Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, October 10, 2014

SHIWATA kugawa mashamba Nyerere Day



MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umeandaa ibada maalum ya kumkumbuka Baba wa taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere itakayofanyika katika mashamba yao yaliyopo kijiji cha Ngarambe, Mkuramga mkoa wa Pawani.

Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana kuwa katika ibada hiyo itaongozwa na Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum kwa upande wa Waislam na Padri John Solomon kwa upande wa Wakristo.

Taalib alisema katika ibada hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mercy Silla na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo wamealikwa kuhudhuria ambayo itakuwa sambamba na ugawaji wa mashamba kwa wanachama ambao wamekubali kulima katika shamba la SHIWATA lenye ekari 500.

Alisema SHIWATAitaendelea kuenzi fikra za Hayati Mwalimu Nyerere alizowahi kuzifanya na kuziendeleza wakati wa uhai wake ambako wasanii waliitikia mwito kwa kuanzisha kijiji chao cha Mwanzega chenye ukubwawa hekari 300 za makazi ambako mpaka sasa zimejengwa nyumba 66 na nyingine zinajengwa na kukabidhiwa Desemba mwaka huu.

Alisema SHIWATA yenye wanachama zaidi ya 8,000 imekuwa ikihamasisha wanachama wakewajenge nyumba katika kijiji chao ambacho Serikali imekitambua rasmikwa kukizindua kupitia Mbio za Mwenge wa Uhuru Julai mwaka huu.

Ofisa Habari wa SHIWATA

No comments :

Post a Comment