Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, August 3, 2014

HAWA NDIYO WASANII WAKALI ZAIDI BONGO



Kutoka kushoto, Irene Paul, Jacklyne Wolper na Riyama Ally
WAKATI Elizabeth Michael 'Lulu' akitajwa kama msanii wa kike wa filamu anayependwa na watu kupitia tuzo za 'Tanzania People's Choice Award', Jacklyne Wolper na Irene Paul wametajwa ndiyo wakali zaidi kati ya wasanii wa kike nchini.
Lulu alishinda tuzo mwezi uliopita sambamba na King Majuto na watangazaji wengine wa redio na runinga.
Hata hivyo katika utafiti uliofanywa na MICHARAZO kwa mwezi mmoja kwa kuhoji mashabiki wa filamu wasanii Wolper, Irene, Riyama Ally, Irene Uwoya, Shamsa Ford na Bi Hindu ndiyo  'walifunika' miongoni mwa waigizaji wa kike nchini.
Irene Paul, Shamsa na Wolper ndiyo waliotajwa mara nyingi na mashabiki wakifuatiwa na Riyama, Irene Uwoya, Bi Hindu, Mariam Ismail, Cathy, Sandra na Aunty Ezekiel.
Irene Paul ametajwa kama mmoja wa wasanii wa kike wenye kipaji halisi na wanaojua kugeukageuka katika nafasi yoyote na kusifiwa kupitia filamu za Fiona na 'Kibajaj'.
Uwoya yeye alipata kifyagio kupitia 'Ngumi ya Maria' na Apple wakati Wolper alifunika kupitia 'Ulimi' na 'Ndoa Yangu' aliyoigiza na marehemu Steven Kanumba.
Kwa upande wa waigizaji wa kiume waliotajwa kufunika ni  Jacob Stephen 'JB', Mohammed Mwikongi 'Frank', Kulwa Kikumba 'Dude', Nurdin Mohammed 'Chekibudi' na Amri Athuman 'King Majuto'.
Wengine katika 10 Bora ni Salum Mboto, Jimmy Master, Mtunisi, Gabo wa Zagamba na Mzee Jengua.

No comments :

Post a Comment