Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, August 27, 2013

AIRTEL YAGAWA VITABU KWA SHULE YA SEKONDRI YA BWELANYAKE KARAGWE


Meneja Mahusiano ya Kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi akimkabithi Afisa elimu msaidizi sekondari wilaya ya karagwe bi Siberia Ruboha vitabu vya ada na kiada wakati Airtel ilipotembelea wilaya ya karagwe mkoani bukoba

Afisa mauzo wa kanda ya ziwa Mohamed Kabeke akikabithi vitabu Afisa elimu msaidizi sekondari wilaya ya karagwe  bi Siberia Ruboha wakati Airtel ilipotembelea wilaya ya karagwe mkoani bukoba, akishuhudia ni  Meneja Mahusiano ya Kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi
Airtel yagawa vitabu kwa shule ya sekondari ya Bwelanyake Karagwe
Airtel Tanzania imeendelea na mradi wake wa kusambaza vitabu katika shule ya Sekondari nchini chini ya mradi wa ‘Shule yetu’ ambapo shule mbalimbali za sekondari nchini zimenufaika na mradi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Meneja Mahusiano ya Kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi alisema kampuni ya Airtel inaendelea kukabiliana na changamoto katika sekta ya elimu nchini hasa tatizo la vitabu vya kiada kwa shule za sekondari.
Kupitia mradi wa ‘Shule yetu’ watoto wengi wa kike watanufaika kwani mradi huu unalenga hasa katika  kumkwamua mtoto wa kike kutoka katika ujinga, umaskini na maradhi,”

Hawa aliongeza kwa kusema Leo tunatoa msaada wa vitabu kwa shule ya sekondari ya Bwelanyake hapa Karagwe Bukoba ikiwa ni mwendelezo wa shughuli zetu za kijamii katika kupambana na tatizo la vitabu mashuleni. Vitabu hivi vitawawezesha wanafunzi wa shule ya Bwelanyake kupata nafasi ya kujifunza na kujisomea na kuwawezesha walimu kupata nyenzo muhimu za kufundishia.

Kwa upande wake Afisa elimu msaidizi sekondari wilaya ya karagwe  bi Siberia Ruboha alisema “elimu ndio ufunguo wa maisha hivyo tunawashukuru sana Airtel kwa kushirikiana na Serikali kupunguza tatizo la vitabu vya kiada vya shule za sekondari hapa nchini. Tunaamini msaada huu wa vitabu tulioupata leo utasaidia katika kuinua kiwango cha ufaulu na kuongeza taaluma zaidi kwa wanafunzi wetu na kuongeza idadi ya wanafunzi wa masomo ya sayansi hapa shuleni. /Nachukua fursa hii kuwaomba wanafunzi wavitumie fursa hii kujisomea na wavitunze vitabu hivi ili viweze kutumika na wanafunzi wengi zaidi na kutoa matunda bora na mengi zaidi.

Mpaka sasa Airtel kupitia mradi huo imewafikia shule takribani  900 za sekondari nchi nzima kwa kuzipatia vitabu vya kiada hasa kwenye masomo ya Fizikia, Hisabati, kemia na Biolojia. mradi huu wa Shule yetu unasambaza vitabu kwa shule za sekondari kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne pamoja na vitabu vya  walimu kwa ajili ya kufundishia.

KOCHA SUPER D ,YASSIN ABDALA WAMPOKEA FRANCOIS BOTHA LEO PAMOJA NA RAIS WA WBF



Mgeni rasmi katika mpambano wa Kimataifa wa Ubingwa wa WBF Bondia bingwa wa Dunia wa Uzito wa Juu Zamani, Francois Botha 'Wwite Buffalo' katikati baada ya kupokelewa alipowasili katika uwanja wa kumataifa wa Julius Nyerere Dar es salaas leo wengine kushoto ni Raisi wa TPBO Yassini Abdalla na Rais wa World Boxing Federation ,Howard Goldbeg pamoja na Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Nchini Rajabu Mhamila 'Super D'  Mpambano wa ubingwa wa Dunia wa chama hicho unafanyika kwa mara ya kwanza kwa kuwakutanisha Mabondia Fransic Cheka na Phil Williams wa Marekani siku ya August 30 katika ukumbi wa Diamond Jubilee siku ya ijumaa hii Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

BONDIA WA DUNIA FRANCOIS BOTHA WA PILI KUSHOTO AKIWA NA JAY MSANGI RAISI WA WBF ,HOWARD GOLDBEG,YASSINI ABDALL, NA KOCHA WA KIMATAIFA WA MCHEZO WA MASUMBWI NCHINI RAJABU MHAMILA 'SUPER D'

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa Masumbwi Nchini Rajabu Mhamila wa pili kutoka kulia akifuraia jambo na Francois Botha pamoja na yassini Abdalla kulia

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwafikisha wageni katika hotel ya Southern sun wa pili ni Rais wa WBF, Howard Goldbeg, Rais wa TPBO, Yassini Abdallah na mmoja wa Majaji wa mpambano huo pamoja na Bondia bingwa wa Uzito wa Juu Duniani Francois Botha Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

BONDIA WA DUNIA FRANCOIS BOTHA WA PILI KUSHOTO AKIWA NA JAY MSANGI RAISI WA WBF ,HOWARD GOLDBEG,YASSINI ABDALL, NA KOCHA WA KIMATAIFA WA MCHEZO WA MASUMBWI NCHINI RAJABU MHAMILA 'SUPER D'

Kipanya LEO



KUTOKA KWENYE VIWANJA VYA BUNGE MJINI DODOMA LEO




IMG_0407 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge  wa Mbinga Magharibi Capt. John Komba, bungeni mjini Dodoma Agosti 27,2013.
IMG_0409 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka  bungeni mjini Dodoma Agosti 27, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
IMG_0432
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,  ambaye pia ni Mbunge wa Songwe, Philipo Mulugo kwenye viwanja vya bunge Mjini Dodoma AGOSTI 27,2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KAMPUNI YA CLORIDE EXIDE CHASAIDIA KITENGO CHA EMER GENCY MUHIMBILI



Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa kampuni ya Choloride Exide Bw,Gabriel Ondoyo kulia na  Mratibu wa Masoko wa Kampuni hiyo Bw, Robert Hiza wakikabidhi Betri za kampuni hiyo kwa  Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Dharurua  'Emer Gency Medicine Profesa, Victor Mwifongo kwa ajili ya magari ya kitengo hicho Dar es salaam leo kushoto ni Kaimu Dereva Mkuu Sultan Kitanga na Mkuu wa Idara ya Ufundi ENG,Leonard Elizeus Picha na Mpiga Picha wetu
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa kampuni ya Choloride Exide Bw,Gabriel Ondoyo kushoto na  Mratibu wa Masoko wa Kampuni hiyo Bw, Robert Hiza wakishusha betri walizopereka mhuimbili
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa kampuni ya Choloride Exide Bw,Gabriel Ondoyo kulia na  Mratibu wa Masoko wa Kampuni hiyo Bw, Robert Hiza wakishusha betri walizopereka mhuimbili
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa kampuni ya Choloride Exide Bw,Gabriel Ondoyo kushoto na  Mratibu wa Masoko wa Kampuni hiyo Bw, Robert Hiza wakiwa katika picha ya pamoja baadhi ya maofisa wa kitengo hicho

Mkuu wa Madereva wa Kitengo cha Emer gency Medicini Bw. Kafuru Rashidi akikagua betri hizo baada ya kukabidhiwa
Baadhi ya Madereva wa kitengo hicho wakikagua

Baadhi ya waudumu wakiendelea na shughuli zao katika gari la wagojwa kushopto ni Nikijaeli Ngareni na Josephine Lazaro

Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Dharurua  'Emer Gency Medicine Profesa, Victor Mwifongo kushoto akibadilishana namba za mawasiliano na
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa kampuni ya Choloride Exide Bw,Gabriel Ondoyo
Mratibu wa Masoko wa Kampuni hiyo Bw, Robert Hiza 


Na Mwandishi Wetu

MRATIBU wa Masoko wa Kampuni ya Chloride Exide Bw, Robert Hiza leo ametoa msaada wa Betri mbili katika kitengo cha Emer Gency Medicine ya hospitali ta Taifa Muhimbili

Msaada huo wa kwanza kutoa inaendana na miaka 50 ya kampuni hiyo ambapo watatoa viti mbalimbali katika hospital za Selekari vikiwemo Sora kwa ajili ya umeme wa jua
Akipokea msaada huo 
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Dharurua  'Emer Gency Medicine Profesa, Victor Mwifongo amewashukuru kampuni ya Chloride Exide kwa kuliona hilo kwani ni mara ya kwanza katika kitengo chao kupokea msaada kama huo

na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kusaidia vitu mbalimbali ikiwemo ata magari kama yapo tunaomba msaada mana hapa kiterngo chetu ni cha mambo ya dharura na kinategemewa sana kama mnavyojua

Nae
Mkuu wa Madereva wa Kitengo cha Emer gency Medicini Bw. Kafuru Rashidi amenderea kutoa shukrani kwa kampuni hiyo kwa kuliona hilo kwani yeye kama Dereva ameona ni jambo bora sana

Chadema yaanza kumliza Nkamia, yashinda uchaguzi jimboni kwake



 Kaimu Katibu wa Chadema Wilaya ya Dodoma Mjini, Jella Kheri Mambo, akiwa Ofisini kwake.
Ofisi ya Chadema Wilaya ya Dodoma Mjini

Na Bryceson Mathias, Kondoa

KATIKA hali inayoonesha ni kumliza Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kijiji cha Mlongila Kata ya Jangalu, Jimbo la Kondoa Kusini, Kimeshinda kwa kishindo uchaguzi wa Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho.

Hatua ya Chadema kuonesha kinakubalika hadi vijijini, kilishinda uchaguzi huo uliofanyika Jumamosi, Agosti 24, ambapo Mgombea wa Chadema, Sariah Bakari Lubuva Alishinda kwa kura 184 na kuwatupa mbali wagombea wenzake baada Mwenyekiti aliyekuwepo kujiuzulu.

Akizumza na Mwandishi wa habari hizi Katibu Mkuu wa Chadema mkoani Dodoma, Stephen Masawe, alithibitisha mgombea wao Lubuva kushinda kwa kura (184), dhidi ya kura za Chama cha Mapinduzi (CCM) waliopata (96) na Chama cha wananchi (CUF) waliopata (9).

“Hizo ni salamu na Mvua za rasharasha kwa Nkamia anayedai anapenda kuzungumza na mwenye Mbwa badala ya Mbwa, lakini Chadema tunazungumza na Nguvu ya Umma yenye Hati Milki ya Tanzania”.alisema Masawe.

Wakati huo huo Kaimu Katibu wa Wilaya ya Dodoma Mjini (Chadema), Jella Kheri Mambo, amekanusha Kauli ya Viongozi wa CCM Mkoa wa Dodoma wanaomtuhumu kuwa yeye na wenzake waliojiunga Chadema wako huko kwa Mkopo.

Alisema Kauli ya viongozi wa CCM Mkoa ni ya Fisi aliyenyatia mkono wa mtu akidhani utaanguka, lakini hadi safari inakwisha haukuangua naye akaambulia Patupu asiupate.

“Nilikataa zawadi ya uongo wa Ufisadi wa Makusanyo ya Mil.1,5/= badala ya Sh. Mil.5/- zilizostahili kukusanywa kwa nyumba 500 za Kata ya Uhuru kila nyumba 10,000/-. Viongozi hao wakafanya njama kuniondoa, hivyo siwezi kurudi CCM“.alisema Mambo.

Aidha badala yake Mambo amesema, hivi karibuni Chadema Dodoma Mjini kinaanza kampeni maalum (M4C) ya Mlango kwa Mlango kuzungukia Kata 37 wilayani humo,ili kuongeza Idadi ya wanachama wake, mbali ya wale inaowapata kwenye Mikutano ya hadhara kila mara.

Nilikuwa mmuumini wa Azimio la Arusha na sera za Chadema ni hizo ambazo mimi ni muumini wake. Wananchi na Viongozi wapuuzeni CCM walioshindwa kuwatetea wananchi badla yake wanawafanya watumwa wa kuwasomeshea, kuwalisha na kuwavisha watoto wao”.alisema Mambo.

Sunday, August 25, 2013

MSONDO NGOMA YATUMBUIZA KWA MARA YA KWANZA BILA GURUMO BAADA YA KUSTAAFU MUZIKI


Baadhi ya wasanii wa bendi ya msondo ngoma wakitumbuiza kwa mara ya kwanza baada ya mwanamziki mkongwe wa bendi hiyo muhidini Gurumo kustaafu kutoka kushoto ni Shabani Lendi,Hamisi Mnyupe,Saidi Mabera,Juma Katundu na Shabani Dede.Picha na www.burudan.blogspot.com
Baadhi ya wasanii wa bendi ya msondo ngoma wakitumbuiza kwa mara ya kwanza baada ya mwanamziki mkongwe wa bendi hiyo muhidini Gurumo kustaafu kutoka kushoto ni Shabani Lendi,Hamisi Mnyupe,Saidi Mabera,Juma Katundu na Mustafa Pishuu.Picha na www.burudan.blogspot.com
Wasanii wa bendi ya msondo wakiwajibika wakati wa onesho lao kutoka kushoto ni Abdul Ridhiwani,Eddo Sanga,Othumani Kambi na Juma Katundu picha na www.burudan.blogspot.com
Wasanii wa bendi ya msondo wakiwajibika wakati wa onesho lao kutoka kushoto ni Abdul Ridhiwani,Eddo Sanga,Othumani Kambi na Juma Katundu pamoja na Mustafa Pishuu picha na www.burudan.blogspot.com
Wasanii Hamisi Mnyupe kushoto na Romani Mng'ande wakiwajibika jukwaani

WANAWAKE WAFUNGUA KLABU YA MCHEZO WA BAO MTAA WA KASULU ILALA


Wachezaji wa Mchezo wa bao wakicheza wakati wa mazoezi ya mchezo huo yaliyofanyika katika klabu yao iliyopo Mtaa wa Kasuru Ilala Dar es salaam jana kushoto ni Salha Wailes na Halima Kaubanika Picha na www.burudan.blogspot.com

Wachezaji wa Mchezo wa bao wakicheza wakati wa mazoezi ya mchezo huo yaliyofanyika katika klabu yao iliyopo Mtaa wa Kasuru Ilala Dar es salaam jana kushoto ni Salha Wailes na Halima Kaubanika Picha na www.burudan.blogspot.com

YANGA YAANZA NA MKONO, YAICHAPA ASHANTI 5-1 TAIFA, HUKO TABORA SIMBA 2-RHYNO 2


 Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu (wa pili kushoto) akiwania mpira na mabeki wa Ashanti, wakati wa mchezo wa fungua dimba la Ligi Kuu ya Vodacom, Tanzania bara uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga imechabanga Ashanti jumla ya mabao 5-1.

Bao la kwanza lilifungwa na Jerson Tegete, katika dakika ya 10, bao la pili likafungwa na Simon Msuva, katika dakika ya 47, na la tatu likafungwa tena na Jerson Tegete, katika dakika ya 57, la nne likawekwa kimiani na Haruna Niyonzima katika dakika ya 73 na lakufunga pazia hilo la mabao ya Yanga, liliwekwa Kambani na Nizar Khalfan, katika dakika ya 90+aliyetokea Benchi akichukua nafasi ya Jerry Tegete.
 Ni Juma Abdul Katikati ya mabeki wa Ashanti.
 Niyonzima akichanja mbuga.
 Sehemu ya mashabiki wa Ashanti
 Sehemu ya Mashabiki wa Ashanti.
 Hivi ndivyo, Haruna Niyonzima alivyowakalisha mabeki wa Ashanti na kukosa bao la wazi katika kipindi cha kwanza.
Mabeki wa Ashanti, walikaa.......

YANGA ilianza na :- Ali Mustafa 'Bartez', Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub 'Canavaro', (c) Mbuyu Twite, Athuman Idd, 'Chuji', Simon Msuva, Salum Telela, Didier Kavumbagu, Jerson Tegete na Haruna Niyonzima.

BENCHI LA AKIBA:-
Deogratias Munishi, Oscar Joshua, Frank Domayo, Bakari Masoud, Nizar Khalfan, Issa Ngao na Husein Javu.

ASHANTI ilianza na:-
Ibrahim Abdallah, Khan Usimba (c), Emaanuel Kichiba, Ramadhan Malima, Tumba Sued, Emmanuel Memba, Fakihi Hakika, Mussa Nampaka, Hussein Sued, Mussa Kanyaga na Joseph Mahundi.

BENCHI LA AKIBA:- 
Daud Mwasongwe, Hussein Mkongo, Paulo Telly, Mwinyi Abdulrahim, Laurent Mugia, Peter Ilunda na Shaban Juma.

HUKO KWINGINEKO: Coastal Union, wameichapa JKT Oljolo 2-0 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Mtibwa na Azam Fc, wametoshana nguvu kwa kufungana 1-1, katika Uwanja wa Manungu Morogoro, Mbeya City na Kagera Sugar wametoka suluhu 0-0, katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya. Huko mkoani Tabora Simba imetoka sare ya 2-2 na Rhyno, katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, JKT Ruvu imewafunga Mgambo JKT 2-0.

MWENYEKITI WA CCM JK AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU DODODMA


 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao maalum cha Kamati Kuu ya CCM, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma leo, Agosti 25, 2013. Kikao hicho kilifanyika kwa ajili ya kukutana Mbunge wa Bukoba mjini Khamis Kagasheki, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera, Constansia Buhiye,  Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Abedi Mushi, Mwenyekiti na Katibu wa CCM wilaya ya Bukoba mjini na Meya wa Manispaa ya Bukoba Anatory Amani, kuhusu mgogoro wa madiwani wanane wa CCM Manispaa ya Bukoba. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
  Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera Constansia Muhiye na Katibu wa CCM wa mkoa huo, Abedi Mushi wakisubiri kuingia ukumbini kukutana na Kamati kuu mjini Dodoma leo.
 Mbunge wa Bukoba mjini Khamis Kagasheki akisubiri kuingia ukumbini kukutana na Kamati Kuu ya CCM Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, akimsikiliza kwa makini Mwana-CCM mwenye ulemavu wa miguu, Shija Luhende kutoka Mwanza, ambaye alimkuta kwenye viwanja vya Makao Mkuu ya CCM mjini Dodoma leo, akitafuta msaada wa baiskeli. 
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM,  Abdallah Bulembo akizungumza na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Jenista Mhagama, nje ya ukumbi, Makao Mkuu ya CCM mjini Dodoma, leo. Picha na Bashir Nkoromo

LIGI ya Mpira wa pete (CHANETA CUP) inayofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine Mkoani Mbeya imeanza kwa kasi baada ya timu nane kutoana jasho katika Mechi za ufunguzi.



 Timu ya Magereza kutoka Mkoani Morogoro iki ichachafya timu ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya maarufu kama Hamambe katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa kutokana na ufundi wa wafungaji wa pande zote mbili



Mwenyekiti wa CHANETA mkoa wa Mbeya dadaMary akiongea na waandishi wa habari

Add caption


LIGI ya Mpira wa pete (CHANETA CUP) inayofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine Mkoani Mbeya imeanza kwa kasi baada ya timu nane kutoana jasho katika Mechi za ufunguzi.
Mechi nne za ufunguzi zililazimika kufanyika Asubuhi kutokana na kufunguliwa kwa pazia la Ligi kuu la mpira wa Miguu kati ya timu ya Kagera Sugar na Mbeya City  katika uwanja huo huo hivyo kupisha muingiliano wa Ratiba.
Katika mchezo wa kwanza ulizikutanisha timu za Polisi Mbeya iliyomenyana vikali na timu ya Tumbaku kutoka Mkoani Morogoro ambapo Timu ya Tumbaku iliibuka kidedea kwa magoli 35 dhidi ya 17 waliyoyapata timu ya Polisi Mbeya.
Mchezo uliofuata ulikuwa kati ya timu ya Jeshi la Uhamiaji kutoka Dar Es Salaam dhidi ya Polisi Arusha na matokeo kuishia kwa Uhamiaji kuibuka na ushindi wa Magoli 27 kwa magoli 19 ya timu ya Polisi ya Arusha.
Timu za Polisi zilizidi kumwagiwa magoli katika Mchezo wa Tatu uliozikutanisha timu ya Polisi Mwanza dhidi ya Timu ya Filbert Bayi ya Dar Es Salaam ambapo timu ya Polisi ililala kwa magoli 21 dhidi ya magoli 33 ya Filbert Bayi.
Timu ya Magereza kutoka Mkoani Morogoro pia ilichachafya timu ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya maarufu kama Hamambe katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa kutokana na ufundi wa wafungaji wa pande zote mbili ambapo hadi kipenga cha mwisho cha mchezo huo Hamambe magoli 28 na Magereza 31.

Na Mbeya yetu

Huyu ndiye Muhidin Mwalimu Gurumo 'Mjomba' Muasisi wa Msondo Ngoma, Sikinde Ngoma ya Ukae na Ndekule



Mzee Gurumo akiwa na wanamuziki wenzake wa Msondo Ngoma, Hassain Moshi na Shaaban Dede
JUZI tasnia ya muziki ilipata simanzi kubwa kutokana na maamuzi magumu aliyoyafanya mwanamuziki gwiji nchini, Muhidin Mwalimu Gurumo 'Mjomba' a.k.a Kamanda alipotangaza kung'atuka kwenye muziki baada ya kuutumikia kwa miaka zaidi ya 50.
April mwaka jana (2012) nilikuwa miongoni mwa watu waliomtembea Mzee Gurumo alipokuwa akijiuguza nyumbani na kubahatika kufanya naye mahojiano yaliyozaa makala ndefu kuhusu alipoanzia alipotoka na alipokuwa akielekea.
Kwa ambao hawakubahatika kuisoma makala hiyo labda wajikumbushe kidogo historia ya mwanamuziki huyo mkongwe ambaye alikuwa tayari kugombana na wamiliki wa bendi mradi kuwatetea wanamuziki wenzake ambao aliamini kama siyo wao wamiliki wasingekuwa na chao na kutambulisha bendi zao.

Naiweka makala hiyo kama ilivyotoka gazeti la NIPASHE bila kupunguza wala kuongeza neno jingine ili mradi tu wasomaji wa blogu hiii mumjue Gurumo na kwa amewatia simanzi kwa uamuzi wake wa kujiondoa kwenye muziki wakati bado watu wanamhitaji kuanzia wanamuziki wenzake, mashabiki na hata taifa kwa ujumla.
=========
HUWEZI kuuzungumzia muziki wa Tanzania hasa miondoko ya dansi, bila kulitaja jina la Muhidin Mwalimu Gurumo (sio Maalim kama baadhi walivyozoea kumuita).
Hii ni kwa sababu mwanamuziki huyo mkongwe, maarufu kama 'Kamanda' au 'Mjomba', aliyewahi kutamba na kuziasisi bendi mbalimbali nchini ameutumia zaidi ya nusu ya umri wake katika mambo ya muziki, hivyo kuwa na mchango mkubwa katika fani hiyo.
Gurumo alianza fani ya muziki katika bendi za mitaani miaka ya 1950 akipitia bendi moja baada ya nyingine hadi leo akiwa na Msondo Ngoma, ingawa ameshindwa kupanda nao jukwaani kwa siku za karibuni kutokana na afya yake kutetereka kwa maradhi aliyonayo.
Mbali na mchango wake binafsi kama mwanamuziki, Gurumo mwenye umri wa miaka 71 amekuwa msaada mkubwa kwa wanamuziki waliowahi kuibuliwa naye au kufanya naye kazi kutokana na misimamo yake thabiti ya kulinda na kutetea haki za wanamuziki.
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kufanya naye kazi na Gurumo ni Shaaban Dede 'Super Motisha', Bennovilla Anthony, Hassan Rehani ‘Bitchuka’ na wengine kadhaa wakiwemo waliotangulia mbele ya haki kama Suleiman Mbwembwe na Tx Moshi William, wamewahi kukiri jambo hilo.
"Kama viongozi wa bendi wangekuwa kama Gurumo katika kupigania na kutetea haki za wasanii, naamini tungekuwa mbali mno, mjomba (jina jingine la utani la Gurumo) huwa hataki mchezo," aliwahi kusema Dede.
Wakati wa mahojiano maalum na yeye yaliyofanyika hivi karibuni nyumbani kwake Mabibo jijini Dar es Salaam, Gurumo alisema kwamba kilichokuwa kikimsukuma kuwapigania wanamuziki wenzake na yeye mwenyewe ni dhamana ya uongozi na hali ya umaskini aliozaliwa nao.
"Unajua mimi nimezaliwa katika familia ya kimaskini na kimekulia kwenye umaskini, hivyo nafsi yangu huwa ngumu kumkandamiza maskini mwenzangu kwani naamini sio haki na dhambi kubwa kwa Mungu," alisema.
"Japo nilikuwa katika nafasi ya kufanya hila kwa kuegemea upande wa wamiliki wa bendi, ila kule kutambua kuwa uongozi niliopewa na wenzagu umetokana na imani  yao kwangu, ndio maana nilikuwa mkali kama pilipili kuwapigania wenzangu," aliongeza.
Gurumo, alisema hata alipokuwa akishawishiwa na baadhi ya wamiliki wa bendi ili kuwageuka wenzake ilimradi yeye aongezwe dau lolote analotaka, hakukubali kirahisi na  wakati mwingine kufikia kuamua kuhama iwapo dai lake halisikilizwi.
"Karibu bendi zote nilizopitia misimamo yangu ilikuwa hivyo na ikitokea uongozi ukawa mbishi  kukaidi madai ninayowasilisha kwao, huwa radhi kuondoka kama nilivyofanya OSS na kwingine," aliongeza.
Gurumo, alisema kutokana na misimamo hiyo mikali, alijikuta kila bendi aliyojiunga nayo wanamuziki wenzake humchangua kuwa kiongozi hadi sasa akielekea kustaafu fani hiyo kutokana na umri kumtupa mkono na maradhi yanayomsumbua kwa hivi sasa.
Alisema, tabia yake ya kutanguliza masilahi ya wanamuziki wenzake mbele kwa kiasi fulani yamechangia kushindwa kujijenga kimaisha kulinganisha na umaarufu wa jina lake na umri alioutumia katika fani hiyo ya muziki.
Gurumo, alisema katika umri wa zaidi ya miaka 40 aliyotumia katika muziki hana cha  kujivunia zaidi ya kujenga nyumba yenye vyumba 17 eneo la Mabibo, kujenga nyumba nyingine katika shamba lake lililopo kijijini kwao Masaki, Kisarawe, mkoani Pwani.
"Nyumba hii kama unavyoiona ambayo nimewapangisha watu na ninaendelea kuikarabati ndio pekee ya kujivunia, pia nina shamba nililojenga kibanda kingine huko Masaki, lakini kwa hadhi yangu nilipaswa kuwa mbali na hapa au vipi?" alisema Gurumo kwa kuhoji.

Gurumo akiwa nje ya nyumba yake ya Mabibo

Alisema, kwa hadhi yake wala asingekuwa akipigana vikumbo na mashabiki wake kwenye daladala aendapo kwenye shughuli zake na hata kwenye kliniki ya matatizo yake kiafya, lakini hana jinsi kwa vile hana uwezo wa kumiliki hata gari ndogo ya kutembelea.
"Naamini wengine wanaweza wasiamini, lakini ukweli ni kwamba sijawahi na wala sijui ni lini nitakuwa na usafari wangu binafsi, natamani lakini tatizo uwezo wa kifedha ndio tatizo, kama sio kujenga banda hili hapa Mabibo, sijui ingekuwaje," alisema.
Alisema, kinachomfanya awe katika maisha hayo licha ya umaarufu wake kimuziki,  Gurumo alisema mbali na kuthamini na kujali wengine, lakini ukweli ni kwamba enzi  akiutumikia muziki hakukuwa na masilahi ya kutosha kama wapatavyo vijana wa sasa.
"Huwa natamani miaka irudi nyuma na zama zile ziwe hivi sasa, ili nami niweze kunufaika na jasho langu katika muziki," alisema huku tabasamu la uchungu likimtoka usoni mwake.

MJOMBA
Mkongwe huyo aliyejifunza muziki tangu akiwa Shule ya Msingi Sungwi, iliyopo Kisarawe akiimba na kupiga dramu katika bendi ya shule, alisema safari yake ya muziki kwa kiasi kikubwa ilichangiwa na mjomba wake aitwaye Seleman Sultan Wamikole.
Alisema mjomba wake aliyemchukua tangu akiwa mdogo baada ya baba yake mzazi  Mwalimu Mohammed Gurumo, kufariki na kumuacha katika maisha magumu na ndugu zake wakiwa na mama yao Mwazani Sultan aliyefariki mwaka 1981.
Alisema kutokana na hali ilivyokuwa nyumbani kwao, mjomba wake huyo alimchukua na kuja kuishi nae Dar es Salaam maeneo ya Ilala ambapo moja kwa moja alimwandikisha katika madrasa ambako alipata fursa ya kuimba kaswida.
Alisema kuwa baadaye alipata hamu ya muziki hasa kutokana na kuvutiwa na kazi za nyota wa wakati huo, Salum Abdallah 'SAY' na Luambo Luanzo Makiadi 'Franco'.
Alisema mjomba wake huyo akishirikiana na mama yake walitambua kiu kubwa aliyokuwa nayo katika sanaa ya muziki na hivyo wakamruhusu kujiunga jumla ambako alizidi kuiva na baadaye kufuatwa na bendi mbalimbali.
"Kwa kitendo nilichofanyiwa na mjomba kwa kunitunza, kunilea na kunisaidia katika harakati zangu za muziki, ilinifanya nimtungie wimbo maalum nilikuwa OSS miaka ya  1980, wimbo uliitwa 'Shukrani kwa Mjomba'," alisema Gurumo.
Alisema anaamini kama sio mjomba na mama yake ambaye hadi leo anamliza akikumbuka alivyofariki, huenda asingefikia mahala alipo sasa kimuziki.
Mtunzi na muimbaji huyo mahiri nchini, alisema licha ya kipaji cha kuzaliwa, lakini Salum Abdallah na Franco ni watu waliochangia kufika kwake hapo alipo kwani enzi zao walimvutia mno.
"Ni kweli kipaji cha muziki nimezaliwa nacho na kukirithi kutoka kwa mama yangu Mwazani aliyekuwa kiongozi wa kundi la ngoma, ila kuvutiwa na Salum Abdallah na Franco ni sababu ya mimi kufika hapa nilipo, niliwapenda mno wanamuziki hawa," alisema.

SAFARI
Gurumo alisema baada ya kujifunza muziki kwenye makundi mbalimbali ya mitaani,  mwaka 1959 ndipo alipoanza kutambulika rasmi baada ya kuchukuliwa na bendi ya  Kilimanjaro Chacha.
Alisema alijiunga na bendi hiyo kama muimbaji ingawa pia alikuwa anamudu kupiga  dramu chombo alichokuwa akikipiga katika bendi ya shule na ndani ya bendi hiyo ndipo alipotunga kibao chake cha kwamba kilichoitwa 'Wakati Nikiingia Bar'.
Hata hivyo Gurumo alisema hakukaa sana Kilimanjaro Chacha kwani mwaka 1962  alihama na kwenda kujiunga bendi ya Rufiji Jazz alipokutana na wakali kama Salum  Nonde, Mbarouk Khalfan na wengine.
Alisema alijiunga na bendi hiyo kutokana na kushawishiwa na safari ambayo Rufiji Jazz ilikuwa ikitarajia kufanya mkoani Arusha na pia maslahi, hata hivyo miezi michache baadaye aliiacha bendi hiyo na kuhamia Kilwa Jazz B mwaka 1963.
Mzee Gurumo akiwa na baadhi ya tuzo zake wakati huo nilipomtembelea nyumbani
"Masilahi na ujana ndiyo ulionifanya niikache bendi ile na kutua Kilwa Jazz B, ambapo  kutokana na kipaji kikubwa cha uimbaji nilichokuwa nacho, uongozi wa Chama cha Wafanyakazi (NUTA) uliamua  kunichukua na kutua NUTA Jazz mwaka 1964," alisema.
Alisema kuwa alipotua NUTA alitunga kibao kilichokuja kumpa umaarufu cha kilichoitwa 'Mwangele', kikiwa na maana 'Mchumba' kwa lugha ya Kingoni na kisha kufuatiwa na nyimbo nyingine kadhaa.
"Kwa kweli idadi ya nyimbo nilizotunga nikiwa NUTA sizikumbuki kwa wingi wake, ila baadhi ni kama "Nimuokoe Nani', 'Kaka Seleman', 'Amina', Msondo Ngoma Na.1-4 na 'Maneno ya Nyerere'," alisema.
Gurumo alisema baada ya kuipandisha NUTA  iliyokuwa ikifahamika baadaye kwa jina la JUWATA, hasa alipowachukua wanamuziki nyota kama Bitchuka 'Stereo' na Said Mabera aliyekuwa akipuliza 'trumpet' katika bendi moja ya Arusha, Shirika la Teksi (TTTS) lilimfuata ili kuasisi bendi yao.
"TTTS walinifuata na kunieleza nia yao ya kutaka kuanzisha bendi na nikakubaliana nao ambapo walinilipa Sh 50,000, nikaondoka Juwata Jazz mwaka 1978 na kuasisi bendi ya Mlimani Park 'Sikinde' nikiwa na wanamuziki wenzangu wa Juwata na wengine kutoka Dar International," alisema.
Aliwataja baadhi ya waasisi wa bendi hiyo iliyokuja kufahamika kama DDC Mlimani Park kabla ya miaka mitatu iliyopita kurejea jina lake la awali baada ya kutemwa na mwajiri wao,  Shirika la Maendeleo mkoa wa Dar es Salaam, ni Hassani Bitchuka na marehemu Abel Baltazar aliotoka nao Juwata.
Wengine ni Joseph Mulenga 'Spoiler', Salum Machaku, Cosmas Chidumule, Hamis Juma  'Maalim Kinyasi', Ibrahim Mwinchande, Abdallah Gama na George Kessy kabla ya kuongezwa nguvu na akina Michael Enoch 'Teacher', Joseph Benard na Habib Jeff.

‘KASSIM WA KUTUMIA’
Alisema ndani ya Sikinde, kama kawaida aliendelea kutamba na utunzi wa nyimbo zilizotwaa umaarufu mkubwa ukiwemo wa 'Kassim' uliokuwa na sehemu mbili.
Gurumo alisema kibao hicho ni tukio la kweli lililomhusu rafiki yake aitwaye Kassim aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni ya mizigo uwanja wa ndege (DAHACO), ambaye alikuwa akisifika enzi hizo kwa ulevi na kusahau familia yake.
"Huu wimbo nilimtungia rafiki yangu ambaye alikuwa akiendekeza starehe kupita kiasi na kila nilipokuwa nikimsihi apunguze,  alikuwa akinitaka nimuimbe ndipo ataacha ulevi," alisema.
Alisema kuwa baada ya hapo, ndipo alipoamua kutunga 'Kassim namba 1', ambapo mwenyewe (Kassim) alikuwa akijisikia fahari, ingawa hakuacha ulevi hadi alipopatwa matatizo kazini na kuchacha ambapo kidogo aliacha pombe na yeye kumtungia Kassim Na.2'.
Gurumo alipokuwa amelazwa hospitali
Gurumo alisema mpaka sasa hajui kama jamaa yake huyo aliacha pombe na pia hajui kama yu hai au la kwa vile ni miaka mingi imepita bila kuonana naye.
"Sijui kama yu hai au la, ila nyimbo zile zilimhusu yeye katika kumkataza anasa ingawa pia nilikuwa natoa ujumbe kwa jamii," alisema.
Mkali huyo ambaye ni shabiki wa kutupwa wa Simba, akiwa ni mmoja wa wanachama wake tangu mwaka 1972 na pia anayeishabikia Manchester United ya Uingereza, alisema alikaa na Mlimani Park hadi mwaka 1985 alipojiunga na safari Sound (OSS) akiwa na Bitchuka.
Alisema alipotua OSS aliwakuta baadhi ya wanamuziki wake ambao wengi wao walitokea Zaire (sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo) wakilala chini na kuushinikiza kuwanunulia vitanda kama anataka aifanyie kazi bendi hiyo.
Alisema kuwa kwa bahati nzuri, uongozi ulimsikiliza  na kuwanunulia wanamuziki wote vitanda kama alivyotaka na kuanza kufanya kazi ikiwemo kubadili mtindo wa bendi hiyo wa 'Dukuduku Yee' na kuwa 'Ndekule'.
Gurumo alifichua kuwa mitindo yote aliyoasisi katika bendi za NUTA Jazz, Mlimani Park na OSS ya 'Msondo Ngoma', 'Sikinde Ngoma ya Ukae na 'Ndekule' ni ngoma ya asili ya kabila lake la Kizaramo ambazo mama yake alikuwa akiimba na kuzicheza enzi zake.
Alisema jambo hilo la kutumia ngoma za makabila ya kabila lake, ndilo ambalo hata wanamuziki nyota wa nchi za Kongo na mataifa mengine ya Afrika Magharibi wamekuwa wakifanya na kuutangaza muziki wao kimataifa tofauti na ilivyo nchini.
Mzee Gurumo akiwa na Nyoshi El Saadat
"Hata Wakongo na wanamuziki wa kimataifa kutoka nchi kama Senegal, Cameroon, Nigeria na Chad wamekuwa wakibuni muziki wao kwa kutumia ngoma za makabila yao, bahati mbaya vijana wengi wameshindwa kuumiza vichwa nao kubuni kazi zao na kuishia kunakili kazi za wenzao bila kujua wanawasaidia kuwatangazia, kwa kulikwepa hilo ndio maana nilikuwa nakubuni miondoko ya kabila langu la Kizaramo," alisema.
Gurumo, alisema sio jambo baya wanamuziki wa Tanzania kuiga kazi za wenzao, kitu alichodai ni vigumu kukikwepa, lakini alidai ni vema kama wangekuwa wakibuni vionjo vitakavyowatofautisha na wanamuziki hao wanaowaiga.
Alisema kwa muono wake ukiondoa Msondo na Sikinde zinazopiga muziki unaotambulika kama dansi la Tanzania, karibu bendi zote zinapiga muziki kwa kuwaiga wakongo, hata kwa zile bendi ambazo zilikuwa zikiaminika kuwa ni kilelezo rahisi kuitambulisha Tanzania kimataifa.

ULEVI
Gurumo hafichi kitu juu ya ujana wake kwa kueleza mbali na 'ubitozi' aliokuwa nao, pia alikuwa 'gangwe' enzi zake na pia aligeuzwa mtumwa wa pombe kutokana na kuwa mlevi aliyepitiliza.
Alisema, alikuwa anakata kilaji isivyo kawaida jambo ambalo lilikuwa likimfanya akorofishane na mama yake mzazi aliyetishia kumuachia 'laana' kama angeendelea kuendekeza ulevi.
"Kwa wanaonijua sidhani kama hili ni jipya, nilikuwa mlevi haswaa, kiasi mama alishindwa kunivumilia na kutishia kuniachia laana kama nisingesikilia wito wake wa kuachana na pombe," alisema.
Alisema, baada ya kushindana na 'shetani' kwa muda mrefu akikorofishana hata na mkewe, Pili bint Said Kitwana, hatimaye aliachana na ulevi mwaka 1982, miezi michache tangu mama yake mzazi kufariki.
"Ilikuwa ni kazi ngumu kuachana na pombe, lakini kwa heshima ya mama niliacha, pia shinikizo la mke wangu kipenzi ambaye ninampenda na kumsifia kwa uvumilivu wake, niliacha miezi michache baada ya mama kufariki na hadi leo situmii hiyo kitu," alisema.
Gurumo akiwa na wanamuziki wenzake wakongwe walipokuwa wakiandaa nyimbo maalum za Tanzania All Stars
Gurumo, alisema binafsi anajutia masuala ya ulevi akidai ni kati ya mambo yaliyochangia kumkosesha kufanya mambo ya maendeleo pamoja na kuihatarisha ndoa yake, kama mkewe asingekumvumilia kwa miaka 20 tangu walipooana mwaka 1962.
"Naamini ulevi uliopitiliza kwa hakika ni mbaya kama vijana wa sasa mnavyosema kwamba 'ulevi ni noma', nusura ndoa yangu ivunjike kwa ajili ya kuendekeza hii kitu, hata nilipotangaza kuachana na pombe si mke wangu wala marafiki zangu waliokuwa wakiamini hadi walipoona siku zikienda bila kupiga kilaji," alisema Gurumo.
Gurumo alisema hakuna kitu anachofurahia maishani mwake kama siku alipooana na mkewe, aliyezaa nae watoto wanne, Mariam aliyemzaa mwaka 1981,  Mwalimu, 28, Omar na Mwazani pamoja na alipoachana na pombe.
"Hivyo ndivyo vinavyonifurahisha hadi leo, nilipomuoa mke wangu na nilipoacha pombe, ila kwa huzuni ni kifo cha mama yangu, huwezi kuamini hadi leo huwa nikikumbuka natokwa machozi kwa namna mama alivyokuwa anikipenda na tulivyokuwa tunapendana na kuishi kwa upendo na furaha," alisema.
Gurumo, alisema maisha yake yamekuwa mikononi mwa mama yake kutokana na baba yake kufariki mwaka 1948 wakati akiwa na miaka nane tu, ndio maana amekuwa akimkumbuka kila mara marehemu mama yake.

BITCHUKA
Gurumo anayekula vyakula vyote halali na vyenye manufaa kwa afya yake na kunywa juisi na soda, alisema hakuna tukio lisilofutika kichwani mwake kama siku alipoamua kumsimamisha kazi 'swahiba' wake, Hassani Rehani Bitchuka.
Hassain Rehani Bitchuka
Alisema, alifanya uamuzi huo aliouita kuwa mgumu kuwahi kukutana nao maishani kama mwanamuziki mwaka 2005, baada ya Bitchuka kugoma kushiriki kwenye onyesho la pamoja kati ya Msondo Ngoma na African Stars 'Twanga Pepeta'.
"Bitchuka aligoma kushiriki onyesho hilo kwa madai asingeweza kufanya onyesho na watoto, kitu ambacho kiliwaudhi wanamuziki wenzake na wote waliniangalia mimi kama kiongozi wao nitafanya nini kwa kosa alilofanya 'swahiba' wangu ambaye tumekuwa katika 'udugu' tangu nilipomchukua toka Arusha mwaka 1973," alisema.
Alisema, hata hivyo alilazimika kusimama kidete kama kiongozi kwa kuweka kando 'uswahiba' wake kwa Bitchuka, ili kuinusuru Msondo na kuitisha kikao nilichotangaza kumtimua kundini, jambo ambalo anadai hadi leo humpa tabu kubwa kutokana na uhusiano aliokuwa nao na Bitchuka kwa mjda mrefu.
"Kwa kweli jinamizi la tukio lile hadi leo huniwewesesha, lakini tayari nilishazungumza na Bitchuka na kunielewa, pia unajua wakati mwingine ukiwa kiongozi unapaswa kufanya maamuzi magumu bila kutarajiwa," alisema.
Alipoulizwa juu ya msanii gani kwa sasa anayemuona kama ndiye mrithi atakayeendeleza gurudumu la muziki wa dansi nchini, Gurumo bila kificho alimtaja Husseni Jumbe mmiliki wa bendi ya Talent.
"Kwangu namuona Jumbe kama ndiye tumaini pekee la maendeleo ya muziki wa dansi kutokana na kipaji kikubwa alichonacho akitunga, kuimba, kupanga muziki na kujaliwa sauti ya kipekee," alisema.
Kuhusu muziki wa kizazi kipya, alisema upo juu kwa vile unatangazwa mno na vyombo vya habari, ila haoni kama ni muziki wenye nguvu unaoweza kuufunika muziki wa dansi.
"Promo ndio inayoubeba muziki huu, kitu kinachowalemaza wasanii wake kushindwa kuwa wabunifu na kujiona wamefika mbali, wakati wana kazi kubwa hususani ya kujifunza kupiga ala mbalimbali ili wapige muziki wao utakaokubalika kimataifa tofauti na sasa wakitegemea kila kitu kifanywe studio," alisema.
Hata hivyo alikiri wanaoufanya muziki huo na taarabu wamekuwa na mafanikio makubwa kimaisha kwa vile soko limewapokea vema, jambo ambalo hata yeye hupata wivu akifikiria anapowaona vijana wakiendesha magari wakati yeye akitembea kwa miguu licha ya muda mrefu aliotumia kwenye fani hiyo ya muziki.

SWAHIBA WA JK
Gurumo, alisema fani yake ya muziki imemsaidia kufahamiana na wengi wakiwemo viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi, huku akimtaja Rais Jakaya Kikwete kwamba ni mmoja wa viongozi 'rafiki' zake.
Alisema, urafiki huo ndio anaoamini ulimfanya Rais Kikwete kuvunja shughuli zake na kumtembelea hospitalini kumjulia hali alipolazwa kwa mara ya kwanza kutokana na maradhi yanayomsumbua.
Gurumo, alisema kitendo cha Rais Kikwete kuacha kazi zake kwendsa kumjulia hali na kumsaidia katika matibabu yake kumemfariji mno, kwa vile katika kulazwa kwake na hata sasa akiendelea kujiuguza nyumbani hakuna kiongozi yeyote wa serikali wakiwemo wa Wizara wa Habari na Utamaduni, kuwahi kwenda kumjulia hali.
Rais Kikwete akimtunukia tuzo Mzee Gurumo wakati wa uzinduzi wa TBC
"Huwezi amini ni yeye na mkewe, Mama Salma ndio waliokuja kunijulia hali hospitalini, akianza mwenyewe kisha mkewe kitu ambacho kinanifariji hadi leo nikiamini Rais Kikwete anatujali na kututhamini wasanii," alisema.
Aliongeza kuwa, ukiondoa kufarijika kwake kutembelewa hospitalini na Rais Kikwete na mkewe, Mama Salma, pia kitendo kilichofanya na Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka cha kuandaa onyesho maalum kwa ajili ya kumchangia ni kitu ambacho kitabaki kichwani mwake na kumpongeza mwanamama huyo maaraufu kama 'Iron Lady'.
"Kwa kweli sikutarajia kama Asha Baraka angeweza kufanya kitendo kile ambacho ni wazi ninaonyesha ni jinsi gani anavyothamini na kujali mchango katika muziki. Nadhani watu wengine wanapaswa kuiga mfano wake, ni mtu ambaye ameonyesha mapenzi kwangu na kujali mchango wangu katika muziki, namshukuru na kumpongeza," alisema.
Gurumo, anayechizishwa na rangi nyekundu na nyeupe na ambaye anapenda kutumia muda wake za ziada kujishughulisha na mambo ya Kilimo kwenye shamba lake lililopo Masaki, alisema katika maisha yake kisanii amewahi kupata tuzo mbili tu zote za mwaka 2008.
Alisema tuzo hizo ni ile ya Kili Music Award kama Mwanamuiki Mkongwe na ile ya Hall of Fame, huku aliyekuwa mdau mkubwa wa muziki nchini aliyekuwa akifanya shughuli zake Umangani, Is'haka Kibene alimtengenezea na kumpa tuzo maalum kumtambua kama 'Kamanda wa Muziki wa Tanzania.
Mzee Gurumo akipokea msaada wa fedha toka kwa Asha Baraka 'Lady Iron' anayetajwa na gwiji huyo kama mwanamke wa mfano Tanzania katika kuuthamini mchango wake kisanii Tanzania
UBUNIFU
Gurumo, aliyeanza kuonekana tena kwenye jukwaa la bendi yake ya  Msondo baada ya kuwa nje kwa wiki kadhaa kutokana na kulazwa hospitalini, alisema muziki wa Tanzania umepiga hatua kubwa kimaendeleo, ingawa alikiri kwamba kukosekana kwa ubunifu miongoni mwa wananamuziki na wasanii wake ni tatizo linaloukwaza usitambe nje.
Alisema, hata muziki wa kizazi kipya (bongofleva) ambao umekuwa ukitajwa kama wenye maendeleo makubwa kwa wasanii wake, alisema unashindwa kutamba kimataifa kwa sababu wasanii hao hawaumizi vichwa kubuni vitu vipya.
Mkongwe huyo alisema tatizo la wasanii kupenda kuiga kazi za wenzao wa nje na kuzifanya zao kwa kuziimba kiswahili, ndilo linalowafanya wasitambe kimataifa na kutaka kuwepo kwa mabadiliko kuanzia sasa.
Alisema suala la kuiga kazi za nje halijaanza sasa, bali kitamboi kirefu akikiri hata wao (wakongwe) walikuwa wakifanya hivyo, ila alisema ubunifu wa ziada ndio uliowafanya waonekane mahiri katika soko la kimataifa.
"Kuiga ni jambo lisilokwepeka, lakini ni wajibu wa wasanii wa sasa kuumiza vichwa na kubuni vitu vipya ambavyo vitawatofautisha na wanaowaiga. Sio Bongofleva wala dansi kote wamelemaa kwa kuiga kazi za wenzao," alisema.
Alisema cha ajabu hata bendi za zamani ukiondoa Msondo Ngoma na Mlimani Park, zote hushindana kupiga muziki wa kikongo bila kujua wanasaidia kuutangaza muziki wa nchi hiyo na kuzidumaza bendi zao tofauti na Msondo na Sikinde.
Aliongeza anahisi bendi hizo zimeamua kuingia kwenye mkumbo huo kutokana na upepo wa soko ulivyo, japo alisema kimezifanya bendi husika zisiwasisimue mashabiki wake kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

KUSTAAFU
Gurumo, alisema hana muda mrefu kabla ya kutangaza kustaafu fani ya muziki kutokana na hali yake ya kiafya na umri mkubwa alionao akitaka kuwapisha wanamuziki wenye damnu changa kuendelea gurudumu la fani hiyo.
Mzee Gurumo alipotangaza kung'atuka kwenye muziki kando yake ni Meneja wa Msondo, Said Kiberiti na Juma Mbizo
Alisema, ingawa hajajua ni lini atafanya hivyo ila hadhani kama utamalizika mwaka huu wa 2012 kabla ya kutimiza azma hiyo na kudai atakapostaafu atajikita kwenye kuwasaidia vijana chipukizi.
Gurumo, alisema mipango yake ni kuanzisha chuo cha muziki anachotaka kukijenga Masaki, Kisarawe iwapo atapata mtu wa kumsaidia kufanikisha hilo kwa lengo la kutaka kuendeleza vipaji na kuudumisha muziki wa Tanzania.
"Sina muda mrefu kabla ya kustaafu rasmi muziki, sitajiweka kando kabisa na ndoto zangu ni kutaka kujenga chuo cha muziki katika shamba langu lililopo Masaki, lakini natatizwa na hali ya kiuchumi, hivyo kama serikali au mtu yeyote mwenye uwezo kifedha akinisaidia nitafurahi kwa vile nataka kuendeleza muziki wetu," alisema.
Alisema, anaamini vijana wanapaswa kujifunza mengi kutoka kwake na kwa wakongwe wengine ili kuufanya muziki wa Tanzania uendelea kudumu hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kidunia.

FAMILIA
Muhidini Mwalimu Gurumo, alizaliwa mnamo mwaka 1940 katika kijiji cha Masaki, Kisarawe akiwa ni mtoto wa pili kati ya watatu wa mzee Mwalimu Mohammed Gurumo.
Baba yake alifariki wakati Gurumo akiwa na miaka nane tu na hivyo maisha yake ya utotoni kuwa chini ya mama yake mzazi kabla ya kuchukuliwa na mjomba wake aliyemsaidia kuingia kwennye muziki.
Gurumo, alifanikiwa kufunga ndoa na mkewe, Pili bint Said Kitwana na kubahatika kuzaa nae watoto wanne, ambapo ni mmoja tu aitwae Mariam ndiye aliyerithi kipaji chake cha muziki akiimba kundi moja la taarabu lililopo Temeke.
Mkongwe huyo anayemtaja Said Mabera 'Dokta' kama mmoja wa wanamuziki viongozi anayemzimia, alisema katika maisha yake ya ndoa hakuna anachokifurahia kama kudumu kwa ndoa yake na mkewe ambayo imetimiza miaka 50 mwaka huu.
Alisema, kama sio uvumilivu wa mkewe, huenda ndoa hiyo ingevunjika kitambo kutokana na ukweli ukiondoa ulevi na kazi yake ya sanaa, pia ukorofi aliokuwa nao uliochangiwa na ujana ni kati ya mambo yaliyotaka kuivunja ndoa yake.
"Sio siri najivunia kuwa na mke mvumilivu kama huyu, kuna mambo niliyomfanyia kwa muda mrefu ndani ya ndoa yetu, lakini alinivumilia hadi leo tukiingia mwaka wa 50 tangu tuoane mwaka 1962," alisema.
Aliongeza, kuwa anaamini ndoa yao ilikuwa mipango ya Mungu ndio maana wamedumu na kuzeeka pamoja wakiwa ndio kwanza wanapendana kama wameoana jana, jambo ambalo linamfanya kila mara kumshukuru Mungu.

MKEWE
Pili Bint Said Kitwana, alikiri kwamba ndani ya uhusiano wa kimapenzi hadi kuja kuoana na Gurumo alipitia katika misukosuko mingi, lakini anashukuru Mungu alijaliwa uvumilivu na kuidumisha hadi leo.
Mama huyo alisema ugomvi wake mkubwa na mumewe ilikuwa ni tabia yake ya ulevi, hali iliyomfanya mara kwa mara kukwaruzana nae akimsihi aache.
Mzee Gurumo akiwa na mkewe, Pili bint Said
Alisema, kuna wakati mumewe alikuwa akiondoka nyumbani Ijumaa kwenda kwenye maonyesho na asionekane hadi Jumatatu akiletwa na rafiki zake akiwa 'bwii', kitu kilichokuwa kikimuuma.
"Tatizo kubwa baina yangu na Gurumo ilikuwa suala la ulevi, hata alipokuja kuacha sikuamini," alisema.
Aliongeza, jingine ni tabia ya kuwa na 'kuchakachua nje', na kumfanya aumie roho hasa wanawake zake wa nje kumfuata na kumtukana na hata wakati mwingine kutaka kupigana nao hasa anapoamua kuambatana nae kwenye maonyesho.
Alisema, ukiondoa matatizo hayo, Gurumo ni mume bora, mpole, mkarimu  na baba anayejali familia mwenye mapenzi ya dhati, ndio maana aliamua kumvumilia hadi leo na kutoa wito kwa wanandoa wengine kuvumiliana katika ndoa zao ili kuzifanya zidumu kama ilivyo kwao.
Pia, alisema kitu kinachomfurahisha kwa Gurumo ni tabia ya kutochagua chakula cha kula, akidai hula chakula chochote isipokuwa 'kitimoto'.
Mama huyo alisema kwa namna mumewe alivyojitolea ndani ya taifa hili kupitia fani yake ya muziki ni vema serikali ikamkumbuka kwa kumsaidia angali akiwa hai, badala ya kusubiri aje afe ndipo wajitokeze kumwagia sifa lukuki.
"Naiomba serikali imsaidie mzee huyu, huwa naumia roho tunapokuwa tukipelekana klinini jinsi abiria ndani ya daladala wanavyotushangaa, najua ni kutokana na jina kubwa la Gurumo na hali aliyonayo kimaisha," alisema.
Aliongeza, ingelikuwa ni amri yake angependa kuona Gurumo akipumzika masuala ya muziki baada ya kuutumikia kwa zaidi ya miaka 50.

Mwisho

NB:Inawezekana Mzee Gurumo aliuzingatia ushauri huo wa mkewe na kuamua kupumzika muziki majuzi akitarajiwa kuagwa rasmi kwa matamasha ili kumchangia fedha za 'pensheni' yake katika muziki. MICHARAZO inamtakia kila la heri mkongwe huyo na Allah SW ampe siha, afya na umri mrefu zaidi Inshallah.