Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 30, 2011

VIMWANA WA TWANGA KUONYESHA NYONGA ZAO LEO USIKU MANGO GARDEN 'TWANGA CITY'



Mratibu wa Shindano la Kimwana wa Twanga Maimatha.





Bendi ya African Stars “Twanga Pepeta” Jumamosi tarehe 30-04-2011 inataraji kutumia onyesho lake katika ukumbi wa Mango Garden Kinondoni, kuwasugulisha kisigino washiriki wa shindano la Kimwana wa Twanga Pepeta 2011.
Sugua Kisigino ni mtindo unaotumiwa na Twanga Pepeta na ni moja ya staili zitakazotumika kwenye shindano hilo, hivyo washiriki watatumia fursa hiyo ili kufahamu jinsi ya kucheza staili hiyo.
Washiriki watatumia onyesho hilo ili kusalimu mashabiki wa Mango Garden ukumbi ambao una historia ndefu na Twanga Pepeta.
Onyesho rasmi la utambulisho wa Vimwana wa Twanga Pepeta 2011 unatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 06-05-2011 ndani ya Club ya Sun Cirro iliyoko Sinza na Fainali itakuwa Ijumaa tarehe 03-06-2011.
Burudani ya Utambulisho wa Shindano la Kimwana wa Twanga Pepeta 2011 itatolewa na Wakali wa Dansi Tanzania, African Stars Band “Twanga Pepeta” na Msanii Abbas Kinzasa maarufu kama 20 percent au asilimia ishirini, pamoja na shoo kali ya Nyonga teketeke ya Vimwana wa Twanga Pepeta.
MAIMARTHA JESSE
MRATIBU WA SHINDANO.
http://bongoweekend.blogspot.com/

No comments :

Post a Comment