Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, December 31, 2009

WAZIRI MKUU MSATAAFU RASHIDI MFAUME KAWAWA AFARIKI DUNIA

RAIS JAKAYA KIKWETE AMETANGZA RASMI LEO KUHUSU KIFO CHA SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA MAPEMA ASUBUHI IKULU, JIJINI DAR. RAIS JK AMETANGAZA PIA SIKU SABA ZA MAOMBOLEZO KITAIFA AMBAPO BENDERA ZITAPEPEA NUSU MLINGOTI NCHI NZIMA. MAANDALIZI YA MAZIKO YANAENDELEA NA JK KAOMBA SUBIRA NA ITATANGAZWA WAKATI WOWOTE MAMBO YAKISHAKAMILIKA.MZEE KAWAWA AMEFARIKI AKIWA NA UMRI WA MIAKA 80.MZEE KAWAWA ALIKUWA MPENZI MKUBWA WA MICHEZO. HAPA AKIWA REFA KATIKA MCHEZO WA WABUNGE NA MAWAZIRI ENZI HIZOMZEE KAWAWA AKIWA NA TAIFA STARSMZEE KAWAWA ENZI ZA UHAI WAKE ALIPOTEMBELEA UWANJA MPYA WA TAIFA

MAMA YAKE AMANI MISANA NA DJ JUICE AZIKWA LEO

Amani Misana mwenye tisheti nyekundu Mtangazaji wa Radio Times akitoka katika kaburi baada ya kumlaza mama yake katika mwandani wa mapumziko ya milele katika makaburi ya Magomeni Jijini Dar es Salaam, Bi Asia ambaye nini Mama wa Amani Misana na Hussein Juma (DJ JUICE) ambao ni wafanya wa Radio TIMES FM, Alifariki jana mkoani TangaNdugu, Jamaa, Marafiki na Wafanyakazi wa Radio Times FM wakisaidia shughuli ya mazishi ya Mama yake Amani Misana mtangazaji wa Radio wa Times FM pamoja na DJ Juice.Amani Misana Mwenye tisheti nyekundu akishudia ndugu jamaa marafiki na watangazaji wa Radio Times Fm wakilihifadhi vema kaburi la mama yake, Bi Asia.Shekhe Akisoma Talakini mara baada ya mazishiEEEH MWENYEZI MUNGU ILAZE ROHO YA MAMA YETU ASIA MAHALA PEMA PEPONI AMINA!!!

Wednesday, December 30, 2009

TAIFA STARS - IVORY COST KARIBUNI MUONE

Wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars wakifanya mazoezi katika uwanja wa karume jijini Dar es Salaam ikiwa ni maandalizi ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Ivory Cost utakaopigwa hapo Januari 4 katika uwanja wa Taifa.
Mwenye mpira ni mchezaji wa kimataifa wa Tanzania anayeichezea klabu ya Vancouver Whitecaps ya nchini Canada, NIzar KhalfANI.
Timu ya taifa ya Ivory Cost inatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam siku ya Jumamosi ambapo itacheza michezo miwili, mchezao wa kwanza itacheza na Taifa Stars Januari 4 na mchezo wa pili itacheza na timu ya taifa ya Rwanda Januari 7.

KAWAMBWA - TANZANIA ITANUFAIKA NA FAINALI ZA DUNIA 2010

Jumla ya shilingi bilioni 7 zimetengwa na Serikali pamoja na Sekta binafsi kwa ajili ya maandalizi ya wageni watakaokuja Tanzania kabla ya kuanza kwa Michuano ya Kombe la Dunia litakaloanza mwezi Juni hapo mwakani Nchini Afrika Kusini.
Akizungumza na waandishi wa Habari katika ukumbi wa mkutano wa Wizara ya Miundo Mbinu,Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya FIFA Mheshimiwa Shukuru Kawambwa amesema kamati yake inayoundwa na Mawaziri 2 na Manaibu Waziri 3 imeandaa mikakati kabambe kuhakikisha wageni watakuja nchini kwa kuuona na kucheza katika Uwanja wetu Wataifa kabla ya kuanza Michuano hiyo mikubwa ya Kombe la Dunia.
Amesema hatua zilizochukuliwa ni pamoja na mkakati wa kitaifa wa kuhakikisha Tanzania inanufaiki na fainali za kombe la Dunia 2010, na kusema ikiwa ni kuvutia timu shiriki kuja hapa nchini kabla ya kwenda Afrika kusini ambapo tunaamini timu hizo za taifa zitakuja na mashabiki wake ambao watalazimika kulala katika mahoteli yetu lakini wanaweza kupata fursa ya kutembelea sehemu za utalii.
Amesema Kuandaa vivutio ambavyo vitawashawishi watalii ama mashabiki ambao watakuja hapa nchini kabla ya fainali na baada ya fainali za Dunia 2010.
Ameongeza kuwa njia nyingine itakayotumika ni pamoja na kutumia matangazo katika magazeti, tovuti, picha za video na vijarida mbali mbali ambavyo vitakuwa vikielezea vivutio vya utalii wa Tanzania.
Naye Raisi wa Shirikisho la Soka la Tanzania Leodga Chilla Tenga amesema mpaka sasa wanaendelea kuwasiliana na Nchi ambazo zitashiriki Michuano hiyo ambayo ni mara ya kwanza kufanyika Afrika ijapokuwa kuna ushindani wa hali ya juu katika kufanikisha hilo.

UJIO WA KIFIMBO CHANGAMOTO RT NA TOC

Waziri wa habari Utamaduni na michezo George Huruma Mkuchika ameipongeza Kamati ya Olimpic kwa jitihada zake za kuhakisha Tanzania inashiriki katika michuano ya Jumuiya ya Madola Oktoba mwakani Mjini Delh nchini India.
Mkuchika ameyasema hayo wakati wa mapokezi ya kifimbo cha malkia wa Pili wa Uingereza.
Mkuchika amesema kutoakana na heshima kubwa iliyoipata Tanzania kwa kukimbiza kifimbo hicho kwa misimu minne mfululizo na hivyo ana iamani kwamba itakuwa changamoto kwa wanamichezo na kuhakikisha wanafanya vizuri katika michuano ijayo.

TWENDENI TUKAISHANGILIE STARS

Watanzania wametakiwa kuiunga mkono Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars katika mchezo wake wa kirafiki na Ivory Coast hapo Januari 4 utakaofanyika katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam majira ya saa moja na nusu usiku.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa TFF Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka la Tanzania Fredrick Mwakalebela amesema timu ya Ivory Coast itawasili Jumamosi ya wiki hii ikiwa na msafara wa watu hamsini na watafikia hotel ya Kempisk.
Amesema Ivory Coast itacheza michezo miwili mmoja na Taifa Stars Januari 4 na mchezo mwingine itacheza na Timu ya Taifa ya Rwanda Januari 7 kwenye uwanja wa Taifa.
Akitaja viingilio vya mchezo huo Mwakalebela amesema viingilio vitakuwa ni vya aina saba tofauti, ambavyo ni Kijani mzunguko sh 5000, Bluu Mzunguko sh7000, Rangi ya Chungwa nyuma ya magori 10,000.
Rangi ya Chungwa mkabala na jukwaa kuu sh 20,000,
Viti maalum VIP C 30,000
Viti maalum VIP B 40,000
Viti maalum VIP A 50,000

HUU NI UUNGWANA?

Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwa wamejitokeza kwa uchache kusajili laini zao za simu Mitaa mbali mbali ya jiji la Dar es Salaam, baada ya kuongezewa muda wa miezi sita, kabla ya hapo watu waliyokuwa wakijitokeza ni wengi na kusababisha foleni kubwa. Jamani wa Tanzania kweli huu ni uungwana? kwanini kila siku mpaka dakika za mwisho ndiyo tuanze kusukumana? kwanini tusubiri mpaka siku ya mwisho? hivi kweli zoezi lingesitishwa tarehe 31 Desemba 2009 si tungeilaumu tena Serikali!!!(Picha na Rajabu Mhamila

MFAHAMU MALIKIA MPYA WA MUTWASHI

Abeti Masikini "The Nightengale of Zaire" alipokuwa akitamba enzi zake
*Mkali wa kike wa muziki kizazi kipya anayetisha sasa
*Ni baada ya akina mama kushindwa 'kuzalisha' vipaji
*JB Mpiana 'alizima' zake, amkubali kwa asilimia zote

katika safu hii ya wanamuziki na muziki wa Afrika, hasa wa nchini Kongo ambao kwa kiasi kikubwa umeteka soko la muziki karibu Afrika yote, nitazungumzia sauti za gharama za akina mama.
Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu ni kwanini wanamuziki wa kike, nyota waliowahi kuwika miaka ya nyuma nchini Kongo kutoka enzi ya akina Abeti Masikini hadi leo washindwe kuwarithisha kipaji hicho kwa mabinti wa kizazi cha sasa?
Hii imekuwa ni tofauti kubwa kwa upande wa wanaume, ukizungumzia kutoka enzi ya akina Dkt. Nico Kasanda, Luambo Rwanzo Franco Makiadi, uje enzi za akina Papa Wemba, Bozi Boziana, Aurus Mabele, Koffi Olomide, 'ushuke' kwa akina JB Mpiana, Werrason Makanda, Alain Mpela, na sasa wanaotamba katika kizazi kipya akina Ferre Gola 'Shetani' na Fally Ipupa.
Hao niliowataja wote nitawaelezea katika makala yatakayofuata baada ya haya, katika kuwachambua wanamuziki wa kiume wa Kongo, wakali na wenye sauti za gharama, kuanzia ya kwanza kama ya Mandal Chante, Lora Mwana Dindo na Papa Wemba hadi nzito za akina Madilu System, sasa nirudi kwa malkia hao wa Kongo.
Ni ukweli usiopingika kwamba wanamuziki wa kiume wamekuwa wakirithishana ama iwe rasmi, mfano kutoka kwa mzazi hadi mtoto kama ilivyo kwa Dindo Yogo aliyerithiwa na mtoto wake Lora Dindo Yogo, Vick Longomba aliyerithiwa na Lovy Longomba na Awilo Longomba, au urithi usio rasmi kwa maana ya kizazi cha wanamuziki kujizalisha chenyewe kihistoria.
Kama nilivyoeleza tumeshuhudia makundi mengi yakichuana na kuleta ushindani mkubwa wa muziki tangu enzi za akina Dkt. Nico hadi leo hii tunaendelea kushuhudia akina Fally Ipupa wanavyochuana na Ferre Gola na wengine wengi.
Hali hii iko tofauti kwa wanawake, ushindani uliokuwepo enzi ya akina Abeti Maskini, enzi ya akina Mbilia Bel alivyokuwa akilumbana na wifi yake M'Pongo Love na baadaye Faya Tess, leo hii hakuna.Meje 'MJ 30' aliyejitiwisha mikoba ya T Shala Mwana akimwaga radhi kwa kunengua bila nguo ya ndani (sehemu iliyozzibwa) ndiye anayekuja juu kwa sasa nchini Kongo.
Hakuna kizazi cha wanamuziki wa kike cha kujisifia tangu hao akina Mbila Bel na Tshala Mwana walipowika na kuondoka zao katika ushindani na sasa wakipiga muziki wa 'vilabuni' tu hata kama wanatoa albamu, lakini muziki wao si wa ushindani na wanaendelea kuwepo katika anga la muziki hata katika umri wao mkubwa ni kutokana na kukosa upinzani au ushindani wa kweli kwa wasanii wa kike wabichi.
Je, vipaji vyao hivyo vimerithiwa na akina nani? Hata kama si katika muziki wa dansi, tuzungumzie tu muziki wa kizazi kipya kama wa Zouk ambao kwa Wakongo (unapigwa na wanawake zaidi), nani anatisha? Ni wachache na zaidi nitakuelezea binti mmoja matata sana anayeibukia na kutisha katika fani hiyo kwa sasa.
Ni pengine ni kutokana na uhaba huo wa vipaji kwa upande wa watoto wa kike, na ndiyo maana wengi walikuwa wakifikiri kuwa, Monique Seka 'Queen of Afro-Zouk' ni raia wa Kongo, baada ya kutamba sana na albamu yake ya Missounwa.
Mwanamama huyu alitamba sana katika muziki wa Zouk, huyu ni mzaliwa wa Ivory Coast, alipoibukia katika anga la muziki, wengi walidhani ni 'toleo jipya' la muziki wa kizazi cha Kongo, lakini huyu ni raia wa Ivory Coast.
Ndiyo maana hapo juu nimeainisha kuwa akina mama hawa wa Kongo waneshindwa 'kuzalisha' kilicho bora kwa maana kushindwa kuibuka kwa mabinti wakali wa kizazi kipya katika muziki wa Kongo, lakini pia nikasema kuwa, hata kwa muziki wa kizazi kipya imekuwa tabu, kwa maana ni mwanamke gani kwa sasa nchini Kongo anayetamba kama ilivyo kwa akina Fally Ipupa, au kama ilivyokuwa enzi za akina M'Pongo Love?
Kwa sasa huyo anayetisha anajulikana zaidi kwa jina la Meje Bula 30 pia MJ 30. Binti huyu ni mkali wa miondoko ya Zouk, anatisha kama alivyokuwa anatisha Tshala Mwana katika miondoko ya Mutuashi, lakini binti huyu naye amekuwa akimwaga radhi na zaidi ya Tshala Mwana, yeye anacheza bila nguo ya ndani na kumwaga radhi!
Nadhani kama ni kumrithi Tshala Mwana, huyu atakuwa zaidi ya urithi. Ukiachilia mbali na huyo, binti mwingine ambaye naweza kusema ni wa muziki wa kizazi kipya ni Tata Muasi, huyu anafanya muziki wa rhumba na ni mwanamuziki pekee wa kike wa Kongo anayefanyakazi zake Uingereza.
Tata Muasi amejijengea umaarufu nchini Uingereza kiasi cha kuitwa 'Queen of African rumba' au Malkia wa rhumba la Kiafrika na hasa, baada ya kuachia albamu yake katika CD na DVD Novemba 3, 2007 inayojulikana kwa jina la Mimitah.
Ukiondoa wasanii hawa mabinti wawili wanaotesa kwa sasa, ambapo nitawazungumzia baadaye katika makala haya, zaidi ya hao hakuna, na labda tuangalie malkia wa Kongo katika uimbaji na hata unenguaji waliotamba tangu miaka ya 1960, wakati wa akina malakia Abeti Masikini.

*Abeti Masikini

Mkali huyu alizaliwa mwaka 1956, huko Kisangani, Congo (DRC). Kwa miaka 9 ya kwanza katika maisha yake, baba yake alikuwa akimfundisha kupiga kinanda (organ).
Kisha baadaye akaanza kuimba kwaya ya Kanisa la Kilomoto na katika matamasha yaliyohusisha familia. Uimbaji wake ulikuja baada ya yeye kuvutiwa na mwimbaji mmoja wa Kifaransa aliyeitwa Edith Piaf.Malkia wa miondoko ya Mutuashi, Tshala Mwana, picha ya kushoto alivyokuwa akitamba enzi za ujana wake na picha ya kulia ni ya juzi alivyotumbuiza hapa nchi Tanzania, Desemba mwaka huu alipokuja na JB Mpiana.
Juhudi zake Abeti, zilimfanya aweze kushinda mashindano ya vipaji ya kuimba yaliyoandaliwa na Piaf. Wengine waliomvutia hadi kujikita zaidi katika muziki ni wanamuziki wa kike Miriam Makeba wa Afrika Kusini na Mireille Matheiu wa Ufaransa.
Ushindi alioupata katika mashindano ya vipaji ya uimbaji yalimfanya Abeti ajulikane sana jijini Kinshasa na muda mfupi akapachikwa jina la kisanii na kuanza kuitwa "the Nightengale of Zaire".
Mwaka 1971, alikutana na mtengeneza muziki (prodyuza) raia wa Togo aliyeitwa Gerard Akueson. Akueson alikuwa akifanya kazi na msanii Bella Bellow, mwanamuziki wa Togo, ambaye ndiye aliyekuwa anamrekodia kazi katika studio yake.
Baada ya kukutana na prodyuza huyo, akajikuta akiimarika zaidi katika muziki wa Kiafrika hasa katika miondoko ya 'soukous parfume' na baadaye rhumba.
Mwaka 1972 alialikwa na Bruno Coquatrix, kufanya onesho katika ukumbi wa L'Olympia, Ufaransa na mambo aliyofanya katika onesho hilo yalikuwa ni makubwa na kuwa chanzo cha mafanikio yake katika muziki.
Katika onesho hilo la mafanikio, Abeti 'alikamua' ipasavyo mbele ya watazamaji wapatao 3,000, waliohudhuria na huo ukawa mwanzo wa mafanikio yake makubwa.
Mwaka 1974 akachaguliwa kuwa balozi wa Umoja wa Mataifa (UN), kutokana na kufanya vizuri katika albamu yake ya 'Bibile' kwa ushirikiano mkubwa na Gerald Akueson.
Maonesho mengine yaliyompatia heshima kubwa mwanamuziki huyu ambaye hapa Tanzania anafahamika zaidi kwa kibao chake cha 'Makayabu' ni aliyoyafanya China, hasa wakati wa mgomo wa Tien An Men Square mwaka 1989.
Hata hivyo maisha ya msanii huyu yalikomaa mwaka 1991, Abeti alifia jijini Paris, Ufaransa baada ya kuugua kwa muda mrefu na ilizuliwa kuwa msanii huyo alikufa kwa maradhi ya UKIMWI, japo hakuna taarifa zilizo rasmi kuhusu tetesi hizo.
Albamu yake ya Souvenirs Souvenirs ilitolewa miaka mitano, baada ya yeye kufariki, ilitolewa chini ya lebo ya Blue Silver katika CD mwaka 1996. Albamu zake nyingine ni Bibile ya mwaka 1975, 10e anniversair, 1er best of, En Colere, Je suis fache na Scandale de jalousie.
Kwa kifupi huyo ndiye Abeti Masikini, mmoja wa malkia wa Kongo aliyekuwa na kipaji au sauti ya gharama ambayo bado haijarithiwa na wasanii mabinti waliokuja au wanaoendelea kuja baada ya yeye kutoweka. Pengine katika muktadha huo, tumtupie jicho msanii, malkia mwingine wa Kongo aitwaye M'Pongo Love.

Je wanamuziki wa Tanzania tunajifunza nini hapa?
SOMA GAZETI LA MAJIRA KILA SIKU

SIMBA NA YANGA KUKUTANISHWA KATIKA MASUMBWI

BONDIA Rashid Matumla mshabiki wa timu ya Simba na joseph Marwa mshabiki wa timu ya Yanga (kg 76) wametamba kuoneshana kazi katika pambano lao la kirafiki litakalofanyika 1 januar 2010 katika uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Akizungumza kwa njia ya simu Marwa amesema atampa Matumla kichapo ambacho ajawai kuchapwa tangia ahanze ngumi kwani anajiamini kwa mazoezi aliyofanya nae Matumla amesema kuwa anasubili siku itimie tu kwani yeye ni mtu wa vitendo na si vinginevyo
Pambano hilo limeandaliwa na Ramadhani Uhadi na kuratibiwa na Shumbili Dawa litasimamiwa na chama cha ngumi za kulipwa Tanzania (TPBC).
Akizungumza Dar es Salaam jana mdhamini wa pambano hilo Uhadi alisema maandalizi ya mapambano hayo yamekamilika.
Uhadi alisema mapambano hayo yatatanguliwa na mapambano ya utangulizi kati ya Francis Miyayusho (bingwa wa afrika) na rashidi Ally (bingwa wa Tanzania) (kg54), Chiwa Hussein na Sweet Kalula(kg48), Mbaruku Kheri na Ramadhani Kido (kg 79) na Freddy Sayuni na Omary Ramadhani(kg51).
Aidha mpambano uho uliopangwa kufanyika katika uwanja wa Uhuru unatarajia kuanza mapema na kutakuwa na ulinzi wa uwakika kwa watu na mali zao.

Tuesday, December 29, 2009

KIFIMBO CHA MALIKIA CHA KIMBIZWA DAR ES SALAAM LEO

Raisi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tamzania Leodegar Tenga, akiwa amekishika kifimbo cha Malkia, Dar es salaam wakati wa kukimbiza kifimbo hicho kutoka uwanja wa Uhuru kuelekea Ikulu.(Picha na Rajabu Mhamila)Hapa Raisi wa TFF Leodga Chilla ameanza kutimu mbio na Kifimbo.Maafande wa Jeshi la Polisi nao hawakuwa nyuma, wanakumbushia mchakamchaka wa DepoWasanii wa bendi ya Afrikan stars 'Twanga pepeta' wakiwajibika wakati wa sherehe za kukimbiza kifimbo cha malkia kuelekea Ikulu Dar se salaam jana.(Picha na Rajabu Mhamila)

SIKINDE WAKONGA MASHABIKI DDC KARIAKOO

Wapuliza Saxsaphone wa bendi ya sikinde wakiwajibika katika onesho lao lililofanyika katika ukumbi wa DDC kariakoo kushoto ni Shabani Lendi na Yusufu Bernad.(Picha na Rajabu Mhamila)

SERENGETI KUMWAGA JEZI, VUVUZELA KWA MASHABIKI WA TAIFA STARS

Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Serengeti(SBL), Teddy Mapunda akiwa pamoja na Mabalozi wa Kampuni hiyo kushoto ni Mrisho Ngassa, Mussa Mgosi na Jerryson Tegete wakati wa uzinduzi wa kampeni ya 'shangilia Taifa Stars ishinde' iliyofanyika Dar es salaam jana.(Picha na Rajabu Mhamila)

Monday, December 28, 2009

HAPPYBIRTHDAY GAZETI LA MAJIRA

Gazeti huru la kila siku gazeti la Majira leo limeadhimisha miaka 16 tangu kuzaliwa kwa gazeti hilo.
Gazeti la Majira lilitoka kwa mara ya kwanza mtaani siku ya Jumatatu tarehe 27 mwaka 1993, kama linavyoonekana hapo juu pichani.

Sunday, December 27, 2009

YANGA MABINGWA TUSKER CHALENJI CUP 2009

Kapteni wa klabu ya Yanga Abdi Kassim Baby kulia akimkabidhi kombe Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Imani Madega (katikati)katibu mkuu Laurence Mwalusako(kulia)baada ya kutwaa uchampion wa michuano ya kombe la Tusker kwa kuifunga klabu ya SOFAPAKA 2-1 katika mchezo wa fainali uliyochezwa uwanja wa Uhuru, jijini dar es Salaam.Wachezaji wa Yanga wakifurahia baada ya kulitwaa kombe la Tusker.Waziri wa habari, utamaduni na michezo George Huruma Mkuchika akimkabidhi kapteni wa klabu ya Yanga kombe la Tusker baada ya kumalizika kwa mchezo wa fainali ambapo Yanga iliitandika Sofapaka 2-1.kkutoka kushoto ni golikipa wa Yanga Obren Curcovic, Nadir Haroub "Canavaro", Kigi Makasi na Athumani Iddi "Chuji" wakishangilia baada ya kuvalishwa medali.Kapteni wa klabu ya Sofapaka iliyomaliza ikishika nafasi ya pili akichukua hundi ya Milioni Ishirini.Wachezaji wa Sofapaka wakiwa Hoi baada ya kuzabwa na Yanga 2-1 katika mchezo wa fainali ya kombe la Tusker.Mashabiki wa klabu ya Yanga wakishangilia baada ya kipyenga cha mwisho kupulizwa huku Yanga ikishinda 2-1.Katibu mkuu wa klabu ya Simba Mwina Seif Kaduguda akipokea hundi ya Shilingi milioni kumi ikiwa ni zawadi ya mshindi wa tatu.kama wanaimba vile "Jamani Raha, Jamani Raha eeee Jamani raha, jamani Rahaa eeeeeeeee"IFAHAMU SOFAPAKA KATIKA HISTORIA YAO YA SOKA, KLABU NGENI LAKINI INAYOPATA MAFANIKIO KWA HARAKA, kwanza hii ndiyo maana ya SOFAPAKA.
SOTE (kama) FAMILIA (kwa) PAMOJA KUAFIKIA AZIMIO ndio kirefu cha SOFAPAKA, klabu ya soka iliyoanzishwa kutoka na timu ndogo ya kanisa la M.A.O.S Ministries jijini Nairobi chini ya usimamizi wa Pastor Jimmy Carter Ambajo mwaka 2002.
Klabu hii, ambayo pia ina timu ya wanawake SOFAPAKA QUEENS, imekuwa ikishiriki katika michuano ya kanisa hadi mwaka 2004 wakati mfadhili mkuu ambaye sasa ndiye Rais wao Elly Mboni Kalekwa, mfanyabiashara tajiri mzaliwa wa Congo Kinshasa.
SOFAPAKA, maarufu kama Watoto wa Mungu, iliundwa na timu ya vijana wanaoishi kwenye mazingira magumu, kabla ya kuanza kununua wachezaji nyota kutoka vilabu vingine vikubwa.
Mwaka huu wamenyakua ubingwa wa Kenya na kuwa timu ya mfano sio kwa Kenya tu bali Afrika Mashariki kwa ujumla, hususan Tanzania kwani ni klabu changa lakini imefanya makubwa na kuna kila dalili itafika mbali.
Pamoja na kuukosa ubingwa wa Tusker 2009, wadau wa soka kwa pamoja tunaipongeza SOFAPAKA kwa kuwa timu ya mfano Afrika Mashariki na Kati.

MITIKISIKO NA NGOMA CHINI ILIVYOITEKA DAR

Kundi la OFFSIDE TRICK likikamua katika onyesho la Mitikisiko na Ngoma chini lililoandaliwa na wafanyakazi wa Radio Times FM, na kufanyika katika ukumbi wa Traventine Magomeni.Hawa ni mashabiki wa Mduara wa kilicheza goma la "Poole samaki poole"Wanamvyo mla jichoWanavyo mgeuza geuzaIsha Ramadhani na mama yake walifunika ile mbaya na Mama nipe radhiEast African Melody ndiyo walikuwa wameshikilia usukani wa Burudani

MSONDO NA "HUNA SHUKURANI" MIKOANI MWAKA MPYA

BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini Msondo Music bandi watafanya ziara ya utambulisho wa albam yao mpya ya huna shukrani ambapo Msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kwamba Bendi hiyo kwa sasa ipo mikoa ya kusini kuwapa wapenzi burudani katika kutakiana heri ya mwaka mpya
Alisema katika utambulisho huo kwa mashabiki wa Msondo pia watapata nyimbo mpya kabisa zilizotungwa kwa ajiri ya albam ya mwaka 2010
Akielezea maandalizi zaidi Mhamila alisema licha ya kutambulisha albam bendi hiyo pia wamejipanga kutoa zawadi kwa mashabiki wao, ambapo albam yao mpya,iliyoingia sokoni hivi karibuni kuuzwa mtaani pia wameombwa kununuwa albam hiyo wapate kusikiliza majumbani mwao kwa ajiri ya sikukuu katika ziara hiyo ya utambulisho wa albamu siku ya alhamisi watakuwa Lindi katika ukumbi wa Comit Center, ijumaa Mtwara watapiga katika ukumbi wa Jakaya aidha jumamosi watapiga Masasi katika ukumbi maarufu na jumamosi watakuwa nachingwea katika ukumbi wa nachngwea pub, katika mkesha wa mwaka mpya watakuwa Rwangwa.
Alisema nyimbo zitakazotambulishwa katika dhihara hiyo ni pamoja na wimbo uliobeba albam hiyo, Huna shukrani uliotungwa na Saidi Mabera,Kiapo (husein jumbe) aki yangu ipo wapi (Uluka Uvuluge) Mama Cos, uliotungwa na marehemu (Josephe Maina) Albino (Juma Katundu) Machimbo Isihaka Kitima dj papa upanga) na Cheo ni Dhamana (Eddo Sanga)
Aidha aliwataja wanenguaji watakaokuwa wanatoa burudani katika safu hiyo kuwa ni Amina Said 'quen Emmy' Nacho Mpendu 'mama Nzawisa' na Amiri Saidi 'Dongo' aidha rapa wa bendi hiyo Romani Mng'ande 'Romario' atawachenguwa mashabiki watakaofika katika onesho hilo wakiongonzwa na mkurugenzi wa bendi hiyo Muhidini Gurumo,na kiongozi wa bendi hiyo Saidi Mabela

Friday, December 25, 2009

MARRY CHRISMASS VIWANJANI FANS!

Hi friends
Have a lovelly Marry Chrismass!

I Wish this Christmas that may The Most High, Our Heavenly Father be glorified and to the Men on Earth be peace and the Music of Christmas be played that shall never cease
Merry Christmas and Prosperous New Year
Best Wishes from
Mr. Amry Massare

YANGA DUME KWA SIMBA, SASA KUCHEZA FAINALI NA SOFAPAKA

Fainali ya michuano ya kombe la Tasker sasa itawakutanisha Mabingwa wapya wa Kenya na mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Yanga itakayopigwa siku ya Jumapili katika uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Yanga wamepata nafasi ya kucheza fainali baada ya kuitgandika Simba jumla ya magoli 2-1 katika nusu fainali ya pili iliyochezwa katika uwanja wa Taifa kwa dakika 120 baada ya kumalizika dakika 90 wakiwa sare ya goli 1-1.Pamoja na kupata nafasi hiyo Yanga kucheza fainali, lakini pia imevunjwa mwiko wa kufungwa na Simba katika michuano hiyo ikiwa ni pamoja na kulipa kisasi cha kufungwa na watani wao wa jadi katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu Tanzania Bara msimu huu.
Ushindi huo wa kwanza kwa kocha Kostadin Papic kwa simba, pia amevunja mwiko wa kocha Mzambia Patrick Phiri wa Simba kwani kocha huyo hakuwahi kufungwa na Yanga tangu aanze kuifundisha SImba.
Jerison Tegete ndiyo alikuwa wa kwanza kuwainua mashabiki wa Yanga katika dakika ya 67 kwa shuti kali lililomshinda mlinda mlango wa Simba Juma Kaseja, ikiwa ni kazi nzuri iliyofanywa na Abdi Kasim "Babi"NDeremo na vifijo vya Yanga havikudumu kwa muda mrefu kwani dakika ya 79 Hilary Echesa alizawazisha bao hilo kwa njia ya penati baada ya mchezaji Bakari Mbegu kumwangusha Emmanuel Okwi.Goli la ushindi la Yanga lilifungwa na Shamte Ally aliyeingia akitokea benchi kuchukua nafasi ya Abdi Kassim "Babi" dakika 116 na kupeleka msiba mtaa wa Msibazi na kuwavurugia sherehe za X-MASS