Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, August 26, 2010

NIZAR NA SOMO JIPYA KWA WACHEZAJI WA TANZANIA

Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Nizar Khlafani ambaye amewasili tayari kujiunga na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kimashindano dhidi ya Algeria ikiwa ni mchezo wa kufuzu kucheza michuano ya mataifa ya Afrika mwaka 2012.

NIzar Khalfani akizungumza na mdau wa Sports ya Capital Radio ambayo huruka kila siku saa tatu kamili usiku hadi sa tatu na nusu, MAster Tindwa Mtopa, Nizar amesema wachezaji ili waweze kupata mafanikio wanalazimika kutumia muda wao wa ziada kufanya mazoezi mbali na muda ambao mchezaji anakuwa na kocha.

Amesema hiyo ilikuwa kwake ni moja ya chngamoto kubwa lililokuwa likimkabili wakati alipojiunga na klabu ya Vancouva ambayo mwakani inashiriki ligi ya Marekani.

Nizar amesema Tanzania inavipaji vya wachezaji wa zuri na wenye viwango ingawa wanakabiliwa na changamoto ya nguvu na kujituma.

Amesema ili wachezaji waweze kufanikiwa ni lazima wachukulie mpira kuwa ni kazi kama zilivyo kazi zingine na inamaslahi mazuri endapo mchezaji atajituma na kuwa na malengo.

ROCK CITY MARATHON KUANZA 26 SEPTEMBA

Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Tanzania (RT) Suleiman Nyambui (kushoto)
akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa
mashindano ya riadha yanayojulikana kama Rock City Marathon yanayotarajiwa
kufanyika Mwanza Septemba 26 mwaka huu.Katikati ni Mratibu wa mashindano hayo
kutoka Kampuni ya Capital Plus Ltd ambao ndio waandaaji Raymond Kanyambo na
kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Amant Macha
aliyekuwa mgeni rasmi wa hafla hiyo iliyofanyika Dar es Salaam jana.

KAMPUNI ya Capital-Plus International (CPI) imeandaa mashindano ya riadha ya kilomita 21 yanayojulikana kama "Rocky City Marathon 2010" yatakayofanyika Septemba 26 mwaka huu jijini Mwanza.

Mashindano haya kwa mara ya pili ambapo mara ya kwanza yalifanyika mwaka jana na yanatarajia kufanyika katika uwanja wa CCM Kirumba kuelekea njia tofauti za jiji la Mwanza na kumalizia katika uwanja huo.

Mratibu wa mashindano hayo Raymond Kanyambo amesema katika haitakuwa na tofauti na mashindano yaliyopita kwa kujumuisha wanariadha toka sehemu tofauti hapa nchini Tanzania na nchi Jirani kushiriki katika mbio hizo katika ukanda wa ziwa.

amesema tayahri wamekwishatuma mialiko katika nchi mbali mbali kuwataka wanariadha kushiriki kwa kujiandikisha kupitia vyama vya riadha katika nchi zao ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na Zambia.

Mashindano

RATIBA YA LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA YA PANGWA MONACO

Ratiba ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya hii hapa ambayo imepangwa mjini MOnaco.

Group A Internazionale Werder Bremen Tottenham Hotspur

Twente
Group B Olympique Lyon Benfica Schalke 04

Hapoel Tel Aviv
Group C Manchester United Valencia Rangers

Bursaspor
Group D Barcelona Panathinaikos Kobenhavn

Rubin Kazan
Group E Bayern München Roma Basel

CFR Cluj
Group F Chelsea Olympique Marseille Spartak Moskva

Zilina
Group G Milan Real Madrid Ajax

Auxerre
Group H Arsenal Shakhtar Donetsk Braga

Partizan Belgrado

Wednesday, August 18, 2010

YANGA OYEEEEEEEEEEEE

YANGA JUUUUU YATWAA NGAO YA JAMII KWA KUIFUNGA SIMBA KWA MIKWAJU YA PENATI MITATU KWA MOJA

Nahodha wa yanga mbuna akiwa ambeba nago ya jamii mara baada ya kukabidhiwa
ngao ya jamii ikiwa imeshikwa na baadhi ya viongozi wa yanga katikati ni makamu mwenyekiti wa yanga davis ,kulia doctor na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji
baada ya kazi ngumu vijana wa jangwani wafurahi na ngao ya hisani
Uhuru suleiman akimbebeleza mmoja wa wachezaji wa simba baada ya simba kufungwa katika mchezo wa ngao ya jamii