti wa Kamal steel, Gagan Gupta picha na mpigapicha wetu


baadhi ya viongozi wa umoja wa wafanya biashara wa India wanaoishi nchini wakitambulishwa mbele ya balozi
Baadhi ya wafanyabiashara wa India wakichukua chakula wakata wa sherehe ya wafanyabiashara wa India
WAFANYABIASHARA WA INDIA WANAOISHI NCHINI WAKIJADILI MAMBO MBALIMBALI

Friday, August 22, 2014

MASAI SAFARI BENDI KUZINDUA ALBUM AUGUST 30


Na Mwandishi Wetu
 BENDI ya masai safari ya jijini Dar es salaam inatarajia kuzindua albam yake ya kwanza kabisa

watakayozindua siku ya

August

30 katika ukumbi wa raunch time ya jijini akizungumzia uzinduzi wa albam hiyo rais wa bendi hiyo Fransic Mwaisela amesema kwamba siku hiyo watasindikizwa na bendi mbalimbali wakiongozwa na bendi ya Extra bongo inayo ongozwa na Ali Choki

alizitaja nyimbo zilizomo katika albam hiyo ni sita itakayozinduliwa siku hiyo ikiwa nyimbo ambayo iliyobeba albam ni akuna kama baba ya pili ni njia panda,mikono ni kazi,ndoa ni mpango wa mungu,usiwasikilize wambeya,kilio changu nyimbo hizo ndio zitakazokuwa katika albam hiyo itakayo zinduliwa mwishoni mwa mwezi huu


aliongeza kwa kutaja wasanii wengine watakaokuwepo siku hiyo ni Omari Tego,Maua Tego pamoja na wasanii mbalimbali wa bondo flefa watakaosindikiza uzinduzi uho

bendi hiyo kwa sasa ipo kwenye mazoezi ya nguvu kwa ajili ya kutoa burudani kabambe siku ya uzinduzi wa albam ya bendi hiyo

Luis Figo,Christian Karembeu na Fernando Sanz Duran waahidi kutoa burudani safi kwa watanzania



Mratibu wa Ziara ya Wachezaji wa Zamani wa Timu ya Real Madrid,Ssebo (wa tatu kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mechi ya kirafiki kati ya Tanzania Eleven na Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kesho.Mpaka sasa ni wachezaji watatu tu ndio waliowasili nchini huku wengine kadhaa wakitegemewa kuwasili mchana wa leo.Wachezahi hao ambao wapo nchini hivi sasa ni Luis Figo (wa tatu kulia),Christian Karembeu (kulia) na Beki Fernando Sanz Duran (wa pili kushoto).wengine pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya TSN,Farough Baghoza na Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven,Jamhuri Kihwelo "Julio"
Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven,Jamhuri Kihwelo "Julio" (katikati) akizungumzia namna Timu yake ilivyojiandaa kuwakabili Wakali hao wa soka Duniani wakati wa Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo kwenye Hoteli ya SouthernSun jijini Dar es Salaam.Kulia ni Luis Figo na kushoto ni Fernando Sanz Duran ambao ni wachezaji wa zamani wa timu ya Real Madrid ya nchini Hispania.
Mchezaji Kiongozi wa Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid,Luis Figo akizungumza na Waandishi wa habari juu ya ujio wao hapa nchini.Figo amewaahidi wa Tanzania kuwa yeye na Wenzake watatoa burudani kabambe katika Uwanja wa Taifa jijini Dar hapo kesho.
Mchezaji Fernando Sanz Duran (kati) nae akitoa maneno yake kuhusu mchezo huo.
Mwanasoka Christian Karembeu akizun

CHRISTIAN BELLA KUTOA BURUDANI YA KUFA MTU KATIKA FAINALI YA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) TAREHE 30 AUGUST 2014 PALE MLIMANI CITY



Christian Bella 
Na Josephat Lukaza 
Msanii wa Muziki wa Dansi anayejulikana kama Christian Bella anayetamba na kibao chake cha Nani Kama Mama ni Mmoja wa Wasanii watakaotoa Burudani ya Kufa mtu katika Ukumbi wa Mlimani City Siku ya Jumamosi Tarehe 30 katika Fainali kubwa ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT).

Bella Amehaidi kutoa Burudani ya uhakika ambapo wapenzi wa muziki wake watafurahi na kufurahishwa na show atakayoitoa siku hiyo katika Fainali ya Kumkabidhi Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania.

Katika Fainali hiyo inayotarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Siku ya Jumamosi tarehe 30 huku viingilio vya Kuja kutazama fainali ya Kwanza kubwa vikiwa ni V.I.P Shilingi 50,000 na Kawaida 30,000 huku fainali hiyo ikirushwa live kupitia Kituo cha Runinga cha ITV na milango itakuwa wazi kuanzia Saa 7.30 Usiku.

Tanzania Movie Talents (TMT) ni shindano la Kwanza kufanyika Afrika Mashariki na Kati ambalo limeanzishwa na Kampuni ya Proin Promotions Ltd likiwa na lengo la Kuibua na Kusaka Vipaji vya kuigiza kwa watanzania ambao wana vipaji lakini walikosa fursa ya kuonekana. TMT ilianza Rasmi tarehe 1 April 2014 katika Mkoa wa Mwanza, Kanda ya Ziwa ambapo baadae shindano likaendelea katika Kanda nyingine Tano huku katika Kila Kanda Washindi walikuwa ni watatu huku kanda ya Pwani washindi walikuwa Ni 5 ambapo jumla ya Washindi 20 walipatikana na kuletwa Dar Es Salaam katika kambi na Hatimaye Mchujo kuanza na Kubakiwa na Washiriki 10 ambao leo hii wameingia Fainali ya kuzisaka zile Milioni 50 za Kitanzania.

Katika Fainali hiyo Kubwa kutakuwa na Burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.Sikiliza Moja ya Nyimbo atakazoimba Live Stejini Siku Hiyo ya Fainali

Mtibwa Sugar, Polisi Moro kupimana ubavu kesho Morogoro



Polisi Moro
Mtibwa Sugar
TIMU za Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro zinazojiandaa kushiriki ligi kuu ya Vodacom (VPL) zinatarajia kucheza kesho Jumamosi mechi ya majaribio ya mfumo wa tiketi za elektroniki.
Mechi hiyo itafanyika katika uwanja wa Jamhuri uliopo mjini Morogoro kuanzia saa 10 kwa kiingilio cha sh 1,000.
kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Afisa habari wa Shirikisho la soka nchini TFF Boniface Wambura alisema tiketi za mechi hiyo zitaanza kuuzwa leo kupitia mtandao wa M-Pesa, CRDB Simbanking na maduka 30 ya Fahari Huduma yaliyopo katika wilaya zote za Mkoa wa Morogoro.
Alisema mashabiki 100 wa kwanza watakaoanza kuingia uwanjani wapata jezi za timu ya Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro.
Aliongeza kusema kusema tayari mechi ya majaribio ya tiketi za elektroniki imeshafanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya ambapo timu za Tanzania Prisons na Mbeya City zilichuana na kutoka sare.
Alisema mechi nyingine za majaribio ya tiketi za elektroniki zinatarajiwa kuchezwa Agosti 30 mwaka huu.
Alisema katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kutakuwa na mechi kati ya Coastal Union na Mgambo Shooting wakati katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ni Kagera Sugar dhidi ya mabingwa wa Mkoa wa Kagera, Eleven Stars.
Wambura alisema Septemba 6 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa kutakuwa na mechi kati ya Simba na Mtibwa Sugar.
Alisema mchezo wa ngao ya Jamii utakaozikutanisha timu ya Azam FC na Yanga afrika umepangwa kufanyika Septemba 13 katika Uwanja wa Taifa,uliopo jijini Dar es Salaam.
Mtibwa inatarajiwa kuanza ligi kwa kuikaribisha Yanga kwenye uwanja wa Jamhuri wakati Polisi Moro itakaribishwa tena katika ligi kwa kuumana na Azam kwenye uwanja wa Chamazi Septemba 20.
Wakati huo huo waamuzi wanaotarajia kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu watafanya mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) mwezi ujao.
Mtihani huo utahusisha waamuzi wa daraja la kwanza (class one) wakiwemo wale wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la soka duniani (FIFA).
Alisema mbali ya mtihani huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Septemba 10 mwaka huu, kutakuwa na semina ya makamishna ambao watasimamia mechi za VPL na FDL.
Alisema waamuzi wote wanatakiwa kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi kwa ajili ya mtihani huo

Mshale wa Kifo wa Aisha Bui kutua sokoni Jumatatu



Kava la filamu mpya ya Aisha Bui iitwayo Mshale wa Kifo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPx0qnYQNZb4Qd9X8gzrfKRlztszioPIUrfGGr4eNqhNqQNqRJpZXCUN7PdGYQGfwsrI4eR5bBJRBqwEhnXYTFYbqxf4KoKYse5Q2dw5ilL8SryDtg-vqaUwx2LVziSpgHNTLmy_dJLd8/s1600/10482228_800152790017429_125002049025336857_n.jpg
Aisha Bui katika pozi
FILAMU mpya ya muigizaji nyota wa filamu nchini, Aisha Fat'hi 'Aisha Bui' iitwayo 'Mshale wa Kifo' inatarajiwa kuingia sokoni siku ya Jumatatu, huku mwanadada huyo akitamba kuwa kazi hiyo ni mwanzo wa uhondo kutoka kampuni yake ya Bad Girl Film's.
Akizungumza na MICHARAZO, Aisha Bui alisema filamu hiyo aliyoigiza na wakali kama Mzee Chilo, Gabo wa Zagamba na wengine itaingia sokoni Agosti 25, huku kampuni yake ya bad Girl ikijipanga kuandaa kazi nyingine kali zaidi na hiyo.
Aisha Bui, alisema japo filamu hiyo ni kazi yake ya kwanza kuiandaa, lakini kwa jinsi ilivyoandaliwa kwa umakini mkubwa ni wazi mashabiki watajua ujio wake mpya siyo wa kubahatisha.
"Naiachia filamu yangu Jumatatu, nawaomba mashabiki waniunge mkono kwa kununua nakala halisi, ili kuiwezesha kampuni ya Bad Girl kuendelea kuwapa uhondo zaidi, kuna makubwa yapo njiani kutoka kwangu," alitamba Aisha Bui.
Nyota huyo aliyecheza filamu mbalimbali ikiwamo ya Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love, Revenge of Love, Mirathi, Pain of Love, Crazy Love na The Second Wife, alisema ndani ya filamu hiyo mpya inasimulia kisa cha mfanyabiashara wa dawa za kulevya ambaye anamlazimisha askari Polisi kumsaidia kupitisha mzigo wake.
Hata hivyo kazi haiwi rahisi na kuibua kashkash kwa binti wa askari huyo Myrine nafasi iliyochezwa na Aisha kufanywa kama chambo.
"Ni simulizi linalosisimua na kutia simanzi na bahati nzuri walioiigiza kuanzia mimi mwenyewe, Gabo, Mzee Chilo na wengine tumeitendea haki," alisema Aisha.

Wednesday, August 20, 2014

MABONDIA MOHAMED MATUMLA NA NASSIBU RAMADHANI KUZIDUNDA TENA SEPTEMBA 27 FRIENDS CORNER MANZESE



Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli 
Na Mwandishi Wetu
 MABONDIA Nassibu Ramadhani pamoja na Mohamed Matumla wameingia makubaliano ya kuzipiga kwa mara ya pili siku ya septemba 27 katika ukumbi wa

friends corner hotel manzese Dar es salaam

akizungumzia mpambano huo mratibu wake Yassin Abdallah 'Ostadhi' amesema mabondia hawo wamekubaliana na kusaini mkataba wa kuzipiga siku hiyo

ambapo mabondia hawo walikutana mara ya kwanza na bondia Mohamed Matumla alimshinda kwa point Nassibu Ramadhani hivyo kuufanya mchezo huu kuwa mgumu zaidi kwa Matumla kuendeleza kipigo au Ramadhani kurudisha kisasi

 katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na mapambano ya utangulizi

 bondia Issa omari atamkabili juma fundi.kg 53 raundi nane. na Sadiq momba vs Tasha mjuaji kg 59 raundi nane. wakati Juma mustafa atamkabili Bakari dunda kg 61 raundi sita. huku kina dada Lulu  Kayage akipambana na fatma yazidu.kg 51 raundi nne.

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa 
DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

Alhaj Ali Hassan Mwinyi asema bado viongozi wanatumia madaraka yao kujinufaisha


Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi (katikati) akifungua semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma. Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi (katikati) akifungua semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi akifungua semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma. 
Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi akifungua semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Salome Suzete Kaganda (kwanza kushoto) akizungumza kwenye semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma. Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Salome Suzete Kaganda (kwanza kushoto) akizungumza kwenye semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.

Baadhi ya washiriki katika semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma. Baadhi ya washiriki katika semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma. Baadhi ya washiriki katika semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.Baadhi ya washiriki katika semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma. Baadhi ya washiriki katika semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.Katibu Msaidizi Kanda ya Mashariki, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Getrude Cyriacus (wa kwanza kushoto) akiwasilisha mada juu ya Rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma kwa wanasemina. Katibu Msaidizi Kanda ya Mashariki, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Getrude Cyriacus (wa kwanza kushoto) akiwasilisha mada juu ya Rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma kwa wanasemina. Baadhi ya washiriki katika semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.


Na Joachim Mushi, Dar

RAIS Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi amesema bado viongozi wa umma wanatumia madaraka yao na Ofisi zao kwa kujinufaisha wenyewe na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani hivyo kuna kila sababu ya kuleta sheria ya kuziba mianya hiyo kwa viongozi wanaokwenda kinyume na maadili.

Alhaj Mwinyi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.

Alisema licha ya kuwepo kwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 inayotumika sasa bado kumekuwa na wimbi kubwa la mienendo ya matumizi mabaya ya ofisi na madaraka kwa viongozi wa umma kwa kujinufaisha wenyewe kimaslahi.

"...Maana yake ni kwamba umma sasa haupewi kipaumbele unavyo stahiki. Maamuzi ya viongozi yanatolewa kwa maslahi binafsi na hivyo kudhihirisha kuwepo kwa tatizo la mgongano wa maslahi. Viongozi hao waliopewa dhamana na wananchi wanatumia rasilimali za umma ili kujinufaisha binafsi au shughuli zao ambazo wanazo pembeni," alisema Rais huyo mstaafu.

Alisema hata hivyo sheria ya maadili ya viongozi wa umma imekuwa na mapungufu kwa kuwabana baadhi ya viongozi wa umma na kuwaacha wengine pamoja na watumishi wa umma hivyo kujikuta nao wakijihusisha na mgongano wa kimaslahi.

Hata hivyo, ameongeza kuwa tayari Serikali imeona mianya hiyo na hivyo kuanza mchakato wa kuja na sheria maalum itakayo dhibiti hali hiyo. "...Nadhani mmewahi kusikia mara kwa mara namna ambavyo Rais wetu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiagiza Serikali kufanya jitihada za dhati ili kuhakikisha kuwa viongozi wa umma wanaacha au wanajiepusha na tabia ya kushiriki zaidi kwenye biashara na kuacha jukumu lao...," alifafanua Mwinyi akiwaeleza washiriki wa semina hiyo.

Aidha aliipongeza Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kuanza mchakato wa kutungwa kwa sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma, ambapo itakapo kamilika huenda ikawa suluhisho la mgongano wa kimaslahi kwa viongozi na watumishi wa umma.

Rais huyo mstaafu aliwataka wanasemina kuijadili rasimu iliyowasilishwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na kutoa maoni yao kuiboresha zaidi ili itoke na majibu ya kero ya muda mrefu ya Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma.

Kwa upande wake, Katibu Msaidizi Kanda ya Mashariki, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Getrude Cyriacus akiwasilisha mada juu ya Rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma kwa wanasemina kabla ya mjadala alisema wataalam wa Sekretarieti hiyo wamefanya utafiti kwenye mataifa mbalimbali na kutoka na mapendekezo ambayo yataongoza mjadala kuelekea kupata sheria nzuri.

Naye Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Salome Suzete Kaganda akizungumza katika semina hiyo, alisema Rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma walioiandaa itajadiliwa na wadau mbalimbali ili kupata maoni kabla ya kuwasilishwa kwenye baraza la makatibu wakuu kuboreshwa zaidi kabla ya mchakato kupanda ngazi za juu.

Aidha aliwataka wananchi na wadau wengine kuendelea kuijadili Rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa Maslahi kwa Viongozi wa umma pindi itakapo wafikia na kutoa maoni kwa lengo la kuiboresha zaidi ili itakapo kamilika iweze kufanya kazi vizuri na kujibu kero zilizopo katika eneo hilo la viongozi wa umma.

“...Mapendekezo ya sheria hii hayalengi kuwafanya viongozi kuwa maskini, bali kasi yao ya ukwasi iendane na hali halisi ya kipato chao. Sheria hii itakapopitishwa itapunguza ubinafsi wa viongozi walioko madarakani kujipendelea wenyewe na maeneo wanayotoka.” Alifafanua Jaji Kaganda.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com