Tenga amesema michezo inanafasi kubwa ya kupambana na Maleria kufuatia kuhusisha watu wengi, lakini mchezo wa mpira licha ya kuchezwa dakika 90 hutajwa na kuzungumzwa zaidi ya dakika 90.
Tenga ametolea mfano mchezo wa Simba na Yanga licha ya kuchezwa Jumapili ya tarehe 18 lakini hadi leo bado unajadiliwa, hivyo kupambana na Maleria kupitia michezo itakuwa ni rahisi zaidi kuwafikia watu wengi zaidi pengine kuliko njia yeyote.
Amesema Tayari wamekwishaanza kutoa mafunzo kwa wachezaji wa timu ya taifa TAIFA STARS na wamewateua kuwa mabalozi wa MALERIA HAIKUBALIKI lakini pia wamewagawia vyandarua, wamefanya hivyo pia kwa timu ya U-20 pamoja na timu tisa zilizoshiriki ligi daraja la kwanza dhidi ya matumizi ya chandarua ikiwa ni kinga ya kwanza.
No comments :
Post a Comment