Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 24, 2010

WASHINDI 21 WAPATIKANA ZAIN AFRCAN CHALLENGE

Afisa mawasiliano ya ndani wa Zain Tanzania Dangio Kaniki (kushoto) akimkabidhi simu ya mkononi mshindi katika shindano la kujibu maswali kwa njia ya SMS wakati wa kipindi cha Zain Africa Challenge, Juma Mustafa wa Dar es Salaam baada ya kuibuka mshindi. Shindano hilo limeapata jumla ya washindi 23 kutoka sehemu mbalimbali nchini. Kulia ni meneja wa huduma za jamii wa Zain,Washindi katika shindano la kujibu maswali kwa njia SMS wakati wa shindano la Zain Africa Challenge yanayoonyeshwa katika luninga ya TBC 1 wakiwa katika picha ya pamoja bada ya kukabidhiwa zawadi zao katika makao makuu ya ofisi za Zain jijini Dar es Salaam. Kushoto afisa mawasilano ya ndani wa Zain Dangio Kaniki na kulia ni meneja wa huduma za jamii wa Zain, Tunu Kavishe.Afisa mawasiliano ya ndani wa Zain Tanzania Dangio Kaniki (kushoto) akimkabidhi simu ya mkononi mshindi katika shindano la kujibu maswali kwa njia ya SMS wakati wa kipindi cha Zain Africa Challenge, Salvatory Mkami wa Dar es Salaam baada ya kuibuka mshindi. Shindano hilo limeapata jumla ya washindi 23 kutoka sehemu mbalimbali nchini. Kulia ni meneja wa huduma za jamii wa Zain.

Wednesday, April 21, 2010

MAXIMO ATANGAZA KIKOSI KITAKACHOIVAA RWANDA

kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania TFF Marcio Basilio Maximo (katikati) akitangaza majina ya timu ya Taifa itakayoingia kambini kujiandaa na mchezo wa kufuzu michuano ya CHAN ambayo inajumuisha wachezaji wa ndani, timu ya Tanzania inataraji kukutana na Rwanda.

wachezaji waliyoitwa ni pamoja na.

Golikipa
Shabani Kado Mtibwa
Jackson Chove JKT

FULLBACKS
Shadrack Nsajigwa Yanga
Salum Kanoni Simba
Juma Jabu Simba
Stephano Mwasika Moro UTD

CENTER BACKS
Nadir Haroub (Canavaro) Yanga
Kevin Yondani Simba
Aggrey Morris Azam Fc
David Naftal Simba
Dickson Daudi Mtibwa

MIDFIELDERS
Erasto Nyoni Azam
Nurdin Bakari Yanga
Jabir Aziz Simba
Ibrahim Mwaipopo Azam
Kigi Makasi Yanga
Shaban Nditi Mtibwa
Abdi Kassim Yanga
Uhuru Suleiman Simba
Selemani Kassim Azam

FORWARDS
Mrisho Ngassa Yanga
John BOcco Azam
Mussa Mgosi Simba
Jerson Tegete Yanga
MIchael Mgimwa Moro UTD U-20
Yusuf Abbas Soka African Lyon U-20
Joanas Kajuna African Lyon U-20

SOKA KJUTUMIKA KUPAMBANA NA MALERIA TANZANIA

Raisi wa shirikisho la kandanda Tanzania Leodga Chilla Tenga (katikati) akizungumza na waandishi wa habari za michezo wakati wa ufunguzi wa Semina ya MALERIA HAIKUBALIKI, kushoto ni katibu mkuu wa TFF Fredrick Mwakalebela, na kulia ni Anne mratibu wa Marelia Haikubaliki.

Tenga amesema michezo inanafasi kubwa ya kupambana na Maleria kufuatia kuhusisha watu wengi, lakini mchezo wa mpira licha ya kuchezwa dakika 90 hutajwa na kuzungumzwa zaidi ya dakika 90.
Tenga ametolea mfano mchezo wa Simba na Yanga licha ya kuchezwa Jumapili ya tarehe 18 lakini hadi leo bado unajadiliwa, hivyo kupambana na Maleria kupitia michezo itakuwa ni rahisi zaidi kuwafikia watu wengi zaidi pengine kuliko njia yeyote.
Amesema Tayari wamekwishaanza kutoa mafunzo kwa wachezaji wa timu ya taifa TAIFA STARS na wamewateua kuwa mabalozi wa MALERIA HAIKUBALIKI lakini pia wamewagawia vyandarua, wamefanya hivyo pia kwa timu ya U-20 pamoja na timu tisa zilizoshiriki ligi daraja la kwanza dhidi ya matumizi ya chandarua ikiwa ni kinga ya kwanza.

UZINDUZI WA "UHURU WA KUONGEA" WA ZAIN WAFANA J-MARTIN AFANYA KWELI

Huyu ni J-Martin akitoa burudani wakati wa uzinduzi wa UHURU WA KUONGEA katika jengo jipya la Zain, kiukweli jukwaa lilipendeza sana, watu nyomi, full kujiachia na ZAIN

Hapa Brother J-Martin akikamua kitu cha OYOYO wacha Bwana

Kama vipi tucheze pamoja jamani.....




Chidi Benzi kutoka Ilala aliwakilisha vema kwa upande wa wasanii wa Tanzania, jambo la kupongezwa ni kuweza kupiga bonge la shoo akiwa na bendi yake LIVE.Dar es Salaam Stand up, put yo hands up heya heee Dar es Salaam Stand up put yo hands up chichichichi chidi Benziii yoooooo
Sumu ya penzi ukishailambaa hata kwa maziwa huwezi kukuna" ndivyo anavyoimba Belle 9 wakati wa uzinduzi wa UHURU WA KUONGEA wa ZAIN.

Tuesday, April 20, 2010

RATIBA KILI TAIFA CUP 2010 HII HAPA

Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kufanyika kwa droo ya mashindano ya Kili Taifa Cup katika ukumbi wa mikutano wa TFF leo,wengine ni Salim Madadi (kulia) na Iddy Mshangama wote ni Maafisa wa TFF.

FIXTURE KILI TAIFA CUP - 2010

GROUP 'A' - DODOMA
(a) Dodoma
(b) Kigoma
(c) Singida
(d) U - 20

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Singida V/S U-20 14:00 HRS JAMHURI ST.
2. 5/8/2010 C/D Dodoma V/S Kigoma 16:00 HRS JAMHURI ST.
5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C U-20 V/S Dodoma 14:00 HRS JAMHURI ST.
4. 5/10/2010 D/A Kigoma V/S Singida16:00 HRS JAMHURI ST.

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Singida V/S Dodma 14:00 HRS JAMHURI ST.
6. 12-May-10 D/B Kigoma V/S U-20 16:00 HRS JAMHURI ST.

GROUP 'B' - TANGA
(a) Tanga
(b) Morogoro
(c) Pwani
(d) Temeke

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Tanga V/S Morogoro 14:00 HRS MKWAKWANI
2. 5/8/2010 C/D Pwani V/S Temeke 16:00 HRS MKWAKWANI

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Morogoro V/S Pwani 14:00 HRS MKWAKWANI
4. 5/10/2010 D/A Temeke V/S Tanga 16:00 HRS MKWAKWANI

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Tanga V/S Pwani 14:00 HRS MKWAKWANI
6. 12-May-10 D/B Temeke V/S Morogoro 16:00 HRS MKWAKWANI

GROUP 'C' - MWANZA
(a) Mwanza
(b) Kagera
(c) Shinyanga
(d) Tabora

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Shinyanga V/S Kagera 14:00 HRS C.C.M. KIRUMBA
2. 5/8/2010 C/D Mwanza V/S Tabora 16:00 HRS C.C.M. KIRUMBA

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Kagera vs Mwanza 14:00 HRS C.C.M. KIRUMBA
4. 5/10/2010 D/A Tabora vs Shinyanga 16:00 HRS C.C.M. KIRUMBA

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Shinyanga vs Mwanza 14:00 HRS C.C.M. KIRUMBA
6. 12-May-10 D/B Tabora V/S Kagera 16:00 HRS C.C.M. KIRUMBA


GROUP 'D' - ARUSHA
(a) Arusha
(b) Mara
(c) Manyara
(d) Kilimanjaro



SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Mara V/S Kilimanjaro 14:00 HRS SHEKH AMRI ABED
2. 5/8/2010 C/D Manyara V/S Arusha 16:00 HRS SHEKH AMRI ABED

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Kilimanjaro V/S Manyara 14:00 HRS SHEKH AMRI ABED
4. 5/10/2010 D/A Arusha V/S Mara 16:00 HRS SHEKH AMRI ABED

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Mara V/S Manyara 14:00 HRS SHEKH AMRI ABED
6. 12-May-10 D/B Arusha V/S Kilimanjaro 16:00 HRS SHEKH AMRI ABED

GROUP 'E' - IRINGA
(a) Iringa
(b) Mbeya
(c) Rukwa
(d) Kinondoni

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Rukwa V/S Mbeya 14:00 HRS SAMORA ST.
2. 5/8/2010 C/D Iringa V/S Kinondoni 16:00 HRS SAMORA ST.

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Mbeya V/S Iringa 14:00 HRS SAMORA ST.
4. 5/10/2010 D/A Kinondoni V/S Rukwa 16:00 HRS SAMORA ST.

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Rukwa V/S Iringa 14:00 HRS SAMORA ST.
6. 12-May-10 D/B Kinondoni V/S Mbeya 16:00 HRS SAMORA ST.


GROUP 'F' - MTWARA
(a) Mtwara
(b) Lindi
(c) Ruvuma
(d) Ilala

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Lindi V/S Ruvuma 14:00 HRS NANGWANA ST.
2. 5/8/2010 C/D Mtwara V/S Ilala 16:00 HRS NANGWANA ST.

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Ruvuma V/S Mtwara 14:00 HRS NANGWANA ST.
4. 5/10/2010 D/A Ilala V/S Lindi 16:00 HRS NANGWANA ST.

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Lindi VS Mtwara 14:00 HRS NANGWANA ST.
6. 12-May-10 D/B Ilala VS Ruvuma 16:00 HRS NANGWANA ST.



FIXTURE KILI TAIFA CUP - 2010
QUARTER, SEMI FAINAL AND FAINAL
KILIMANJARO TAIFA CUP 2010
FROM 23 MAY, 2010 TO 29 MAY, 2010
UHURU STADIUM - DAR ES SALAAM

SN - DATE - TEAMS - TIME - GROUND
QUARTER FINAL

1. 23 May, 2010 WINNER GROUP 'A' V/s WINNER GROUP 'B' 14:00 HRS UHURU ST - DSM
2. 23 May, 2010 WINNER GROUP 'C' V/s WINNER GROUP 'D' 16:00 HRS UHURU ST - DSM
3. 24 May, 2010 WINNER GROUP 'E' V/s WINNER GROUP 'F' 14:00 HRS UHURU ST - DSM
4. 24 May, 2010 WINNER GROUP 'G' V/s WINNER GROUP 'H' 16:00 HRS UHURU ST - DSM

SEMI FAINAL

5. 25 May, 2010 WINNER GROUP 'A' V/s WINNER GROUP 'B' 16:00 HRS UHURU ST - DSM
6. 26 May, 2010 WINNER GROUP 'C' V/s WINNER GROUP 'D' 16:00 HRS UHURU ST - DSM

27 May, 2010 REST DAY

7. 28 May, 2010 LOOSER No. '5' V/s LOOSER No. '6' 16:00 HRS UHURU ST - DSM
8. 29 May, 2010 WINNER GROUP '5' V/s WINNER GROUP '6' 16:00 HRS UHURU ST - DSM

OKINAWA GOJU RYU KARATE - DO - JUNDOKAN KURO OBI KAI DOJO WAADHIMISHA MIAKA 37 TANZANIA

OKINAWA GOJU RYU KARATE - DO - JUNDOKAN KURO OBI KAI DOJO waadhimisha miaka 37 tangu kuanzishwa kwa dojo hilo mwaka 1973 na Sensei Nantambu Camara Bomani.Hii ni picha ya muasisi wa mchezo huu hapa Tanzania Sensei Nantambu Camara Bomani.Hawa ndiyo wanaoendeleza mchezo huu wa GOJU RYU katika dojo ambalo Sensei Bomani alianzisha mchezo huu nchini Tanzania katika shule ya msingi ya Zanaki ya Jijini Dar es Salaam.Hawa ni wale ambao wanamikanda myeusi wakionyesha namna ambavyo mtu anaweza kupambana na mtu mwenye kisu na ukamshinda, aliyelala chini ndiye mwenye kisu.Hawa ni wale wenye mikanda ya Kijani wakionyesha umahiri wao katika mchezo wa Goju Ryu ama unaweza ukaiata sanaa ya mipigano.Hawa ni wale ambao wanakaribia kuwa na mkanda Mweusi wakionyesha umahiri wao katika sanaa ya mapigano.Huyu ni Japhet Kaseba Bingwa wa Kick Boxing wa WK1 Dunia naye akifuatilia kwa makini.Mdau mwenzangu huyu Ankal Michuzi naye akifuatilia kwa ukaribu namna mtu anavyoweza kupigana kwa ustadi bila kutumia silaha, au siyo Brother Michuzi...???Waliyo kaa chini ndiyo ambao walitunukiwa mikanda ikiwa ni ishara ya kupandishwa ngazi katika mchezo huo, huku mmoja akipewa mkanda mweusi, aliyesimama kulia ni Sensei Rashid Almasi na aliyening`iniza mewani watano toka kulia ni Sensei Wilfred Malekiu.

J-MARTIN AWASILI BONGO TAYARI KWA BURUDANI YA ZAIN

Mwanamuziki kutoka Nigeria J-Martins kulia akiongea wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere. Msanii huyo ambaye yuko nchini kwa mwaliko wa Kampuni ya simu za mkononi ya Zain alitarajia kufanya onyesho jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja uhusiano wa Zain Muganyizi Mutta.

Monday, April 19, 2010

ZAIN YASAIDIA ELIMU, YATOA VITABU VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 4 TANGA

Mkuuu wa wilaya ya Lushoto Sophia Mjema (katikati) akimkabidhi Frank Glibety mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Kisaba iliyopo wilayani humo vitabu vyenye thamani ya Shilingi milioni 2 ambavyo vimetolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Zain kupitia mradi wake wa “Build Our Nation”. Kwa ajili ya shule hiyo ya Kisaba na shule ya sekondari ya Vugabazo mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Zain, Muganyizi Mutta.

Mkuu wa wilaya ya Lushoto Sophia Mjema (katikati) akimkabidhi Juma kibwana mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Vugabazo iliyopo wilayani humo wiki hii. Vitabu vyenye thamani ya Shilingi milioni 2 ambavyo vimetolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Zain kupitia mradi wake wa “Build Our Nation”. Kwa ajili ya shule hiyo ya Vugabazo na shule ya sekondari ya Kisaba mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Zain, Muganyizi Mutta.

SIMBA OYEEEEEEEEEEE.......



Nahodha wa Simba Nicodemus Nyagawa (kushoto ) na mlinzi wa timu hiyoJuma Jabu wakishangilia huku wakiwa wambeba Kombe la Ubingwa wa LigiKuu ya Bara mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaamjana.Katika mchezo huo Simba iliicharaza Yanga mabao 4-3. (Picha naMohamed Mambo)
Mbali na ushindi huo Simba ilikuwa inakabidhiwa kombe lake mara baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi kuu ya Vodacom msimu huu bila kufungwa hata mchezo mmoja ambapo imeshinda michezo 19 imedroo miwili na bado ina mchezo mmoja mkononi wa kukamilisha ratiba dhidi ya Mtibwa Sugar ya Manungu Mkoani Morogoro.
Katika mchezo wa jana wachezaji watatu walipewa kadi nyekundu ambao ni Wisdom Ndlovu na Amir Maftaha wa Yanga baada ya kucheza mchezo mbaya dhidi ya wachezaji wa Simba Salm Kanoni na Juma Kaseja wakati Hilary Echesa wa Simba alipewa kadi nyekundu baada ya kuvua jezi alipokuwa akishangilia goli la nne alilofunga dhidi ya Yanga.

Thursday, April 15, 2010

ULINZI YASHIKILIA USUKANI LIGI KUU YA KENYA

Klabu ya ligi kuu ya Kenya Ulinzi Stars na Mathare United ndiyo klabu pekee ambazo hazijapoteza mchezo tangu kuanza kwa msimu wa ligi mapema mwezi Februari.

Hata hivyo klabu hizi mbili zimeachana kwa tofauti kubwa ya pointi ambapo klabu ya Ulinzi inashikilia usukani wa ligi huku Mathare ikishika nafasi ya 5.

IKiwa tayari imechezwa michezo nane hadi sasa katika ligi kuu ya Kenya, Ulinzi Stars inaongoza ikiwa na jumla ya pointi 18, ikiwa ni pointi mbele dhidi ya Tusker FC inayoshika nafsi ya pili.Sofapaka inashika nafasi ya 3 ikiwa na jumla ya pointi 14. Sony Sugar inashika nafasi ya 4 huku ikiwa na point 13 wakati Mathare United ikiwa na pointi 12 ikilala nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi.

Gor Mahia inashika nafasi ya 6 ikilingana pointi na klabu ya Mathare United lakini wakitofautiana magoli ya kufunga wakati Nairobi City stars, Western Stima na Sher Karuturi Sports zinashika nafasi ya 7, 8 na 9 zikiwa na pointi 11 kila moja. klabu ya KCB maarufu kwa jina la The Bankers wanahitimisha kumi bora wakishika nafasi ya kumi katika msimamo ikiwa na pointi kumi baada ya michezo ya wikiendi.

Wakati huo huo, Kongowea imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kanda ya Pwani katika michuano ya Copa Coca Cola (Coast Province 2010 COPA Coca-Cola) baada ya kuichapa Gede FC 5-4 kwa mikwaju ya penati katika mchezo uliyopigwa katika dimba la Manispaa ya Mombasa.

Kwa upande wasichana, Furaha Ladies inashika nafasi ya kwanza, baada ya kuichapa Mwakitawa Ladies 1-0.

Jijini Nairobi, kipute kilipigwa Posta Grounds ambapo Indomitable FC ilitwa ubingwa wa jumla baada ya kuichapa Korogocho Youth 3-2 kwa mikwaju ya penati wakati wasichana, Dhapks United walitawazwa mabingwa baada ya kuitoa Pioneer Girls kwa goli la ugenini.

mabingwa waliondoka na kitita cha Shilingi za Kenya 30,000 na kila mshindi wa pili aliweka kibindoni Shilingi za Kenya 20,000.

RENARD AWEKA MIPANGO YA 2012 MATAIFA YA AFRIKA

Kocha mpya wa timu ya taifa ya Angola Herve Renard amejiwekea malengo ya kutaka kufuzu kucheza mataiafa ya Afrika mwaka 2012 kuwa ni kiwango cha kati katika malengo ya mafunzo kwa Palancas Negras.

katika mahijiano yaliyofanyika nyumbani kwake mjini Luanda, Mfaransa huyo amewaomba wananchi wa Angolan kuwa na subira katika kipindi hiki, na kusema "much work to be done" kuijenga upya timu ya taifa ya Angola.

Kocha huyo wa zamani wa Zambia wiki iliyopita alitajwa kuchukua nafasi ya kocha Manuel Jose, Mreno ambaye aliiongoza Angola katika fainali za mataifa ya Afrika mwezi januari.

Jose aliondoka baada ya tumaini la Angola la kutwaa uchampion wa mataifa ya Afrika kutoweka huku michuano ikipigwa katika ardhi ya nyumbani, walitolewa katika hatua ya robo fainali na timu ya taifa ya Ghana.

CARLOS TEVEZ, WAYNE ROONEY, CESC FABREGAS NA DIDIER DROGBA KUWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA MWAKA

Carlos Tevez, Wayne Rooney, Cesc Fabregas na Didier Drogba wametajwa kuwania tuzo ya mwanasoka bora wa mwaka inayotolewa na na chama cha wachezaji wa kulipwa (PFA Player of the Year award).

Rooney ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kutwaa tuzo hiyo.

Nyota huyo wa Manchester United amekuwa na wakati mzuri msimu huu, ingawa inaonekana kanakwamba mafanikio ya kusonga mbele katika michuano ya Carling Cup kudoda. Rooney amefunga jumla ya magoli 34 akiwa na klabu yake ya Man United msimu huu katika michuano yote na yeye mwenyewe kkujitaja kuwa ni moja ya wachezaji wenye kipaji Duniani.

Klabu ambayo msimu huu imekuwa tishio katika ligi kuu ya England, Manchester City inawakilishwa na Carlos Tevez, ambaye naye tangu ajiunge na klabu hiyo ni mwenye mafanikio na kufanikiwa kufunga jumla ya magoli 28 katika michuano yote.

Kama Rooney, Nyota wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas amechaguliwa kuwania tuzo mbili ikiwa ni tuzo kuu ya mwanasoka bora na tuzo ya mwanasoka chipukizi wa mwaka.

Ingawa amekuwa akikalia benchi muda mwingi msimu huu akiuguza maumivu, Fabregas amekuwa chachu ya ushindi katika michezo mingi ya klabu hiyo ya washika bunduki.

Wakipewa jina la muda, yaani Mabingwa wateule, Chelsea inawakilishwa na Didier Drogba licha kutofanya vizuri sana kama ilivyokuwa mwaka uliyopita, lakini bado anatajwa kuwa ni mwiba katika lango la wapinzani.

Aston Villa inawakilishwa na James Milner na Birmingham City inawakilishwa Joe Hart ambao wanawania tuzo mwnasoka mdogo pamoja na Rooney na Fabregas

Wednesday, April 14, 2010

SBL YAIKABIDHI NGORONGORO HEROES MILIONI 83/


Meneja uhusiano Habari na Mawasiliano wa Serengeti SBL Teddy Mapunda kulia akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Kapteni wa timu ya Vijana Ngorongoro Heroes Himid Mao kwenye ofisi za shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF leo, katikati ni kocha mkuu wa timu hiyo Rodrigo Stokla na mwisho kushoto ni Matadi Yasoda Kaimu mkurugenzi Idara ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo.


Kampuni ya bia ya Serengeti SBL leo imetoa jumla ya shilingi milioni 83 kwa shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF ili kufanikisha maandalizi ya timu ya taifa ya vijana Ngorongoro Heroes chini ya Umri wa miaka 20 katika maandalizi ya safari yao kwa ajili ya mchezo wake na timu ya vijana ya nchini Malawi.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja uhusiano habari na Mawasiliano wa kampuni hiyo Tedd Mapunda amesema katika fedha hizo shilingi milioni 50 ni fedsha taslimu kwa ajili ya masuala ya utawala na shilingi milioni 25 kwa ajili ya kulipia tiketi na shilingi milioni 8 zimetumika kwa ajili ya vifaa vya michezo kwa timu hiyo.

"Kama ambavyo tumekuwa tukisaidia michezo tumeona tuisaidie timu hii ya vijana chini ya miaka 20 kwani tunaamini msaada huu utasaidia kujenga na kuimarisha kikosi bora cha timu ya taifa miaka michache ijayo" amesema Tedy Mapunda.

Ameongeza kuwa tunawatakia Ngorongoro Heroes mafanikio katika mchezo wao huo utakaofanyika katika jiji la Blantyre nchini Malawi na tuna imani kuwa watarudi na ushindi hivyo kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania, Ngorongoro Heroes inatafuta tiketi ya kushiriki kombe la mataifa ya afrika kwa timu za vijana chini ya umri wa miaka 20 katika fainali zinazotarajiwa kupigwa nchini Misri mwaka 2011.

Kampuni ya bia ya Serengeti SBL ni mdhamini mkuu wa timu ya taifa ya mpira wa miguu Taifa Stars kwa miaka kadhaa sasa na chini ya udhamini huo mafanikio ya timu ya taifa yamekuwa yakiongezeka mwaka hadi mwaka hivyo SBL wanastahili kupongezwa kwa udhamini huo.

TIMU YA TAIFA YA VIJANA U-20 KUONDOKA KESHO

TIMU ya Taifa ya vijana chini ya miaka 20 Ngorongoro Heroez leo imekabidhiwa bendera ya taifa na Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya michezo Juliana Matagi Yasoda ikiwa ni ishara ya kikosi hicho kwenda kuiwakilisha nchi kwenye mchezo wa awali wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Africa kwa vijana dhidi ya Malawi,mchezo utakaopigwa Jumamosi huko Malawi.

Ngorongoro Heroes itaondoka kesho ikiwa na jumla ya wachezaji 20 na viongozi saba msafara utakaoongozwa na mwenyekiti wa maendeleo ya soka la Vijana Alhaji Ahmed Msafiri Mgoyi.

Akizungumza baada ya kukabidhi bendera Matagi Yasoda amewataka vijana hao kurudi na ushindi.

Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF Leodger Tenga amesema kikosi hicho ndio Taifa Starz ya baadaye.

WACHEZAJI WATAKAOONGOKA KESHO NI
1. KHOMEINY ABUBAKARI
2. AMANI KYATA
3. LEORNAD MUYINGA
4. TUMBA SWEDI
5. KIBANDA JUKUMU JOAKIM
6. HIMID MAO
7. ISSA RASHID ISSA
8. JOHANES SALVATORY
9. ABUU UBWA ZUBERI
10. FURAHA YAHAYA TEMBO
11. THOMAS ULIMWENGU
12. SALUM ABDULL TELELA
13. ABDALLAH BUNU
14. MBWANA SAMATA
15. YUSUPH SOKA
16. RAJABU ISIHAKA ABDALLA
17. MOHAMMED HAMIS THABIT
18. OMEGA SEME
19. SALUM ABUBAKARI
20. SWALEHE KABARI FARAJI

KILA LA KHERI U-20

MECHI YA SIMBA NA YANGA PRESHA TUPU

Watoto wa Jangwani Yanga wametamba wako kwenye morali ya juu kuua mnyama hapo Jumapili kwenye uwanja wa Taifa mchezo utakaopigwa usiku saa 2.

Afisa habari wa Yanga Luis Sendeu amesema kikosi kiko imara na kinaendelea na maandalizi yake vizuri huku leo wakipokea wachezaji wawili wa kigeni wanaotokea nchini Ghana waliokuja kufanya majaribio.

Wakati Watoto hao wa Jangwani wakijinadi hivyo huko Msimbazi nao wanasema wako tayari kuwatia kitanzini watoto hao wa Jangwani.

Meneja wa Simba Innocent Njovu anasema wako kamili na kocha Patrick Phiri anarejea kesho kuwaongezea nguvu zaidi.

TUFANYE MAZOEZI KUJENGA AFYA

Watanzania wameombwa kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio za hisani zinazotarajia kufanyika April 17 mwaka huu.

Kiongozi katika mbio hizo Meritus Magungu amesema mbio hizo ambazo zitakuwa ni matembezi mafupi zitafanyika mara kwa mara ili kujenga afya za vijana.

Matembezi hayo yataanzia tabata segerea na kumalizikia tabata Relini.

SHINYANGA KUJENGA SHULE YA MICHEZO

Mdau wa soka na mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja ameamua kujikita na kuwekeza kwenye sekta ya michezo nchini.

Mgeja amesema sasa ameamua kuwekeza kwenye sekta ya michezo akiwa na malengo ya kuanzisha kituo cha michezo kitakachoanza kujengwa mwezi ujao huko Shinyanga huku hii leo akikabidhi mipira kwa timu mbalimbali zikiwemo za Wilayani Maswa kwenye kata ya Kadoto.

TFF LAWAFUNGIA VIONGOZI, WACHEZAJI LIGI DARAJA LA KWANZA


KAMATI ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania TFF,limewaangushia rungu baadhi ya viongozi na wachezaji wa timu za Daraja la Kwanza kwa utovu wa nidhamu akiwemo Meneja wa Mwanza United, Evarist Hagira ambaye ametozwa faini ya sh. milioni 1 na ushee huku pia akifungiwa miezi sita kujihusisha na michezo.

Kamati hiyo ilikutana Jumamosi jijini Dar es Salaam kujadili mambo mbalimbali yanayohusu ligi daraja la kwanza.

Afisa Habari wa TFF, Frolian Kaijage, amesema baada ya kuitathimini ligi daraja la kwanza waligundua kuna kasoro zilizojitokeza katika baadhi ya michezo ya ligi daraja la kwanza.

Amesema katika mchezo namba 31, kati ya TMK United na Mwanza United, Kocha wa Mwanza United,John Tegete aliwashawishi wachezaji wake kugomea mchezo na kamati imeamua kumfungia miezi mitatu kujihusisha na masuala ya soka.

Amewataja baadhi ya wachezaji wa timu hiyo ambao pia wamekumbwa na rungu hilo la kufungiwa miezi mitatu kujihusisha na soka, kuwa ni pamoja na Hamis Ally, Paulo Joseph, Naftari Matari, Emmanuel Sitta na Othman Othman.

Kaijage amesema mchezo namba tano kati ya Watoto wa A town AFC ya Arusha dhidi ya Mwanza United, mashabiki wa AFC walimfanyia fujo mwamuzi baada ya mpira kumalizika, hivyo nayo AFC imetozwa faini ya Shilingi 150,000.

Ameongeza kuwa mchezo namba 12 kati ya Ruvu Shooting ya Pwani na Coastal Union ya Tanga, waamuzi wa mchezo huo Bamy Bahisha na Mustapha Abdi walichezesha chini ya kiwango, hivyo wamefungiwa miezi mitatu kujihusisha na masuala ya soka.

WATANO MBEYA WASHINDA TIKETI Coca-Cola KWENDA KOMBE LA DUNIA AFRIKA KUSINI


Mbeya Aprili 13, 2010... Promosheni ya Kwea Pipa na Coca-Cola inazidi kupamba moto ambapo wateja watano wa Coca-Cola mkoani Mbeya wamebahatika kushinda tiketi kwenda kushuhudia mechi ya fainali ya Kombe la FIFA la Dunia kati ya Brazil na Ureno itakayochezwa kwenye uwanja wa kisasa wa Moses Mabhida jijini Durban Juni 25, 2010.

Fainali za Kombe la FIFA la Dunia zimebeba uzito wa pekee barani Afrika mwaka huu kwa kuwa tamasha hili linalovuta hisia za mamilioni ya wapenzi wa mpira wa miguu duniani linafanyika kwa mara ya kwanza kwenye ardhi ya Afrika tangu kuanzishwa kwake 1930.

Washindi waliotangazwa jijini Mbeya hivi leo ni sehemu ya wateja wa Coca-Cola 200 ambao kampuni hiyo ya vinywaji baridi itawapeleka Afrika kusini kwenda kuungana na maelfu ya wapenzi wengine wa soka kutoka sehemu mbali mbali duniani kusherehekea kombe la dunia.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza washindi hao, Meneja Mauzo wa Coca-Cola Kwanza, Mkoani Mbeya, Bw.Francis Mroso aliwataja washindi hao kuwa ni Deogras L. Kapesa (43) mfanyabiashara wa Mlowo, Mbozi, Tujelimpoki Frank (24), mfanyabiashara kutoka Kyela, Raphael Paul Ngungwi (33), pia mfanyabiashara wa Makunguru, Mbeya.

Wengine in Ally David Kaisi (23) wa Nzovwe, Mbeya ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini na Kelvin Mallya (36) ofisa kutoka Ofisi ya Uhamiaji Tunduma, Mbeya. Waliobahatika kushinda TV aina ya Sony zenye muundo wa kisasa (flat screen) inchi 32 ni Benedicto George, Daniel Kisunga na Petrol Sanga wote wafanyabiashara.

“Tunafurahi kwamba watu wengi wemejitokeza kushiriki promosheni yetu ya Kwea Pipa na Coca-Cola: Shinda tiketi ukasherehekee Kombe la FIFA la Dunia ambayo inawapa fursa adimu Watanzania 200 watakaobahatika kushinda tiketi kwenda kutazama mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia”, alisema Mroso.

Mbali na tiketi za kwenda Afrika Kusini Coca-Cola pia itatoa zawadi mbali mbali kwa wateja 1,200,000 ikiwa ni pamoja na Televisheni ya muundo mpya (flat screen) aina ya Sony, fulana, kofia na soda za bure.

Ili kushiriki, wateja wanatakiwa kununua chupa zenye ujazo wa 300ml au 350ml za Coca-Cola, Sprite au Fanta na kuangalia chini ya kizibo kuona zawadi walizoshinda. Promosheni hii inafanyika katika mikoa yote ya nchi Tanzania hadi Mei 31 na washindi wataendelea kuchukua zawadi zao hadi Juni 15, 2010.

“Napenda kutoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kuburudika na vinywaji vya jamii ya Coca-Cola: Coca-Cola, Fanta au Sprite na kuweka hai matumaini ya kujishindia tiketi za kwenda kutazama mechi ya kusisimua ya kombe la dunia kati ya Brazil na Ureno”,
Alisema Mroso.

Coca-Cola imekuwa mstari wa mbele katika kuwawezesha Watanzania kushuhudia matukio makubwa ya kimichezo. Mwaka jana Coca-Cola iliwawezesha Watanzania kuliona Kombe halisi la FIFA la Dunia kwa mara ya pili baada ya kuliona mara ya kwanza 2006. Coca-Cola pia iliwawezesha Watanzania kuuona laivu Mwenge wa Olympiki 2008 pamoja na kuwa sehemu ya shamra shamra ya Mbio za Mwenge wa Olimpiki ambazo hutangulia michezo ya Olimpiki, ambayo pia ni michezo inayotambaa ulimwenguni kwa umaarufu.

Tuesday, April 13, 2010

ZAIN YAZINDUA MALIPO YA TSHS 1 SAA 24 - "UHURU WA KUONGEA"

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Zain yazindua Malipo ya Tshs 1 saa 24 - "Uhuru wa Kuongea"
.Ongea kwa Tsh 1 kwa sekunde siku nzima.
.Ongea kwa Tsh 1 kwa sekunde kwa dakika usiku kucha.
.Hakuna kujisajili, Hakuna kikomo cha muda, Hakuna Malipo yaliyofichwa, Hakuna kukatika simu hovyo, Hakuna Msongamano wa simu.

Zain, Kampuni inayoheshimika zaidi Tanzani na inayoongoza kwa ubunifu wa bidhaa na huduma, leo imezidi kudhihirisha umahiri wake katika soko kwa kuzindua mpango mpya wa malipo ya kupiga simu yenye viwango vya chini kuliko vyote nchini wa Tsh 1 kwa sekunde unaojulikana kama " Uhuru wa Kuongea".

"Ninayo fuaraha kubwa kuwatangazia kwmaba kuanzia leo wateja wetu waliyopo na wapya katika mpango wa malipo kabla, moja kwa moja watajiunga na mpango wa Ths 1 kwa sekunde saa 24 ikiwa ni pamoja na kuweza kupiga simu kwa kiwango nafuu kuliko vyote cha Tsh 1 kwa dakika baada ya dakika ya kwanza ya Uhuru wa Kuongea wakati wa usikku. Mbali na kutoa ubunifu wa kisasa wa kiteknolojia pamoja na kuwa na huduma bora zenye kuambatana na mtandao kuenea nchi nzima, Zain imejidhatiti kuongoza katika sekta ya mawasiliano kwa kuzidi kutoa viwango nafuu zaidi kwa wateja wetu, na ndiyo maana tumezindua Uhuru wa Kuongea ikiwa ni kutambua mahitaji ya soko la huduma ya simu na kuzingatia unafuu. Hakuna kujisajili, wala gharama za kuhama kutoka mpango mmoja kwenda mwingine, tunaposema "Uhuru wa kuongea" tunamaanisha hicho hicho," Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania Khaled Muhtadi.

Zain imeamua kuwa wazi na bayana, hakuna haja ya kujiunga, wasiwasi wa muda, malipo yaliyofichwa wala simu kukatika katika kutokana na msongamano. Wateja wa Zain wataweza kujivunia Uhuru wa Kuongea kwa urahisi kabisa saa 24 siku zote za wili wakiwa na uhakika wa mtandao madhubuti na ulioenea nchi nzima.

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa usinduzi wa mpango huo mpya wa malipo Jijini dar es Salaam, Mkurugenzi wa masoko wa Zain Tanzania Ahsan Syed alisema, "Zain imewekza zaidi ya dola za Marekani milioni 500 katika miundo mbinu ya mawasiliano katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kuhakikisha tunawapa wateja wetu huduma bora ya viwango nafuu popote pale walipo nchini. Mpango wetu wa malipo ya Ths 1 ni rahisi na hauna mkanganyiko wowote na ni kwa saa 24 kwa siku. Muda wa usiku kati ya saa tano usiku hadi saa moja Alfajiri, wateja wa Zain watapiga simu kwa viwango vya chini kabisa kwa Tsh 1 kwa dakika baada ya dakika moja ya kwanza. Wateja wa Zain hawatalazimika kuangalia saa zao za mkononi au ukutani kujua kama wako katika muda wa viwango vya malipo ya Tsh 1, na hii ndiyo inatutofautisha na makampuni mengine."

"Tunatambua kwamba kufanikisha kupatika mawasiliano ni eneo ambalo tunatoa mchango mkubwa kwa jamii na kuchangia kushamiri kwa uchumi wa Tanzania. Simu za mkononi zina mchango mkubwa katika uchumi wetu na ndiyo sababu siyo tu kwamba tunaleta bidhaa zenye ubunifu mkubwa lakini pia tunahakikisha mtandao wetu ni wa kutegemewa na uliyosambaa maeneo mengi zaidi nchini Tanzania. Pia tumesambaza mtandao wetu na bidhaa zetu nchi maeneo mengi vijijini ili kuwawezesha mamilioni ya watu wanaoishi maeneo ya vijijini kuwasiliana na ndugu zao wanaoishi mjini na kuwapunguzia adha mbali mbali zinazosababishwa na umbali. kupitia Uhuru wa Kuongea, Zain inazidi kuwathibitishia wa Tanzania maana halizi ya Ulimwengu maridhawa" Mkurugenzi wa Mtandao wa Zain tanzania Thierry Diasonama alisema.

YANGA WAIFUATA SIMBA ZANZIBAR

Watoto wa Jangwani Yanga siku ya Jumatatu wamekwea boti kuelekea kisiwani Unguja Zanzibar kumtembelea mama Karume huku wakiichukulia siku hiyo kama ya mapumziko.

Kocha wa Yanga MSerbia Kostadin Papic anasema safari hiyo ya Zanzibar ni moja ya maandalizi yao japo wengi wanaona ni kama mapumziko ya kutofanya mazoezi.

Papic anasema kwenda Zanzibar na kurejea kesho ni moja ya programme ya maandalizi yao huku akisema hata hivyo mchezo huo wa Jumapili hauna uzito mkubwa kwakuwa tayari Simba washatwaa uchampion huku Yanga ikiwa imeshakamata nafasi ya pili na matokeo yake hayatabadili lolote kwenye msimamo wa ligi.

Nahodha wa Yanga Abdi Kassim amesema kwao ni moja ya mapumziko lakini pia ni mazoezi kwao japo wako tayari kwa mchezo huo wa Jumapili dhidi ya mahasimu wao Simba.

Mahasimu wa Yanga katika soka, Wekundu wa Msimbazi Simba wao wamepiga kambi yao huko kisiwani Unguja Zanzibar kwaajili ya mchezo huo wa Jumapili.

KAMATI YA SIMBA YAKUTANA KUNYOA WAGOMBEA


Kamati ya uchaguzi ya klabu ya Simba imekutana leo kwenye uwanja wa Uhuru Dar Es Salaam kupitia majina ya wale wote walioomba ubosi ndani ya klabu hiyo.

Katika kikao hicho ambacho kilipitia kwa undani majina yote na kutazama kama wametimiza vigezo vyote vya kikatiba vinavyotakiwa kilikuwa kigumu na hatimaye kufikia kile kilichokuwa kikitakiwa.

Uongozi wa kamati hiyo chini ya Damas Ndumbaro wamesema hapo Jumanne saa 6 mchana ndipo watatoa taarifa rasmi za wagombea wote waliotimiza vigezo vinavyotakiwa vya kuwania ubosi ndani ya klabu hiyo.

Hata hivyo taarifa zisizorasmi zinasema kuwa mwenyekiti wa sasa ambaye anatetea kiti chake Hassan Dalali ametemwa.

JULIUS MBILINYI ANG`ARA GOFU YA ZAIN


Julias Mbilinyi ameng’ara katika mashindano ya mchezo wa gofu yanayodhaminiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Zain Tanzania yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Lugalo jijini Dar es Salaam baada ya kupata pointi 39.

Jualias alifuatiwa na Ali Mufuruki ambaye naye pia alijikusanyia pointi 39 lakini Julias alimzidi mpinzani wake katika tofauti ya viwango vya uchezaji.

Kufuatia ushindi huo Julias na Mufuruki walijinyakulia zawadi mbalimbali ikiwemo mwavuli na kalamu, Vyote vikiwa na nembo ya Zain kutoka kampuni ya Zain ambao ndiyo wadhamini wakuu wa mashindano hayo.

Mashindano hayo ambayo uchezwa katika makundi tofauti yalishuhudia washindi wengine kutoka katika kundi la akina mama pamoja na kundi la vijana wa kike na wa kiume.

Kundi la akina mama liliongozwa na Lina Nkya aliyepata pointi 17, kundi la vijana wa kike liliongozwa na Sara Denis aliyepata pointi 31. Akina mama na vijana wa kike walijishindia khanga za Zain.

Kundi la vijana wa kiume liliongozwa na Joshua Amoni aliyepata pointi 37 akifuatiwa na Baraka Masari aliyepata pointi 37, lakini wakatofautiana katika viwango vya uchezaji. Washindi hawa walizawadiwa kalamu za Zain pamoja na miavuli ya Zain.

Kampuni ya simu za mkononi ya Zain Tanzania ina mkakati maalum kwa kushirikiana na klabu ya mchezo wa gofu ya Lugalo ya jijini Dar es Salaam wenye lengo la kukuza mchezo wa gofu kuanzia kwa vijana wadogo ili kukuza vipaji.

CHEKA AMTAKA TENA KASEBA

Bingwa wa dunia Francis Cheka amesema ukimya wake una maana kubwa akijiiandaa na pambano lolote litakalokuja mbele yake huku akiweka bayana yu tayari kurudiana na bingwa wa kickboxing wa WKL na WKC Japhet Kaseba.

Cheka amesema yu tayari wakati wowote kurudiana na Kaseba kama atakuwa radhi kushuka naye ulingoni.

Saturday, April 3, 2010

SIMBA KURUDI DSM JMOS, KADUGUDA AJITOSA UCHAGUZI SIMBA


Wekundu wa Msimbazi Simba wanarejea Jumamosi kutoka kwenye marashi ya karafuu huko kisiwani Unguja Zanzibar wakisema wako tayari kupeperusha Bendera ya Tanzania hapo Jumapili kwenye mchezo wao wa marejeano kombe la shirikisho dhidi ya Lengthens ya Zimbabwe.

Meneja wa Simba Innocent Njovu amesema kikosi kiko vizuri licha ya kuwa majeruhi Kelvin Yondan Mbuyi na David Naftal Tevelu.

Wapinzani wa wekundu hao Lengthens waliokuwa watue Ijumaa sasa watatua Jumamosi jioni kwa ndege ya Kenya Airways KQ.

Kwenye gazeti la The HERALD la Zimbabwe nahodha wa kikosi hicho amesema wanafahamu kuwa Simba watatumia mbinu zote chafu wakati watakapofika lakini wachezaji wanafahamu na wanajiamini kuiondoa Simba nje ya michuano hiyo ingawa waliwafunga mabao 3-0 kwenye ardhi ya nyumbani kwao.

Sehemu ya taarifa hiyo inasomeka We are fully aware that Simba will Employ all dirty tactics as soon as we arrive but the players are oozing with confidence to knock out Simba on there home land despite having sufferd a big 3-0 on our home land
Wakati huohuo Ikiwa imeingia siku ya pili ya kuchukua fomu za kuwania ubosi ndani ya klabu ya Simba mwanachama maarufu na aliyewahi kuwa bosi wa Shirikisho la soka nchini TFF wakati huo ikifahamika kama FAT Alhaji Ismail Aden Rage naye leo amejitosa kuwania kuiongoza klabu hiyo.

Rage amechukua fomu ya kuwania nafasi ya mwenyekiti akiwa ni wa pili kwenye nafasi hiyo baada ya Mohamed Nanyali kufanya hivyo jana lakini akiwa mwanachama wa nne kufanya hivyo baada pia ya hapo jana Geofrey Nyange Kaburu na Mwina Mohamed Seif Kaduguda kufanya hivyo.

Nafasi zinazowaniwa ndani ya klabu hiyo ni Nafasi ya Mwenyekiti,makamu mwenyekiti na wajumbe saba wa kamati ya utendaji huku zile za juu zikilipiwa kwa kiasi cha shilingi laki 2 kila moja na zile za ujumbe zikilipiwa kwa kiasi cha shilingi laki 1.

Uchaguzi wa klabu hiyo unataraji kufanyika May 9 mwaka huu.

YANGA - HATUMBANII TEGETE

UONGOZI wa Dar es Salaam Young African maarufu Yanga umesema hauna mpango wa kumbania Mshambuliwa wao Jerrson Jerry Tegete kusukuma gozi la kulipwa nchini Sweden kwenye klabu ya DULKUD FF ya Sweden.

Afisa habari wa Yanga Luis Sendeu amesema wanataka mchezaji wao arudi kwanza halafu ndio mambo mengine yatafuata baadaye.

Amesema wao ndiyo waliyomruhusu kwenda kufanya majaribio wakiwa wanaamini atafanikiwa kutokana na kiwango chake lakini makubaliano yalikuwa ni lazima arejee baada ya kumaliza majaribio awe amefanikiwa ama la.

Sendeu amesema kumtaka arejee nchini kwanza inatokana na wao kutaka kujua aina ya mkataba ambao wataingia na klabu hiyo kwa mkopo lakini pia kufahamu klabu ya Yanga itafaidika vipi na mchezaji huyo ikiwa na maslahi ya mchezaji mwenyewe.

Wakala wa wachezaji Mzalendo Damas Ndumbaro aliweka bayana kuwa watoto hao wa Jangwani wamekataa Tegete kucheza kwa mkopo kwenye klabu hiyo ya Dalkud FF kiasi cha nafasi yake kupewa Uhuru Suleiamn wa Simba.

TIMU ZA VETERANI SAIDIENI VIJANA KUKUZA MICHEZO

Timu ya soka ya WAZEE Sports ya Zanzibar iliyotua JIJINI ikutokea visiwani Zanzibar kwa michezo ya Pasaka kwa mwaliko wa timu ya Survey Veteran imelazimisha sare ya kufungana mabao 3-3 na timu ya TANZANIA STARZ kwenye mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Leaders Club.

Timu hiyo leo Jumamosi itashuka dimbani kukipiga na timu ya waandishi wa habari za michezo TASWA FC kwenye uwanja wa Posta Kijitonyama kabla ya kukipiga na Mbezi Veteran jioni kwenye uwanja wa IMTU.

Timu hiyo yenye maskani yake huko visiwani Zanzibar itashuka dimbani kucheza na wenyeji wao SURVEY VETERAN hapo Jumapili asubuhi kwenye uwanja wa KINESI urafiki Ubungo.

Survey Veterans iko kwenye maandalizi makali ikijifua kwa mchezo huo ambao ndio utakuwa hitimisho la ziara hiyo ya WAZEE Sports,ziara ya kirafiki ambayo imekuwa ni ya kubadilishana na kutembelean kila mwaka wakati wa Pasaka ambapo mwaka jana Survey Veteran walikwenda Zanzibar.

NGUMI - MASHABIKI THUDHURIE KAMA TUNAVYOKWENDA KATIKA SOKA

Mashabiki wa masumbwi wameombwa kujitokeza kwa wingi katika tamasha la Michezo la Pasaka linalotaraji kufanyika Jumapili wiki hii kwenye Ukumbi wa Rungwe jijini Dar es Salaam.

Mwandaaji wa tamasha hilo Godfrey Madenge amesema Mbunge wa Viti maalum Chadema Halima mdee pamoja na bingwa wa dunia wa kickboxing wa WKL na WKC Japhet Kaseba wanatarajiwa kuwa wageni rasmi.

Aidha amesema lengo la kuandaa tamasha hilo ni kutoa burudani pamoja na kuibua vipaji vya soka kwa vijana.

Amesema vijana wa maeneo ya boko na Tegeta ni wapenda michezo lakini hakuna mtu ambaye anaweza kuwaandalia michezo hivyo ameona ni bora kuwapa furaha ambayo ataiendeleza kila mwaka.

Thursday, April 1, 2010

ZAIN NA MAZINGIRA


Mkurungenzi mkuu wa kampuni ya Zain Tanzania Khaled Muhtad, ofisa uhusiano wa kampuni hiyo Bwana Muganyizi Mutta wakishilikiana na wafanyakazi wa kampuni hiyo katika zoezi la kupanda miti kwenye Barabara ya Bagamoyo Dar es Salaam juzi kiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya uhifadhi wa Mazingira, Kauli mbiu ni ( Panda Miti tunza Mazingira)SIYO MAWASILIANO HATA KAZI ZA KIJAMII ZAIN TUPO