
NIzar Khalfani akizungumza na mdau wa Sports ya Capital Radio ambayo huruka kila siku saa tatu kamili usiku hadi sa tatu na nusu, MAster Tindwa Mtopa, Nizar amesema wachezaji ili waweze kupata mafanikio wanalazimika kutumia muda wao wa ziada kufanya mazoezi mbali na muda ambao mchezaji anakuwa na kocha.
Amesema hiyo ilikuwa kwake ni moja ya chngamoto kubwa lililokuwa likimkabili wakati alipojiunga na klabu ya Vancouva ambayo mwakani inashiriki ligi ya Marekani.
Nizar amesema Tanzania inavipaji vya wachezaji wa zuri na wenye viwango ingawa wanakabiliwa na changamoto ya nguvu na kujituma.
Amesema ili wachezaji waweze kufanikiwa ni lazima wachukulie mpira kuwa ni kazi kama zilivyo kazi zingine na inamaslahi mazuri endapo mchezaji atajituma na kuwa na malengo.
No comments :
Post a Comment