Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 29, 2013

BONDIA IDDY MKWERA AMCHIMBIA MKWALA LUCAS NDULA WA MUHEZA





IDDY MKWERA
BONDIA Iddy Mkwera wa Dar es salaam anatarajia kuzipiga na Lucas Ndula wa Muheza wakati wa kusherekea sikukuu za pasaka jumapili ya march 31 katika viwanja vya wazi vya Jitegemee vilivyopo wilaya ya Muheza Mkoa wa Tanga
Bondia huyo  aliyefika Muheza kwa mbwembwe na kusema atamtwanga
Ndula
K,O ya raundi ya pili ili arudi na ushindi Dar es salaam kwa ushindi mnono unajua mimi nafundishwa na kocha wa kimataifa Rajabu Mhamila 'Super D'  anaejua mbinu zote za masumbwi Duniani na nimefanyia mazoezi miezi miwili hivyo sitarajii kuremba katika mpambano huo kwani kwa sasa nimeamua kucheza mchezo huu na ninawambia mabondia wote walio katika uzito wa kg, 60 kuwa tayali kupambana na mimi

Mchezo huo utakaochezwa katika viwanja vya jitegemee Wilaya ya Muheza Mkoa wa Tanga utakuwa na bule hivyo watu mbalimbali wameobwa kujitokeza kuja kuangalia vipaji vya mchezo huo wenye kupendwa na vijana wengi nchini

Nae mmoja wa wadau wa nchezo wa ngumi Muheza Allan Augastino ambaye aliyetoa galama mbalimbali amesema vijana wengi wanapenda ngumi hivyo nimeamua kuwaletea hapa hapa bila kujali chochote na kugalamia kila kitu ikiwemo mabondia kutoka Dar pamoja na ulingo  maalumu kwa ajili ya kuchezea

Mbali na mbambano uho kutakua na mapambano mengine mbali mbali ambapo Omari Kibwana wa dar atapambana na
Bakari Sendekwa

  Nae kocha wa mchezo huo Muheza, Chalres Muhilu ' Spins' alisema mpambano huo wa wazi umeandaliwa kwa ajili ya kutoa burudani wilayani hapo na kuhamasisha mchezo wa masumbwi

mabondia kutoka Dar wakipambana na Muheza pamoja na kutoa rai kujitokeza kwa wafadhili kudhamini mchezo huo unaopendwa na vijana wengi wilayani humo ndio mana tumeamua kuweka katika viwanja vya wazi ili watu wote wajionee wenyewe mchezo wa ngumi unavyo endeshwa katika mazingira magumu

Nae Kocha wa kimataifa wa mchezo huo Rajabu Mhamila 'Super D' aliyepewa jukumu la kwenda na vijana kutoka Dar ili wakalete changamoto na kuleta amasa ya mchezo huo amesema atakwenda na Omary Kibwana  atakayemenyana na Bakari Sendekwa katika uzito wa kilo 52 na Iddy Mkwera atakaepambana na Lucas Ndula mpambano wa raundi 6

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.
“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D .
--
Super D Boxing Coach
Email.superdboxingcoach@gmail.com
www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mob;+255787 406938
+255774406938
Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

TIMU YA LIVERPOOL YA WATOTO WAFANYA ZIARA YA PASAKA NA KUTOA ZAWADI



Visiting time: Samed Yesil, Jordan Ibe, Kristoffer Peterson, Craig Roddan, Ryan McLaughlin and Jack Dunn
Katika picha: Samed Yesil, Jordan Ibe, Kristoffer Peterson, Craig Roddan, Ryan McLaughlin na Jack Dunn.

Wachezaji vijana wa Liverpool wameonyesha upendo na kuguswa na watoto walioko mahospitalini katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ya Pasaka.

Kama inavyofanywa na watu mbalimbali nyakati kama hizi za sikukuu ya Pasaka na wao pia wamewatembelea watoto na kuwapa zawadi katika hospitali iliyoko karibu na klabu yao ya Liverpool.

 Jumla ya vijana wa klabu hiyo kumi na moja kutoka katika kituo cha kukuzia vipaji cha klabu hiyo, wametembelea hospitali ya Alder Hey jana na kuzungumza na watoto ambapo wataendelea kuwepo hospitalini hapo kipindi chote za sikukuu ya Pasaka.
 
Mlinzi Conor Coady mwenye umri wa miaka 20, ambaye alikuwepo katika kikosi cha kwanza cha Liverpool katika mchezo dhidi ya Anzhi Makhachkala katika michuano ya Ulaya 'Europa League' naye alikuwa ni miongoni mwa hao waliofanya ziara hiyo.
Amekaririwa akisema kinda huyo akisema, ‘Kufanya ziara kwa watoto hao ilikuwa jambo kubwa'.
Ameendelea kwa kusema, ‘Nina wadogo zangu nyumbani kwa hiyo najua nini maana ya watoto hawa kupata ujio wetu hususani kwa kuwapa faraja katika kipindi hiki.’
 
Wachezaji hao waligawanyika katika makundi ili kutoa nafasi ya kuzungumza watoto wengi zaidi pamoja na familia zao.
Coady aliuungana na kundi lililokuwa likitoa zawadi ya Chocolate akiwa na wachezaji wengine Lloyd Jones, Jordan Ibe, Ryan McLaughlin, Jack Dunn, na Brad Smith.
Easter bonus: The Liverpool youth players dropped into Alder Hey Hospital to visit the children
Pia alikuwepo Samed Yesil, ambaye mpaka sasa ameshaichezea ligi ndogo ya Capital One michezo miwili kama ilivyokuwa Kristoffer Peterson, Danny Ward, Adam Morgan na Craig Roddan.
Regulars: The academy players visit the hospital every month to see the children
Alder Hey Children’s NHS Foundation Trust ni moja kati ya vituo vya afya vinavyokusanya watoto wengi barani Ulaya ambapo watoto zaidi ya laki mbili hupatiwa huduma kila mwaka.

MATUKIO MUHIMU KUTOKA RUVUMA


 Baadhi ya waandishi wa Habari mkoani Ruvuma kulia wakimsikiliza mhandisi wa maji taka na mazingira wa mamlaka ya maji safi na taka manispaa ya Songea9SOUWASA) Eddie Emanuel  jana wakati walipotembelea mabwawa ya maji taka katika eneo la Londoni mjini Songea.
Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga wakimsikiliza mwenyekiti wa halmashauri hiyo Oddo Mwisho(hayupo pichani0wakati wa kikao chao hivi karibuni mjini Mbinga.

RAIS KIKWETE AONGOZA MAMIA KUUAGA MWILI WA MBUNGE WA CHAMBANI DAR ES SALAAM LEO



  Kaimu Katibu wa Bunge Mhe John Joel akisoma wasifu wa marehemu
 Rais jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Spika Anne Makinda alipowasili katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Machi 29, 2013 kuongoza waombolezaji katika kuuaga mwili wa Mbunge wa Chambani(CUF),Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika Vikao vya kamati ya Bunge na kufaikiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Baada ya shughuli hii mwili ulisafirishwa kuelekea Chambani, Pemba, kwa maziko.
 Rais jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mbunge wa Monduli Mhe Edward Lowassa na Mbunge wa Mafia Mhe Abdulkarim Shah alipowasili katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Machi 29, 2013 kuongoza waombolezaji katika kuuaga mwili wa Mbunge wa Chambani(CUF),Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika Vikao vya kamati ya Bunge na kufaikiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Baada ya shughuli hii mwili ulisafirishwa kuelekea Chambani, Pemba, kwa maziko.
 Rais jakaya Mrisho Kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Machi 29, 2013 na kuongoza waombolezaji katika kuuaga mwili wa Mbunge wa Chambani(CUF),Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika Vikao vya kamati ya Bunge na kufaikiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Baada ya shughuli hii mwili ulisafirishwa kuelekea Chambani, Pemba, kwa maziko.
 Mama Salma Kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo  katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Machi 29, 2013 ambapo Rais Kikwete aliongoza waombolezaji katika kuuaga mwili wa Mbunge wa Chambani(CUF),Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika Vikao vya kamati ya Bunge na kufaikiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Baada ya shughuli hii mwili ulisafirishwa kuelekea Chambani, Pemba, kwa maziko.
 Wabunge wanawake wakiwa katika maombolezo  katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Machi 29, 2013 ambapo Rais Kikwete aliongoza waombolezaji  kuuaga mwili wa Mbunge wa Chambani(CUF),Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika Vikao vya kamati ya Bunge na kufaikiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Baada ya shughuli hii mwili ulisafirishwa kuelekea Chambani, Pemba, kwa maziko.
 Rais jakaya Mrisho Kikwete akiwa na viongzi wa kitaifa na wabunge katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Machi 29, 2013 ambako aliongoza waombolezaji katika kuuaga mwili wa Mbunge wa Chambani(CUF),Salim Hemed Khamis aliyeanguka ghafla jana katika Vikao vya kamati ya Bunge na kufaikiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Baada ya shughuli hii mwili ulisafirishwa kuelekea Chambani, Pemba, kwa maziko.

UCHAGUZI MIKUU BFT KUFANYIKA JIJINI MWANZA



Viongozi wa sasa BFT, Rasi Joan Minja (kulia) na Katibu Mkuu, Mashaga makore

UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Mchezo wa Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) unatarajiwa kufanyika Mei mwaka huu jijini Mwanza.
Katibu Mkuu wa BFT, Mashaga Makore, aliiambia MICHARAZO asubuhi ya leo kuwa, kuwa uchaguzi huo utafanyika mara baada ya kumalizika kwa michuano ya kimataifa ya Majiji yanayotarajiwa kufanyika jijini humo kati ya Mei 20-25.
Makore alisema mchakato wa kuelekea kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho kitatanguliwa na Mkutano Mkuu wa shirikishi hilo utatangazwa mara baada ya shamrashamra za sikukuu ya Pasaka.
"Uchaguzi Mkuu wa BFT utafanyika mwezi Mei jijini Mwanza mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya kimataifa ya ngumi inayoshiriki miji mikuu ya Afrika Mashariki na Kati, ambapo utatanguliwa na Mkutano Mkuu," alisema Makore.
Makore alisema maamuzi hayo yalifikiwa na Kamati yao ya Utendaji iliyokaa hivi karibuni na kutoa wito kwa wadau wa mchezo huo wenye uwezo na sifa za kuongoza shirikisho hilo kujiandaa kuijitosa kuwania uongozi kwenye uchaguzi huo.

JENGO LA GHOROFA 16 LAANGUKA KATIKATI YA JIJI



 Mtoto Maisamali Karim (6) ambaye ameokolewa kutoka katika madrasa ya Msikiti wa Khoja Shia Ithna Asheri Jamaat iliyoangukiwa na jengo hilo katika mtaa wa Indira Gandhi. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Changamoto ya uokoaji ni ngumu, lakini vikosi mbalimbali vinaendelea na zoezi hilo, ili kunusuru maisha ya waliofukiwa na kifusi.
 Hizi nia aina ya nondo ambazo kimsingi sio imara kuweza kuhimili ujenzi wa ghorofa ndefu kama hili, kuna haja mamlaka husika likatupia macho kampuni za ujenzi ili kuokoa maisha ya wajenzi na watumiaji wa majengo hayo.
 Askari wakiimarisha ulinzi wakati zoezi la uokoaji likiendelea.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea, huku nondo nyembamba zikionekana na kuacha maswali miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
 Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
Waokoaji.

 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (CP), Suleima Kova kuhusu jengo la ghorofa 16 lililoanguka majira ya saa mbili asubuhi katika makutano ya mtaa wa Indira Ghandi na Barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi. Katika ajali hiyo watu wawili wamekufa papo hapo. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Waokoaji wakiwa kazini.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum (CP), Suleima Kova.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum (CP), Suleima Kova akiwa katika eneo la tukio. Kulia ni Mbunge wa viti maalum (NCCR-Mageuzi James Mbatia.

CRDB CHINA DESK YAZINDULIWA



 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei (kushoto), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu na  Balozi wa China hapa nchini, Lü Youqing wakiwasili katika hoteli ya Serena.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi huo.
 Balozi wa China hapa nchini, Lü Youqing akitoa hotuba yake.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu akizungumza katika hafla hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa.


DAR ES SALAAM, Tanzania

MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei, amewataka wajasiriamali na wawekezaji wanaofanya biashara zao kati ya Tanzania na China, kuchangamkia fursa pana ya ukuzaji mitaji yao na pato kwa kutumia huduma mpya ya CRDB China Desk.

Dk Kimei aliyasema hayo jana wakati wa hafla ya uzinduzi wa China Desk, inayotolewa na CRDB, itakayo wahudumia wafanyabiashara, wajasiriamali na wawekezaji wanaofanyakazi zao baina ya mataifa hayo rafiki.
“China Desk, ni huduma yenye fursa inayoweza sio tu kusaidia kukuza mitaji na kutanua wigo wa maendeleo, bali kudumisha ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo baina ya China na Tanzania, ambao uliasisiwa karibia nusu karne iliyopita,” alisema Dk Kimei katika hafla hiyo.

Aidha, akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, aliiomba CRDB kuboresha utoaji wa mikopo ya riba nafuu kwa wajasiriamali wadogo na wa kati, ili kuharakisha ukuaji wa pato la Mtanzania na Taifa kwa ujumla.

Dk Nagu alibainisha kuwa, taasisi za kipesa nchini zina mchango mkubwa kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kukuza pato lao, kama zitakuwa tayari kuwapa mikopo yenye masharti nafuu na riba ndogo, ili kusaidia harakati zao za kujikwamua na kukuza uchumi wa taifa.

“CRDB mnastahili pongezi kwa huduma hii, inayokuja wakati ambao Tanzania kama Taifa, lilimpokea rais mpya wa China, Xi Jinping katika ziara ya kikazi. Taasisi nyingine za kifedha zitambue umuhimu wa ushirikiano baina ya mataifa haya na kubuni huduma kama hizi,” alisema Dk Nagu.

Aliongeza kwamba, kwa kuwa harakati za kumkomboa Mtanzania zimeshika kasi, huku China ikijitoa kadri iwezavyo kuisaidia Tanzania, kuna haja huduma kama hizo za China Desk zikaambatana na mikakati endelevu ya kimandeleo, na taasisi nyingine nazo zinastahili kuiga.

Kwa upande wake, Balozi wa China hapa nchini, Lü Youqing, aliipongeza CRDB kwa kufuata nyayo za waasisi wa China na Tanzania, kiasi cha kubuni na kuzindua China Desk – dawati litakalowanufaisha wajasiriamali na wafanyabiara wa kila upande.

“Huduma hii ni harakati chanya inayofuata nyayo za waasisi wa ushirikiano baina ya China, Rais Mao Tse Tung na Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere. Vizazi na vizazi vitabaki kujivunia na kila mmoja atajisikia yu nyumbani anapokuwa katika moja ya nchi hizo,” alisisitiza Youqing.

COSMAS KIBUGA KUZICHAPA NA SWEET KALUU JUMALIPILI HII




Bondia mwenye makeke mengi na asiyekubali kushindwa ulingoni na , Cosmas Kibuga, anatarajia kupanda ulingoni siku ya jumapili wiki hii katika ukumbi wa Texas Manzese, kuzipiga na bondia mkongwe, Sweet Kalulu, katika pambano la kirafiki la kusherehekea  Pasaka. 
Akilizungumzia pambano hilo muandaaji wa mchezo huo, Miraji Msusa, alisema “burudani yetu ni kuangalia ngumi na kushangilia na najua ngumi nzuri zipo katika hawa mabondia wasio na majina na wenye upinzani mkali ,nikaonelea lazima katika sikukuu hii ya pasaka tusiiache ipite hivihivi bila kupata starehe yetu,  kusubiri mpaka tarehe 7 april kwenye pambano kubwa la pale ccm mwinjuma-mwanayamala  ni mbali, Nikaafikiana na cosmas kibuga na sweet kalulu ambao ni wapinzani mitaani wamalizie kiu yao hiyo''. alisema

Wednesday, March 27, 2013

Ngumi Taifa kuanza Aprili mwishoni



Katibu Mkuu, BFT, Makore Mashaga
Na Mwandishi Wetu
MASHINDANO ya Taifa kwa mchezo wa ngumi za ridhaa yanatarajia kuanza mwishoni mwa mwezi ujao baada ya kufanyika kwa mashindano ya ngazi za chini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Mashaga Makore, alisema kuwa washindi watakaopatikana katika ngazi za chini ndiyo watakaoingia kwenye mashindano ya Taifa.
Amesema kuwa kwa sasa mashindano hayo yataanza katika ngazi ya Kata, Wilaya, Mkoa baada ya hapo washindi watashiriki mashindano ya Kanda ambapo Kanda nne zimetengwa kwa ajili ya mashindano hayo kabla ya Taifa.
“Mwaka huu tumefanya tofauti na miaka iliyopita ambapo sasa tumeanzia ngazi za chini ili kuwapata mwachezaji ambao wataliwakilisha taifa kwenye michuano mbalimbali.
“Kabla hatujaanza mashindano ya Taifa kutakuwepo na mashindano ya Kanda ambayo yatashirikisha mabondia au timu zilizofanya vizuri ngazi ya Kata, Wilaya na Mikoa, hao ndiyo watakuwa na sifa ya kushiriki ngazi ya Taifa,” almesema Makore.
Almesema katika Kalenda ya BFT ya mwaka huu, kuna mabadiriko mbalimbali ambayo yanamtaka kila mjumbe wa Kamati ya Utendaji kuwajibika kulingana na majukumu aliyopewa.
“Mwanzo shughuli zote zilikuwa zinafanywa na uongozi wa BFT wakati kuna kamati zake, lakini hivi kuna tofauti katika Kalenda ambapo kila mmoja anatakiwa kufanya kazi kwa mujibu wa maagizo ya kamati yake inavyomtaka afanye ili kukuza na kuendeleza mchezo huu,” amesema Makore.

MASHINDANO JUDO AFRIKA MASHARIKI HAKUSHIKIKI ZANZIBAR HATARI TZ BARA YAMALIZA KAZI



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgOUupg8u3JI8QzjuGJ1MtJzHo1FF3053LjlTugC9k2fzELfdUDZeEpZtAJi_AkryOVIZCRm8s8xTvF6UFAw3kOutJKlYlbi_CGfkPlKCkDW0HSD-HyQE2WiUKWayOu0IMcsPG5lXB6Ado/s1600/IMG_6536.JPG 
  Mchezaji wa Tanzania Bara Gofrey Edward akimuagusha chini na kumdhibiti mchezaji wa timu ya Burundi Halfan Mkurunziza katika mchezo wa Fainali ya Judo Afrika Mashariki mchezaji wa Tanzania ameshinda katika mchezo huo.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEigAgWTDqZFroYxnViZav5NsJbjhzlYu1g5-dz0L8J2kyga50_WOu-bJhAiTCcmlppu41MYJxGtDbtslIXgt7PY9wUHG3E0aDo6ll9MAR58QnCBeChJd40ky7BEIeyw43klBKsna5KoL1I/s1600/IMG_6545.JPG Moja kati ya waamuzi wa mchezo huo wakiwa kazi ya kuhesabu alama za washiriki wa michuano ya judo  ya afrika mashariki na kati inayofanyika Zanzibar .
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3IAHMVFWd1MKZ7vW2alogI_5B0nk6vzeYiAYwlJkXvMa9dKn6eQeKYcY6EgoXDTbwHScSynoqdZ0UaNyFhhd5BCzNYR5q3jBBW5HXKc0S09ekKOlZK1V_kmAv7kttDMWW4ei81vC7gKI/s1600/IMG_6541.JPG 
Mchezaji wa Judo wa Zanzibar Masoud Amour akijaribu kumuagusha mchezaji wa Kenya George katika mchezo wa fainal mchezaji wa Zanzibar alishinda  fainal hiyo.

DOUBLETREE BY HILTON YAKABIDHI TAA ZA KUTUMIA MIONZI YA JUA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MIKOCHENI A



Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mikocheni A jijini Dar es Salaam, Salehe Makwiro (kulia) akipokea sehemu ya msaada wa taa 200 za kutumia mionzi ya jua kwa ajili ya wananfunzi wa darasa la saba ambao watazitumia kwa ajili ya kujisomea. Kulia ni Mkurugenzi wa Mauzo wa Hoteli ya Doubletree by Hilton, Florenso Kirambata na Meneja Mkuu wa Doubletree by Hilton, Sven Lippinghof.
Meneja Mkuu wa Doubletree by Hilton, Sven Lippinghof akiwaelekeza wanafunzi wa Shule ya Msingi Mikocheni A jijini Dar es Salaam jinsi ya kutumia taa zinazotumia mionzi ya juu mara baada ya kukabidhi taa 200 kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la saba katika shule hiyo.
Mkurugenzi wa Mauzo wa Hoteli ya Doubletree by Hilton, Florenso Kirambata akiwafundisha jinsi ya kutumia taa zinazotumia mionzi ya jua wanafunzi wa Shule ya Msingi Mikocheni A jijini Dar es Salaam leo, wakati uongozi wa hoteli yhiyo ulipokabidhi msaada wa taa 200 kwa wanafunzi wa darasa la saba wa shule hiyo kwa ajili ya kuwasaidia wakati wa kusoma. (Picha na Habari Mseto Blog)

ADVANC BANK WAZINDUA TAWI JIPYA TEMEKE DAR





 Mwakilishi wa Mbunge wa Temeke, Thabit Mussa akikata utepe wakati wa uzinduzi wa jengo la benki ya Advanc, Temeke jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Peter Moelders na kulia ni Kaimu Meneja wa benki hiyo, Boniface Mhali na diwani wa Temeke, Hamisi Msombo. (Picha na Habari Mseto Blog)
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Advanc, Peter Moelders akisakata muziki wa asili na msanii wa kundi la Wanne Star, wakati wa uzinduzi wa benki hiyo, Temeke jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa kundi la  Wanne Star na kundi lake akitumbuiza wakati wa uzinduzi wa tawi la benki mpya ya Advanc, Temeke jijini Dar es Salam jana

DAR ES SALAAM, Tanzania 

BENKI ya Advanc imetakiwa kuonyesha tofauti yao na benki zingine kwa kutoa riba nafuu na masharti yanayowezekana kwa wakopaji ili kulisaidia Taifa kiuchumi kupitia wajasiriamali wadogo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tawi la benki hiyo wilayani Temeke jana, mwakilishi wa mbunge wa Temeke, Thabit Massa alisema ingawa kuna benki nyingi nchini lakini riba na masharti magumu yanafisha ari ya watu kukopa.

Mwakilishi huyo wa mbunge alisema kufunguliwa kwa tawi hilo kunafanya Temeke kuwa na matawi saba sasa ya benki lakini bado hakujawa na mafanikio tarajiwa na mbaya zaidi baadhi ya benki hizo hazina huduma nzuri kwa wateja.

“Lugha nzuri hakuna na hata mikopo imekuwa ikitolewa kwa kujuana baina ya wakopaji na watendaji wa baadhi ya benki jambo ambalo sio jema na linashusha imani ya wateja kwa benki” alisema na kuongeza kuwa anatarajia mabadiliko.

Alisema beni hiyo inatakiwa ije na mambo tofauti ili kuleta tija kwa wakazi wa eneo hilo tofauti na ilivyo sasa na awali Mtendaji mkuu wa benki hiyo, Moelders alisema wamekuja ulata mapinduzi makubwa katika uduma za kibenki nchini.

“Benki yetu walengwa wake na wananchi wa kawaida na wale waliopo vijijini na kabla ya mwisho wa mwaka huu itafungua matawi mawili Jijini Mwanza na mwakani watazindua matawi mengine ya idadi hiyo Jiji la Mbeya.
Alisema