Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, August 3, 2013

MAKAMU WA RAIS AKABIDHI ZAWADI ZA WASHINDI WA SHINDANO LA TATU LA KUHIFADHI QUR'AN TUKUFU JIJINI DAR



 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza za waumini wa dini ya Kiislamu, wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la tatu la kuhifadhi Qur'an Tukufu, iliyofanyika jana usiku Agosti 2, 2013 katika Msikiti wa Istiqaama, jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi ya Sh. milioni 2, mshindi wa kwanza wa kuhifadhi Juzuu 30, Abdulkarim Khamis, wakati wa hafla ya kuwakirimu na kukabidhi zawadi kwa  washindi hao iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala jijini Dar es Salaam, jana usiku.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi ya Sh. milioni 1.5, mshindi wa kwanza wa kuhifadhi Juzuu 20, Maryam Nassor (8), wakati wa hafla ya kuwakirimu na kukabidhi zawadi kwa washindi hao iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala jijini Dar es Salaam, jana usiku.
 Mtoto Maryam Nassor (8) akisoma moja ya haya iliyo katika kitabu cha Juzuu kwa kichwa, wakati wa hafla ya kuwakirimu na kukabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la tatu la kuhifadhi Juzuu iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala jijini Dar es Salaam, jana usiku.
 Zoezi la utoaji zawadi likiendelea.
 Zoezi la utoaji zawadi likiendelea.
 Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, kuzungumza na waumini wa dini ya Kiislamu, wakati wa hafla ya Kuwakirimu na kukabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la tatu la kuhifadhi Juzuu, iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala jijini Dar es Salaam, jana usiku.
 Sehemu ya waumini wa dini ya Kiislamu, waliohudhuria hafla hiyo.
 Sehemu ya waumini wa dini ya Kiislamu, waliohudhuria hafla hiyo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu baada ya kukabidhi zawadi za washindi wa shindano la tatu la kuhifadhi Juzuu, wakati wa hafla ya kuwakirimu wasindi hao iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala jijini Dar es Salaam jana usiku.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu baada ya kukabidhi zawadi za washindi wa shindano la tatu la kuhifadhi Juzuu, wakati wa hafla ya kuwakirimu wasindi hao iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala jijini Dar es Salaam jana usiku.

Friday, August 2, 2013

NASSIBU RAMADHANI AMTAMBIA JUMA FUNDI




IMG_4971
Promota wa mpambano wa masumbwi Side Mkigoma (katikati) akiwainua mikono juu mabondia Juma Fundi (kushoto) na Nassibu Ramadhani.
BONDIA Nassibu Ramadhani amejigamba kuwa atamchakaza mpinzani wake Juma Fundi wakati wa mpambano wao utakaopigwa siku ya Idi pili katika ukumbi wa friends corner Manzese

Aliongeza kwa kusema unajua mimi anaeniumiza kichwa kwa sasa ni Fransic Miyeyusho pekee kwa Tanzania hii kwa kuwa nilicheza nae na nikashindwa kummudu ata hivyo ipo siku nitaomba mpambano mwingine wa marudiano nae hivyo nimemuweka kiporo

Bondia huyo aliendelea kujinasibu kwa kusema kwa sasa mimi ni nambari One hivyo fundi ategemee kipigo cha mbwa mwizi kwa ni ato furukuta
Naomba mashabiki wangu wa ngumi mjitokeze kuja kunishangilia ata kama wewe sio shabiki wango njoo uone ngumi nitakazokuwa nikicheza na utamini kuwa mimi ni kiboko yao

Ramadhani ambaye ucheza kwa kasi kubwa sana awapo ulingoni amekuwa kivutio kikubwa kwa mashabiki na kumpachika jina la Mann Paquaio wa Philipins kwa kuwa wote wanatanguliza mguu wa kulia mbele 

Siku hiyo kutakuwa na uhuzwaji wa DVD mpya kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa masumbwi zatakazokuwa zikisabazwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'

pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi wakisindikiza mpambano huo

USAJILI WA WACHEZAJI WA LIGI KUU KUFIKIA TAMATI AGOSTI 5



Beki wa Kimataifa wa Uganda, aliyewahi kuichezea Klabu ya Simba, Joseph Owino (katikati) akisaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Klabu hiyo. Kushoto ni Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang'ale 'Kinesi' na (kulia) ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Simba, Said Pamba.
**************************
Na Boniface Wambura, Dar
Usajili wa wachezaji kwa hatua ya kwanza msimu huu (2013/2014) sasa utafungwa Jumatatu (Agosti 5 mwaka huu) badala ya Agosti 3 mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa awali.
Uamuzi wa kusogeza mbele umetokana kuchelewa kupata disc ya usajili msimu huu ambayo ndiyo inayotumika kwa usajili wa elektroniki unaofanywa kwa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom. Disc hiyo ambayo hutolewa na kampuni ya NAS Technology ya Tunisia tayari imeshawasili.
Kutokana na mabadiliko hayo, sasa kipindi cha pingamizi kitakuwa kati ya Agosti 6 na 12 mwaka huu wakati Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji itakutana Agosti 13 na 14 mwaka huu kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.
Hatua ya pili ya usajili itaanza tena Agosti 15 mwaka huu ikihusisha wachezaji ambao watakuwa hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu. Timu zitakazoruhusiwa kusajili ni zile ambazo zitakuwa hazijajaza nafasi zote za usajili. Dirisha dogo za usajili litafunguliwa kuanzia Novemba 15 mwaka huu hadi Desemba 15 mwaka huu.
Pia klabu za Ligi Kuu ya Vodacom zinapowasilisha usajili wao zinatakiwa kuambatanisha nyaraka zinazoonesha viwanja vyao vya mazoezi, nakala za bima kwa wachezaji pamoja na benchi la ufundi. Masuala hayo yameelezwa kwenye Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom

BAADA YA ROSE NDAUKA KUHUSISHWA KATIKA FUMANIZI...!! HAYA NDIYO MANENO YA MCHUMBA WAKE ROSE KUHUSU SAKATA HILO





BAADA ya msanii wa filamu nchini Rose Ndauka kuripotiwa kufumaniwa akiingia gesti na msanii chipukizi wa muziki wa bongo fleva Nassoro Ayoub 'Dogo Nasry' huku akiwa amevaa baibui kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, mumewake mtaarajiwa Maliki Bandawe 'Chiwaman' amjia juu msanii huyo kwa madai ya kumchafua mpenzi wake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Chiwaman aliweka wazi kuwa msanii huyo Nasry ambaye alimuomba Rose aweze kushiriki kwenye video yake, walishindwa kufikia maamuzi kutokana na kiwango cha malipo kuwa madogo, na badala yake msanii huyo alimuomba wapige picha kama ukumbusho.

Alisema kuwa kitendo hicho cha kupiga picha na msanii huyo wakati wapo katika mazungumzo ya awali ya kukubaliana malipo ndizo picha alizotumia msanii huyo na kudai kuwa alikuwa naye nyumba ya wageni kitendo ambacho si cha kweli.

"Hawa wasanii wachanga wanatafuta umaarufu vibaya kwa kuwachafua watu, ilikuwa amemuomba Rose ashiriki kwenye video yake na ndipo walipokutana kwa ajili ya mazungumzo hayo na alikuwa na mdogo wangu sasa hapo masuala ya gesti yametokea wapi" alisema Maliki.

Aliongezea kuwa "kama nilikuwa sijui hicho kitu na kwa jinsi mambo yalivyokuwa ningeweza kumuacha mchumba wangu ninayempenda kwa dhati, ila msanii huyo alichokifanya siyo jambo sahihi, kwani alimuomba apige naye picha na Rose alikubali huku bila kujua nia yake ".

Maliki alisema kuwa huyo msanii anatafuta umaarufu kwa kuchafua majina ya watu wengine, kitu ambacho hakina mashiko kwenye jamii.

Nyota wa zamani wa Coastal Union afariki kwa ajali ya gari Morogoro





SOURCE: SALUTI5

WAFUGAJI WATAKA KATIBA MPYA KUWARUHUSU KUUA SIMBA WANAOVAMIA MIFUGO YAO NCHINI.



Wafugaji  wakazi wa Mlowa  jimbo la Isimani  mkoa  wa Iringa  wakiwa katika mkutano wa kukusanya maoni ya katiba  mpya jana. PICHA http://richard-mwaikenda.blogspot.com/
Mfugaji  akitoa maoni yake  juu ya katiba  mpya  na  kulalamikia  simba  wanaoua mifugo  yao
Mwenzeshaji  Happy Kikoga  kutoka  kituo cha msaada cha sheria na  haki  za  binadamu akiwasomea  rasimu  ya  katiba wananchi  wa Mlowa Isimani
Mmoja kati ya  wanawake  wakazi wa Mlowa  akichangia katika mkutano huo kwa  kutaka  wanaopandikiza chuki  za kidini  kupewa adhabu kali.
WAFUGAJI jamii ya  kimasai na Mang'ati  wakazi  wa Mlowa  jimbo la Isimani  wilaya ya  Iringa  vijijini mkoani Iringa  wametaka katiba mpya ijayo  kuwaweza kuwatetea wafugaji kwa  kuingiza  kipengere  kitakachowaruhusu  wao  kuingia katika  hifadhi ya  Taifa ya  Ruaha  kuwasaka  simba  wanaoua mifugo  yao  kuwaua.
Wafugaji  hao  walitoa  maoni hayo juzi  katika  ofisi  za serikali ya  kata  wakati  wakichangia rasmu ya katiba mpya  zoezi lililoendeshwa na kituo  cha  msaada cha sheria na  haki  za  binadamu.
Walisema  kuwa  Simba  wameendelea kuwatesa na  kila  wakati  wanaendelea  kuua mifugo yao na  pindi  wanapofanya msako  wa  kuwasaka  askari  wa  wanyamapori  wanawachukulia hatua  kali .
Hivyo  walisema  ili  katiba  ijayo  iweze kutambua haki za  wanyama  wengine na  pia  kutambua  uwepo  wa  wafugaji ni  vema kuingizwa  kipengere  kinachowapa nafasi  ya  kuwaua  simba wanaokula  wanyama  wao.
Mbali ya  kutaka  kuwekwa kwa  kipengere  hicho  bado  wafugaji hao  walitaka  kutambuliwa  rasmi  na katiba  ijayo badala  ya ilivyo sasa  ambapo  wamekuwa wakihamishwa  kama  wanyama . Pamoja na  wafugaji hao kwa upande  wake wananchi  wa kawaida  wameeleza  kusikitishwa na hatua  iliyofikiwa ya mchakato  huo wa katiba  mpya  hatua ya  kukusanya maoni  juu ya rasmu wakati  wao hata katiba  iliyopita  hawaijui na rasmu  hiyo  hawajapata  kuoina.

UCHAWI WATUMIKA MAONYESHO YA WAKULIMA KANDA YA MASHARIKI NANE NANE KUWAVUTA WATU KATIKA MABANDA MOROGORO.



 Msanii wa salakasi, Hassan Mkenjula a.k.a Spider Man akionyesha uchwi unaotokana na mazoezi katika moja ya mabanda kwenye maonyesho ya wakulima kanda ya mashariki namna anavyoweza kulala akiwa juu ya kamba yanayofanyika kwenye uwanja wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere Nane Nane Manispaa ya Morogoro. 
PICHA WWW.JUMAMTANDA.BLOGSPOT.COM
 Baada ya kuvaa nguo zote Spider Man akion
ekana huku akitembea juu ya kamba baada ya kuvaa nguo ikiwemo fulana, tai na suruali.
 Baada ya kuvaa zote juu ya kamba hiyo.
 akimalizia kuvaa mguu wa kushoto.
 akivaa mguu wa kulia.
 suari kabla ya kuivaa akiwa juu ya kamba hiyo.
 akivaa.
 Akionyesha fulana kabla ya kuivaa.
 
Alianza hivi wakati akifuata nguo ili aweze kuvaa.

Thursday, August 1, 2013

STARTIMES KUONGEZA VIPINDI NA CHANALI,MAADHIMISHO YA MIAKA MITATU




Ofisa Habari wa Kampuni ya Startimes  Erick Cyprian kushoto akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuongezaka kwa chanal wakati wa kipindi hiki cha kutimiza miaka mitatu tangu ianzishwe kampuni hiyo kulia ni Ofisa Masoko wa Kampuni hiyo Zuhura Hanif Picha na SUPER D

Ofisa Habari wa Kampuni ya Startimes  Erick Cyprian kushoto akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuongezaka kwa chanal wakati wa kipindi hiki cha kutimiza miaka mitatu tangu ianzishwe kampuni hiyo kulia ni Ofisa Masoko wa Kampuni hiyo Zuhura Hanif Picha na SUPER D
Ofisa Habari wa Kampuni ya Startimes  Erick Cyprian kushoto akizungumza  kwa msisitizo wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu kuongezaka kwa chanal wakati wa kipindi hiki cha kutimiza miaka mitatu tangu ianzishwe kampuni hiyo kulia ni Ofisa Masoko wa Kampuni hiyo Zuhura Hanif Picha na SUPER D

Ofisa Habari wa Kampuni ya Startimes  Erick Cyprian kushoto akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuongezaka kwa chanal wakati wa kipindi hiki cha kutimiza miaka mitatu tangu ianzishwe kampuni hiyo kulia ni Ofisa Masoko wa Kampuni hiyo Zuhura Hanif Picha na SUPER D

EAST AFRIKA MELOD KUWASHA MOTO Traventine Hotel IDDI PILI


BENDI Kongwe ya muziki wa Taarabu Nchini East African Melody imetangaza kutoa burudani wakati wa shamra shamra za sikukuu ya iddi  pili  katika  ukumbi wa Traventine Hotel akizungumzia onesho hilo  mwandaaji wa onesho hilo Habbas Husseni 'Chezntembaa'

Amesema ameamua kuchukua bendi hiyo itoe burudani ili ikonge nyoyo za mashabiki mbalimbali wa taarabu ambapo walikosa raha hizo wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani

Katika Shamra shamra hizo za sikukuu ya iddi  watakuwa wakitambulisha nyimbo zao tatu mpya  ambazo ni Rabb nilinde ulioimwa na Mwanahawa Ally, Ukewenza sio dili,ulioimbwa na Mwanaidi Shabani na Stara ulioibwa na Sabaha Muchacho,
Ambapo siku hiyo wageni waalikwa ni Pr. Muhamed Elyas, Bi Shakirla ,Muhamed Issa Matona na wengine ambapo kiingilio 5000, ndani ya ukumbi wa Traventine Hotel iliyopo magomeni jijini Dar es salaam

Bendi hiyo imeakikisha kukonga nyoyo za mashabiki wao jukwaani kwa kuwa watakuwa wa kwanza kusikiliza nyimbo zao mpya wakiwa live jukwaani

NEY WA MITEGO ATUMA 'SALAMU ZAO’




Na Elizabeth John

MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Emmanuel Elibariki ‘Ney wa Mitego’ Anatarajia kuachia kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Salamu zao’ hivi karibuni.

 Ney wa Mitego ni kati ya msanii ambaye anafanya vizuri katika soko hilo, na pia anasema ameamua kufanya kazi hiyo kwa lengo la kuburudisha na kuwaelimisha wapenzi wa kazi zake.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Ney wa Mitego alisema kazi hiyo anatarajia kuanza kuisambaza wiki ijayo ambapo kwa sasa anatarajia kuanza ‘kushuti’ picha mbalimbali kwa ajili ya video ya kazi hiyo.

“Wiki hii naanza kushuti katika sehemu mbalimbali, mashabiki wanatakiwa kuupokea vizuri wimbo huu kwani ni bonge la kazi, kama wanavyonijua mashabiki wangu sijawahi kufanya vibaya katika kazi zangu, naomba tu wakae mkao wa kula kwaajili ya kazi hiyo,” alisema Ney wa Mitego.


Msanii huyo ambaye kwasasa anatamba na kibao chake cha ‘Nasema nao’, aliwaomba mashabiki waipokee kazi hiyo kwani ina ujumbe mzito kwa jamii yote

PAULINE ZONGO AVUNJA UKIMYA




BAADA ya ukimya wa muda mrefu, mwimbaji nyota wa muziki wa kizazi kipya na  dansi, Pauline Zongo ameibuka upya na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Misukosuko ya mapenzi.

Pauline amerekodi kibao hicho na kundi jipya la muziki linalojulikana kwa jina la Ndege Watatu, linaloundwa na wanamuziki wengine wawili wa kike, Khadija Mnoga na Joan Matovolwa.

Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Pauline alisema tayari kibao hicho kimeshaanza kurushwa kwenye vituo mbalimbali vya redio nchini na kupokewa vizuri na mashabiki.

Mwanadada huyo, aliyekuwa mmoja wa wasanii wanaounda kundi la East Coast amesema, wameamua kuunda kundi hilo kwa lengo la kuleta changamoto mpya katika muziki.

Pauline alisema aliamua kuwa kimya kwa muda mrefu kwa sababu ya kulea mtoto wake wa pili mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu. Mtoto wake wa kwanza ana umri wa miaka sita.

Alisema ukimya wake huo pia ulilenga kusoma mwelekeo wa muziki na pia kujipanga upya kabla ya kurudi ulingoni akiwa na vitu tofauti.

Mwanamama huyo, ambaye ni mwajiriwa wa bendi ya TOT Plus alisema, wameamua kuliita kundi lao kwa jina la Ndege Watatu kwa sababu sauti zao zinafanana na wanakijua wanachokifanya.

Pauline alisema uamuzi wake wa kujiunga na TOT Plus ulilenga kukuza kipaji chake cha muziki na pia kuwaonyesha mashabiki kwamba ana uwezo mkubwa katika fani hiyo.

"Kusema kweli, huwezi kuwa mwanamuziki kama hujui kupiga ala yoyote ya muziki,"alisema mwanamama huyo, ambaye ana uwezo wa kupiga gita, drums na kinanda.

Licha ya kundi lake la TOT kumruhusu kuwa mwanamuziki huru, Pauline alisema hawezi kutoa albamu kila mwaka kwa vile akifanya hivyo, hawezi kupata manufaa makubwa.

Alisema mwanamuziki anatakiwa kusonga mbele akiwa na mabadiliko badala ya kufanya kitu kile kile kila mwaka.

Mwanamama huyo alisema hakujifunza muziki kutoka kwa mtu yoyote. Anasema kuna siku alilala akaota ndoto anapiga gita, drums, kinanda na kuimba na alipozinduka usingizini, akaamua kutimiza ndoto yake hiyo.

Pauline anakiri kuwa, asili yake ni Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Anasema mama ni Mcongo na baba yake ni Mtanzania.

"Mimi nilizaliwa Congo. Wakati huo baba alikuwa akija Congo kibiashara ndipo akakutana na mama na kwetu tupo watoto wengi tu. Baadaye ikatokea kutokuelewana kati ya baba na mama, hivyo mimi na mdogo zangu tukaja Tanzania na baba na ndugu zangu wengine walibaki na mama Congo,"alisema.

Pauline anasema pia kuwa ni kweli kwamba anaye pacha wake wa kiume anayeitwa Paul Zongo, ambaye kwa sasa ni prodyuza wa muziki nchini Afrika Kusini. Alisema Paul ameshiriki kutengeneza nyimbo za kundi la Malaika la Afrika Kusini na wanamuziki wengine wa nchi hiyo.

Alipoulizwa iwapo ni kweli amezaa mtoto wake wa pili na mwigizaji filamu nyota wa Bongo, anayejulikana kwa jina la Mtunisi, alikiri kwamba ni kweli.

"Ndio ni kweli, lakini kwa sasa tumeshaachana, kila mtu ana maisha yake. Nina mchumba wangu, ambaye Mungu akitujalia, mwishoni mwa mwaka huu tutafunga pingu za maisha. Tumeshakaa kwenye uchumba kwa miaka miwili sasa.Mchumba wangu naye ni pacha kama mimi, tunapendana sana,"alisema.

Je, ni kitu kipi ambacho Pauline anakijutia katika maisha yake?

"Kiukweli sitaki kuficha, uhusiano nilioingia na baba mtoto wangu naujutia sana. Laiti ningesikiliza ushauri wa watu wengi, yasingenikuta yaliyonikuta,"alisema.

"Nilikuwa sisikilizi yote niliyokuwa naambiwa juu ya tabia za mwanaume huyo, lakini baada ya kuyaona, niliishia kujuta maana mapenzi yake yalinipotezea hata mwelekeo wa maisha yangu. Lakini kwa sasa nina nguvu mpya na nipo huru, nimejifunza siku nyingine sitafanya makosa,"alisisitiza.

Pauline alianzia muziki akiwa na kundi la East Coast lililokuwa na wasanii mahiri kama vile Crazy GK, Khamis Mwinjuma 'Mwana FA' na Ambwene Yesaya 'AY' kabla ya kuhamia TOT.

Akiwa East Coast, alijipatia umaarufu mkubwa aliposhiriki kuimba kibao cha Sister Sister akishirikiana na Crazy GK wakati akiwa TOT, aling'ara kupitia kibao cha Mnyonge Mnyongeni, alichokiimba kwa kushirikiana na Badi Bakule na Abdul Misambano.

DIMPOZ AISAMBAZA 'TUPOGO’



Na Elizabeth John

BAADA ya kushindwa kuitambulisha mara kadhaa ngoma yake mpya inayofahamika kwa jina la ‘Topogo’, mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, ameisambaza ngoma hiyo katika vituo mbalimbali vya redio.

Dimpoz amehairisha utambulisho wa ngoma hiyo zaidi ya mara moja ambapo mara ya mwisho alitakiwa kuitambulisha katika ukumbi wa Kimataifa Club Bilicanas, Juni 30 kabla hajausambaza wiki iliyopita.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Ommy Dimpoz alisema ameamua kuusambaza wimbo huo bila kuutambulisha kutokana na sababu ambazo zipo nje ya uwezo wake na anawaomba wapenzi wa kazi zake waupokee wimbo huo kwa mikoni miwili.

Alisema katika wimbo huo, kamshirikisha nyota kutoka Nigeria, J Martin na kwamba anaamini kutakuwa na changamoto nyingi kwa wasanii wa bongo kutokana na uwepo wa mkali huyo.

 “Kiukweli J Martin ni msanii mkubwa na ana uwezo wa kulitawala jukwaa anapokuwa kazini; naamini nitafanya vizuri zaidi, ndiyo maana nimeamua kushirikiana naye, cha muhimu ni sapoti katika kazi zangu,” alisema Dimpoz.

Licha ya kutoka na nyota huyo, Dimpoz kwa sasa anatamba na kibao chake cha ‘Me and You’ alichomshirikisha chipukizi wa muziki huo, Vanesa Mdee, mbali na kuwa na vibao vingi ambavyo vimefanya vizuri katika tasnia ya muziki wa bongo fleva.

Juma Kaseja kutua Lupopo FC -DRC



Mlinda mlango wa Taifa Stars Juma Kaseja
NAHODHA wa timu ya soka ya taifa ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Juma Kaseja amesema kwamba amefanya mazungumzo tu na wakala wa klabu ya St. Eloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), lakini bado hajaingia Mkataba na klabu hiyo ya Lubumbashi.

Akizungumza jana mchana, Kaseja amesema kwamba mtu aliyejitambulisha kwake kama wakala wa Lupopo alimfuata wakafanya mazungumzo na kufikia makubalino juu ya dau la usajili, mshahara na mambo mengine ya msingi.

Hata hivyo, kipa huyo namba moja Tanzania amesema kwamba baada ya mazungumzo hayo na maafikiano, wakala huyo amepeleka majibu Lupopo ambao wakiafiki ndipo masuala ya Mkataba yatafuatia.

“Nimezisikia hizo habari, kwamba mimi tayari ni mchezaji wa Lupopo, hapana, si kweli. Ni kwamba tumefanya mazungumzo tu na wakala wao na tumefikia makubaliano, nasubiri hadi nisaini Mkataba ndipo nitajihesabu tayari ni mchezaji wa Lupopo,”alisema Kaseja.

Baada ya kuitumikia Simba SC tangu mwaka 2003, Kaseja hakuongezewa Mkataba klabu hiyo mwishoni mwa msimu naye ameamua kwenda kuanza maisha mapya sehemu nyingine.

Pamoja na Simba SC kutomuongezea Mkataba Kaseja, ameendelea kuwa kipa chaguo la kwanza timu ya taifa mbele ya kocha Mdenmark, Kim Poulsen.

Iwapo Kaseja atafanikiwa kuingia Mkataba na Lupopo atakwenda kuwa mpinzani mkuu wa wachezaji wenzake wa Taifa Stars, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea Tout Puissant Mazembe ya Lubumbashi.

Kaseja alicheza pamoja na Samatta na kiungo Mganda wa Mazembe, Patrick Ochan katika klabu ya Simba mwaka 2010 kabla ya 2011 wachezaji hao kuuzwa DRC. 

CCM YAIPONGEZA SERIKALI KURUDISHA NYUMA SUALA LA WANANCHI KULIPIA KODI LAINI ZA SIMU



NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeipongeza serikali, kwa uamuzi wake kurejesha bungeni kwa ajili ya mdajala zaidi, muswada wa sheria ulioanzisha kodi mpya ya tozo ya sh. 1,000 kwa laini ya simu.

Taarifa ya CCM iliyotolewa leo mjini Dodoma, na Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye imesema uamuzi huo umedhihirisha kwamba serikali inawasikiliza na kuwajali wananchi wake.

Akiripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari leo, Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa amekaririwa akisema kwamba mjadala kuhusu muswada wa sheria ya kodi hiyo ya tozo hiyo utafanyika wakati wa mkutano wa Bunge unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.

Baada ya kupitishwa na bunge Juni mwaka huu, na utekelezwaji wake kuanza rasmi Julai mwaka huu, CCM ilikuwa miongoni mwa wadau waliopinga vikali kuanzishwa kwa kodi ya tozo hiyo, ikieleza kwamba ni mzigo na usumbufu usio wa lazima kwa watumiaji wa simu ambao wengi matumizi yao ni ya kawaida.

Katika taarifa hiyo, CCM imesema kwa kuwa wabunge wengi ni wa chama hicho, watumie fursa hiyo kuhakikisha sheria ya tozo hiyo inaondolewa na wakati huohuo watumie uwezo wao wote kuhakikisha wanaishauri serikali vizuri kupata njia mbadala itakayotumika kuziba nafasi itakayokuwa imeachwa kwa kuondolewa tozo hiyo.

"Kimsingi hatua hii imetupa faraja na hivyo CCM inaipongeza Serikali kwa kuamua kusitisha sheria ya kodi ya tozo hiyo ya sh. 1,000 kwa laini ya simu kwa kuwa ingesababisha usumbufu na adha isiyo ya lazima kwa wananchi", imesema CCM katika sehemu ya taarifa yake.

MTEMVU AGAWA MISAADA YA VYAKULA KWA VITUO VYA YATIMA TEMEKE


 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu akiwakabidhi msaada wa vyakula watoto yatima wanaolelewa katika Kituo cha Dar Alqaama Tandika katika sherehe ya kutoa misaa kwa vikundi mbalimbali vya yatima, Dar es Salaam hivi karibuni.
                                        Akiwakabidhi watoto wa Kituo cha Hiyari Chang'ombe
                                              Upendo Maganga wakipata msaada huo
                                                                  Upendo Bokolani wakipata msaada huo
                                        Kituo cha WAVIBA KILAKALA wakipokea msaada
                                               Kituo cha Faraja kikipokea msaada huo
 Mwenye ulemavu wa viungo, Zamda akipokea msaada wa vyakula kutoka kwa Mtemvu
                                                  Aisha Shabani akipokea msaada huo
                                        Mwasiti Mtebwa akipata msaada
 Mama Mwandoro akipata msaada
                                                           Ashura Sadiki