Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, December 2, 2012

MIAKA 20 YA CLUB BILICANAS NA MIAKA 13 YA CLOUDS FM KATIKA PICHA




Bendi ya muziki ya dansi ya Sky Light ikitumbuiza katika sherehe za kutimiza miaka 20 ya Club Bilicanas na miaka 13 ya Clouds FM. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
Sherehe hizo zilipambwa na shamrashamra za aina mbalimabli ikiwemo kukati keki pamoja na kufungua shampeni
Dk. Lilian Mtei akizungumza katika hafla hiyo.
Mwakilishi wa Clouds FM, Wasiwasi Mwabulambo akizungumza katika hafla hiyo
 Tukate keki
 Mmoja kati ya wafanyakazi wa kwanza wakati Bilicanas Club inaanzishwa miaka 20 iliyopita, Monika Victor akimlisha keki, Dk. Lilian Mtei wakati wa hafla ya kutimiza miaka 20 ya klabu hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo. 
 Maandalizi ya keki
 Pili Mitemo  ambaye alimwakilisha mumewe aliyekuwa Meneja wa kwanza wa klabu hiyo, ambaye kwa sasa ni marehemu akipokea keki kutoka kwa Dk. Lilian Mbowe kwa ajili ya kuwapa wadau waliojitokeza katika hafla hiyo
 Mzee Ali Ramadhan Mkude nae akuwa mbali katika mnuso wa Bilicanas Club kutimiza miaka 20 tangu kuanzishwa
 Mdau Bi. Agnes Mbowe akillishwa kipande cha keki na Dk. Lilian Mtei.
 DJ Ibrahim Tuwa 'Dj Ibra' akilishwa keki wakati wa hafla hiyo
Dk. Lilian Mtei akimlisha kipande cha keki Meneja Msaidizi wa Vinywaji wa Club Bilicanas, Amandus Agant wakati wa Birthday ya Bilicanas Club kutimiza miaka 20.
 Monica Victor akigawa keki kwa wadau waliofika katika sherehe hizo.
 Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka akiwa na mmiliki wa blog ya Bongoweekend, Khadija Kalili pamoja na wadau wengine. 
Watu wa mataifa mbalimbali wakicheza muziki katika ukumbi wa Bilicanas. 
Na Andrew Chale

WADAU  mbalimbali  wa burudani  usiku  wa kuamkia jana walifurahia kwa pamoja  na kula keki ya miaka 20 ya klabu ya Kimataifa ya Bilicanas na miaka 13, ya Clouds Fm,  iliyoambatana na shamrashamra mbalimbali ndani  na nje ya  ukumbi huo.

Sherehe hizo ziliongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bilicanas Group, Dk. Lilian Mtei  ambapo aliwashukuru wadau hao kwa kuwa bega kwa bega na klabu hiyo, tangu 1992. “Tunawashukuru sana kwa kuwa nanyi mara zote inatia faraja kwetu na tutaendelea kutoa huduma bora siku zote|” alisema Mbowe.

Mtei pia aliwashukuru wafanyakazi mbalimbali waliofanikisha ukumbi huo kufikia hapo na kutoa heshima ya kipekee kwa wafanyakazi  waliokuwapo  tokea inaanza hadi ilipofikia miaka 20 na hatimaye  kukata keki hiyo.

“Uwepo wa miaka 20, tuna kila sababu ya kuwapongeza wafanyakazi  tuliokuwa nao toka mwanzo hadi leo, na kwa heshima ya pekee  Mama Victor na Mrs Mitemo  ndiyo watakao kata keki hii” alisema Mtei.

Keki hiyo ilikatwa na wafanyakazi   hao  Monica  Victor   na Pili Mitemo  ambaye alimwakilisha mumewe aliyekuwa Meneja wa kwanza wa klabu hiyo, ambaye kwa sasa ni marehemu.

Aidha, kwa upande  Clouds FM, iliwakilishwa na Wasiwasi Mwabulambo ambaye alipongeza klabu Bilicanas kwa kuwa mstari wa mbele katika kuinua sanaa nchini hasa kwa kuwasaidia wasaidia wasanii kufikia malengo yao.

Kwa upande wake  Ibrahim Tuwa ‘Dj Ibra’ aliyekuwa akisherehesha  shughuli hiyo, aliwaomba wadau kuendelea kuwaunga mkono na wataendelea na huduma bora zaidi ha hapo. Dj Ibra alijiunga na Bilicanas tokea 2002,ambapo mpaka sasa ana miaka 10 kwenye klabu hiyo  iliyowahi kuwa na madj maarufu waliopita  hapo ambao wengi wao wapo kwenye vituo vya televisheni na redio.

JUMUIYA YA WAZAZI KURUDISHA MALI ZAKE ZILIZOVAMIWA KINYUME CHA SHERIA





DAR ES SALAAM, Tanzania

JUMUIYA ya Wazazi nchini imesema itahakikisha inarudisha mali zake zote zilizovamiwa kinyume cha sheria ikiwemo Shule ya Kaole ambayo ni ya kihistoria kati ya nchi ya Msumbiji na Tanzania.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Abdallah Bulembo alisema huo ni mkakati wa uongozi mpya uliyoingia madarakani hivi karibuni.
Alisema kitendo alichofanya Mkurugenzi wa shule za Green Acle, Julian Bujugo hakikubaliki kwani kimevunja mikatiba ya nchi mbili ya kulifanya eneo hilo kuendelea kuwa la kumbukumbu ya wapigania uhuru wa nchi ya Msumbiji.
“Haitafika Januari mwaka ujao Shule ya Kaole itakuwa imeisharudishwa mikononi mwa Jumuiya kwani shule ile ni ya nchi mbili naitaendelea kuwa ya kumbkumbu ya FLELIMO”alisema Bulembo.
Bulembo alisema eneo la Kaole haliwezi kuuzwa na kumilikiwa na watu wengine na baadala yake litabaki kuwa la watu wa msumbiji kutokana na ukweli kwamba kuna makaburi ya ndugu zaao ambapo hutembelea eneo hilo mara kwa mara.
“Tumemuita Bujugo kesho tukutane naye na kumjulisha kuwa alichofanya ni ukiukaji wa sheria hivyo anapaswa kuanza mchakato wa kukabidhi shule hiyo haraka kwa jumuiya”alisema.
Akifafanua zaidi, Bulembo alisema Jumuiya hiyo ilikumbwa na matatizo mengi hapo awali kutokana na baadhi ya watendaji kutokuwa waaminifu kuuza baadhi ya mali.
Alisema baada ya uongozi mpya kuyabaini hayo, inawatahadharisha wale wote waliyovamia mali za jumuiya hiyo kutambua kuwa wakati umefika kwa kuzirudisha hata kama ni kwa fidia kidogo watakayopewa na Jumuiya kinyume chake watawaburuza mahakamani.
Akizungumzaia maendeleo ya shule za jumuiya hiyo, Bulembo alisema zipo shule 71 ambapo kati hizo, 53 zimekuwa zikifanya vizuri kitaaluma.
Alisema kutokana na hali hiyo wamefikia muafaka na Kamati ya Shule hizo kuanza mchakato wa kuzibadili zile 18 ambazo hazifanyi fizuri  kuwa za ufundi (VETA), ambapo alisema Veta yao itakuwa tofauti kwani itapokea vijana wengi wanaomaliza darasa la saba na siyo kidato cha nne, kwani kundi hilo linasahaulika pindi liingiapo mitaani.
“Niwatowe wasiwasi wazazi wenzangu kuwa Jumuiya haina mpango wa kuuza baadhi ya shule zake zinazofanya vibaya bali mpango wetu ni kuziimalisha kiufundi ili ziweze kupokea kundi hilo la watoto wetu wanaomaliza elimu ya msingi” alisema Bulembo
Vilevile alisema kuwa hivi sasa shule zao siyo za huduma tena bali zitakuwa za kibiashara kama nyingine kwa sababu sera zilizoanzisha shule hizo awali zimepitwa na wakati.

WAMA YATOA MSAADA WA BOTI NA VIFAA VYA UVUVI KWA KIKUNDI CHA VIJANA MANISPAA YA LINDI





Boti ya Kikundi cha  Mwambao Fishing group iliyopewa jina la” Nani Kama Mama” wakati wa uzinduzi jana  ikiondoka katika bandari ya Lindi tayari kwa kazi ya uvuvi (Picha na Freddy Maro)


 Mke Wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa msaada vifaa vya kwa wawakilishi wa kinduchi cha Mwambao Fishing Group katika bandari ya Lindi jana jioni.
 Mke Wa Rais Mama Salma Kikwete na viongozi wengine pamoja na wawakilishi wa kikundi cha Mwambao Fishing group waki vuta kamba kuzindua rasmi Boti ya kikundi hicho jana wakati wa sherehe za makabidhiano yaliyofanyika katika bandari ya Lindi jana jioni
Na Freddy Maro, Lindi
 Vijana kikundi cha Mwambao Fishing Group  wa Mji ya Lindi wamemshukuru mke Rais mama Salma Kikwete baada ya kuwakabidhi Boti ya Uvuvi na vifa vyake katika hafla fupi iliyofanyika katika bandari ya Lindi jana jioni.

Akisoma risala kwa niaba ya wanachama wa kikundi hicho, Katibu Msadizi wa kikundi Bwana Jackson John Mnenje alitoa ahadi ya kutunza boti hiyo na na kuvitumia kwa malengo  waliyojiwekea ikiwamo kununua boti nyingine baada ya mwaka mmoja kutokana na faida itakayo tokana na biashara za uvuvi.
“Juhudi alizofanya Mama Salma, zinaonyesha jinsi anavyoguswa na hali ngumu ya maisha ya Watanzania na dhamira aliyonayo ya kutukwamua kutoka katika hali hii.Tunamshukuru Mungu kwani leo sisi tumebahatika na kujiunga na Watanzania wengi wanaofaidika na juhudi zake za kuboresha maisha ya Watanzania,” wanakikundi hao walisema katika risala hiyo.

Kutokana na bei kubwa ya vifaa hivyo, vijana hao wamesema kati ka risala yao kuwa, wasingeweza kamwe kununua vifaa hivyo bila msaada huo uliotolewa na Mama Salma Kikwete na kwamba utakuwa kichocheo kikubwa  cha kukabiliana na na changamoto  za maisha zinazowakabili.

Akizungumza kabla ya kukabidhi Msaada huo,mke wa Rais Mama Salma Kikwete alisema msaada huo ni utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2010 na 2015 inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuongeza kuwa ilani hiyo imetambua kuwa uvuvi ni moja ya sekta za uchumi ambazo hazijapatiwa msukumo wa kutosha.

“Kuongeza ufanisi na tija na kubadili maisha ya wavuvi ni moja ya Mapinduzi yanayolengwa katika ilani ya CCM ya 2010 -2015 na mpango uliopo ni wa kuimarisha ushirika wa makundi ya ujasiriamali ikiwa ni njia moja kubwa ya kuwawezesha  wananchi  wa kawaida kumiliki na kuendesha uchumi,” alisema Mama Salma.

Mama Salma amesema kuwa Taasisi anayoingoza ya Wanawake na Maendeleo WAMA itaendelea kuwasaidi wananchi katika maeneo yao ya kujenga ushirika ulio imara na unaojitegemea kiuchumi na unaoendeshwa na wao wenyewe katika misingi wa uwazi na uwajibikaji.

Mama Kikwete amesema pia kuwa WAMA  inalo jukumu la kuhamasisha na kutoa msaada wa hali na mali kwa wananchi na kuwawezesha kufikia malengo wali yojiwekea kwa kuwapatia nyenzo na vifaa mbalimbali,lakini wajibu wa kujiendeleza na kujisimamia unabakia  wa watu wenyewe.

Mke wa Rais amewahimiza wanachama wa Mwambao Fishing group kujenga mshikamano ili kikundi hicho kipate utulivu utakao wapa fursa ya kupanga mipango ya kujenga na kuimarisha kikundi na kufanya kazi kwa uwazi,kuaminiana na kupeana moyo.

Kikundi cha Mwambao Fishing Group chanye wanachama  25 kilianzishwa mwaka huu katika manispaa ya Lindi kutokana na ushari wa Mama Salma Kikwete aliyewashaur i vijana hao kuunda kikundi na kubuni mradi wa maendeleo utakao wasaidia  kuboresha masiha yao

MPIGA PICHA MKUU TANZANIA DAIMA AACHANA NA UKAPERA


  


Mpiga Picha Mkuu wa gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga akiwa na mke wake, Fridah Mockray wakati wa ibada ya ndoa takatifu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Sinza jijini Dar es Salaam jioni hii. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Mpiga Picha Mkuu wa gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga akiwa katika pozi na mke wake, Fridah Mockray mara baada ya kufunga ndoa katika Kanisa Katoliki Sinza jijini Dar es Salaam jioni hii. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
Mpiga Picha Mkuu wa gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga akipongezwa na mama yake mzazi
Pozi la harusi
Picha ya pamoja
Maharusi wakitoka Kanisani
Matron akisaini cheti

UZINDUZI WA ALBAM YA MASHUJAA LEADERS CLUB ILIVYOJILI





 Wanenguaji wa Mashujaa Band, wakikamua jukwaani wakati wa shoo ya ufunguzi wa uzinduzi wa albam yao, ambao shoo hii waliicheza jukwaani bila kumalizika kutokana na matatizo ya umeme.
 'Mkaanga Chips' wa Mashujaa, akizicharaza Drams.
 Wanamuziki wa Bendi ya Mashujaa wakiingia kwa staili yao ya kucheza muziki wa Kihindi, wakati wa shoo yao ya pamoja, ambayo hata hivyo haikuweza kumalizika.
 Wanenguaji wa Mashujaa, wakikamua jukwaani..
 Makamuzi yakiendelea..
 Shoo ilikuwa ni tamu kwa kweli, lakini haikuwa na raha kutokana na karaha ya umeme.
 Mpiga Tumba wa bendi hiyo, MCD, akizicharaza tumba....
 Sehemu ya mashabiki wa VIP waliolipa kiingilio cha Sh. 100, 000 kila mmoja, wakiwa katika eneo lao la VIP.

Friday, November 30, 2012

SAMSUNG YAZINDUA OFA YA MSIMU HUU WA SIKUKUU


 Meneja Usambazaji wa Samsung Tanzania Bw. Syvester Manyara na Country Trainer wa Samsung Electronics Bw.Joel Laize wakionesha baazi ya simu zilizopo katika Ofa Maalumu ya msimu wa sikukuu ambapo watafanya Droo mbalimbali kwa washindi kujipatia zawadi kem kem kutoka kampuni hiyo 
SAMSUNG YAZINDUA OFA YA MSIMU HUU WA SIKUKUU
“Ni Draw ya zawadi kubwa kwa wateja watakaonunua bidhaa za Samsung”
KAMPUNI ya SAMSUNG Tanzania leo imezindua rasmi ofa maalum ya kipindi hiki cha sikukuu ijulikanayo kama “Samsung Season’s Offer!”. Uzinduzi huu umefanyika katika duka la Samsung lililoko Quality Centre, Dar Es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Mkuu wa Samsung Tanzania Bwana Kishor Kumar alisema, “Ofa hii inalenga kuwazawadia wateja wetu zawadi hizi katika msimu huu wa sikukuu. Ofa hii imeanza rasmi leo Ijumaa tarehe 30 Nov na itaisha Jumamosi tarehe 5 Januari 2013.” Bwana Kishor alielezea zaidi kwamba wateja wote watakaonunua bidhaa za Samsung zilizo katika ofa hii watapata zawadi za papo kwa hapo na pia watapata nafasi ya kujishindia zawadi kubwa katika Draw ya mwisho. Draw ya mwisho itashuhudiwa na wasimamizi kutoka bodi ya Taifa ya michezo ya kubahatisha na itafanyika katika duka la Samsung Quality Centre Jumapili tar 06 January mwakani.
Naye meneja usambazaji wa Samsung Mobile Tanzania Bwana Sylvester Manyara alisema kwamba, “Pamoja na bidhaa nyingine za Samsung, bidhaa zilizo katika ofa hii kabambe ni aina ya Galaxy Note 2, Samsung S3, Galaxy Note 10.1, Samsung S Duos, Samsung ACE Duos, Galaxy Pocket na Galaxy Pocket Duos.” Bwana Manyara aliendelea kuelezea kwamba wateja watakaonunua bidhaa za Samsung kipindi hiki watapata kuponi maalum ambazo watajaza na kuzikusanya ili kujaribu bahati yao katika Draw kubwa ya mwisho. Ofa hii inaendeshwa katika maduka ya Dar Es Salaam, na maduka ya Samsung yaliyoko Mbeya, Arusha, Dodoma na Mwanza.
Bwana Kishor Kumar alimaliza kwa kutaja zawadi zitakazotolewa kwamba ni;
1.    Zawadi ya Kwanza; Samsung LED TV ya Inchi 42’.
2.    Zawadi ya Pili; Samsung Galaxy S3 Mobile Phone.
3.    Zawadi ya Tatu; Samsung Galaxy Note 10.1.
4.    Zawadi ya Nne; Samsung Home theatre.
5.    Zawadi ya tano; Samsung Smart Camera.
Pamoja na zawadi hizi, Samsung itatoa zawadi kwa wateja mbalimbali watakaokutwa wakinunua bidhaa za Samsung, miongoni mwa zawadi hizi ni TV tatu za inchi 32 zitakazotolewa moja kila wiki kwa wiki tatu mfululizo kuanzia wiki hii.
Naye bwana Manyara alimaliza kwa kuwashukuru wateja wa Samsung kwa kuchagua bidhaa hizi bora, aliwaomba waendelee kufurahia bidhaa hizi hata baada ya kipindi cha msimu huu wa sikukuu. Aliwakumbusha kwamba miongoni mwa manufaa ya bidhaa za Samsung ni kwamba bidhaa zake ndio tu zina warantii ya miezi 24 yaani miaka miwili. Aliwakumbusha pia kupiga namba ya huduma kwa wateja endapo wakihitaji ufafanuzi kuhusu jambo lolote kuhusu bidhaa za Samsung. Namba ya huduma kwa wateja wa Samsung ni +255 685 88 99 00.
Samsung inaendesha kampeni hii ikiwa ni wiki chache baada ya kufanya maonyesho makubwa ya bidhaa zake jijini Dar Es Salaam yaliyofahamika kama “Samsung Week”. Samsung inafanya pia shughuli nyingi za kujitolea, hususani msaada wa udhamini wa mafunzo kuinua vipaji vya wanariadha katika shule ya Winning Spirit Arusha, msaada kwa shule na matibabu katika kijiji cha Ilmorijo Monduli Arusha na Lyamungu Moshi nk.

WASANII WAMLILIA SHARO MILIONEA KWA WIMBO MMOJA - KAZA MOYO


Video ya kumuenzi marehemu HUSSEIN a.k.a Sharo Milionea huu wimbo umeimbwa na Shetta, Dayna Nyange, shilole mohamed, Cannal Top, Rich Mavoko, Shadoo, Amazon, Barnabas Elias, Stamina, Dan rock, Suma Mnazaleti, Eric Mlindima, Muba c, Seif

BONGO ALL STARS together we canAudio producer ni C9Kanjenje 
Video directed by Msafiri under KWETU studio
R.I.P Sharo Milionea tutakukumbuka daima milele

TAMADUNI MUZIKI KUZINDUA SANTURI NNE KWA PAMOJA


TIBAIJUKA AZINDUA UJENZI WA NYUMBA 48 ZA NHC MCHIKICHINI DAR



 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka akifunua pazia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa ujenzi wa nyumba 48 za kuuza za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala Mchikichini, Dar es Salaam jana.Anayeongoza kupiga makofi kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
 Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu (kulia), akimkaribisha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Profesa Tibaijuka kuzindua mradi huo.
                        Waziri Tibaijuka akihutubiwa wakati wa hafla hiyo
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli  akihutubia
                                              Profesa Tibaijuka akikagua ujenzi huo
                                           Moja ya majengo yanayojengwa eneo hilo

CHADEMA YATATHMINI UHAI WA CHAMA KINONDONI




 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Willibrod Slaa akifungua Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kinondoni kuhusu Uhai wa Chama uliofanyika Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam jana. Wa pili kushoto ni Ofisa wa Sera na Utafiti wa Chadema, Mwita Mwikwabe Waitara na Naibu Katibu Mkuu Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Subira Waziri (wa tatu kulia). (Picha na Habari Mseto Blog)
 Mbunge wa Ubungo, John Mnyika akizungumza na wajumbe waliohudhuria Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kinondoni
 Ofisa wa Sera na Utafiti wa Chadema, Mwita Mwikwabe Waitara
Baadhi ya wajumbe

Precision Air supports breast cancer screening in Mtwara and Lindi



Precision Air Commercial Director Mr. Patrick Ndekana (left) speaks to journalists (not in picture) in Dar es Salaam yesterday about his company’s support of 9m/- towards a four-days breast cancer awareness and screening campaign that kicks off in Mtwara and Lindi on Wednesday. Looking on is the Aga Khan Health Service’s Head of Nursing Services, Loveluck Mwasha. (Photo by our correspondent)
Aga Khan Health Service (AKHST’s) Head of Nursing Services, Loveluck Mwasha (right) speaks to journalists (not in picture) in Dar es Salaam yesterday about a four-days breast cancer awareness and screening campaign that kicks off in Mtwara and Lindi on Wednesday, which has received a support of 9m/- from Precision Air Services PLC. Looking on is the Precision Air Commercial Director Mr. Patrick Ndekana. (Photo by our correspondent)


By Correspondent 

Precision Air supports breast cancer screening in Mtwara and Lindi By Correspondent Precision Air (PW) has donated 9m/- geared towards supporting the breast cancer awareness and screening campaign that kicks off in Mtwara and Lindi on Wednesday.

 The four-day event that that will run under the theme “Check it, Beat it” is spearheaded by the Aga Khan Health Service, Tanzania (AKHST) and seeks to reach more women, especially those living in areas without sufficient access to health services. 

Speaking to reporters in Dar es Salaam yesterday, the Precision Air Commercial Director Patrick Ndekana said the donation is part of the Airline’s Corporate Social Responsibility Programme (CSR) that aims to promoting screening to reduce the need for major surgery or death cases faced by many Tanzanians. 

Ndekana said Precision Air understands the importance of heath in national development that is why it chose to support the campaign.

 “Our mission is to beat breast cancer by funding such projects that targets our remote communities who do not have access to proper health services nor the financial support to have major surgeries.

 We believe our support will go a long way in saving people’s lives because early detection saves lives.

 “Having our Airline presence in Mtwara, we are aware that the revenue we derive is from a healthy community. 

The airline will only do business if we have less number of people with ill-health. It is only a healthy people who form a healthy nation that brings forth a stable and ever growing economy. 

“Precision air will only continue growing in terms of increasing the number of its fleets and open more routes to serve more customers in this region. We can only achieve that when we have a strong and stable economy in countries we operate,” said Mr Ndekana. 

On her part, representative from Aga Khan Health Service, Tanzania (AKHST) Ms Loveluck Mwasha, Head of Nursing Services, mentioned that the campaign which will be carried in Mtwara and Lindi Regions is targeting a population of 4 million people while at least 500 women are expected to be screened between the two towns.

 The campaign is targeting women, young and old in these two towns - for the Breast Cancer Screening - but will also see men being screened for the same. Ms Mwasha said that an initial site visit to Mtwara and Lindi was made by the Breast Cancer Campaign Team, including the AKHST Medical Director, Dr. Jaffer Dharsee, and Mr. Sisawo Konteh, Head of Outreach Services, of the Aga Khan Health Service, Tanzania, during which they met with the Regional Medical teams in both towns and agreed on the camp models.

 Every year, thousands of Tanzanian women are diagnosed with breast cancer. It is a major life altering event for women who are diagnosed, but for some the diagnosis comes much too late. 

Globally, breast cancer is among the leading causes of cancer-related deaths in women. Early detection of the disease through breast cancer awareness and screening campaigns is vital to reducing the devastating prevalence of this disease amongst women in East Africa.

 Today, Precision Air calls for all citizens in Mtwara to “Check it, Beat it!”

DESIGNERS LINE UP FOR TANZANIA RED RIBBON FASHION GALA 2012



Organiser of Tanzania Red ribbon Fashion Gala Ms.Khadija Mwanamboka (second from right) at the group photo with some of the designers at her Office.
Founder and Chairperson of Tanzania Mitindo House (TMH) Ms. Khadija Mwanamboka together with the Kids from the Tanzania Mitindo House Orphanage Centre.

“My Dream is to be a top designer” One of the Orphan get trained for free at Tanzania Mitindo House Office.
***********************
DESIGNERS AND MODELS – FIRST ROUND
MOROGORO POLYTEX - VITENGE
1. EVE COLLECTIONS
a)Ava
2. SALIM ALI
a) Ben
3. MARTIN KADINDA
a) Alexia
4. EDNA SILVER
a) Nadia
5. GABRIEL MOLLEL
a) Hidaya
6. SHELLINA IBRAHIM
a) Neema
7. FRANKOO DESIGNS
a) Elgiver
8. Hameed
a) Victor
9. ASIA IDARIOUS KHAMSIN
a) Jamila
TANZANIA RED RIBBON FASHION GALA 2012
FASHION SHOW – SECOND ROUND
DESIGNERS AND MODELS
1. MUSTAFA HASSANALI
a) Jamila
b) Elgiver
c) Alexia
2. Hameed Abdul
a) Ben
b) Hidaya
3.SHELLINA IBRAHIM
a) Neema
b) Jamila
4.GABRIEL MOLLEL
a) Nadya
b) Ava
5.EDNA SILVER
a) Neema
b) Ben
7.EVE COLLECTIONS
a)Ava
b) Hidaya
6. SALIM ALLY
a)Neema
b)Victor
8. MARTIN KADINDA
a) Nadia
b) Alexia
9.FRANKO DESIGNS
a)Ben
b)Victor
10.ASIA IDARIOUS KHAMSIN
a) Elgiver
b)Jamila