Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, February 28, 2014

MASHINDANO YA SAFARI LAGER NYAMA CHOMA ILALA WAPATA MAFUNZO



Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kushoto akifafanua jambo wakati wa mafundisho ya uchomaji nyama bora kwa wachoma nyuma wa bar mbalimbali za Ilala

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kushotoakijibu maswali mbalimbali ya kuhusu uchomaji wa nyama kwa njia ya kitabu alichonacho kwa ajili ya uchomaji nyama bora

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akimkabidhi cheti Richard Mushi kwa ajili ya kushiliki semina ya uchomaji mzuri wa nyama

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akimkabidhi cheti Mary Komba kwa ajili ya kushiliki semina ya uchomaji mzuri wa nyama

Baadhi ya washiliki walioshiliki katika semina ya uchomaji nyama wakiwa katika picha ya panmoja

DR.MAGUFULI AKAGUA MRADI WA MABASI YAENDAYO KASI (BRT) JIJINI DAR ES SALAAM: BARABARA YA KIMARA HADI KIVUKONI KUKAMILIKA NDANI YA MIEZI SITA




Waziri wa Ujenzi Dr.John Pombe Magufuli Kituo cha BRT kivukoni jijini Dar es salaam leo akiwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam
 Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (aliyekaa kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe (katikati) pamoja na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale (aliyesimama) wakisafiri kwa basi kukagua utekelezaji wa ujenzi wa barabara za mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkuu wa DART Asteria Mlambo (kulia) akimwongoza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Said Meck Sadiki anayefuatana na Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha kuegesha mabasi ya haraka kinachojengwa eneo la Jangwani, jijini Dar es Salaam.
Msimamizi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka kutoka TANROADS Mhandisi Barakaeli Mmari (aliyeshika kijiti) akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi kuhusu utekelezaji wa mradi wa mabasi yaendayo haraka katika eneo la Kimara jijini Dar es Salaam  

Kampuni ya Strabag International GmbH inayotekeleza ujenzi wa barabara ya Morogoro kuanzia Kimara hadi Kivukoni hapa jijini Dar es Salaam imetakiwa kuhakikisha kuwa inakamilisha ujenzi wa sehemu hiyo ndani ya kipindi cha miezi sita ijayo kama mkataba wao unavyoelekeza. 

 Waziri wa Ujenzi Mhe. Magufuli alitoa agizo hilo wakati akiwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara kwa ajili ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (Dar es Salaam Bus Rapid Transit - BRT) ambao umeelezewa kuwa na changamoto nyingi kiasi cha kusababisha usumbufu kwa watumia barabara hiyo kwa kipindi kirefu. 

 Akimpatia taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Patrick Mfugale alimjulisha Waziri Magufuli kuwa kwa hivi sasa changamoto nyingi zimefanyiwakazi na mradi unaendelea kusimamiwa kwa karibu ili kuhakikisha kuwa hukuna ucheleweshaji zaidi katika hatua hii iliyobaki.  Mkataba wa ujenzi wa barabara hizi pamoja na vituo vya mabasi ulisainiwa mwezi Desemba mwaka 2012 ukiwa umepangwa kukamilika katika kipindi cha miaka mitatu kwa gharama ya Shilingi bilioni 280. 

 Kwa upande mwingine Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Said Meck Saddik ambaye aliambatana na Waziri Magufuli katika ziara hiyo, amewataka wafanyabiashara wanaoendesha shughuli zao ndani ya sehemu ambayo mkandarasi anaendelea na kazi waondoke kwani hiyo mbali ya kuwa kinyime na taratibu za uendeshaji biashara zilizowekwa lakini pia imekuwa ni moja ya kisingizio kinachotolewa kwamba uendeshaji wa shughuli hizo unachangia kuchelewa kukamilika kwa ujenzi huo. 
 Waziri Magufuli akizungumza wakati wa kuhutimisha ziara hiyo, amemtaka mkandarasi kuhakikisha anaukamilisha mradi huo kwa muda na viwango vilivyokusudiwa. 

“Na kwa wale walio ndani ya eneo la ujenzi ni lazima sheria ichukue mkondo wake” alisisitiza Waziri Magufuli huku akimtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Kindondoni Mhandisi Mussa Natty kuhakikisha anasimamia zoezi hilo la kuondoa haraka wale wote wote walioingia katika eneo hilo la barabara kinyume na sheria. 

 Aidha, Waziri Magufuli alielezea kushangazwa kwake kwa kuchelewa kuondolewa kwa nyaya za Tanesco katika maeneo ya City Squire na Morocco kwani fedha za kutekeleza kazi hiyo tayari zimelipwa muda kirefu. 
“Ucheleweshaji wa ainaa hii ndiyo unaotoa mwanya kwa mkandarasi kuanza kutoa visingizio vya kutokamilika kazi hii kwa wakati” ametahadharisha Mhe. Magufuli. 

 Hata hivyo katika hatua nyingine Mhe. Magufuli amemtaka mkandarasi kuharakisha taratibu za kuifungua barabara hiyo upande wa kuingia Dar es Salaam ambako kwa sasa hivi hakuna shughuli kubwa zinazofanyika ili kupungiuza adha ya msongamano wa magari yanayopishana katika njia moja ya upande wa kutokea mjini katika barabara hiyo ya Morogoro hasa kwa eneo kati ya Ubungo na Kiamara. 

 Naye Msimamizi wa mradi huo kutoka TANROADS Mhandisi Barakaeli Mmari ameelezea kuwa, utekelezaji wa mradi huu wa usafiri wa haraka utajengwa katika awamu sita.  Awamu ya kwanza ambayo ujenzi wake ndio huu unaoendelea inahusisha barabara zenye jumla ya kilometa 20.9 ambazo ni Kimara – Kivukoni, Magomeni – Morocco na Faya – Karikaoo. Hadi sasa mkandarasi amekwisha kamilisha asilimia 55 ya mradi

BENKI YA DUNIA 'YABANA' MSAADA KWA UGANDA




Benki ya dunia.
Benki ya dunia imebana msaada wa dola milioni 90 kwa Uganda , siku chache tu baada ya Rais Yoweri Museveni kuidhinisha sheria mpya dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.
Sheria iliyoidhinishwa na Rais Yoweri Museveni, ilitiwa saini Jumatatu na inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.
Wafadhili wengine tayari wameanza kusitisha misaada Uganda. Wahisani kama Denmark na Norway wamesema kuwa wataanza kufadhili mashirika moja kwa moja badala ya serikali.
Aslimia 20% ya bajeti ya Uganda inategemea michango ya wafadhili.

Mpaka sasa nchi tatu za Ulaya zimeamua kukata misaada yao kwa mamilioni ya dola.
Wizara ya fedha ya Uganda imesema inasubiri mawasiliano rasmi ya nchi husika, na iko tayari kukabiliana na athari za hatua hiyo.

Hadi kufikia sasa Waziri wa Fedha Wa Sweden, akiwa mjini Kampala, alisema waekezaji kutoka nchi yake watakuwa na wakati mgumu kuweka pesa zao nchini Uganda kwa sababu watakuwa na hofu kuwa sheria yo yote inaweza kupitishwa kuwadhulumu watu.
Jana serikali ya Uholanzi ilisema itazuia kwa muda misaada kwa Serikali ya Uganda. Norway na Denmark pia zimetangaza kupunguza au kusimamisha kwa muda misaada yake kwa Uganda.
CHANZO NI BBC SWAHILI

Thursday, February 27, 2014

SAFARI NYAMA CHOMA YATOA MAFUNZO KWA BAR ZA TEMEKE

Supervisar Onesmo Swilla akizungumza na wauzaji wa nyama choma wa bar mbalimbali za Temeke Dar es salaam

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akionesha vifaa vya kupimia joto chakula wakati wa mafunzo kwa wachoma nyama wa bar za Temeke

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akipima nyama iliyokuwa tayali kwa ajili ya kuliwa wakati wa mafunzo hayo

Baadhi ya wachoma nyama wa TEmeke

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya nyama choma Carpar Kimario baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo yaliyofanyika kilwa road pub Dar es salaam

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya nyama choma Chavalimembe Lutambi baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo yaliyofanyika kilwa road pub Dar es salaam

Jaji mkuu wa shindano la Safari lager nyama choma Lawrence Salvi kulia akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya nyama choma Jerome Kavishe baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo yaliyofanyika kilwa road pub Dar es salaam
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya nyama choma wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mafunzo yao

Wednesday, February 26, 2014

MSAADA KWA AJILI YA MAMA WANNE WAPOKELEWA MBEYA




Aida Nakawala (25) mkazi wa kijiji cha Chiwanda, Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, ambaye alijifungua watoto wanne kwa mkupuo (Quadruplets) usiku wa kuamkia Mwaka mpya wa 2014 katika Hospitali ya Wazazi ya META jijini Mbeya.

Msaada  toka wingereza toka Bi Gladness Sariah, na msaada toka DSM  kwa Norah SilverBoutique 
Joseph Mwaisango wa Mbeya yetu akiwakilisha msaada toka kwa familia ya mama Masawe wa DSM kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha NURU kilichopo Uyole Mbeya


KITUO cha Mtandao wa kijamii cha Mbeya yetu(www.mbeyayetu.blogspot.com) kimepokea Misaada mbalimbali kutoka kwa wasamaria wema kwa ajili ya Kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Nuru kilichopo Uyole Jijini Mbeya na  Aida Nakawala (25) mkazi wa kijiji cha Chiwanda, Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, ambaye alijifungua watoto wanne kwa mkupuo (Quadruplets) usiku wa kuamkia Mwaka mpya wa 2014 katika Hospitali ya Wazazi ya META jijini Mbeya.
Msaada wa kwanza ulipokelewa hivi karibuni wenye thamani ya shilingi Laki Moja kutoka Familia ya Masawe wa Dar Es Salaam kwa ajili ya kituo cha Nuru ambapo Mbeya yetu iliuwasilisha kama ulivyo.

Mbali na msaada huo pia Mtandao huu ukishirikiana na mtandao wa kijamii wenye makao yake makuu Jijini Dar Es Salaam wa www.michuzi.blogspot.com ulipokea kutoka kwa Msamaria mwema wa Uingereza, Bi Gladness Sariah, ambaye alitoa maboksi mawili yenye nguo na vitu kadhaa vya watoto.
Aidha katika kuonesha wengi wameguswa na tukio la Mwanamke huyo kujifungua watoto wanne  ambao wanaendelea vizuri pia Msamaria  mwema mwingine aliyejulikana kwa jina la  Dada Norah SilverBoutique toka DSM ambaye ametoa Maziwa Lactogen Dazan Mbili yaani makopo 24 pamoja na nguo ambavyo vimewasili salama katika ofisi ya Mbeya Yetu.
 Shukrani kwa Wazee wa Kazi, Serengeti Freight Forwarders ya huko Uingereza na ofisi za Michuzi Media Group (MMG) kuwezesha  kufika kwa mizigo hii Mbeya.
Kutokana na kupokelewa kwa mizigo hiyo ambapo kituo cha Nuru kilikabidhiwa Katoni Mbili za Sukari, Sabuni na Biskuti pia Tunatarajia kuanza  safari ya kwenda huko Chiwanda Wilaya ya Momba Kilomita zaidi ya 260 kwenda na kurudi  kesho majira ya saa Moja asubuhi.
Hivyo ni wito wetu kwenu kuendelea kutuombea na kutuunga mkono katika safari hiyo ili tuweze kuifikisha salama mizigo hiyo ikiwa ni pamoja na kuangalia maendeleo ya Watoto hao ambapo watakuwa wameshatimiza mwezi mmoja na siku 24.
Tunawashukuru sana tena sana mungu awabariki. 


Kama umeguswa na hili na unataka kutoa msaada tafadhali wasiliana na: issamichuzi@gmail.com ama jmwaisango@yahoo.com 

nasi tutafikisha ubani wako. 
Serengeti Freight wametoa ofa ya 
kusafirisha bure misaada ya aina 
Na Mbeya yetu

Monday, February 24, 2014

KUTOKA BUNGENI: WAZIRI MKUU AKIWA NA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJINI DODOMA LEO


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014. Kulia ni mbunge wa Sumve Richard Ndassa.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Singida Magharibi Mohamed Bissanga na Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa ,wote wakiwa ni wabunge wa Bunge Maalum la Katiba, nje ya ukumbi wa Bunge Mjiji Dodoama Februari 24, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo, Pinda akizungumza na Katibu wa Bunge, Thomas Kashilillah, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014. (Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)

NGUMI ZAPIGWA MBAGALA


BONDIA Mussa Shuza kushoto akioneshana umwamba na Dackson Kawiani wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Amenya Pub mbagala rangi tatu Kawiani alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Mabondia Ibrahimu Ahmed kushoto na Mohamed Kashinde wakioneshana ubabe wakati wa mpambano wao uliofanyika mbagala Dar es salaam Kashinde alishinda kwa point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Hassani Kidebe kushoto akioneshana ufundi wa kutupa makonde na Shabani Mtengela wakati wa mpambano wao Mtengela alishinda kwa point mpambano huo Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

WAMILIKI WA MAENEO YA BIASHARA WAOMBWA KUTOA KIPAUMBELE KWA WANAWAKE WAJASIRIMALI


DSC_0935
Mwenyekiti wa Tancraft, Elihaika Mrema akizungumza na waandishi wa habari umuhimu wa jumuiya kubwa za wafanyabiashara na pamoja na serikali kuwaunga mkono wajasirimali wanawake nchini, Kushoto ni Esther Kasenga Msaidizi wa Katibu, Kulia Mweka hazina wa Chama cha Tancraft, Bi.Louise Judicate na Wapili kulia ni Katibu wa Tancraft, Bi. Vicky Shayo.
Na Damas Makangale, MOblog Tanzania

WAMILIKI Wote wa maeneo ya biashara nchini wameombwa kutoa nafasi ya maeneo ya biashara kwa wajasirimali wanawake ili kumkomboa mwanamke kutoka katika dimbwi la umaskini na utegemezi. MOblog inaripoti. Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wajasirimali wanawake jijini Dar es Salaam leo mchana, Mwenyekiti wa Tanzania Handcraft Association (Tancraft), Elihaika Mrema amesema kuwa wanawake wafanyabiashara wadogo wana matatizo na changamoto kadhaa mojawapo ni maeneo ya kuuzia bidhaa zao.
DSC_0939
Pichani juu na chini ni Baadhi ya Wajasiriamali Wanawake wakifuatilia hotuba ya mwenyekiti wa TANCRAFT Bi. Elihaika Mrema alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika jengo la Biashara la DAR FREE MARKET lililopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na Ubalozi wa Kenya nchini.
“hata kama mjasirimali mwanamke ukimpa mtaji wa biashara na mafunzo changamoto kubwa ni kupata eneo la kuweza kuuza hiyo bidhaa yake aliyotengeneza kwa mikono yake mwenyewe,” amesema Mrema
Mwenyekiti, Mrema amesema kuwa chama cha Tancraft kilianzishwa mwaka 2006 chini ya usimamizi wa Board of External Trade (BET) na Small industrial Development Organization (SIDO) na kina wanachama zaidi ya 300 kutoka mikoa yote Tanzania.
DSC_0937
DSC_0967
Hii ni moja ya zawadi ya kikombe kwa Chama cha Wajasiriamali Wanawake Tanzania (TANCFRAFT) walichowahi kupata kwa kuonyesha bidhaa zenye ubora wa kimataifa.
Amesema kuwa Tancraft ni chama cha wajasirimali wanaotengeneza bidhaa kwa kutumia mali ghafi za kutoka nchini kama vile nguo za batik, vikapu, minyaa, vitu vya ufinyanzi,vinyago, shanga, bidhaa za ngozi, chakula na usindikaji wa aiana zote zikiwemo asali.
“malengo makuu ya chama yalikuwa ni pamoja na kuwatafutia wanachama wake soko la pamoja kwa ajili ya kuuzia bidhaa zao,” alilisisitiza Mrema
Amesema kwamba chama cha wanawake wa wajasirimali kimepata sehemu ya Dar es Salaam Free Market ambapo wajasirimali wakinamama watapata fursa ya kufanya biashara zao bila kulipa ushuru kama walivyokuwa katika maeneo ya Chang’ombe mikono.
DSC_0849
Mkurugenzi Mtendaji wa J & L Enterprises, Bi. Louise Judicate Mushi, akitoa maelezo ya bidhaa zake za mchai chai za aina mbili black na green tea na mishumaa, amesema kwamba Green Tea ni mchai chai wa kijani kabisa ambao umesagwa kwa matumizi bora kwa afya ya binadamu
Amesema uzuri wa kinywaji hicho unaweza kunywa kikiwa cha moto au baridi, mchai chai ni dawa ya kushusha sukari, homa, presha, misuli na sumu za mwilini.
DSC_0859
Mkurugenzi Mtendaji wa J & L Enterprises, Bi. Louise Judicate Mushi akimuonjesha aina ya chai mmoja wa waandishi wa habari kutoka kituo cha Channel Ten Bw. Salum Mkambala.
DSC_0874
Mjasiriamali Fatuma Amour kutoka kampuni ya Famour Designer, akizungumzia ubunifu wake wa mavazi na ujasirimali utengenezaji wa nguo za wakinamama na wakinababa na Carpet za ngozi, viatu vya ngozi, vikapu na Batiki. Fatuma amesema alianza biashara miaka karibu 12 iliyopita katika biashara yake ya vitu vya asili vya kiafrika na changamoto kubwa kwake ni kujitangaza. Kushoto ni mwandishi wa habari kutoka Mwananchi Communications, Bi. Maimuna Kubegeya.
DSC_0871
Maimuna Kubegeya akiangalia moja ya bidhaa zinazotengenezwa na Mjasiriamali Fatuma Amour kwenye jengo la Biashara la DAR FREE MARKET lililopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na Ubalozi wa Kenya nchini ambapo watakuwa hapo kwa muda wa mwaka mmoja.

MFUKO WA PENSHENI WA PPF WAENDESHA SEMINA KWA WAFANYAKAZI WA TANESCO WALIOHUDHURIA MKUTANO WA MAJADILIANO ULIOFANYIKA MWISHONI MWA WIKI MJINI TANGA.


Meneja wa Kanda ya Kinondoni na Tanga wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahra Kayungwa akitoa mada ya jinsi mwanachama wa mfuko wa Pensheni wa PPF anawezaje kupata mafao yake kwa haraka na kwa wakati pindi anapostaafu kazini katika mkutano uliofanyika kati ya Wafanyakazi wa Tanesco na Maofisa wa mfuko wa Pensheni wa PPF uliofanyika mwishoni mwa Wiki mjini Tanga.
Afisa Mwandamizi wa Uwekazaji Kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw Godbless Robin akielezea jinsi PPF inavyowekeza katika Kujenga Nyumba za Bei nafuu na kuwauzia pamoja na Kuwakopesha wanachama wao waliojiunga na Mfuko wa Pensheni wa PPF kwenye mkutano na wafanyakazi wa Tanesco uliofanyika katika Hoteli ya Navera iliyopo mjini Tanga.
Meneja wa kanda ya Kinondoni na Tanga wa mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahra Kayungwa akiwaelezea baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco juu ya faida wanazopata wanachama wa PPF mara baada ya kujiunga katika Mfuko huo,katika Mkutano uliofanyika jijini Tanga Mwishoni  mwa wiki katika hoteli ya Navera.
Katibu Mkuu Msaidizi wa Tuico Makao Makuu, Bw Perese Jonathan akichangia mada wakati wa mkutano wa Tuico Kati ya Wafanyakazi wa Tanesco na Maafisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF kwenye mkutano uliofanyika mjini Tanga Mwishoni mwa Wiki.
Meneja wa Kanda ya Kinondoni na Tanga wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahra Kayungwa akiwafundisha wafanyakazi wa Tanesco kanuni ya jinsi ya kupata mafao ya Mkupuo na mafao ya kawaida ya Kila Mwezi kutoka mfuko wa Pensheni wa PPF katika mkutano uliofanyika Mjini Tanga mwishoni mwa Wiki, Anayeshuhudia kushoto ni Afisa wa PPF, Bi Chevu Sepeku.
Meneja Mahusiano na Masoko wa mfuko wa Pensheni wa PPF,  Bi Lulu Mengele akisisitiza jambo wakati akichangia mada kwenye mkutano wa Tuico Tanesco uliofanyika Katika Hoteli ya Navera Mjini Tanga Mwishoni Mwa Wiki.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa majadiliano wa TUICO tawi la Tanesco ambao pia ni wafanyakazi wa Tanesco wakinyanyua mikono juu tayari kwa kuuliza maswali kwa maofisa wa mfuko wa pensheni wa PPF ambao ndio walikuwa waendesha mada katika mkutano huo uliofanyika mwishoni mwa wiki Mjini Tanga katika Hoteli ya Navera.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa majadiliano wa Tuico tawi la Tanesco wakipitia vitabu vya PPF kwaajili ya kujiongezea uelewa kuhusu mfuko wa Pensheni wa PPF kwenye mkutano wa majadiliano wa Tuico tawi la Tanesco uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Tanga.
Mwenyekiti wa TUICO Tanesco Tawi la Mwanza, Bw. Salehe Mkele ambae pia ni Msimamizi wa Wasoma Mita Tanesco Mwanza, akitoa ushuhuda wake wa jinsi ya baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco Mwanza ambao wamekopeshwa na walionunua nyumba za Bei Nafuu zilizokuwa Zikiuzwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF.

Nyamwela afyatua mpya na Tundaman



MNENGUAJI kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Mussa Hassan 'Super Nyamwela' amefyatua wimbo mpya uitwao 'Nyengele' akimshirikisha nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Tundaman ikiwa ni maandalizi yake ya kupakua albamu yake mpya na ya tatu.
Akizungumza na MICHARAZO, Super Nyamwela alisema wimbo huo ambao ni wa nne katika maandalizi ya albamu hiyo baada ya 'Duvele Duvele', na Maneno Maneno ameurekodia katika studio za C9 Records na anatarajia kuachia wiki ijayo.
Nyamwela alisema katika wimbo huo kama ulivyo 'Duvele Duvele' na 'Tumechete'  umepigwa kiasili kwa ajili ya kuleta vionjo tofauti na kutamba kuwa utakuwa funika bovu kwa namna Tundaman alivyompiga tafu.
"Nipo katika maandalizi ya mwisho ya kuachia audio na video ya wimbo wangu mpya uitwao 'Nyengele' ambao nimeuimba na Tundaman ikiwa ni maandalizi kutoa albamu yangu ya tatu baada ya 'Master of the Tample' na 'Afrika Kilomondo', " alisema Nyamwela.
Nyamwela alisema amepanga ndani ya mwaka huu albamu hiyo ya tatu itakuwa imekamilika na pia itafanyiwa uzinduzi , japo hajajua itafanyika mwezi gani na ukumbi gani.
"Nataka nikamilishe nyimbo zote audio na video kabla ya kuizindua rasmi," alisema Nyawela.