Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 29, 2015

SELCOM YAONGEZA MAPATO YA TAZARA COMPUTER TRAIN KASI



 
 
KAMPUNI ya Selcom Tanzania imesema kwa kushirikiana na Tazara imefanikiwa kuongeza mapato ya fedha kwa mfumo wa ukatisha tiketi ulioanza kutumiwa na shirika la reli la Tazara.

Akizungumza na mwandishi  wa gazeti hili, Bw. Juma Mgori,  ambaye in Meneja Ukuzaji Biashara na Masoko wa Kampuni ya Selcom Tanzania, alisema  kupitia vifaa vyao vya kukata tiketi (POS), wananchi wameondolewa adha kubwa waliyokuwa wakiipata wakati wa kukata tiketi katika shirika reli la Tazara.

Alisema kuwa, kutokana na mpango huo,  TAZARA imefanikiwa kuongeza mapato kwa abiria kukatiwa tiketi kwa mfumo wa mashibe hizo.

Mfumo huo ni rahisi na bora zaidi na hivi karibuni kampuni ya Selcom inatarajia kuzindua kadi zake mpya za malipo zijulikanazo kama SELCOM PAYPOINT CARD ambazo mbali na malipo mbalimbali na uwezo wa kutuma Pesa kwenye mitandao yote.

 Kadi hizo zinaweza kuwa njia sahihi kwenye njia za usafiri kama treni, mabasi ya mikoani na hata daladala.

Bw. Mgori alisema kuwa, kadi hizo ni salama na zenye uwezo mkubwa zikiwa zimethibitishwa na kuidhinishwa katika viwango vya nchini na hata vya kimataifa.

"Tunajivunia ubunifu wetu huu ambao unafanyika hapa nyumbani na kampuni ya kizawa na wataalamu wazawa. Ikumbukwe pia kadi hizi hivi sasa zinatumika na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa wale wastaafu kutoa Pesa zao na ziko kwenye majaribio.

SUPER D AHAMASISHA UWANDIKISHAJI WA VITAMBULISHO VYA KUPIGIA KURA


 
 
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akiweka alama za vidole wakati wa uhandikishwaji wa vitambulisho vya kupigia kura iliyokuwa ikifanyika katika kitongoji cha Buguru Dar es alaam kulia ni muhandikishaji wa kituo hicho Karim Ibrahimu
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akiweka alama za vidole wakati wa uhandikishwaji wa vitambulisho vya kupigia kura iliyokuwa ikifanyika katika kitongoji cha Buguru Dar es alaam kulia ni muhandikishaji wa kituo hicho Karim Ibrahimu


Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchinini Rajabu Mhamila  Super D akitia saini kitambulisho chake kabla akijatoka kwa karani wa Karim Ibrahimu

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' askiangalia picha yake kabla akijatengenezwa kitambulisho kwa karani Karim Ibrahimu ilikuwa mpiga picha anapopigwa picha na mtu mwingine

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akiweka akionesha kitambulisho chake
Rajabu Mhamila akiwa ametulia

Wednesday, July 22, 2015

NJAMA ZA MAKABURU KUMG'OA MKURUGENZI WA KONYAGI MGWASSA ZAGUNDULIKA



 Rais Jakaya Kikwete (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), maarufu kwa jina la Konyagi . David Mgwassa Kombe la ushindi wa mwaka wa uzalishaji bora nchini katika hafla ya Shirikisho la Wenye Viwanda nchini (CTI) Jijini Dar es Salaam.Mwandishi Wetu

MKAKATI wa kumng'oa Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi (TDL) David Mgwassa umebainika kutokana na kuwepo kwa njama zinazoendeshwa kwa siri na makaburu.

Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu umebaini kuwa kiongozi huyo amekuwa akipigwa vita kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni mafanikio yanayopatikana chini ya uongozi wake.

Makaburu hao wamekuwa wakifanya njama mbalimbali za kumng'oa kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kutaka kushika wadhifa wa mkurugenzi huyo kwa kutoa taarifa ambazo si za kweli kwa uongozi wa ngazi za juu nchini Afrika Kusini na Uingereza.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa kiongozi huyo ametakiwa kukabidhi ofisi ifikapo Julai 30, mwaka huu.

Chanzo hicho kimeeleza kuwa tayari taarifa za kuondolewa kwa kiongozi huyo zimezagaa katika viwanda vya TDL na Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) pia tangazo la kumbadilisha limetolewa kupitia kwenye mtandao wa kijamii wa WhatsApp na kutangaza Kenya na Uganga.

Kutokana na taarifa hizo baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha TDL wameazimia kugoma ili kushinikiza mkurugenzi huyo kuendelea na madaraka yake.

"Tumesikia taarifa kuwa mkurugenzi wetu anaondolewa madarakani kwani tumeshangazwa sana kutokana na kuishi naye vizuri na kupatikana kwa mafanikio mengi tangu ashike wadhifa huo na pia ameboresha maisha yetu kwa kutuongezea mishahara," alisema mfanyakazi mmoja ambaye hakutaja jina lake kuandikwa gazetini kwa kuwa si msemaji wa wafanyakazi.

Hata hivyo kuna taarifa kuwa Bw. Michael Benjamin anatarajia kushika wadhifa wa Bw. Mgwassa.

Mtandao huu ulimtafuta Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Steve Kilindo ili kuzungumzia taarifa hilo alikiri kuwepo kwa mabadiliko hayo lakini hana taarifa zaidi kuhusiana na sakata hilo.

"Kweli kuna mabadiliko hayo ya uongozi lakini taarifa za ndani sina," alisema.
                         Mike Benjamin kutoka Afrika Kusini anayetarajia kurithi cheo hicho

Friday, July 17, 2015

MABONDIA WA KIKE KUZIDUNDA KESHO


Promota Stamili Mmtengwa katikati akiwainuwa juu mabondia Mwanne Haji kushoto na Lulu Kayage baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika sikukuu ya Iddi Mosi katika ukumbi wa Frends Corner  Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Mmwanne Haji kushoto na Lulu Kayage wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika siku ya Iddi Mosi Katika ukumbi wa Frends Ccorner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Lulu Kayage akipimwa na Ddokta Michael Madadidi kwa ajili ya mpambano wake na mwanne Haji

Promota Stamili Mmtengwa katikati akiwainuwa juu mabondia Habibu Pengo kushoto na Yonas Segu

Bondia Mwanne Hhaji akipimwa Afya na Dokta Mmixchael Midadi

Bondia Lulu Kayage akipimwa na Ddokta Michael Madadidi kwa ajili ya mpambano wake na mwanne Haji

Tuesday, July 14, 2015

NHIF YAIPIGA TAFU TIMBERLAND JOGGING YA YOMBO KILAKALA


Mlezi wa kikundi cha Timberland Jogging cha yombo Kilakala  Carren Mgonja akiwazungumza na maofisa wa Mfuko wa Afya ya Jamii NHIF walipowatembelea makao yao makuu 

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha Timberland Jogging wakisoma vipeperushi vya Mfuko wa Afya ya Jamii NHIF 

Mlezi wa kikundi cha Timberland Jogging cha yombo Kilakala  Carren Mgonja kushoto akipokea fulana kutoka kwa Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii NHIF .Eugen Mikongoti wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa kikundi hicho Samir Choray na maofisa wa NHIF

 Mlezi wa kikundi cha Timberland Jogging cha yombo Kilakala  Carren Mgonja kushoto akipokea msaada wa fulana kutoka kwa Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii NHIF .Eugen Mikongoti wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa kikundi hicho Samir Choray na maofisa wa NHIF
Makao makuu ya kikundi cha Timberland Jogging wanachama wakiwa na maofisa wa NHIF baada ya kugawa msaada wa fulana pamoja na ahadi ya kufanya kazi p-amoja na kikundi hicho kilichopo Yombo Kilakala

MAKAMU MWENYEKITI WA BODI YA LIGI, SAID MOHAMED AFUNGUA KOZI YA MAKOCHA WA MAKIPA



Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Salum Madadi (kushoto) akimtambulisha Mkufunzi wa FIFA Elaxander kutoka Ufaransa (wa pili toka kushoto) wakati wa ufunguzi wa kozi ya makocha wa magolikipa inayoendelea katika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana. Wa pili toka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu nchini, Said Mohamed na kulia ni Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa


Mkufunzi wa FIFA Elaxander kutoka Ufaransa (aliye katikati ya waliosimama) kwa pamoja na washiriki  wa kozi ya makocha wa golikipa inayoendelea katika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam


MAKAMU Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi nchini, Said Mohamed amewataka washiriki wa kozi ya makipa kutumia vizuri mafunzo watakayopata katika kuendeleza mpira nchini.

Said Mohamed ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya TFF, aliyasema hayo jana wakati akifungua kozi ya makocha wa golikipa inayoendelea katika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.

“Naishukuru FIFA kwa kuipa Tanzania nafasi ya kuendesha mafunzo hayo ya makocha wa makipa kwa mara ya kwanza nchini pia nawaomba washiriki wa kozi hii mtumie vema nafasi kwa ajili ya kuendeleza mpira wa miguu”, alisema Said

Naye mshiriki Mohamed Mwameja ‘Tanzania One’ ambaye amewahi kuidakia Simba na timu ya Taifa alishukuru kupata kozi hiyo na kusema itawasaidia kujua makosa yao kwani wamekuwa wakifundisha kwa uzoefu ambao waliupata wakati wakicheza.

“Sisi tunafundisha kwa kutumia uzoefu tuliopata kutoka kwa waliotufundisha wakati tukicheza hivyo kozi hii itatufanya tujitambue wapi tulikuwa tukikosea ili turekebishe na tupate makipa bora”, alisema Mwameja

 Jumla ya makocha 31 wanashiriki kozi hiyo kutoka vilabu vyote viliyovopo Ligi Kuu ya Tanzania Bara na Zanzibar na magolikipa wa zamani walio wahi kudaka timu za Taifa.

Kozi hiyo inaendeshwa na mkufunzi wa FIFA Elaxander kutoka nchini Ufaransa, ambaye alidumu kama golikipa kwa miaka 20 na inatarajiwa kufungwa Julai 17, mwaka huu 

Monday, July 13, 2015

MABONDIA WA KIKE KUMALIZA UBISHI SIKU YA IDDI MOSI KATIKA UKUMBI WA FRENDS CORNER MANZESE DAR






Na Mwandishi Wetu

 MABONDIA wa kike kupanda uringoni siku ya Iddi Mosi katika ukumbi wa frends corner Manzese Dar es Salaam mambondia hawo ni Lulu Kayage ambaye atavaana na Mwanne Haji katika mpambano wao wa raundi sita uzito wa kg 49 

Mratibu wa mpambano uho Dikumbwaya Mtengwa siku hiyo pia kutakuwa na ngumi kazi za wanaume wa shoka alisema bondia

Yonas Segu atapambana na Habibu Pengo mpambano wa raundi nane uzito wa kg 63 na  Nassibu Ramadhani Kudura Omar mpambano wa kg 53 raundi sita wakati Shadrack Juma atakabiliana na Bakari Ostadhi 
mbali na mipambano hiyo ya ngumi pia kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazo ambatana na sherehe ya sikukuu ya Iddi

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi

pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

BONDIA MOHAMED MATUMLA KUMVAA KOBA DONATI IDI PILI BAGAMOYO



Na Mwandishi Wetu

BONDIA Mohamed Matumla anatalajia kupanda tena uringoni siku ya Idi pili katika ukumbi wa TASUBA uliopo Bagamoyo Mkoa wa Pwani kupambana na Koba Nodat katika uzito wa KG 57 mpambano wa raundi sita Matmla anapambana mpambano uho baada ya mpambano wake wa mwisho kumtwanga Mchina kwa point

mratibu na promota wa mpambano uho Muhsin Sharif amesema amesema mbali na mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi litawakutanisha bondia Iddi Pialali kutoka Kiwangwa Bagamoyo na Mesharck Mwankemwa kutoka Mbeya mpambano wa raundi nane kg 66 wakati bondia machachari katika tasnia ya mchezo wa masumbwi nchini Vicent Mbilinyi atavaana na Khalidi Hongo mpambano wa raundi nne wakati Twalibu Tuwa atavaana na Sudi Sudi

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi

pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha