Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 30, 2011

DVD YA SUPER D BOXING COACH KUPATIKANA KIURAISI KESHO PTA

Rajabu Mhamila Super D (kushoto) akisisitiza jambo wakati anaelekeza vitu vya msingi vilivyomo katika Video ya mafunzo ya mchezo wa ngumi kulia ni Said Chaku, Amri Massare na Antoni Ruta

Edson Joel na Zaituni Kibwana wakiangalia kava ya Super D Boxing Coach leo
Kocha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D (kushoto) akitoa maelekezo yaliyomo katika DVD yake ya mafunzo ya mchezo wa ngumi kwa wadau wa mchezo huo kutoka kulia ni Saidi Chaku, Amri Masare, Zainabu Kiliware, Edson Joer na Antoni Ruta Dar es salaam leo ambapo VIDEO CD hazo zitapatikana kwenye mapambano yote ya ngumi nchini

MTOTO WA MFALME, WILLIAM AFANYA KUFURU KWA KUFUNGA NDOA YA KIFAHARI ILIYOGHARIMU MABILIONI YA PESA



Mwana mfalme William akifungishwa ndoa na Aksofu Rowan William katika kanisa la Westminster Abbey jijini London.

MTOTO wa mfalme wa Uingereza, Prince William na Kate Middleton wamefunga ndoa katika kanisa la Westminster Abbey jijini London.

Takriban wageni 1,900 walishuhudia tukio hilo ndani ya kanisa, na mamilioni wakifuatilia majumbani mwao kwa njia ya televisheni.


Maharusi hao walishangiliwa na maelfu ya watu waliojipanga barabarani kuelekea kasri ya Buckingham Palace ambako Malkia amewaandalia karamu wageni 650.


Wana ndoa hao wapya walitumia gari liliovutwa na farasi la muundo wa mwaka 1902 ambalo lilitumiwa na wazazi wake Prince William wakati wa ndoa yao mwaka 1981.


Maharusi hao baadaye walijitokeza kwenye roshani ya kasri ya Buckingham na kuwasalimu maelfu ya watu waliokwenda kuwasherehekea.


Baada ya kulishana viapo vya ndoa Askofu mkuu wa Canterbury, Rowan Williams, aliwanadi rasmi kuwa "mume na mke".


Kuanzia sasa maharusi hao watajulikana kama Duke na Duchess wa Cambridge.


MAPACHA WATATU NA WANAUME TMK KUTUMBUIZA IKWETA GRILL LEO



BENDI ya muziki wa Dansi ya Mapacha Watatu na Kundi la muziki wa kizazi kipya TMK Wanaume Family, leo watafanya onesho moja kwenye Ukumbi wa Ikweta Grill uliopo Mtoni kwa Azizi Ali, Temeke.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa onesho hilo, Zahor Said alisema kuwa maandalizi ya onesho hilo yamekamilika kama walivyopanga na wapenzi wote wa burudani katika sehemu za Temeke na maeneo ya jirani watarajie mambo makubwa.
Alisema katika onesho hilo litakaloanza saa 3 usiku, watoto wa Temeke, Wanaume Family watakuwa wa kwanza kufanya makamuzi yao juu ya jukwaa ikiwa ni mara yao ya kwanza kufanya onesho kwenye ukumbi huo.
Said alisema mapacha wao watatoa burudani yao ikiwa ni pamoja na kupeleka tuzo zao za Kili Music Awards ambazo walizitwaa kutokana na umahiri wao.

SHINDANO LA MISS TANZANIA LAZINDULIWA RASMI KILIMANJARO KEMPINSKI DAR ES SALAAM

Kutoka kushoto ni Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala akiwa katika picha ya paoja na warembo waliowahi kuvaa Crown ya Miss Tanzania anaye fuata baada ni Angela Damas, Nasreen Karim, Jacqueline Ntuyabaliwe, Hoyce Temu, Saida Kessy na Richa Adhia.

Wadau hawa wakifuatilia uzinduzi wa mashindano haya ya urembo ambayo yamezinduliwa rasmi.
Mratibu wa Miss Tabata Fred Ogot akiwa na Miss Tabata 2010 Consolata Lukosi.
Mbunifu wa mitindo mbalimbali ya mavazi nchini Ally Rhemtullah.

Muandaaji wa Kituo cha Kurasini Miss Kurasini Bibie Zuhura naye alikuwepo.

Somoe Ng'itu kulia na Khadija Kalili
Mhariri wa Habari za Michezo na Burudani Suleiman Mbuguni na Khadija Khalili.

Mama wa Bongoweekendblog nikijiegesha nje mara baada ya hafla hiyo.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency pia Mratibu wa Miss Tanzania Hashim Lundenga akizungumza kwenye uzinduzi huo uliofanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski Dar es Salaam.

Kampuni ya Viodacom usiku huu imezindua rasmi shindano lake la urembo la Miss Tanzania kwa kipindi cha maka 2011.Hapa Meneja udhamini wa Kampuni hiyo George Rwehumbiza amesema kuwa wao ndiyo wadhamini wakuu wa shindano hilo.Waliosimama nyuma yake ni baadhi ya warembo waliowahi kutwaa taji la Miss Tanzania.

Meneja Udhamini wa Kampuni hiyo ametoa wito kwa wazazi kuwapa ushirikiano vijana wao wenye nia ya kushiriki katika shindano hilo na hivyo kuonyesha vipaji vyao ."Pia nachukua fursa hii kuwaomba wasichana kokote walipo hapa nchini wajitokeze kwa wingi kushiriki katika shindano hili na kuonyesha vipaji vyao mbalimbali katika kuitumikia jamii yetu".

Hawa ni baadhi ya warembo Miss Tanzania ambao walikuwepo katika uzinduzi wa rasmi wa shindano na nembo mpya ya mdhamini wao Kampuni ya simu ya Vodacom waling'ara kwa miaka tofauti na kupeperusha bendera ya Taifa katika mashindano ya dunia .Kutoka kushoto ni Angela Damas Miss Tanzania (2001),Nasreen Karim (Miss Tanzania 2009),Jacqueline Ntuyabaliwe (Miss Tanzania 2000),Genevieve Mpamnaga (Miss Tanzania 2010) na Saida Kessy (Miss Tanzania 1997).

Hapa tukishangweka SHOSTITO Miss Tanzania 1999 pia alikuwa Miss Ilala kwa mwka huo Hoyce Temu asiyechuja , Dina, Khadija nyuma ya Hoyce na menye kivazi cha buluu ni Somoe.

VIMWANA WA TWANGA KUONYESHA NYONGA ZAO LEO USIKU MANGO GARDEN 'TWANGA CITY'



Mratibu wa Shindano la Kimwana wa Twanga Maimatha.





Bendi ya African Stars “Twanga Pepeta” Jumamosi tarehe 30-04-2011 inataraji kutumia onyesho lake katika ukumbi wa Mango Garden Kinondoni, kuwasugulisha kisigino washiriki wa shindano la Kimwana wa Twanga Pepeta 2011.
Sugua Kisigino ni mtindo unaotumiwa na Twanga Pepeta na ni moja ya staili zitakazotumika kwenye shindano hilo, hivyo washiriki watatumia fursa hiyo ili kufahamu jinsi ya kucheza staili hiyo.
Washiriki watatumia onyesho hilo ili kusalimu mashabiki wa Mango Garden ukumbi ambao una historia ndefu na Twanga Pepeta.
Onyesho rasmi la utambulisho wa Vimwana wa Twanga Pepeta 2011 unatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 06-05-2011 ndani ya Club ya Sun Cirro iliyoko Sinza na Fainali itakuwa Ijumaa tarehe 03-06-2011.
Burudani ya Utambulisho wa Shindano la Kimwana wa Twanga Pepeta 2011 itatolewa na Wakali wa Dansi Tanzania, African Stars Band “Twanga Pepeta” na Msanii Abbas Kinzasa maarufu kama 20 percent au asilimia ishirini, pamoja na shoo kali ya Nyonga teketeke ya Vimwana wa Twanga Pepeta.
MAIMARTHA JESSE
MRATIBU WA SHINDANO.
http://bongoweekend.blogspot.com/

WAFANYAKAZI IDARA YA HABARI (MAELEZO) WAMUAGA RASMI MKURUGENZI CLEMENT MSHANA ALIYETEULIWA KUONGOZA TBC


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Clement Mshana (kushoto) akikabidhiwa zawadi iliyoandaliwa na wafanyakazi wa Idara hiyo na Ofisa Habari Mwandamizi, Anna Itenda (kulia)wakati wa hafla fupi ya kumuaga rasmi iliyofanyika leo jijini Dar es salaam. Mshana ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete kuwa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) .
Clement Mshana, akizungumza na wafanyakazi wa Idara hiyo leo jijini Dar es salaam wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na wafanyakazi hao.

Wafanyakazi wa Idara ya Habari (MAELEZO) wakiwa katika picha ya pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara hiyo Clement Mshana (katikati) baada ya hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika kwenye ukumbi wa Idara hiyo jijini Dar es Salaam leo mchana. Picha Zote na Aron Msigwa-MAELEZO

HAPPYBIRTHDAY PRINCESS ASIA MAHMOUD ZUBEIR


Pichani ni Mtoto Princess Asia 'Checha' leo anatimiza miaka minne ya kuzaliwa. Anawasalimu mama yake Dina Ismail mwendeshaji wa Blog ya Mamapipiro.blogspot.com, Baba yake Prince Mahmoud Zubeir.Pia anamsalimu Dada yake Precious na mdogo wake Prince Akbar wote wakiwa Kinondoni Dar es Salaam. Babu na Bibi Checha wanaoishi Tabata, mwisho awawasalimu Aunt Ankal Abbas,Aunt zake Amina na Miski.Mwendeshaji wa Blogu hii nakupongeza Baby Checha pia nakuombe kwa mungu akujaalie umri mkubwa na undelee kuwa mtoto mtiifu kwa wazazi wakubwa na wadogo pia endelea na moyo huohuo wa kupenda shule

Wednesday, April 27, 2011

MBWANA MATUMLA ANOGESHA NGUMI ILALA


Bondia Mbwana Matumla (kulia) akioneshana umwamba wa kutupa makonde na Omari Bayi wakati wa tamasha la kuamasisha mchezo wa ngumi uliofanyika, Dar es Salaam jana mabondia wote wanajiandaa na mapambano yao yatakayofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA sabasaba Dar es salaam
Baadhi ya wadau wa Mchezo wa ngumi wakibadilishana mawazo
BABY IKOTA SUPER D MNYAMWEZI AKISALIMIANA NA HABIBU KINYOGOLI

KANUMBA ATOKA NA Ramsey WA NIGERIA


Msanii wa filam kutoka Nigeria, Ramsey Tokumbo(kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana baada ya kufanya kazi na msanii Stevin Kanumba kushoto ambapo alieleza mafanikio aliyoyapata na kuondoka

Hadija Khalili akipiga picha na Kanumba wa Bongo mover

Monday, April 25, 2011

NGUMI KUPIGWA PANANDIPANANDI ILALA BUNGONI KESHO


MABONDIA wa ngumi za ridhaa wa mkoa wa Ilala wanatarajia kupanda ulingoni kesho katika ukumbi wa Panandipanandi, Ilala Dar es Salaam. ambapo kutakuwa na ngumi kutoka kwa mabondia mbalimbali toka pande zote za mkoa wa DAr es Salaam

Tamasha hilo litakalokuwa likitimua vumbi kila wiki inatarajia kuwakutanisha mabondia wa Ilala na wa sehemu nyingine za Dar es Salaam ili kuweza kujipima nguvu katika kuinua mchezo huo katika mkoa huo.

Katika Tamasha hilo kesho bondia Mbwana Matumla anayejiaandaa kwa ajili ya kushiriki katika kuwania ubingwa wa UBO pambano linalotarajia kufanyika siku ya Mei mosi katika ukumbi wa PTA dhidi ya Mkenya Gabriel Ochieng atachuana na mabonmdia Yohana Robert na Issa Sewa.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Mratibu wa Tamasha hilo kupitia Taasisi ya Kinyogoli foundation, Habibu Kinyogoli alisema mapambano yote yatakuwa katika raundi nne huku pambano la Mbwana likiwa katika uzito wa Kg 55 likiwa ni sehemu ya maandalizi ya pambano lake hilo.

Alisema, mkakati huo wa kuanzisha Tamasha akishirikiana na kocha msaidizi wa timu ya mkoa huo Rajabu Mhamila 'Super D' utasaidia kuinua vipaji vipya vya mchezo huo kwa kiasi kikubwa kwani kutawajenga wachezaji kujikita katika mchezo huo na kuufanya kama ndio ajira yao.

Alisema, katika kulifanikisha hilo anawaomba wadau mbalimbali kuwasaidia kuwadhamini ili waweze kufikia malengo yao katika kuinua vipaji hivyo.pia alisema kutakuwa na wageni waalikwa ambao watatoa mada mbalimbali kuhusu kuinua mchezo wa ngumi Tanzania akiwemo mdau wa ngumi.Innocente Melleck na mwingine Benedictor Hulilo ambao watakuwa wageni waalikwa

MASHINDANO YA SAFARI LAGER DARTS AFRIKA MASHARIKI YAMALIZIKA


Mratibu wa michezo ya DARTS Innocente Melleck akipanga zawadi mbalimbali za vikombe vilivyotolewa kwa washiriki
Mratibu wa michezo ya DARTS Innocente Melleck akipanga zawadi mbalimbali za vikombe vilivyotolewa kwa washiriki
Wachezaji kutoka Kenya wakishangilia baada ya kuimba wimbo wao wa Taifa
Wachezaji wa Kenya wakiimba wimbo wa Taifa

Wachezaji wa Uganda wakimba wimbo wa Taifa wakati wa Fainali
Mchezaji wa mchezo wa vishare, Julieth Kantumbare kutoka, Uganda akirusha wakati wa mashindano ya Afrika Mashariki yaliyomalizika Dar es salaam mwishoni mwa wiki ambayo yalizaminiwa na kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Safari
Mchezaji wa mchezo wa vishare, Dinah Amoding kutoka, Uganda akirusha wakati wa mashindano ya Afrika Mashariki yaliyomalizika Dar es salaam mwishoni mwa wiki ambayo yalizaminiwa na kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Safari
Baadhi ya mashabiki wakifatilia mashindano ya DARTS yaliyomalizika Dar Es Salaam jana

Sunday, April 24, 2011

MISS KILIMANJARO HUYU HAPA


Baadhi ya Warembo watakaowania taji la miss Kilimanjaro wakiwa katika pozi, Dar es salaam jana kabla ya kwenda kuweka kambi rasmi itakayoanza mwanzoni mwa mwezi ujao mkoani Kilimanjaro. kutoka kushoto ni Catherine Edwin,Diana Lymo na Jackline John


Catherine Edwin
Jackline John
Diana Lymo

MISS TABATA MATAMBO YANAENDELEA..!!





Warermbo wakiwa katika pozi wakisubiri siku ya mchuano
Warembo wanaoshiriki shindano la Miss Tabata 2011 wakiwa katika picha za pamoja katika pozi tofauti wakati wa mazoezi yao katika Ukumbi wa Dar West Park Tabata jijini Dar es Salaam. Warembo hawa wanachuana kuwania taji linaloshikiliwa na Miss Tabata 2010 Consolatha Lukosi.