Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, January 25, 2016

WAKAZI WA KATA YA NAMAYUNI WAPONGEZA MTANDAO WA SIMU ZA MKONONI WA HALOTEL.



Na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Halotel ndio mtandao pekee unaotoa huduma za mawasiliano kwa njia ya Simu za mkononi katika kata ya Namayuni iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi.

Mtandao huu ndio unawasaidia wakazi wa kata ya Namayuni kuweza kuwasiliana na ndugu na jamaa  wa maeneo hayo na sehemu nyingine kwa njia ya simu ya mkononi kwa kuwa wamejengewa mnara unao wawezesha kuwasiliana kwa njia simu za mkononi.

 Diwani wa Kata ya Namayuni iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi, Hussein Sungura amepongeza mtandao wa simu za mkononi wa Halotel na kusema kuwa umeisaidia sana jamii ya wakazi wa kata ya Namayuni mkoani humo kutokana na hapo awali kutokuwepo na mtandao wowote wa simu.

" Tunawashukuru sana Kampuni ya simu za mkononi ya Halotel kukumbuka kama kunaviumbe huku na kutuwekea mnara katika kata yetu kwakua kabla ya mtandao huu tulisafiri na kupanda juu ya vilima ili kutafuta mtandao(network) ili tuweze kuwasiliana na watu wengine kwa njia ya simu."

Nao wakazi wa Kijiji cha Namayuni wamesema kuwa Mtandao huu wa Halotel "umetusaidi sana katika huduma mbalimbali hasa kutufichia siri katika mawasiliano kwani tulikuwa tunaenda umbali mrefu kwenda kutafuta mtandao, kwa sasa tunakaa ndani tuu na tunawasiliana na ndugu na jamaa  bila mtu yoyote kujua kama tumewasilana na nani".

Wafanyakazi wa mtandao wa Halotel wametembelea kata  ya Namayuni kwaajili ya Kampeni ya HALO MAISHA inayoendelea katika maeneo mbalimbali  yaliyofikiwa na mtandao huo nchi zima ili kila jamii ifaidike na spidi kubwa ya intaneti na upatikanaji wa huduma nzuri za mtandao huo.
 Wanafunzi wakisoma kupitia Kompyuta zilizounganishwa na intaneti ya spidi kubwa walizopewa  na kampuni ya Simu za mkononi ya Halotel katika shule ya sekondari ya Lugoba iliyopo Msata- Bagamoyo Mkoani Pwani.
Mtaalamu wa masuala ya mtandao  wa kampuni ya Halotel, Kilwa Masoko Mkoani Lindi, Sebastian Inocent akifafanua changamoto mbalimbali zinazo wapata wakazi wa kijiji cha Namayuni.

Afisa habari wa kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Halotel, Frank Mwakyoma akizungumza na wananchi wa kijiji cha Namayuni kilichopo kata ya Namayuni Kilwa Masoko Mkoani lindi mara baada ya wafanyakazi wa kampuni hiyo kuwatembelea katika kijijini hapo.
 Wakazi wa Kijiji cha Namayuni wakipata maelekezo walipo tembelea kibanda cha kusajili laini jijini  hapo.

 Vijana wakipiga simu kwa ndugu na jamaa wakiwa kijijini hapo.

Baadhi ya waandishi wa habari.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Lugoba iliyopo Msata mkoani Pwani, Abdala Sakasa akizungumza wakati wafanyakazi wa kampuni ya Simu za Mkononi ya Halotel walipotembea katika shule hiyo kujionea jinsi wanafunzi wanavyotumia Kompyuta zilizounganishwa na intaneti yenye spidi ya kazi ili kusaidia wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Lugoba hasa wa kidato cha tano na cha sita kwa kusoma na kuongeza uwezo wao katika masoma kutokana na  wanafunzi hao kukosa baadhi ya vitabu. Wanafunzi wa shule hiyo wamefurahia uwepo wa mtandao wa Halotel kwani ndio mtandao pekee uliochelewa kufika hapa nchini na kuweza kutoa kompyuta 19 zilizounganishwa na intaneti katika shule hiyo.
Mwalimu wa somo la Kompyuta na maswala ya mawasiliano(ICT), Emmanuel Mhizi akifafanua jambo mbele ya wafanyakazi wa kampuni ya simu za mkononi ya Halotel walipotembelea shuleni hapo mkoani Pwani. Mwalimu wa  Kulia ni Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya  Lugoba, Benjamini Nyamatwema.

Mhizi amesema kuwa wanachangamoto kubwa katika kupanga zamu za wanafunzi wa shule hiyo kwani shule hiyo inawanafunzi 1391 na kompyuta zenye intaneti ni  19 tuu, kwa mujibu wa ratiba ya wanafunzi kuingia kwenye chumba hicho wanaingia wanafunzi 30 kwa kila kipindi ili kila mwanafunzi aweze kuingia katika chumba cha kompyuta.
Wanafunzi wakiwa katika Darasa la kompyuta ambalo Kampuni ya Halotel walijitolea kwa kuwapa kompyuta hizo pamoja na kuwaunganishia Intaneti  spidi kubwa ya bure kwa miaka mitatu mfurulizo iki kuweza kuwasaidia wanafunzi hao katika kujisomea machapisho mbalimbali yaliyopo kwenye mitandao mbalimbali.
Mwalimu wa somo la Kompyuta na maswala ya mawasiliano(ICT), Emmanuel Mhizi akiwakagua wanafunzi kwa uangalifu katika darasa hilo. 
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Lugoba akiendelea kujisomea somo alilolifungua  walipotembelewa na wafanyakazi wa Kampuni ya Halotel mkoani humo.
 Walimu wa Shule ya Sekondari ya Lugoba iliyopo Msata- Bagamoyo Mkoani Pwani wakijadiliana jambo wakati wanatembea.
 Diwani wa Kata ya Namayuni iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi, Hussein Sungura akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wakazi wa kijiji cha Namayuni mkoani humo walipotembelewa na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Halotel ambayo ndio mtandao pekee uliowafikia wananchi na wakazi wa kata hiyo. 
Wakazi wa kata ya Namayuni na wanakijiji cha Namanyuni wakimsikiliza Diwani wa Kata ya Namayuni iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi, Hussein Sungura mara baada ya kutemelewa na wafanyakazi wa kampuni ya Simu za Mkononi yz Halotel mkoani humo.

Mkazi wa Kijiji cha Namayuni akizungumza na simu wakati amekaa akitumia mtandao wa simu wa Halotel akiwasiliana na mtu aliyepo Zanzibar bila kwenda kupanda kwenye kilima kama zamani.
Aidha mzee huyo alielezea furaha yake kwa ujio wa mtandao wa Halotel unavyowasaidia na kuwafichia siri zao, kwani mwanzoni kila mtu alijua kuwa ndio anaenda kuongea na simu na mpaka kusababisha kuaga na kwenda umbali furani kwaajili ya kutafuta netiweki ili aweze kuzungumza na mtu ambaye anamtafuta.
 Mwenyekiti wa Kijini cha Namayuni, Ally Mtumbwe akizungumza na waandishi wa habari Kilwa Masoko Mkoani Lindi kata ya ya Namayuni kijijini cha namayuni mara baada ya wafanyakazi wa mtandao wa Halotel kutembelea kijijini hapo. 
 Mkazi wa Kijiji cha Namayuni akielezea jinsi mtandao huo ulivyorahisisha biashara kutokana na kujengewa mtandao wa Halotel amesema kuwa mtandao huo umewasaidia kwa kuagiza bidhaa anazozihitaji ukitofautisha na zamani ambapo ilibidi kuzifuata hata kama hajui kama bidhaa anayoitaka ipo au haipo, hata hivyo amesema kuwa Halotel imewasaidia kuokoa muda sana.
 Mkazi wa kijiji cha Namayuni akiuliza swali kuhusiana na mtandao huo kuhusiana na kama unaweza kutuma pesa  au kupokea pesa.
Watoto wa Kijijini cha Namayuni wakipata picha na mwandishi wa gazeti la The Citizen kijijini hapo.
 Afisa masoko wa kampuni ya Halotel , Charle anayepiga picha kwa simu akiwa na baadhi ya waandishi wa habari katika kijini cha Namayuni, Klwa Masoko mkoani Lindi.


Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI MJINI DODOMA.


                         Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora , Angela                   Kairuki akiteta na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Ashatu                                                      Kijaji bungeni mjini Dodoma Januari 25, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majalaliwa akisalimiana na Mbunge wa Nkansi Ally Kessy kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Januari 25, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majalaliwa akisalimiana na Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Januari 25, 2016. Katikati ni Mbunge wa Nkansi, Ally Kessy.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Songwe, Philip Mulugo kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januari 25, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wazee kutoka jimbo la Chemba Ofisini kwake bungeni mjini Dodoma Januari 25,2016. Kushoto kwake ni Mbunge wa Chemba Juma Nkamia. 

 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

BONDIA VICENT MBILINYI AENDELEA KUJIFUA NA KUTAFUTA WAPINZANI


VICENT MBILINYI KG 63 TANZANIA 2016

Bondia Vicent Mbilinyi akielekezwa jinsi ya kutupa makonde wakati wa mazoezi yake yakawaida Picha na SUPER D BOXING NEWS
Na Mwandishi Wetu
BONDIA Vicent Mbilinyi amendelea kujifua baada ya kumchakaza bondia mkongwe wa siku nyingi Deo Njiku sasa anaendelea na mazoezi ya nguvu kwa aji ya kuwasambalatisha mabondia wengine watakaopita mbele yake

bondia huyo mpaka sasa ameshacheza michezo tisa na kushinda 7 kupoteza  na droo 1 ambapo imemuweka katika rekodi nzuri ya mchezo uho kwa mwaka jana

akizungumza na mwandishi wa habari hizo Mbilinyi amesema kwa sasa yupo fiti kucheza na mtu yoyote kwa keshaiva kikamilifu baada ya kupata mazoezi ya aina mbalimbali yanayo mjengea kujiamini katika mchezo wa masumbwi akiwa chini ya kocha wa kimataifa wa mchezo uho Rajabu Mhamila 'Super D'

aliendelea kwa kusema kuwa nilingia katika ngumi za kulipwa kama najitolea lakini siku zinavyozidi kwenda ndio najijengea mashabiki na kujulikana zaidi katika mchezo niupendao hivyo na ahidi sito waangusha na wala sito lewa sifa wanazonipa nitaendelea kujifua ili niendelee kupambana zaidi katika mchezo

nae kocha anaemnowa bondia huyo Super D amesema kuwa Mbilinyi ana moyo wa kufika mbali hivyo ameonesha nia ya kucheza mchezo uhu katika mazingila magumu hivyo kwa mwaka 2016 ni wake wa kutoka katika mchezo wa ngumi

na naisi katika uzito wake kwa sasa akuna wa kumsumbua kwa sababu amekutana na mabondia wa lika zote ambao wanatamba na waliotamba

Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa sasa anawasimamia mabondia wake akiwemo Ibrahimu Class 'King Class Mawe' Shabani Kaoneka, Shomari Milundi, Vicent Mbilinyi Mwenyewe na mwanadada Lulu Kayage ambao wote wapo chini ya Super D Boxing Promotio ambayo kazi yake kubwa ni kuwafundisha na kuwatafutia mipambano mbalimbali  ya nje na ndani

BONDIA FRANSIC CHEKA ATUA NCHINI NA KUMPIGIA MIKWALA MSERBIA GEARD AJOTOVIC

Bondia Fransic Cheka 'kulia' akizungumza na waandishi wa habari awapo pichani juu ya maandalizi yake ya mchezo wa ngumi ambapo aliweka kambi nchi ya Zambia kwa wiki mbili kwa ajili ya kumkabili Mserbia Geard Ajetovic
kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27 kushoto ni
meneja wake, Juma Ndambile wa Kampuni ya Advanced Security Limited Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Fransic Cheka 'kulia' akizungumza na waandishi wa habari awapo pichani juu ya maandalizi yake ya mchezo wa ngumi ambapo aliweka kambi nchi ya Zambia kwa wiki mbili kwa ajili ya kumkabili Mserbia Geard Ajetovic
kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27 kushoto ni
meneja wake, Juma Ndambile wa Kampuni ya Advanced Security Limited Picha na SUPER D BOXING NEWS



Na Mwandishi wetu

Dar es Salaam.  Bondia  Francis Cheka amerejea nchini kutoka Zambia na kusema Mserbia Geard Ajetovic aiandae kupokea kipigo kikali katika pambano lao la mabara la uzito wa super middle la  Shirikisho la Masumbwi ya  Kulipwa Duniani (WBF).

Cheka na Ajetovic watapambana kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27 katika pambano lililoandaliwa na kampuni ya Hall of Fame Boxing and Promotion.

Akizungumza jana, Cheka alimpongeza  meneja wake, Juma Ndambile wa Kampuni ya Advanced Security Limited kwa kumwezesha kuweka kambi nje ya nchi ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya mchezo huo kwa upande wake.

Alisema kuwa Ndambile na kampuni yake imeonyesha kuwa wanajali na wanamalengo makubwa ya kumwendeleza kutokana na ukweli kuwa amekaa katika kambi ya kisasa yenye mabondia na makocha wazuri nchini Zambia.

“Kwanza naishukuru kampuni ya Advanced Security Limited kwa kufanikisha kambi hii, nimejifua vya kutosha nchini Zambia, mazoezi yalikuwa magumu na yalihitaji uvulivu mkubwa, kwa kutambua lengo langu ni nini, nilifanya kwa juhudu zote na sasa nipo tayari kwa pambano, hata kesho (leo) nipo tayari kwa bondia yoyote duniani,” alisema Cheka.

Alisema kuwa kutokana na siku kuwa nyingi, ataendelea na mazoezi hapa hapa nchini huku akisubiri mipango mengine ya meneja wake kwa upande wa maandalizi.

Meneja wa Cheka, Juma Ndambile ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Advanced Security Limited alisema kuwa  lengo la kampuni yao ni kufanya mapinduzi na kuleta maendeleo katika mchezo wa ngumi za kulipwa hapa nchini.

Ndambile alisema kuwa Cheka ni bondia mwenye kipaji na hakuwa tayari kuona kipaji hicho kinapotea na kuchukua jukumu la kumwendeleza. “Mimi na kampuni yangu tuna mipango ya kuwamiliki mabondia wengi hapa nchini, kama ilivyo kwa Cheka, nao watapata fursa ya kufanya mazoezi nje ya nchi na kupata mapambano ya kimataifa ya ubingwa ili kuiletea sifa taifa,” alisema Ndambile.

Alisema kuwa wanataka kutumia vizuri fursa waliyopewa na WBF ambayo inamtaka Cheka ashinde pambano hilo ili aweze kuwania ubingwa wa Dunia hapa hapa nchini.

Sunday, January 24, 2016

MABONDIA ABDALLAH PAZI NA GORGER DIMOSO WASAINI KUZIPIGA MARCH 5 BAGAMOYO MKOA WA PWANI

Bondia Georger Dimoso kushoto akitunishiana misuli na Abdallah Pazi baada ya kutia saini za makubaliano ya kuzipiga march 5 katika ukumbi wa tasuba Bagamoyo mkoa wa pwani Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Geoger Dimoso akisaini mkataba wa kuzipiga na Abdallah Pazi wa pili kushoto kulia ni mlatibu wa mpambano huo Pembe Ndava na kushoto ni kocha Mbaruku Heri

Mabondia Georger Dimoso kushoto akitunishiana misuli na Abdallah Pazi wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika March 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa Pwani katikati ni mratibu wa mpambano uho Pembe Ndava Picha na SUPER D BOXING NEWS

Na Mwandishi Wetu

MABONDIA Abdallah Pazzi na Gerger Dimoso wamesaini mkataba wa kuzipiga Bagamoyo mkoa wa Pwani March 5 katika uzito wa kg 74

akizungumza wakati wa kutiliana saini Promota wa mpambano uho Muhusin Sharif amesema kuwa wameamua kupeleka mpambano uho Bagamoyo kwa ajili ya wakazi wa mkoa wa pwani wapate burudani ya masumbwi siku hiyo

aliongeza kwa kusema kuwa anaomba makampuni mbalimbali kutoa sapoti kwa ajili ya udhamini wa mapambano hayo kwa kuwa Bagamoyo mchezo huo unapendwa na ndio unachipukia hivyo anaomba sapoti kwa makampuni na taasisi mbalimbali kusaidia mchezo uho ili uendelee kukua hapa nchini

ambapo kwa Bagamoyo atuna jukwaa 'ring' la ngumi ata moja mpaka tukodishe kutoka Dar es salaam yaje hapa ndio vijana wapate kucheza hivyo naomba wadau mbalimbali wajitokeze kuchangia upatikanaji wa jukwaa hiro kwa ajili ya mchezo wa ngumi ili zisonge mbele

siku hiyo mbali na mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine ya kukata na shoka ambapo bondia Sadiq Momba atakumbana na Baina Mazola katika uzito wa kg 59 na Adam Yahaya atakumbana na Selemani Bagaiza katika uzito wa kg 49 na Juma Khan atapambana na Bruno Vivuaviwili na Abdallah Zamba atakumbana na Twalibu Tuwa

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

Wednesday, January 20, 2016

MABONDIA SADIQ MOMBA NA BAINA M,AZOLA WASAINI KUZIPIGA MARCH 5 TASUBA BAGAMOYO


Mabondia Sadiq Momba kushoto wakitambiana na Baina Mazola baada ya kutia saini ya kuzipiga march 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa pwani katikati ni promota Muhusin Sharif Picha na SUPER D BOXING NEWS

Promota wa mchezo wa masumbwi Muhusin Shsharif katikati akiwa pamoja na mabondia Sadiq Momba kushoto na Baina Mazola mara baada ya mabondia hawo kutiliana saini ya kuzipiga march 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa Pwani Picha na SUPER D BOXING NEWS
KIONGOZI TOKA SHIRIKISHO LA MASUMBWI PST PEMBE NDAVA KATIKATI AKISAINI MKATABA WA KUKUBALI KUPIGANA BONDIA BAINA MAZOLA KUSHOTO NA KULIA NI PROMOTA MUHUSINI SHARIFU


Promota wa masumbwi nchini Muhusini Sharif Katyikati akiwainuwa mikono juu mabondia Sadiq Momba kushoto na Baina Mazola wakati wa kutambulisha mpambano wao utakaofanyika katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa Pwani Picha na SUPER D BOXING NEWS
BONDIA SADIQ MOBA AKITIA SAIN YA KUZIPIGA NA BAINA MAZOLA MARCH 5 KATIKA UKUMBI WA TASUBA BAGAMOYO MKOA WA PWANI WANAOSHUDIA KULIA NI PROMOTA MUHUSINI SHARIFU NA KIONGOZI TOKA SHIRIKISHO LA MASUMBWI PST PEMBE NDAVA

Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Sadiq Momba na Baina Mazola jana wamesaini mkataba wa kuzipiga march 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo Mkoa wa Pwani uzito kwa kg 59
akizungumza wakati wa kutiliana saini kwa ajili ya mpambano huo promota Muhusini Sharif amesema ameamua kuwapambanisha mabondia hawo wanaotamba kwa sasa kwenye uzito uho kwa ajili ya kuleta chachu ya mchezo wa ngumi nchini

unajua Sadiq Momba ni bondia maarufu ambaye anakwenda sana nje ya nchi kwa ajili ya mapambano mbali mbali na amekuwa anafanya vizuri awapo nje ata hivyo mpambano wake wa mwisho nchini Thailand amepigwa kwa T.K.O ya raundi ya tatu na kurudi nyumbani hivyo anacho itaji ni ushindi na kupigana na mtu mwenye point za kutosha kumrudisha kileleni

na Baina Mazola katika uzito wake yeye  ni namba tatu katika boxrec nchini hivyo nae anataka kuwa zaidi ya bondia Momba na ndio anatishia amani katika uzito uho kwa sasa

nae bondia Momba amesema baada ya kupoteza mpambano wake nje ya nchi sasa wadogo zake wanamtaka kucheza nae kwani inaonekana kiwango changu kimepungua na kudiliki watoto wadogo kunitaka mimi ata ivyo nashukuru uhu mchezo mimi ni kazi yangu naitegemea ivyo nitaakikisha simpi nafasi ata chembe kwa kumpiga kipigo kibaya sana ambacho ajawai kupigwa tanga aanze mchezo wa masumbwi nchini 

nae bondia Mazola amesema kwa sasa yupo vizuri sana na anawaomba mashabiki zake kuwa na moli ya kwenda bagamoyo ambapo promota kafanya vizuri sana klupereka mpambao huu uko sisi mabondia wote wawili tuna umarufu mkubwa sana maeneo ya manzese na vitongoji vyake ata hivyo nita akikisha nampiga Momba kama begi kwa kuwa sasa ana jipya nimeona stail zake zote anazotumia kupigana sijaona jipya hivyo ajiandae kwa kipigo tu

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile





Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi

pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

MABONDIA SADIQ MOMBA NA BAINA M,AZOLA WASAINI KUZIPIGA MARCH 5 TASUBA BAGAMOYO


Mabondia Sadiq Momba kushoto wakitambiana na Baina Mazola baada ya kutia saini ya kuzipiga march 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa pwani katikati ni promota Muhusin Sharif Picha na SUPER D BOXING NEWS

Promota wa mchezo wa masumbwi Muhusin Shsharif katikati akiwa pamoja na mabondia Sadiq Momba kushoto na Baina Mazola mara baada ya mabondia hawo kutiliana saini ya kuzipiga march 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa Pwani Picha na SUPER D BOXING NEWS
KIONGOZI KUTOKA KATIKA KAMPUNI YA MCHEZO WA NGUMI ZA KULIPWA PST PEMBE NDAVA KATIKATI AKISAINI MKATABA WA KUKUBALI KUPIGANA BONDIA BAINA MAZOLA KUSHOTO NA KULIA NI PROMOTA MUHUSINI SHARIFU

Promota wa masumbwi nchini Muhusini Sharif Katyikati akiwainuwa mikono juu mabondia Sadiq Momba kushoto na Baina Mazola wakati wa kutambulisha mpambano wao utakaofanyika katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo mkoa wa Pwani Picha na SUPER D BOXING NEWS
BONDIA SADIQ MOBA AKITIA SAIN YA KUZIPIGA NA BAINA MAZOLA MARCH 5 KATIKA UKUMBI WA TASUBA BAGAMOYO MKOA WA PWANI WANAOSHUDIA KULIA NI PROMOTA MUHUSINI SHARIFU NA KIONGOZI KUTOKA NGUMI ZA KULIPWA PST PEMBE NDAVA

Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Sadiq Momba na Baina Mazola jana wamesaini mkataba wa kuzipiga march 5 katika ukumbi wa Tasuba Bagamoyo Mkoa wa Pwani uzito kwa kg 59
akizungumza wakati wa kutiliana saini kwa ajili ya mpambano huo promota Muhusini Sharif amesema ameamua kuwapambanisha mabondia hawo wanaotamba kwa sasa kwenye uzito uho kwa ajili ya kuleta chachu ya mchezo wa ngumi nchini

unajua Sadiq Momba ni bondia maarufu ambaye anakwenda sana nje ya nchi kwa ajili ya mapambano mbali mbali na amekuwa anafanya vizuri awapo nje ata hivyo mpambano wake wa mwisho nchini Thailand amepigwa kwa T.K.O ya raundi ya tatu na kurudi nyumbani hivyo anacho itaji ni ushindi na kupigana na mtu mwenye point za kutosha kumrudisha kileleni

na Baina Mazola katika uzito wake yeye  ni namba tatu katika boxrec nchini hivyo nae anataka kuwa zaidi ya bondia Momba na ndio anatishia amani katika uzito uho kwa sasa

nae bondia Momba amesema baada ya kupoteza mpambano wake nje ya nchi sasa wadogo zake wanamtaka kucheza nae kwani inaonekana kiwango changu kimepungua na kudiliki watoto wadogo kunitaka mimi ata ivyo nashukuru uhu mchezo mimi ni kazi yangu naitegemea ivyo nitaakikisha simpi nafasi ata chembe kwa kumpiga kipigo kibaya sana ambacho ajawai kupigwa tanga aanze mchezo wa masumbwi nchini 

nae bondia Mazola amesema kwa sasa yupo vizuri sana na anawaomba mashabiki zake kuwa na moli ya kwenda bagamoyo ambapo promota kafanya vizuri sana klupereka mpambao huu uko sisi mabondia wote wawili tuna umarufu mkubwa sana maeneo ya manzese na vitongoji vyake ata hivyo nita akikisha nampiga Momba kama begi kwa kuwa sasa ana jipya nimeona stail zake zote anazotumia kupigana sijaona jipya hivyo ajiandae kwa kipigo tu

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile

Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

Monday, January 11, 2016

MCHUMIATUMBO ASAINI KUPIGANA NA BENK MWAKALEBELA JANUARY 30


Bondia Alphonce Mchumiatumbo kushoto akipokea mkataba alio saini kutoka kwa Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Chaurembo Palasa kwa ajili ya kupambana na Benk Mwakalebela wa Mbeya Picha na SUPER D BOXING NEWS


 Na Mwandishi Wetu

BONDIA Alphonce Mchumiatumbo amesaini mkataba wa kuzipiga na Benki Mwakalebelajanuary 30 katika ukumbi wa sativa Kyela Mbeya mpambano uho wa raundi nane wa uzito wa juu utafanyika kwa mara ya kwanza katika mkoa uho

akisaini mkataba uho mbele ya Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Chaurembo Palasa amesema ata akikisha kuwa mabondia wa uzito wa juu wanakuwa juu zaidi kwa mapambano hayo katika uzito uho

Mchumiatumbo alisema kuwa kwa sasa yupo katika mazoezi mazito chini ya kocha wake
Juma Urungu 'Mkebezi' 


ambapo kwa siku amekuwa akifanya mazoezi mara mbili au tatu kwa ajili ya kujiandaa na mpambano uho

nae Rais wa  TPBC Chaurembo Palasa ameongeza kwa kusema chama chao kimejizatiti kuinua mchezo wa ngumi kwa kufata taratibu na sheria za mchezo uho wa masumbwi nchini

kwanza wata akikisha kila bondia anapima afya na uzito wake kwa usalama wa mabondia wenyewe na usalama wao wawapo mchezoni

aliongeza kwa kusema kuwa watapima afya siku tano kabla ya mpambano huo ili kujilidhisha na afya za mabondia hawo wenye uzito wa juu nchini ambapo mabondia hawo wamekuwa adimu sana hapa nchini

BONDIA MCHUMIATUMBO KUMKABILI BENK MWAKALEBELA JANUARY 30 KYELA MBEYA


Bondia Alphonce Mchumiatumbo kushoto akipokea mkataba alio saini kutoka kwa Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Chaurembo Palasa kwa ajili ya kupambana na Benk Mwakalebela wa Mbeya Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Alphonce Mchumiatumbo kulia akisoma mkataba wake na kocha wake Juma Urungu 'Mkebezi'

Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Chaurembo Palasa kulia akizungumza na promota juu ya mpambano wa Alphonce Mchumiatumbo katikati

Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Chaurembo Palasa kulia akimpatia kiasi cha fedha bondia Alphonce Mchumiatumbo kushoto ni

Bondia Alphonce Mchumiatumbo akisaini mkataba wa kupambana na Benki Mwakalebela January 30

Friday, January 8, 2016

MABONDIA KAONEKA NA MAPAMBANO KUZICHAPA FEB 14 TANDIKA


Mabondia Shabani Kaoneka kushoto akitunishiana misuli na Imani Mapambano baada ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kupambana feb 14 katika ukumbi wa musoma bar uliopo tandika maguruwe katikati ni mdau wa mchezo wa masumbwi Zahoro Maganga 'Super Diego'  picha na SUPER D BOXING NEWS
Mdau wa mchezo wa masumbwi nchini Zahoro Maganga 'Super Diego'  kushoto akimsainisha bondia Shabani Kaoneka kwa ajili ya mpambano wake na Imani Mapambano feb 14 katika ukumbi wa musoma bar uliopo tandika maguruwe kulia ni Rais wa TPBO Yassin Abdallah
picha na SUPER D BOXING NEWS

Na Mwandishi Wetu
Mabondia Shabani Kaoneka na Imani Mapambano wamesaini mkataba wa kuzipiga siku ya feb 14  uzito wa kg 74 katika ukumbi wa musoma bar uliopo tandika maguruwe

mpambano huo wa raundi nane utasimamiwa na oganaizesheni ya ngumi za kulipwa TPBO chini ya rais wake Yassin Abdallah 'ostadhi' mpambano huo wenye kugombaniwa kwa kila mmoja kuwa juu ya mwenzie ambapo bondia Kaoneka ni namba 11 katika viwango vya ubora nchini ambapo amepigana mapambano 13 akishinda 5 kupigwa 5 na sale 3

 atakuwa na kibarua kizito cha ku lilia namba yake kwa mtu wa chini yake Imani Mapambano anaeshikilia nafasi ya 12 ya ubora kwa mabondia wa Tanzania akiwa amecheza mapambano 7 akishinda 4 na kupoteza 3

katika mpambano mwingine utawakutanisha mabondia Hassan Mwakinyo atakae pambana na Salumu Salumu katika mpambano wa raundi sita siku hiyo

ANT LATIFA MASASI HATOA HUDUMA ZA AFYA KWA WATOTO YATIMA WANAOLELEWA KATIKA KITUO CHA DARUl-ARQAM CHLDRENS HOME


Muhudumu wa Afya ya baba mama na mtoto wa kituo cha alafa kilichopo wilaya ta Temeke Bi, Latifa Masasi kushoto akichukuwa vipimo vya damu ya mtoto Raban Mansur wakati alipotembelea kituo cha watoto yatima cha Darul-Arqam Childrens Home kilichopo tandika magorofani kwa ajili ya kuwapima afya watoto wanao lelewa katika kituo hicho
Muhudumu wa Afya ya baba mama na mtoto wa kituo cha alafa kilichopo wilaya ta Temeke Bi, Latifa Masasi kushoto akichukuwa vipimo vya damu kwa mtoto Abdulatif Said kwa ajili ya kujua afya yake kushoto ni Hamis Rajabu
wakati alipotembelea kituo cha watoto yatima cha Darul-Arqam Childrens Home kilichopo tandika magorofani kwa ajili ya kuwapima afya watoto wanao lelewa katika kituo hicho

Muhudumu wa Afya ya baba mama na mtoto wa kituo cha alafa kilichopo wilaya ta Temeke Bi, Latifa Masasi kushoto akichukuwa vipimo



Muhudumu wa Afya ya baba mama na mtoto wa kituo cha alafa kilichopo wilaya ta Temeke Bi, Latifa Masasi kushoto akichukuwa vipimo vya damu kwa mtoto Aman Ramadhani kwa ajili ya vipimo
wakati alipotembelea kituo cha watoto yatima cha Darul-Arqam Childrens Home kilichopo tandika magorofani kwa ajili ya kuwapima afya watoto wanao lelewa katika kituo hicho

Sunday, January 3, 2016

CHEKA KUPANDA URINGONI FEB 23 DAR ES SALAAM


Promota Juma Msangi kushoto akitambulisha mpambano wa bondia Fransic Cheka atakaepambana na Geard Ajetovic wa Serbia mbele ya waandishi wa habari Dar es salaam jana mpambano utakaofanyika feb 27 katika uwanja wa leaders club wengine ni Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi' pamoja na Meneja msaidizi wa bondia  Faransic Cheka  Picha na Picha na SUPER D BOXING NEWS
Promota Juma Msangi kushoto akitambulisha mpambano wa bondia Fransic Cheka atakaepambana na Geard Ajetovic wa Serbia mbele ya waandishi wa habari Dar es salaam jana mpambano utakaofanyika feb 27 katika uwanja wa leaders club wengine ni Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi' pamoja na Meneja msaidizi wa bondia  Faransic Cheka  Picha na Picha na SUPER D BOXING NEWS