Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, January 11, 2015

IKOTA APANIA KUJUA MCHEZO WA MASUMBWI KWA KUWA UPO KATIKA DAMU YAKE



Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimwelekeza jinsi ya kurusha makonde bondia Zainabu 'Ikota' Mhamila ambaye ni binti yake anaependa ngumi kwa ajili ya kujiweka fiti katika mazoezi picha na SUPER D BOXING NEWS

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimwelekeza jinsi ya kurusha makonde bondia Zainabu 'Ikota' Mhamila ambaye ni binti yake anaependa ngumi kwa ajili ya kujiweka fiti katika mazoezi picha na SUPER D BOXING NEWS

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimwelekeza jinsi ya kurusha makonde bondia Zainabu 'Ikota' Mhamila ambaye ni binti yake anaependa ngumi kwa ajili ya kujiweka fiti katika mazoezi picha na SUPER D BOXING NEWS

 Bondia Zainabu Ikota Mhamila kushoto akifundishwa jinsi ya kutupa makonde na baba yake mzazi wakati wa mazoezi yaliyofanyika shule ya uhuru Dar es salaam picha na SUPER D BOXING NEWS
ZAINABU 'IKOTA' MHAMILA  NA RAJABU MHAMILA  SUPER D



Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akiwa na binti yake baada ya mazoezi

RAIS KIKWETE AKABIDHI VITABU 201 KWA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI



Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza   Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange  alipokuwa akimjshukuru kwa kutoa vitabu 2752 kwa Chuo cha Ulinzi na makataba zingine za  JWTZ wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vitabu 201 kwa ajili ya Maktaba ya Chuo cha Ulinzi (National Defence College - NDC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam Ijumaa January 9, 2015.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi baadhi ya vitabu   na  Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange. Rais Kikwete amekabidhi  vitabu hivyo 201 kwa ajili ya Maktaba ya Chuo cha Ulinzi (National Defence College - NDC)  iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam Ijumaa January 9, 2015. Rais kikwete, ambaye ameshachangia jumla ya vitabu 2752 katika  maktaba ya chuo hicho na chuo cha Monduli katika vipindi tofati,  amesema elimu imo vitabuni, na ili kuelemika yapaswa mtu asome vitabu, na kwamba taasisi ya elimu inakamilika ikiwa na vitabu.PICHA/IKULU

Thursday, January 8, 2015

MABONDIA IDDI BONGE NA ALIPHONCE MCHUMIATUMBO KUZIPIGA FEB 14


NA MWANDISHI WETU

MABONDIA wenye uzito wa juu nchini Aliphonce Mchumiatumbo na Iddi Kipandu 'Iddi Bonge' watapambana Feb 14 katika ukumbi wa P.T.A sabasaba wakigombania ubingwa wa taifa pamoja na pikipiki akizungumzia mpambano huo promota Shabani Manyoka amesema kupitia kampuni ya Mahamba Incorporation Limited wameamua kuandaa mpambano huo wa uzito wa juu ambao ni admu sana nchini kufanyika na ndio mabondia wanaokubalika Duniani kote

mpambano huo wa raundi kumi utakuwa ni wa aina yake kwa kuwa kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi ambapo bondia Iddi Mnyeke atapambana na Yonas Sego wakati Sahani Kaoneka atamkabili Saidi Mbelwa, na Deo Samweli akipambana na Adam Ngange Juma fundi atakabiliana na Bakari Ostadhi na Amani Bariki 'Manny Chuga' atapambana na Mohamed Kashinde siku hiyo pia kutakuwa na mpambano mwingine wa utangulizi wa uzito wa juu kati ya Bank Mwakalebela atakae mkabili Frank Kimbwilo

Manyoka aliongeza kwa kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha ndani na nje ya ukumbi huo ambapo amesha wasiliana na walinzi mbalimbali
siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali 
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

Serikali yatumia Shilingi Bilioni 881 katika Mradi wa REA Awamu ya Pili


Mmoja wa wakazi kutoka katika Kata ya Nkoma iliyopo  Wilayani Meatu mkoani Simiyu  (kushoto) akitoa neno la shukrani mbele ya  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) baada ya Wizara ya Nishati na Madini  kusambaza umeme  katika kata hiyo kupitia  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili. Kijiji cha Nkoma ni moja ya vijiji  170  vilivyopo mkoani Simiyu vilivyofaidika na mradi wa umeme  vijijini  unaotekelezwa na  REA Awamu ya Pili.
Mtaalamu kutoka  Kampuni ya  LTL (PVT) LTD inayosambaza miundombinu  ya umeme vijijini katika Wilaya ya Maswa  chini ya mradi wa REA Awamu ya PIli  Michael  Marenye (kulia), akifafanua hatua iliyofikiwa ya uunganishaji wa umeme  katika  Kata ya Balyanaga mbele  ya  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) mara Waziri  Muhongo alipofanya mkutano  na wakazi wa Kata Balyanaga ili  kusikiliza kero zao.

Na Greyson Mwase, Maswa.
Meneja Utaalamu Elekezi  kutoka  Wakala wa Nishati  Vijijini (REA) Gissima Nyamohanga amesema kuwa serikali imetumia shilingi bilioni 881 katika mradi wa kusambaza umeme  vijijini  unaotekelezwa na  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili.
Nyamohanga aliyasema hayo kwenye  sherehe za uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini unaofadhiliwa na REA uliofanyika katika kata ya Shishiyu wilayani Maswa mkoani  Simiyu.
Alisema kuwa Mradi wa  REA  Awamu ya Pili  utaiwezesha  idadi ya  vijiji  vilivyounganishwa   na umeme 3734  kati ya vijiji 15,180 ambayo ni asilimia 24.6 kufikia vijiji 5,234 ambayo ni asilimia 34.5 ifikapo  mwezi Juni mwaka huu.
Aliongeza kuwa mradi wa REA Awamu ya Pili wa miaka miwili  ulioanza mwaka 2013, lengo lake lilikuwa  ni kuhakikisha kuwa vijiji vyote Tanzania vinapatiwa umeme hivyo kuboresha maisha  ya wananchi na kukuza uchumi wa nchi.
Akielezea mchango wa mradi wa usambazaji wa umeme  vijijini  unaotekelezwa na  REA katika kuboresha maisha  ya wananchi Nyamohanga alisema kuwa awali wananchi  wote walikuwa wakilipa  shilingi  467,000 kama  gharama ya kuunganishiwa umeme ambayo ilikuwa ni kubwa na kupelekea  wananchi wachache wenye uwezo kuwa na  nishati ya  umeme huku  ikiacha kundi kubwa la wasio na uwezo kuishi  gizani.
Alisema kuwa katika Awamu ya Kwanza ya REA gharama za uunganishaji wa umeme  zilishuka kutoka  shilingi 467,000 hadi shilingi 177,000 na kuongeza kuwa katika kuhakikisha  kila mwananchi anakuwa na uwezo wa kuunganishiwa umeme  Serikali iliamua  kubeba  gharama zote kupitia REA Awamu ya Pili na wananchi kutakiwa kuchangia shilingi 27,000 tu kama kodi ya ongezeko (VAT)
Alieleza kuwa mara baada ya kumalizika  kwa Awamu ya Pili ya REA, viongozi wataainisha  vijiji ambavyo havijapata  umeme REA Awamu ya Pili, ambapo vitajumuishwa katika mradi wa REA Awamu ya Tatu.
Nyamohanga alieleza michango mingine kuwa ni  kufungua  fursa za ajira na uwekezaji kwa vijana wa kitanzania, ufaulu  kuongozeka kwa shule za sekondari na kuboreshwa kwa huduma za afya.
“Kwa mfano kwa shughuli za kiuchumi bei ya kusaga  debe la mahindi ilikuwa ni shilingi 1,000 itashuka  hadi shilingi  500 kutokana na kwamba mashine za kusaga zitakuwa zinatumia  umeme badala ya  dizeli kama zamani,” alisema Nyamohanga
Wakati huohuo Meneja wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) Kanda ya  Ziwa Mhandisi  Joyce Ngahyoma akielezea jinsi ya kuunganishwa na huduma ya umeme kwa wananchi wa vijiji  vilivyopitiwa na mradi wa REA  Awamu ya Pili alisema kuwa wananchi wanaoishi  mita 30 karibu na miundombinu ya umeme wataunganishiwa kwa shilingi  27,000 na kuwataka kuchangamkia fursa hiyo kwa kuboresha makazi yao.
Alisema kwa wananchi wenye  nyumba zenye  vyumba viwili na vioski hawahitaji kufunga mfumo wa umeme kwenye nyumba zao (wiring) badala yake watashauriwa kununua kifaa maalumu kijulikanacho kama “UMETA” (Umeme Tayari) kinachoweza kutumika kama mfumo kwa kuwa na uwezo wa kuunganisha taa mbili na vifaa vingine  kama  vile jiko, friji na pasi.
Aliendelea kusema kuwa kifaa hicho kinachouzwa kwa gharama ya shilingi 37,000 kitakuwa ni mali ya mteja na endapo atahama makazi basi atakuwa huru kuhama pamoja na kifaa chake.

MADA MAUGO NA KALAMA NYILAWILA WASAIDI KUZIPIGA MARCH 8 P.T.A SABASABA




Mabondia Mada Maugo kushoto na Kalama Nyilawila wakitunishiana misuli wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika March 8 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Picha na SUPER D BOXING NEWS
Katibu mkuu wa chama cha ngumi za kulipwa nchini Antoni Rutta katikati akiwainua mikono juu mabondia Mada Maugo na Kalama Nyilawila wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika march 8 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Picha na SUPER D BOXING NEWS


Mabondia Mada Maugo kushoto na Kalama Nyilawila wakitunishiana misuli wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika March 8 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Picha na SUPER D BOXING NEWS
mabondia wakiwa katika picha ya pamoja kushoton ni Emilio Norfat,Nassibu Ramaradhani,Mohamed Matumla na Amosi Mwamakula

RIDHIWANI KIKWETE AAPA KUPAMBANA NA MATAPELI WA ARDHI JIMBO LA CHALINZE


 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete,akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, wakati wa ziara ya kikazi pamoja na kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge miezi  sita iliyopita.Ridhiwani kutoruhusu hata kipande cha heka moja kuporwa na matapeli katika jimbo lake la Chalinze.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Kijana Salumu Khamis akiuliza swali mbele ya Mbunge Ridhiwani Kikwete kuhusu tatizo la maji katika Kijiji cha Fukayosi
 Mkuu wa Miradi wa Mkoa wa Pwani wa Tanesco, Leo Mwakatobe, akielezea jinsi umeme utakavyosambazwa katika Kijiji cha Fukayosi na vijiji vingine Jimbo la Chalinze.
 Mwenyekiti mpya wa Serikali ya Kijiji cha Fukayosi, Salum Mkwecha akimshukuru mbunge kwa ahadi mbalimbali alizozitoa katika miradi mbalimbali katika kijiji hicho.
 Ridhiwani akibadilishana mawazo na mmoja wa watawa baada ya kumalizika kwa mkutano katika Kijiji cha Fukayosi Jimbo la Chalinze.
 Mwenyekiti mstaafu wa Kata ya Fukayosi,Adam Masoud  akimuomba Mbunge Ridhiwani kuhikisha anaweka miundombinu ya barabara na maji na masuala ya afya katika Kijiji cha Mkenge,wakati wa ziara yake katika Kata ya Fukayosi ya kuwashukuru kwa kumchagua pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuangalia jinsi ya kuzitafutia ufumbuzi.
 Mkazi wa Kijiji cha Mkenge, Khamis Mwanga akielezea kero ya barabara ya Mwavi hadi Mkenge ambayo alidai inarudisha nyuma maendeleo ya kijiji hicho hivyo kumtaka Ridhiwani awasaidia kuijenge barabara hiyo ili iweze kupitika bila matatizo katika vipindi vyote. Ridhiwani aliwajibu kuwa tayari barabara hiyo imepata mkandarasi anayetarajia kuanza kazi katika siku chache zijazo.
 Katibu wa CCM Tawi la Mkenge, Omar Seleman akimuomba Mbge Ridhiwani asaidie kumalizia ujenzi wa msikiti wa Mkenge, Ombi ambalo alilikubali na kuahidi kupaua kwa gharama zake.
 Ridhiwani akijibu maswali mbalimbali ya wananchi wakati wa mkutano katika Kijiji cha Mkenge
 Ridhiwani akikagua maendeleo ya ujenzi wa msikiti wa Mkenge ambao ameahidi kuchangia mabati na mbao za kupaua jengo hilo la ibada.
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Fukayosi, Olnjurie Marigwa akihtubia katika mkutano uliofanyika katika kijiji cha Mwavi, Kata ya Fukayosi
 Masoud Fundikira akimuomba Mbunge wao Ridhiwan, anzishe mashindano ya mpira wa miguu kuwania kikombe cha Ridhiwani Cup ili kuendeleza michezo katika jimbo hilo. Ridhiwani alilikubali ombi hilo kwa kuanzia kutoa misaada ya mipira na jezi katika kila timu ya kata za jimbo hilo.
 Ridhiwani akihutubia katika Kijiji cha Mwavi ambapo aliahidi kufuatilia kwa karibu kuhusu suala la alilogawiwa Mkorea ili kijiji cha mwwavi kipate haki.
 Katibu wa CCM Wilaya ya Bagamoyo Kombo Kamote, akiwafunda viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Mwavi waliochaguliwa hivi karibuni ili wawatendee haki wananchi.
 Ridhiwani akihutubia katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Kidomole, ambapo aliwajia juu anaowaita matapeli wanaouza ardhi katika Jimbo la Chalinze bila kufuata sheria na utaratibu. Alisema kuwa hayuko tayari kuona hata heka moja ya jimbo hilo ikikuzwa bila utaratibu.
Ridhiwani akiagana na Meya wa  Morogoro, Amir Nondo ambaye ni mzaliwa wa Kata ya Kiwangwa katika jimbo hilo la Chalinze.

Bondia mtanzania Omari Kimweri anayetesa Australia kutoa sapoti ya mafunzo ya ndondi Dar


Omari Kimweri

.Kutua Februari, apania kuzalisha akina Mayweather kibao nchini

NA Mwandishi wetu

NDONDI ni miongoni mwa michezo maarufu mno hapa Tanzania na duniani kwa ujumla.

Wapo wanamichezo waliojipatia heshima kubwa duniani kutokana na kufanikiwa kupitia mchezo wa ndondi.

Miongoni mwa wanamichezo hao ni nguli Mohammed Ali, Mike ‘Iron’ Tyson, Evender Holyfield, Floyd Mayweather, Manny Pacquiao na wengineo wengi.

Kwa hapa nchini, wapo mabondia waliojitengenezea majina wakiwamo Emmanuel Mlundwa, Habibu Kinyogoli 'Masta' Michael Yombayomba, Stanley Mabesi 'Ninja' Rashid Matumla, Ibrahimu Class 'King Class Mawe'  na wengineo wengi.

Lakini ikumbukwe kuwa ndondi ndio mchezo uliotoa mwanamichezo anayelipwa zaidi duniani kwa sasa ambaye si mwingine bali ni Mayweather, akifuatiwa na mwanasoka raia wa Ureno anayekipiga katika klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo.

Anayeshika nafasi ya tatu ni mchezaji wa mpira wa kikapu LeBron James, wakati mwanasoka anayechezea Barcelona ya Hispania, Muargentina Lionel Messi akishika nafasi ya nne, huku wa tano akiwa ni mkali wa mpira wa kikapu, Kobe Bryant.

Pamoja na mafanikio hayo katika ndondi, Tanzania imeonekana kuzidi kulala usingizi wa pono katika suala zima la kuvumbua na kuendeleza vipaji vya mchezo huo kama sehemu ya kutatua tatizo sugu la ajira linaloitesa nchi yetu kwa sasa.

Unapopita huko mitaani, unaweza kukutana na vijana wadogo wakiwa wanafanya mazoezi ya ngumi kwa kutumia vifaa visivyo rasmi ambavyo mwisho wa siku, huishia kuwadumaza badala ya kuwajenga kama walivyotarajiwa.

Hali hiyo imetokana na kukosekana kwa vifaa vya kujifunzia mchezo huo, zikiwamo kumbi na hata wataalam wa kuwapa ujuzi wa kuwawezesha kufikia mafanikioi ya akina Mayweather.

Ni kwa kufahamu hilo, wapo wadau wa ndondi ambao wamekuwa wakijitoa kusaidia vipaji vya ndondi hapa nchini, miongoni mwao akiwa ni Kocha wa Kimataifa wa Ndondi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’.

Bondia huyo wa zamani, ameshawahi kufanya jitihada kadha wa kadha kuendeleza ndondi hapa nchini, ikiwamo kutoa mafunzo kwa vijana chini ya klabu yake ya Ashanti Boxing Club na kupitia DVD zake zenye mapambano makali yaliyowahi kufanyika hapa nchini na duniani kwa ujumla, yakiwahusisha mabondia nyota.

Katika kuonyesha jinsi anavyoguswa na ndondi, Februari mwaka huu Super D atakuwa na ugeni mkubwa wa bondia Mtanzania anayefanya kazi zake nchini Deer Park, Victoria, Australia, Omari Kimweri ambaye anatua nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wanamasumbwi wa Tanzania.

Akizungumza Dar es salaam jana, Super D anasema kuwa ujio wa Kimweri ni fursa nyingine adimu kwa mabondia wa Tanzania katika kuona ni vipi wanaweza kutimiza ndoto zao za kutoka kimaisha kupitia mchezo huo.

Anasema kuwa Kimweri atatua akiwa na vifaa mbalimbali vya masumbwi ambapo pia atatoa mafunzo na mbinu mpya zinazotumiwa na mabondia wa nje kwa mabondia pamoja na kushuhudia mapambano kadhaa yatakayofanyika kwa kipindi atakachokuwapo hapa nchini.

“Kimweri anakuja akiwa na msafara wa watu kadhaa, akiwamo mwanasoka wa kike, Melanie Gines ambaye ni raia wa Hispania. Akiwa hapa nchini, Melanie atapata fursa ya kukutana na wanasoka wa kike wa hapa , kwani amechezea timu nyingi za Ulaya,  Hispania,” anasema Super D.

Anasema kuwa ujio wa Kimweri umewezeshwa kwa kiasi kikubwa na promota wake, Brian Amatruda ambaye ni miongoni mwa mapromota maarufu nchini kwao Australia, akiwa amekubali kutoa baadhi ya vifaa vya kisasa kutoka Hispania na Marekani kwa ajili ya ziara hiyo.

Super D anasema kuwa Kimweri ambaye ni bingwa wa WBO, atatua nchini akiwa na mikanda yake yote aliyowahi kutwaa, ukiwamo wa ubingwa wa Australia, lengo likiwa ni kuwahamasisha vijana wa kitanzania kujikita zaidi katika ndondi.

“Nimezungumza na Kimweri na ameonyesha kuwa na uchungu wa kuwainua mabondia wa hapa nchini ili waweze kutimiza ndoto zao na anafanya hivyo chini ya mradi wake wa ‘Kimweri Project’ na atakuwa hapa nchini kwa wiki moja,” anasema.

Anasema kuwa ujio wa bondia huyo uliochagizwa na Super D Boxing Coach and Promotion, umelenga kuwahamasiaha mabondia kucheza mara kwa mara ili kupandisha viwango vyao kwani hiyo ndio siri ya mafanikio ya wanamasumbwi wengi duniani.


Mbali ya mafunzo kutoka kwa Kimweri, pia katika ziara zake zote sehemu mbalimbali nchini, kutakuwa na uuzwaji wa DVD za Super D zenye lengo la kutoa mafunzo kupitia mapambano ya mabondia maarufu duniani, akiwamo Floyd Mayweather,Manny Paquaio, Mohamerd Alli, na wa hapa nchini kama Mbwana Matumla, Francis

Miyeyusho,Ibrahimu Class' King Class Mawe' ambaye ni bingwa wa WPBF Africa na wengineo.
OMARI KIMWERI
bondia  Omari Kimweri ambaye ni bingwa wa uzito wa flyweight nchini Deer Park, Victoria, Australia anatalajia kucheza mpambano wake mwingine march 13 mpambano utakaopigwa katika ukumbi wa
The Melbourne Pavilion, Flemington, Victoria, Australia
   
No comments:

Airtel kuzindua Airtel UNI 255 J-mosi maalum kwa Wanafunzi UDSM katika Viwanja vya Mabibo Hostel




Afisa Masoko wa Airtel Henrick Bruno akionyesha moja kati ya vocha za Airtel UNI255 maalum kwa vyuo vikuu nchini tayari kwa uzinduzi jumamosi hii.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
· Ney wa Mitego, Roma Mkatoliki, Shilole kupamba uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel UDSM 
 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imebainisha kuwa mwishoni mwa wiki hii itazindua rasmi huduma mpya maalum kwaajili ya kutoa huduma nafuu za mawasiliano kwa wanafunzi walioko vyuoni katika chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM ambapo hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo inayojulikana kama Airtel UNI 255 kwa vyuo vikuu vilivyopo Dar es salaam itafanyika katika viwanja vya Mabibo hostel 
 Akiongea kuhusiana na uzinduzi wa huduma hiyo Meneja uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando amesema “Airtel Uni 255 ni huduma pekee yakibunifu toka Airtel Maalum kwa wanafunzi wa vyuo yenye kuwapa unafuu wa kuwasiliana wawapo chuoni, sasa wanafunzi wote wa chuo wanapotaka kupata nyongeza ya vile wanavyosoma kwenye mtandao huduma  hiii  ndio jibu sahihi kwao kutokana na unafuu wake kwenye inteneti, kupiga simu na hata sms. Huduma hii tayari tumeshaizindua kwa vyuo vikuu vingine vya Dodoma, Mbeya, Iringa, Mwanza na imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa watumiaji wakiwemo wanafunzi na wale wote wanaotumia huduma hii maeneo ya vyuo”
 “Airtel tumeona ni vyema tuizindua hapa katika vyuo vya Dar es salaam wiki hii siku ya Jumamosi pale mabibo hostel ambapo mbali na uzinduzi kutakuwa na tamasha kubwa litakalopambwa na watoa burudani nguli akiwemo Ney wa Mitego, Roma Mkatoliki, Shilole pmaoja na DJ maarufu jiji Dj Zero aliongeza kusema Mmbando 
 Nae meneja wa huduma hiyo ya UNI 255 Anethy Muga alisema “Airtel tumeoana hii ni huduma maalum kwa wanafunzi na ndio maana tukaona ni vyema kuizindulia katika Hostel zao pale mabibo ambapo tunaamini wanafunzi wengi wa chuo kikuu hapa jijini wanaifahamu na wanaishi mabibo hivyo wanakaribishwa katika uzinduzi huo ambapo kiingilo chake ni BURE”
 Burudani zitakuwa zakutosha kupitia Airtel UNI 255  siku hiyo.
 Kampuni ya simu za mkononi ya airtel ilianzisha huduma ya UNI255 ili kuendana sambamba na mkakati wao wa kusaidia vyuo vikuu nchini kutumia ipasavyo huduma za mtandao ili kuboresha sekta ya elimu kwa lengo la kusaidia wateja wake walioko vyuoni kufikia malengo yao.

Thursday, December 25, 2014

SUPER D BOXING COACH AMSAIDIA VIFAA MUSSA CHITEPETE WA SONGEA


Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akimkabidhi vifaa bondia Mussa Chitepete wa Songea vilivyotolewa na Super D kwa kushilikiana na marafiki zake wa kwenye mtandao wengine kulia ni Kiliani Shayo na Rajabu Mkamba ambaye ni mdau mkubwa wa kuhamasisha kusaidia mchezo wa masumbwi Picha na SUPER D BOXING NEWS
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D katikati akionesha vifaa alivyompatika Mussa Chitepete wa Songea kushoto kulia ni mdau wa Rajabu Mkamba ambaye ni mdau mkubwa wa kuhamasisha kusaidia mchezo wa masumbwi Picha na SUPER D BOXING NEWS
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D katikati akionesha vifaa alivyompatika Mussa Chitepete wa Songea kushoto kulia ni mdau wa Rajabu Mkamba ambaye ni mdau mkubwa wa kuhamasisha kusaidia mchezo wa masumbwi Picha na SUPER D BOXING NEWS




Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimtambulisha bindia wa kike ambaye ndie bingwa wa wanawake kwa sasa Halima Ramadhani

KOCHA SUPER D AMPIGA TAFU YA VIFAA BONDIA MUSSA CHITEPETE WA SONGEA VIFAA


Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akimkabidhi vifaa bondia Mussa Chitepete wa Songea vilivyotolewa na Super D kwa kushilikiana na marafiki zake wa kwenye mtandao wengine kulia ni Kiliani Shayo na Rajabu Mkamba ambaye ni mdau mkubwa wa kuhamasisha kusaidia mchezo wa masumbwi Picha na SUPER D BOXING 


Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akimkabidhi vifaa bondia Mussa Chitepete wa Songea vilivyotolewa na Super D kwa kushilikiana na marafiki zake wa kwenye mtandao wengine kulia ni Kiliani Shayo na Rajabu Mkamba ambaye ni mdau mkubwa wa kuhamasisha kusaidia mchezo wa masumbwi Picha na SUPER D BOXING 
Na Mwandishi Wetu

KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kwa kushilikiana na marafiki zake wa kwenye mtandao wa kijamii wa watsupp wamemkabidhi vifaa bondia Mussa Chitepete wa Songea kwa ajili ya kuhamasisha mchezo wa masumwi nchini

Super D alimkabidhi vifaa hivyo bondia huyo hivi karibuni alivyotembelea jijini Dar es salaam kuja kushiliki mchezo wa masumbwi ambapo alipatiwa glove,gum shit,clip bandeji pamoja na kamba kwa ajili ya kurukia

vifaa hivyo vilivyotolewa na super D kwa kushilikiana na mdau mkubwa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mkumba ambaye ndie mwamasishaji mkubwa katika mtandao huo kwa ajili ya kusaidia mabondia

baada ya kukabidhiwa msaada huo bondia Mussa Chitepete wa Songea alishukulu wadau 
 mbalimbali kwa kumpatia vifaa na kumpongeza kocha Super D kwa kuanzisha mtandao ambaoumekuwa muhimu sana kwangu kwa mimi kupata vifaa najua sitotumia peke yangu wapo na wenzangu tutakao tumia nao pamoja vifaa hivi ambavyo itakuwa chachu ya kuinua mchezo wa masumbwi Songea

nae mdau mkubwa wa masumbwi nchini Rajabu Mkamba amesema kwa kushilikiana na Super D wamefanya mambo mengi kwa ajili ya kuinua mchezo wa masumbwi nchini hivyo atutoishia hapa tutaendelea kutoa sapoti kwa mabondia na wadau mbalimbali ili mchezo usonge mbele na wadhamini wajitokeze kusaidia ili vijana wawe na moyo wa kucheza mchezo wa masumbwi