Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, November 27, 2009

SERENGETI KUDHAMINI SAFARI YA KUUTANGAZA MLIMA MREFU AFRIKA

Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya bia ya Serengeti jaji, Mark
Bomani (kulia) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni.12 kwa Mratibu
wa Kamati ya kupanda Mlima Kilimanjaro Bw. Joseph Kitani, wakati
wa uzinduzi wa Sherehe za kupanda Mlima uho, Dar es salaam jana,
anaeshughudia katikati ni Mjumbe wa Kamati hiyo na Diwani wa Kata
ya Mchikichini Bw. Leonard Lupilya.(Picha na Rajabu Mhamila)

MSONDO KUWABURUDISHA WA ZANZIBAR

Wanamuziki wa MSONDO MUSIC BAND wakiwajibika wakati wa
onesho lao lililofanyika Dar es salaam juzi kushoto ni Eddo Sanga na
Rashidi Mwezingo.(Picha na RAJABU mhamila)
Bendi ya Msondo Ngoma Music inatarajia kufanya onesho maalumu kwa wakazi wa Zanzibar wakati wa sikukuu ya Idd el Hajj kesho
Akizungumza jana,Msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' alisema pia watatumia onesho ilo kutambulisha nyimbo zao zilizo katika albam mpya ya huna shukurani,hikiwa na nyimbo za Kiapo Mama Cos, Haki yangu.na nyingin
''Onesho litafanyika katika ukumbi wa Gymkhana Zanzibar, tunaamini mashabiki wetu wa Zanzibar watafurahia hili onesho la aina yake kwa kuwa tumejipanga vema alisema Mhamila
Pia alisema watatambulisha wimbo mpya wa mwanamuziki Eddo Sanga uitwao Lipi jema na kwamba kwa sasa kundi hilo lipo juu, hivyo kuwataka mashabiki wa Zanzibar wajihandae kupata vitu vya uhakika Nae Mkurugenzi wa kundi hilo Muhidini Gurumo alisema wamejipanga vizuri na kuwa Idd Pili watatumbuiza kwenye ukumbi wa CCM kata 14 Temeke jijini Dar es salaam

ZAIN WAZINDUA HUDUMA YA VIFUNGU VODOGOVIDOGO

Meneja Masoko wa Kampuni ya Zain, Bw. Costantine Magavilla
(kushoto) akionesha waandishi wa habari jinsi ya kujiunga na huduma
mpya ya Internet inayopatikana kwa urahisi yenye vifungu
vidogovidogo, kulia ni Meneja wa Mawasiliano wa Kampuni hiyo Bi.
Beactrice Mallya.(Picha na Rajabu Mhamila)

Wednesday, November 25, 2009

MAREALE - KOMBE LA MACHIFU LIPO

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Executive Solution, Aggrey Marealle (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam kuhusu Mashindano ya Kombe la Chifu Marealle, kwa mwaka Huu yatakayozinduliwa rasmi mjini moshi mwanzoni mwa mwezi ujao sambamba na sherehe za Siku ya Uhuru kulia ni Meneja Matukio wa Kampuni hiyo. Carol Ndosi.(Picha na Rajabu Mhamila)

WANAFUNZI WAFANYA KWELI KATIKA SANAA ZA JUKWAANI

Baadhi ya wasanii wa kikundi cha Bongo Wookeez, wakicheza wakati wa Tamasha, lililowakutanisha shule mbalimbali za jiji la Dar es salaam lililodhaminiwa na kampuni ya Vodacom kwa ajili ya kuwaleta karibu na huduma mbalimbali za kampuni hiyo.(Picha na Rajabu Mhamila)Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ilala, wakicheza wakati wa Tamasha, lililowakutanisha shule mbalimbali za jiji la Dar es salaam juzi lililodhaminiwa na kampuni ya Vodacom kwa ajili ya kuwaleta karibu na huduma mbalimbali za kampuni hiyo.(Picha na Rajabu Mhamila)

Sunday, November 22, 2009

BUSTER AFANYA KWELI DAR

Wanamuziki wa Marekani wakiwajibika wakati wa onesho la Fiesta lililofanyika, Dar es salaam na kudhaminiwa na Kampuni ya Zain na Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) kulia ni Busta Rhymes na Spliffstar.(Picha na Rajabu Mhamila)

Saturday, November 21, 2009

ISAKA STEPHANO MISS UTALII TANGA

Iska Stepahano jana alitangazwa mshindi wa Fainal za Miss Utalii Mkoa wa Tanga baada ya kuwashinda wenzake 9 katika kinyang’anyiro kilichofanyika katika Ukumbi wa Beach Resort kandokando ya Bahari ya Hindi ambapo mgeni Rasmi alikuwa ni Wilaya ya Mkinga, Kinawilo Edward aliyemvisha taji baada ya kutangazwa Mshindi.Katika fainal hizo ambazo zilitikisa mkoa wa Tanga, jumla ya washiriki kumi walipanda jukwaani katika mavazi mbalimbali ambayo yalibunia na mbunifu wa mavazi wa kimataifa hapa nchini, Fatma Amour, ambaye aliingia hapa hivi karibuni akitokea nchioni Marekani ambako alikuwa katika mwaliko wa kuonyesha mavazi na kujifunza masuala ya Usanii.Warembo hao wakiwa katika mavazi ya aina tofauti yakiwemo ya Utamaduni wa Tanzaniana Asili ya Kiafrika, ambapo Vikundi mbalimbali vya Muziki vilitumbuiza akiwamo Mwanamuziki Mkongwe wa Muziki wa Dansi Mwinjuma Mumin, mwanamuziki wa Kizazi Kipya, Maunda Zoro,na Kassim Mganga
Katika shindano hilo mshindi wa kwanza alipata kitita cha shilingi laki tano taslim, wa pili laki moja na nusu, wa tatu laki moja , wa nne laki moja na wa tano kiasi cha shilingi laki moja, wakati barozi wa Tanga Beach Resort ambaye pia ni Miss Utalii Tanga 2009- Iska Stephano alikabidhiwa TV yenye thamani ya shilingi laki 4, huku washiriki wengine wakipata kifuta jasho cha shilingi helfu hamsini kila mmoja.
aidha katika shindano hilo Mbunifu wa Mavazi wa Kimataifa Fatma Amour, alimvisha Taji, la kiasili lililotengenezwa kwa Ustadi Mkuu ambao uligharimu kiasi cha shilingi laki moja na Nusu, likiwa na Alama ya Bendera ya Taifa.Warembo walioshiriki Fainal hizo ni pamoja na Iska Stephano, Lyna Lucas, Judith Assey, Vaileth Michael, Imakulata Njuu, Ashura Nasri, Ummy Ally, Grece Joseph, Mariam Rajabu, na Fuse Kilenge Asile, ambapo waliofanikiwa kuingia hatua ya tano bora ni pamoja na IIska Stephano, Lyna Lucas, Vaileth Michael, Judith Assey na Grece Josephat.Washindi watano katika fainal hizo watashiriki katika hatua ya Kanda ya Mashariki ambayo inajumuisha mikoa ya Dar es Salaa, Morogoro, Pwani, Mtwara, na lindi,

Friday, November 20, 2009

KOMBE LA DUNIA TANZANIA

Kombe la Dunia lipo ziarani nchini Tanzania. Ziara hiyo imezinduliwa rasmi leo jioni nchini Tanzania na Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Ziara ya kombe hilo katika sehemu mbalimbali duniani, ni ishara ya kuwapa fursa mashabiki mbalimbali wa soka ulimwenguni,nafasi ya kuliona kombe hilo “live” na hata kupiga nalo picha kwa kumbukumbu nk. Hizo zote ni miongoni mwa shughuli mbalimbali kuelekea South Africa 2010.

Wakati nikimuangalia Rais Kikwete akiwa amejawa na tabasamu wakati akilinyanyua kombe hilo na kulibusu,nilijiuliza, hivi itakuja tokea kweli siku moja Rais wa Tanzania(yeyote yule atakayekuwa madarakani) kulinyanyua Kombe la Dunia baada ya kulipokea toka mikononi mwa nahodha wa Taifa Stars baada ya kulitwaa?

Well…naamini kila kitu kinawezekana. Sina tu uhakika kama tuna mipango madhubuti(ya mbali au karibu) ya kutimiza ndoto hizo.Tusiishie tu kuliona kombe kwa mbali au kulinyanyua pale tusipostahili.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amelinyanyua juu kombe la FIFA la dunia wakati alipozindua rasmi ziara ya kombe hilo hapa nchini na kupiga nalo picha jioni hii kwenye uwanja wa taifa rais aliingia kwenye kibada maalum kilichojengwa kwenye uwanja huo kwa ajili ya kuhifadhia kombe hilo akalibeba na kulinyanyua juu huku akilibusu kombe hilo , Rais Jakaya amemtaka rais wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Rodger Tenga pamoja na kamati zake kufanya kazi ya kusimamia na kuinua kiwango na vipaji vya mpira wa miguu nchini badala ya kusimamia timu ya taifa tu na mapato ya milangoni kwani hawako TFF kwa ajili ya kujenga nyumba zao Binafsi bali wapo kwa ajili ya kuendeleza na kukuza soka nchini, Rais Jakaya amelaani kitendo cha shirikisho hilo kuwapa adhabu ya kuwafungia muda mrefu hadi miezi sita wachezaji na kusema hiyo ni kuwakomoa na kudidimiza vipaji vyao badala ya kuviendeleza ziara ya kombe la FIFA la dunia inaratibiwa na wadhamini wa kombe hilo Cocacola na linatembezwa nchi mbalimbali Duniani, aliyeko kulia katika picha ni Hedi Hamer mwakilishi wa FIFA.

Wednesday, November 18, 2009

KOMBE LA DUNIA TANZANIA

Meneja Masoko wa CocaCola, Rita Tsehai akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu ratiba na utaratibu utakaotumika wakati wa ujio wa Kombe la Dunia linalowasili leo Jijini.Kulia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela.
WAZIRI wa Habari Utamaduni na Michezo George Mkuchika anatarajiwa kuiwakilisha Serikali wakati kombe halisi la Dunia litakapowasili leo kwenye uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa katika ziara ya kuzitembelea kila nchi ya Bara la Afrika chini ya udhamini wa kampuni ya CocaCola.Kombe hilo ambalo ni alama kuu ya michezo nikielelezo cha ubora wa soka dunia ni linatarajiwa kutua nchini kuanzia majira ya saa 10 jioni na kualakiwa na na viongozi mablimbali wa SErikali na Shirikisho la soka nchini pamoja na mashabiki wa mchezo wa soka.
Akizungumza Dar es Salaam jana Meneja Masoko wa kamuni ya Coca Cola Tanzania Rita Tseai alisema kampuni hiyo imejiandaa kuchangamsha mapokezi hayo ambayo yatapambwa na burudani mbalimbali kwa ajili ya kuongeza hamasa kwa wapenzi wa mchezo wa soka.
"Kutokana na hamasa inayotaokna na kombe hili ambayo ni nembio kuu ya soka Dunia, Coca Cola inafanya kazi kwa karibu na maafisa wa uwsanja wa ndegewa Mwalimu Nyerere na wahusika wengine kuhakikisha uwsalama unakuwepo na kuifanikisha ziara hii kwa ujumla", alisema.
Alisema likiwa nchini maelfu ya mashabiki wanatarajia kujitokeza kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na viwanja vya Forodhani, Zanzibar kuliona kombe hilo na kupiga nalo picha ambapo pia aliongeza kuwa watapata nafasi ya sinema maalumu ambayo itakuwa ikionyesha matukio kadhaa muhimu ya kukumbukwa ya kombe la Dunia la FIFA na burudani nyingine nyingi.
"Baada ya kuwasili kombe hilo siku ya itakayofuata (ijumaa) litakuwa hapa uwanja wa Taifa kwa ajili ya mashabiki wa soka kuja kuliona na kupiga nalo picha ambapo kwa upande wa uwanjani mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali", alisema
Alisema sehemu ya kwanza ya ziara ya kombe hilo itafika kilele Desemba 3 mwaka huu huko Cape Town , Afrika Kusini ambapo ratiba ya mwisho ya fainali za kombe la Dunia za mwaka 2010 itapangwa kwa tena kwa mara ya pili mwezi januari kwa ajili ya katika nchi kadhaa duniani ambapo itafikia kilele chake mwezi Aprili mwakani.
Alisema ya kombe hilo kwa mwaka huu ni ndefu zaidi duniani ambapo FIFA ikishirikian na kampuni ya Coca Cola italitembeza kombe hilo halisi katika mataifa 86 ziara ambayo itachukua siku 225.

AZAM KUFUNGUA SHULE YA MICHEZO CHAMANZI

Azam FC leo hii majira ya saa nne asubuhi, imefanya mkutano maalum na waandishi wa habari klabuni kuzungumzia mambo mbalimbali yanayohusu klabu. mkutano wa leo umekuwa wa pili na waandishi wa habari tangia kuanza kwa msimu huu wa ligi 2009/2010
Ikumbukwe kuwa wiki chache kabla ya kuanza kwa ligi hii tulifanya mkutano kama huu ambapo pamoja na mambo mengine, tulimtambulisha nahodha wetu mpya Salum Swedi, na kuzungumzia mipango ya klabu katika ushiriki wetu ligi kuu.

Ushiriki wa Klabu ligi kuuMkutano wa leo, umekuja kufuatia kumalizika kwa raundi ya kwanza kwa mafanikio makubwa sana na klabu inatoa shukrani na heshma kubwa kwa wadau wote wa klabu ya Azam FC, hapa tunazungumzia mashabiki wetu, waandishi wa habari wote wa vyombo vyote vya habari, Viongozi wa mpira ngazi ya wilaya ya Ilala na mkoa wa Dar es Salaam, wachezaji na viongozi wa timu ambao kwa pamoja tumeiwezesha klabu yetu kwenda likizo ikiwa inashika nafasi ya pili.
Dhamira ya pili ya mkutano wa leo ilikuwa ni kuzungumzia mipango ya maendeleo ya klabu ya Azam FC pamoja na kujibu hoja na maswali kutoka kwa waandishi wa habari za michezo kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Ujenzi wa uwanja na kituo cha michezo cha Azam FC,

Klabu ya Azam FC kupitia kwa makamu mwenyekiti wake mzee Said Mohammed imeweka bayana mipango ambayo inaendelea ya ujenzi wa uwanja na kituo bora cha mazoezi na makazi ya wachezaji katika eneo la Chamanzi wilaya ya Temeke. Kwa sasa eneo la ukubwa wa zaidi ya ekari 20 limeshapatikana na wataalamu wa usanifu na michoro toka nje ya nchi wanafanyia kazi kuweza kupata mchoro bora wa kiwango cha kimataifa utakaonendana matakwa ya mpira wa miguu na hadhi ya klabu ya ligi kuu.

Mafanikio makubwa kwa timu ya vijana

Mzee Said Mohammed amesema kama makamu mwenyekiti na kwa niaba ya bodi nzima ya wakurugenzi wa Azam FC anajivunia kuona ushiriki wa kiwango kikubwa kwa wachezaji wa timu ya vijana wa Azam FC Academy, ikumbukwe kuwa nyota wanaotamba sasa na Azam FC kama Mau Bofu Ally, Himid Mao Mkami, Awadh Mohammed na Tumba Swedi wamesajiriwa na kikosi cha Azam FC U-20.
Azam FC ndiyo klabu ya kwanza ya ligi kuu kuanzisha kikosi cha vijana bila kushurutishwa na mtu yoyote, na pia imekuwa timu ya kwanza kuweza kuwatumia vijana wa kikosi cha pili kwenye michezo ya ligi kuu kama tunavyoweza kuziona klabu kama Arsenal, Aston Villa, Liverpool na Manchester United zikifanya pale England
timu yetu ya vijana ndiyo mabingawa wanaoshikilia kombe la Uhai Cup kwa wachezaji wa umri chini ya miaka 20 kwa vilabu vya ligi kuu

Viongozi wa Kuajiriwa

Azam FC imekuwa klabu ya kwanza nchini kuwa na viongozi wa kuajiriwa na wakati shirikisho la mpira nchini lilipotangaza ulazima wa kuwa na Viongozi wa kuajiriwa, klabu ya Azam FC ilifanya kazi ya kupeleka tuu majina ya viongozi wake kwani tayari walikuwepo ofisini, haya pia ni mafanikio kwa klabu yetu ambayo tungependa kuyaweka wazi kwa Umaa.

Hakuna mchezaji yoyote wa kuachwa?
Kocha mkuu wa klabu ya Azam FC akichangia katika mkutano huo amesema kwa sasa kutokana na kiwango kizuri kwa kila mchezaji, hakuna mpango wa kumuondoa mchezaji yoyote. klabu itaendelea kuwa na wachezaji wote waliokuwepo kwenye raundi ya kwanza. Ikumbukwe kuwa Azam FC ndiyo timu inayoongoza nchini kwa kuwa na wachezaji wengi timu za Taifa ambapo Vladmir Niyonkuru (Burundi) Erasto Nyoni, Salum Swedi, Ibrahim Mwaipopo, Aggrey Morris, Himid Mao, na John Bocco (Taifa Stars) huku Selemani Kassim Selembe akichezea Zanzibar. utitiri huu wa wachezaji timu za taifa unaonesha ubora wa kikosi cha Azam FC.

Usajili

Klabu imetangaza kumsajiri kiungo kinda na nyota kutoka Mafunzo ya Zanzibar na timu ya taifa ya Zanzibar Selemani Kassim maarufu kama Selembe. Hadi sasa Selembe ndiye mchezaji pekee aliyesajiriwa na Azam FC kuongeza nguvu kwa ajili ya raundi ya pili inayotarajiwa kuanza Januari mwakani
Akijibu swali toka kwa mhariri wa Sports Extra Clouds FC Ibrahim Masoud Maestro, aliyetaka kujua siri ya mabadiliko ya ghafla ya kiuchezaji na morali wa wachezaji tangia Itamar Amorin achukue mikoba na Naider Dos Santos. Kocha mkuu wa Azam FC ItamarAmorin amesema anadhani ni tofauti ya mawasiliano pekee, Itamar amesema mtangulizi wake ambaye ni Mbrazil mwenzake alikuwa kocha mzuri sana lakini wakati mwingine matokeo hayaletwi na ubora wa mbinu za kocha pekee bali hata mfumo, mawasiliano, bahati na wakati.

Kuhusu wachezaji wa Kigeni

kiwango kilichooneshwa na wachezaji watanzania kimekuwa kikubwa sana kuliko wachezaji wa kigeni, Wachezaji watanzania wamebadilika sana, wamecheza kwa bidii na maarifa makubwa sana katika raundi ya kwanza kuliko wageni. na hili unaweza kuliona katika orodha ya wafungaji bora ambapo licha ya ligi kuu kuwa na lundo la washambuliaji wa kigeni lakini orodha hii inashikwa na watanzania wakiongozwa na John Bocco Adebayor wa Azam FC aliyemaliza raundi ya kwanza akiwa na magoli tisa

Kujitoa kombe la Tusker

Kumekuwa na minong’ono isiyo rasmi juu ya uamuzi wa Azam FC kujitoa kwenye michuano ya Tusker Challenge Cup ambapo Makamu Mwenyekiti Mzee Said Mohammed ameona umuhimu wa kulitolea ufafanuzi
Ukweli ni kwamba Azam FC haikujitoa kwa sababu michuano hii inadhaminiwa na kinywaji bali ni kutokana na sababu za kitaalam na kiungozi zaidi.
Kwanza Azam FC ina wachezaji Tisa kwenye timu za Taifa ambazo zinajiandaa na michuano ya Challenge Cup na katika timu yenye wachezaji 24, unapoondoa wachezaji tisa unaiacha na wachezaji 15 ambapo kati yao kuna wachezaji wa kigeni kama Ibrahim Shikanda ambao wakiondoka timu inabaki na wachezaji ambao hawatoshi kujiandaa vema na ushiriki wa michezo hii.
Wachezaji wa Azam FC waliopo timu za Taifa zinazojiandaa na Challenge Cup ni Vladmir Niyonkuru (Burundi) Erasto Nyoni, Salum Swedi, Ibrahim Mwaipopo, Himid Mao, na John Bocco (Kilimanjaro Stars) huku Selemani Kassim Selembe na Aggrey Morris, wakichezea Zanzibar
Pia Azam FC ni klabu inayoendeshwa kwa kufuata misingi ya uweledi (professionalism), tulikwisha jiwekea ratiba yetu (calendar) ambapo ratiba ya klabu ilikuwa ikionesha mapumziko kwa wachezaji wakati raundi ya kwanza itakapo malizika, endapo utawarudisha wachezaji kambini hasa wale wa kigeni utalazimika kuwalipa, kuharibu ratiba ya mwalimu, na kupoteza pesa za nauli kwenye mashirika ya usafiri ambako tulifanya booking. Azam FC iliomba kujitoa kutokana na taarifa ya ushiriki wetu kutufikia kuwa ya mmno na kwa bahati nzuri TFF walikubaliana na ombi letu alisema.

MATUMLA, MARWA KUPANDA TENA ULINGONI

Mratibu wa mapambano ya ngumi, Ramadhani Uhadi katikati wakati wa utambulisho wa pambano kati ya Rashidi Matmla (kushoto) na Joseph Marwa litakalopigwa baadae mwezi huu jijini Dar es salaam.(Picha na Rajabu Mhamila)

Tuesday, November 17, 2009

Mechi ya Algeria na Misri, wabongo mnajifunza nn?

Mashabiki wa soka wa Algeria wakishangilia Novemba 15, 2009 wakati wakisubiri kukata tiketi mbele ya Ofisi za Algerian Airways agency kwa ajili ya safari ya klwenda Sudan kwenda kuishangilia timu yao ya taifa wakati ikicheza na Misri hapo Novemba 18 mjini Khartoum.

Ilikuwa ni cku ya majonzi makubwa km vile ni msiba wa kitaifa baada ya
misri kuwafunga algeria magoli 2 bila majibu licha ya kuwa algeria
walikuwa na nafasi kubwa ya kushinda plus kushindwa kuzi2mia vizuri
nafasi za kufunga walizokuwa wakizipata. Mji ulikuwa kimya watu
wakiugulia maumivu ya magoli hayo.
Tofauti na wabongo ambao wangeanza kulaumu km co kocha bac wachezaji,
waalgeria wameonyesha ushirikiano mkubwa ktk kuisupport timu yao ya
taifa ili iweze kucheza fainali za kombe la dunia.
Kwa kweli mji unapendeza, bendera ya nchi inapepea kila pande,
majumbani mpaka kwenye magari. Wenye kufanya tracksuit, matshirts,
kofia ili mradi kila m2 anaonyesha uzalendo kwa nchi yake. Nyimbo
zime2ngwa mahsusi kwaajili ya kushangilia, zinapigwa kwa sauti ya juu,
kwenye restaurants, majumbani, madukani, kwenye magari, wenye simu nao
wameweka ringin tone ilimradi raha tu!
Kikubwa zaidi, ni kushuka kwa nauli kutoka algeria kwenda khartoum,
sudan kushuhudia mechi live, nauli go and return ni sh 20,000 Dinary
kwa m2 mmoja hapo ni pa1 na malazi na chakula wakiwa huko sudan ni
sawa na punguzo la asilimia zaidi ya 70 kutoka kwenye nauli ya awali
ya 90,000 Dinary!
Ina maana sehemu ya nauli imetolewa na sponsers plus the government!
No need for viza, ni ww tu na passport yako, visa utaipatia airport,
mnaona mipango mizuri ya serikali?!
Wabongo mpo hapo??

Huyu ni mdau wa viwanjani yuko masomoni nchini Algeria!!!
Wewe je unasemaje???

TAFCA - YAWASHANGAA WANAOMZODOA MAZIXIMO

Katibu mkuu wa Chama cha Makocha hapa nchini TAFCA Egini Mwasamaki ameomba watanzania wakae kimya na waache kumuingilia kocha mkuu Mbrazil Maxio Maximo ili afanye kazi yake vizuri.
Akizungumza na kipindi cha michezo cha Radio Times FM Mwasamaki amesema Maximo yeye ni kocha ambaye anaifahamu vyema kazi yake na mchezo iliyochezwa Misri na Yemeni ni majaribio na si ushindani hivyo si lazima timu ifunge.
Aidha ameongeza kwamba kitendo cha kumkosoa na kumzomea hakijengi ila anapofanya vizuri pia asifiwe na ushauri si lazima haupokee na kuufanyia kazi bali silaha ya kufundiosha anayo mwenyewe.

TAARIFA YA MSIBA WA MZEE ABUSHIRI KILUNGO!

MZEE ABUSHIRI KILUNGO (PICHANI) AMEFARIKI DUNIA USIKU WA KUAMKIA LEO (16/11/2009) NYUMBANI KWAKE TANDIKA,MTAA WA KIVUNGO BAADA YA KUUGUA UGONJWA WA KISUKARI KWA MUDA MREFU.
MAREHEMU KILUNGO AMBAYE ALIWAHI KUWA NAIBU MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM MIAKA YA NYUMA NA PIA ALIWAHI KUWA MWENYEKITI WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA DAR (DRFA).
MAREHEMU KILUNGO AMEACHA MKE NA WATOTO WATANO WATATU WAKIWA NI WA KIUME NA WAWILI WA KIKE.MAZISHI YATAFANYIKA LEO (17/11/2009) SHAMBANI KWAKE TUANGOMA,NJE KIDOGO YA JIJI LA DAR ES SALAAM.
TUNAMUOMBEA KWA MWENYEZI MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MZEE WETU ABUSHIRI KILUNGO MAHALI PEMA PEPONI
-AMIN

RT YAKABIDHI VIFAA VYA RIADHA KWA WAZIRI WA ULINZI

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Nchini (RT) Suleiman Nyambui (kushoto) akimkabidhi seti ya jezi za kukimbilia, waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Lawrence Masha, Dar es salaam wakati wa hafla ya makabidhiano na wadau mbalimbali wa ulinzi shirikishi anaeshuhudia kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi, Bw.Said Mwema.(Picha na Rajabu Mhamila)

SERENGETI YAWAPA VIFAA VYA MICHEZO TSN

Meneja wa Habari Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Teddy Mapunda (kulia) akimkabidhi Vifaa vya michezo vyenye thamani ya laki 8, Mwenyekiti wa Standard News Papers (TSN) Sports Club, Nasongelya Kilyinga, Dar es salaam kwa ajili ya mashindano mbalimbali yanayowakabili anae shuhudia katikati ni Mjumbe wa Club hiyo, Abdallah Msuya.(PIcha na Rajabu Mhamila)

MSONDO NGOMA KAZINI

Waimbaji wa bendi ya Msondo music wakiwajibika wakati wa onesho lao lililofanyika juzi katika ukumbi wa afri center Ilala (kushoto) ni Eddo Sanga na Rashidi Mwezingo.(PICHA NA RAJABU MHAMILA)

YANGA WAHITIMISHA LIGI KUU BARA MZUNGUKO WA KWANZA

Mabingwa watetezi Yanga wamekamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi kuu Tanzania Bara kwa kuizaba timu ya Tanzania Prison kwa Jumla ya magoli 4-2 katika mchezo uliyopigwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
mashujaa wa Yanga katika mchezo huo alikuwa ni Mrisho Khalfani Ngasa aliyefunga magoli mawili, Kigi Makasi na Athumani Iddi Chuji kwa shuti la mbali.
Magoli ya Tanzania Prison yalifungwa na John Matei na Jackob Ibrahim.
Yanga imemaliza msunguko wa kwanza wa Vodacom Premiur League ikiwa imejikusanyia jumla ya pointi 21 ikishika nafasi ya tatu nyuma ya Azam FC inayoshikilia nafasi ya pili huku wakiwa pointi 12 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Simba wenye pointi 33.

Monday, November 16, 2009

MAXIMO - KUIZOMEA STARS NI USHAMBA

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars Mbraziri Marcio Basilio Maximo Amesisitiza kuwa mchezaji asiye na uwezo, Utaifa,Ubinafsi na nidhamu nje na ndani ya Uwanja asahau kuitwa kwenye kikosi chake.
Akizungumza na waandishi wa Habari katika Ofisi za TFF Maximo amesema kuwa kutofanya vizuri kwa Taifa Stars hata yeye hapendi matokeo mabaya lakini tukumbuke tulipotoka na sasa tupowapi na kufanya vizuri kwa timu si mafanikio ya muda mfupi jinsi Watanzania tunavyofikiri.
Maximo ameongeza kuwa tusifikirie wachezaji wa Timu ya Taifa tulionao kwa sasa ambao umri wao unafikia ukingoni bali tuwe na mipango endelevu ikiwa ni pamoja na kuimarisha michezo kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 na 21 ili kupata Timu ya Taifa Bora hapo baadae.
Timu ya Taifa inatarajiwa kuingia kambini kesho kutwa kujiandaa na Mashindano ya Chalenji itakayoshirikisha jumla ya Nchni 11 itakayoanza kutimua vumbi mwishoni mwa mwezi huu huko Nchni Kenya.

DAA - KUENDESHA MBIO ZA WAZI

Chama cha riadha Dar es Salaam DAA, Kwa kushirikiana na Shirikisho la Riadha Tanzania RT, kimeandaa mbio za wazi za mchezo huo zitakazonyika Desemba tano hadi sita katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Katibu wa DAA, Lucas Nkungu amesema mashindano hayo ya siku mbili yanashirikisha wachaezaji wote kutoka Tanzania Bara na Visiwani

WUSHU - KUZINDUA RASMI FEBRUARI 2010

Ungozi wa chama cha Wushu Tanzania wanatarajia kuzindua chama hicho mwanzoni mwa February
mwakani ili kujulisha wachezaji na wapenzi kutambua kuwepo kwa chama hicho.
Akizungumza na kipindi cha michezo cha Radio Times FM Rais wa Mchezo huo hapa nchini Mwarami Shaweji Mitete amesema kwa muda mrefu walifanya jitihada za kusajili chama hicho ndipo mwezi Agost mwaka huu na uzinduzi huo utakuwa kama changamoto ya kukutana na wachezaji mbalimbali na kupanga mikakati ya pamoja.
Amesema kwasasa chama hicho kinaendeshwa bila kuwa na fedha za kutosha kutokana na viongozi kukosa fedha kwa wadhamini mbalimbali.Hata hivyo Wachezaji watano waliondoka wiki iliyopita nchini China kushiriki mafunzo ya mwaka mmoja wamefika salama isipokuwa wana matatizo ya kiafya inayosababishwa na hali ya hewa.
Wachezaji hao ni Omary Upinde, Ramadhani Maneno, wachezaji wawili kutoka katika kundi la mama Afrika, na wawili kutoka katika kundi la Bagamoyo.
Wushu ni mjumuiko wa michezo ya kichina inayochezwa na sakarakasi, Kungfuu, Taichii na Tajakwan.

SIMBA - MECHI 11 DOLE TU

Mnyama Simba avunja rekodi ya klabu Yanga katika ligi kuu Tanzania kwa kumaliza duru la kwanza wakiwa na jumla ya 33 ikiwa ni pointi tatu zaidi Yanga katika msimu uliyopita.
Simba imevunja rekodi hiyo ya Yanga iliyowekwa msimu uliyopita baada ya kuwazamisha mabingwa Ngao ya Hisani Mtibwa Suger katika mchezo uliyopigwa kunako uwanja wa Uhuru.
Wauaji wa Simba ni Mussa Hassan Mgosi, Uhuru Suleiman na David Naftari aliyefunga goli la tatu akiunganisha mpira uliyopigwa na Emmanuel Okwi.
Simba imemaliza duru la kwanza la ligi kuu ikiwa inaongoza kwa jumla ya pointi 33 ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja.

YANGA - TUNASIBIRI BARUA

Klabu ya Yanga imekanusha kupokea taarifa ya kurejea kwa wachezaji iliyowauza kwa mkopo katika klabu ya Moro United na African Lyon.
Lusi Sendeu ni Afisa Habari wa klabu ya Yanga amesema taariaf hizo nao wamezisikia katika vyombo vya habari lakini hawana taarifa nazo, na kudai pindi zitakapowafikia watalifanyia kazi na kutoa maamuzi.
Taarifa za kuaminika mchezaji Casto Mumbala aliyekuwa akicheza kwa mkopo African Lyon na Abubakari Mtiro aliyekuwa kwa mkopo Moro Unted imebainishwa wametemwa kufuatia viwango vyao kushuka.

Friday, November 13, 2009

KOMBE LA DUNIA LA TUA KENYA

Raisi Mwai Kibaki na waziri Mkuu Raila Ondiga wakilipokea kombe la Dunia la FIFA (FIFA World Cup Trophy) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyata JKIA. Mashabikiwa soka hapo kesho watapata nafasi ya kulishuhudia kommbe hilo siku ya Jumamosi katika uwanja wa Nyayo.

Raisi Mwai Kibaki akizungumza katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta amesema ujio wa kombe hilo ni tukio la kihistoria nchini Kenya na nichangamoto kwa taifa hilo katika kuendeleza michezo.Amesema kushinda kombe la Dunia ni ndoto za kila mchezaji na kuwasili nchini Kenya ni nafasi ya pekee ya kuimarisha ndoto na kurekebisha hali ya soka la Kenya amesema Raisi Kibaki.Kibaki, pia amezungumzia nia ya kuunda kamati kufanya kazi ya kuziarika timu zilizofuzu kombe la Dunia kufanya mazoezi nchini Kenya , kabla hazijaenda Afrika ya Kusini.
Amesema kuwa Kenya ina miundo mbinu bora yakuweza kuwasilianan na pande zote za Dunia ni ni masaa machache kwa Ndege kwenda Afrika Kusini.
Raisi Kibaki amesema kufanyika kwa kombe la Dunia kwa mara ya kwanza barani Afrika 2010 kutaifanya Kenya kupata nafasi ya kufaidika kwa Timu nyingi na mashabiki wengi wa Soka watakaopita kwenda Afrika Kusini.
Safari ya kombe la FIFA la Dunia inadhaminiwa na Coca-Cola.
Safari ya Kombe la Dunia ni ya siku 70 katika mataifa 52 ya Africa litaishia Afrika Kusini Desemba 3 huku mataifa 32 yatashirika fainali zijazo za kombe la Dunia.

YANGA - KWAHERI BARASA

Uongozi wa klabu ya Yanga umempa mkono wa kheri popote aendako Winga machachari atumiae guu la kushoto Mkenya Mike Barasa kufuatia mchezaji huyo kutoonyesha ushirikiano wa kutosha kama atabakia Jangwani ama laa.
Luis Sendeu Akizungumza bila kumeza mate wala kusita na waandishi wa vyombo mbali mbali vya Habari za michezo katika Jengo lenye Mvuto pengine kuliko vilabu vyote amesema wameamua kuutangazia Umma juu ya hatma ya mchezaji huyo kuwa kwa sasa hawatakuwa naye.
Yanga katika hatua nyingine wamewakumbusha Wanachama wao kuwa waanze kuzilipia kadi zao kabla ya uchaguzi hapo mewakani.

MABINGWA ZANZIBAR KUKUTANA NA SIMBA NA YANGA

Katika kudumisha Muungano wa Tanzania Shirikisho la Soka Nchini TFF limejumuisha Klabu ya Mafunzo ya Zanzibar kuungana na Simba,Yanga na Mtibwa Sukari katika kinyan'ganyiro cha michuano ya Tusker Chalenji Cup itakayoanza kutimua vumbi Decemba 14 hadi 27 mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi ya TFF Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho hilo Sunday Kayuni ametanabaisha kuwa walipata barua kutoka Chama cha soka cha Zanzibar ZFA kwa Timu zao kushindwa kushirikishwa katika michuano hii hivyo TFF imekiri kuteleza na kuamua kuwapa nafasi hiyo Timu ya Mafunzo.
Kayuni ameongeza kuwa tayari Timu mbili toka Kenya zitakazoshiriki michuano hiyo ambazo ni Sofapaka ambao tayari wamekwishatangaza ubingwa wa ligi kuu nchini Kenya na Tusker na kufikisha jumla ya Timu sita zitakazoshiriki kwenye Mashindano hayo.
Lakini wakati TFF ikiiteu timu ya Mafunzo kushiriki michuano ya kombe la Tasker, Mwenyekiti wa Timu ya JKT Ruvu Meja Charles Mbuge amesikitishwa na Uamuzi huo na kusema kuwa TFF wanapepesuka katika kufikia maamuzi yao.
Wakati huo huo Shirikisho la soka la Tanzania TFF linaendendelea kuwakumbusha Vilabu vyote hapa Nchini kutumia kipindi cha usajili ipasavyo badala ya kuchelewa na kuleta matatizo hapo baadae.
Sunday Kayuni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF ameyasema hayo kwenye Ofisi za Shirikisho hilo kuwa kila mara wanapokea simu kutoka sehemu mbali mbali wakiulizia juu ya Usajili utaanza lini na kumalizia lini.

SIJASHINDWA NIMETOLEWA - ELIZABETH

Aliyekuwa mwakilishi wa Tanzania katika mashindano ya Big Brother, Elizabeth Gupta,(kushoto)akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam kuusu mashindano hayo kulia ni Meneja mwendeshaji, Ronald Shelukindo.(Picha na Rajabu Mhamila)

MWAKILISHI wa Tanzania katika mashindano ya Big Brother, Elizabeth Gupta, amesema kuwa kila kitu mtu akitaka kufanya kwa ajili ya mafanikio, anaweza kutimiza malengo yake.
Akizungumza Dar es Salaam, Elizabeth alisema kuwa licha ya kutoka katika jumba hilo nchini Afrika Kusini, bado ataonekana kuwa mmoja wa wanawake waliofanya vizuri katika mashindano hayo lakini bahati haikuwa yake.
Alisema kuwa ametoka katika jumba hilo ikiwa ni siku 63 tangu aingie, lakini amejitahidi kadri ya uwezo wake na anatarajia kufanya vizuri zaidi katika miaka ijayo.Elizabeth alisema kuwa imekuwa ni vigumu sana kwa yeye kuibuka na ushindi kutokana na mwaka huu sheria mbalimbali zimebadilika ikiwa ni pamoja na nchi nyingine kuwakilishwa na zaidi ya watu wawili.
"Nafurahi sana kurudi nyumbani salama, nimeweza kufanya vizuri kadri ya uwezo wangu hivyo natarajia kufanya vizuri zaidi katika miaka ya karibuni, hata kama sijabahatika kuwa mshindi wa kwanza katika jumba la Big Brother, bado mie najiona mshindi" alisema Elizabeth.
Alisema kuwa anatarajia kutafuta chuo kwa ajili ya kujiendeleza katika sanaa na hivyo anaahidi kufanya mabadiliko makubwa katika medani hiyo.
Elizabeth aliwasili nchini jana usiku akitokea Afrika Kusini baada ya kutolewa katika jumba la Big Brother.

Wednesday, November 11, 2009

UCHAGUZI TBF WASUASUA

Uchaguzi wa Shirikisho la mpira wa kikapu uliopangwa kufanyika Novemba 28 mwaka huu unaweza usifanyike kutokana na sikukuu ya Idd Alhaj.
Uchaguzi huo uliosogezwa mbele mara tatu mfululizo unaonekana kusuasua kutokana na ukata wa kifedha.
Hadi hii leo wagombea waliojitokeza ni 25, baadhi yao ni Nafasi ya Urais, Richard Kasesela, Mussa Mziya, Jakson Kalikumtima na Phaes Magesa, katika Nafasi ya Makam wa Rais Ahmed Rajab Ahmed, Alijua Mwakalinga ma Alexander Msoffe.
Wengine nafasi ya katibu Msaidizi ni Robert Manyerere, John Nash, Oden Mmbaga, Prosper Mushi na Selemani Semunyu anayewania nafasi ya kamisheni ya watoto.

TIMU ZAJITOKEZA NGUMI ZA VIJANA

Zaidi ya timu kumi za mchezo wa ngumi zimethibitisha kushiriki mashindano ya mchezo huo ya vijana yanayotarajiwa kuanza Nov 24 hadi 29 mwaka huu kwenye uwanja wa ndani wa Taifa uliopo jijini hapa.
Katibu Mkuu wa Chama cha Ngumi za ridhaa hapa nchini BFT, Makore Mashaga amefahamisha kwamba mashindano hayo ya kutafuta klabu bigwa ya vijana vijana inashirikisha wachezaji kutoka klabu zote hapa nchini.
klabu zilizothibitisha ni Sifa, Magereza, JKT, Kariakoo, Azimio, Mavituz, Mtoni, Mbagala, Makongo, Urafiki, Mlandizi, Luaha Galax na Temeke.

HASHEEM THABIT AVUNJIKA TAYA

Kocha mkuu wa klabu ya kikapu ya Memphis Grizzlies Drew Graham akimtibu mchezaji wa kati wa klabu hiyo Hasheem Thabeet wakati wa kota ya kwanza ya mchezo wa jana wa NBA dhidi ya Portland Trail Blazers.

Mchezaji wa kati wa timu ya Memphis Grizzlies Hasheem Thabeet amevunjika taya lake la chini siku ya jana, alipokuwa akichezea na timu yake wakiminyana na Portland Trail Blazers, mchezo amabo ulimalizika kwa Blazers kutoka na ushindi wa pointi 93 kwa 79.Hii sasa inamaanisha kuwa Hasheem hatokuwemo kwenye msafara wa timu yake ya Grizzlies itakapokuwa ikienda kucheza na Houston Rockets usiku wa leo.
Hata hivyo habari si mbaya sana za kuumia kwake kwani baada ya uchunguzi wa madaktari imefahamika kuwa, hatohitaji upasuaji, ili kutibu maumivu na wakasema anatarajiwa awe amepona si muda mrefu sana kuanzia sasa, na ni wazi kuwa hii ni taarifa njema ambayo Thabeet atakuwa amefurahishwa nayo, timu yake na Watanzania kwa ujumla.

Tuesday, November 10, 2009

TAIFA STARS JUMATANO KUCHEZA TENA NA YEMEN

Timu ya taifa kesho inatupa karata yake ya tatu katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Yemen.
Afisa Habari wa shirikisho la kandanda Tanzania TFF Florian Kaijage ambaye ameambatana na Taifa Stars nchini Yemen amesema timu imejiandaa vema kuhakikisha inalinda heshima ya Taifa katika mchezo huo ambao ni wa pili.
akizungumza nami kwa njia ya simu nimemuuliza, moja kwa moja toka Yemen amesema hali ya wachezaji ni nzuri na wamaefanya mazoezi jana na leo.
Kaijage amesema ni Mrisho Ngasa pekee ndiye aliyekuwa akisumbuliwa na Malaria lakini kwa sasa hali yake ni nzuri na leo amefanya mazoezi.
Amesema katika mchezo wa Kesho Taifa Stars inauhakika wakuibuka na ushindi dhidi ya Yemen katika mchezo wa pili wa kirafiki.

SIMBA, YANGA, AZAM FC NA MTIBWA - TUSKER CUP

Yanga sasa kukutana na Simba kabla ya kuanza duru la pili la ligi kuu Tanzania bara watakapo kutana Desemba katika michuano ya kombe la Tasker Chalenji.
Fredrick Mwakalebela ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Nchini TFF ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi za Shirikisho kuwa vigezo vilivyotumika kuteua vilabu hivyo ni kutokana na msimamo wa Ligi kuu unavyoendelea kwa sasa kwa Timu hizo kushika nafasi za juu.
Klabu zilizochaguliwa kushiriki michuano hiyo ni Simba, Yanga, Azam FC na Mtibwa Suger.
Klabu hizo za Ligi kuu Tanzania Bara zimetakiwa kujiandaa mapema kabla ya kuanza kwa Mashindano ya Tusker Challenge Cup litakapoanza kurindimba hapo Decemba 14 hadi 27 jijini Dar es Salaam mwaka huu.
Wakati huohuo Afisa Masoko wa Tusker ambao ni wadhamini wakuu mashindano hayo Gasto Lyaruu amekabidhi hundi ya kiasi cha shilingi milioni thelathini kwa Shirikisho hilo na kusema wametoa fedha hizo kwaajili ya kuanza kufanya maandalizi mapema ikiwa ni pamoja shughuli za uendeshaji kabla ya Mashindano hayo.

SIMBA YATAMBA KUTWAA UCHAMPION WA TUSKER CHALENGE CUP

Uongozi wa wekundu wa Msimbazi Simba umeshangazwa na taarifa zilizo enea kuwa klabu hiyo inampango wa kumsajili winga wa Timu ya Yanga Mike Barasa katika dirisha dogo la usajili unaoendelea hivi sasa.
Afisa Habari wa Simba Cliford Mario Dimbo ametanabaisha umma kuwa taarifa hizo si za kweli isipokuwa wanasubiri Kocha Mkuu Patrick Phiri kuwa ni aina gani ya wachezaji atakaowahitaji.
Ndimbo pia amejigamba katika shindano la Tusker Challenge Cup litakaloaanza Decemba kuwa watahakikisha wanalichukua tena kutokana na kikosi chao kusheheni wachezaji wazuri kuliko vilabu vyote vitakavyoshiriki katika michuano hiyo.
Simba kesho inateremka katika dimba la Uhuru kucheza na timu ya Rovu Shooting ikiwa ni mchezo wa kirafiki kocha akiutumia kujaribu wachezaji wake ambao hawakupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.

MKWASA AKABIDHIWA MIKOBA AFRICAN LYON

Baada ya Timu ya soka ya Afrikan Lyon inayoshiriki ligi kuu Tanzania bara Jahazi lake kuelekea kuzama ikiwa ni ya pili toka mkiani ikiwa na pointi zake Saba, Uongozi wa klabu hiyo imemsainisha mkataba Kocha mkuu wa timu ya taifa ya wanawake Charles Bonifasi Mkwassa ili kuinusuru timu hiyo ili isishuke daraja.
Akizungumza na kipindi cha michezo na burudani Msemaji wa Afrikan Lyon Hassan Mvula amesema wanaufahamu uwezo wa Mkwassa na ndiye atakayeliokoa jahazi hilo lisizame.
Mvulla amesema wanaamini uzoefu wa ligi ya soka Tanzania aliyonao Mkwassa pamoja na uzoefu wake katika timu ya taifa ya wanawake utaisaidia klabu hiyo kuhakikisha wanabaki ligi kuu.
Naye Kocha Boniface Mkwassa amesema atafanya jitihada za maksudi ili kuhakikisha mzunguko wa ligi kuu unamalizika na timu ya Afrikan Lyon inabaki katika nafasi yake.
Amekiri anajukumu la kuifundisha timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania ambayo inajiandaa na michuano ya nchi za Magharibi mwa Afrika, lakini endapo atapatikana mtu mwingine wa kuifundisha timu ya taifa ya wanawake yuko tayari kuachia ngazi.
Amesema licha ya mapenzi yake katika kufundisha soka la wanaume, lakini michezo hivi sasa ni ajira hivyo swala la maslahi ni muhimu kwa mwanamichezo yeyote, hivyo naye amekwenda African Lyon kufuata donge nono la fedha.

POOLTABLE WAHITAJI MILIONI 14 KUSHIRIKI DUNIA

Chama cha mchezo wa pooltable cha kulipwa hapa nchini PT, kinasaka fedha zaidi ya million 14 za maandalizi ya timu ya taifa itakayoshiriki mashindano ya kimataifa ya mchezo huo yatakayoafanyika mwishoni mwa juni na kumalizika July mwakani nchini Uingereza.
Rais wa PT, Chatta Michael amefahamisha kwamba wanatarajia kufanya mashindano ya ndani ya nchi ili wapatikane wachezaji wa tano watakaoshiriki mashindano hayo, huku chama kkiwa hakina uwezo wa kuzipata fedha za maandalizi hayo.

ZANTEL WAZINDUA HUDUMA MPYA

Mkuu wa Mauzo wa Kampuni ya Zantel Bw. John Mbaga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam, kuusu huduma mpya ya viwango vya sh. 1 na SMS za bule zilizozinduliwa, kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Bihashara wa Kampuni hiyo Bw. Fintan Lawler.(Picha na Rajabu Mhamila)

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Zanziba Telecom Ltd (Zantel) imezindua huduma mpya ijulikanavyo kama Tsh 1 + Sms za bure inayowapa wateja wa mtandao huo malipo kabla ya wanaotumia viwango hivyo kwa sekunde.
Akizindua huduma hiyo Dar es Salaam kwa waandishi wa habari,Mkuu wa Mauzo Bw.John Mbaga amesema kuwa Zantel imeamua kuzindua huduma hiyo kwa wateja wake ili kutimiza ahadi zake walizoahidi awali na kuwapa fursa za kuendelea kutimia mtandao huo.
Bw.Mbaga amesema kuwa mpango huo utaendelea kuwawezesha wateja wake kuongea zaidi na kujipatia Sms za bure zitakazowawezesha kuwasiliana na ndugu,jamaa na marafiki kwa muda wa mchana na usiku."Wateja wetu watafaidika na sms za bure zaidi kwa kila siku kwenda mtandao wa Zantel au mitandao mingine na azma yetu ni kuweka watu karibu,pia tunawakaribisha wateja wapya kujiunga katika huduma hiyo,"amesema.
Amesema kuwa kampuni ya Zantel imejitolea kuhakikisha inaendelea kutoa huduma bora kwa watanzania kwa bei nafuu na inaamini kuwa mtandao huo ndio wa kwanza na wa kipekee Tanzania kutoa sms za bure.