Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, March 13, 2013

HEINEKEN YAZINDUA MICHUANO YA FOOSBALL KWA MASHABIKI WA LIGI YA MABINGWA YA ULAYA (UEFA CHAMPION’S LEAGUE) NCHINI TANZANIA. LEO



Mkurugenzi wa Michezo Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo, Leonard Thadeo kulia akichecheza mchezo wa foosball na Meneja masoko wa Heineken Tanzania, Coreline Kakwezi wakati wa uzinduzi wa michuano hiyo kwa ajili ya mashabiki wa ligi ya mabingwa ya Ulaya iliyozinduliwa Dar es salaam Picha na www.burudan.blogspot.com

Heineken ® yazindua michuano ya foosball yaki pekee ndani ya Afrika mashariki, ikilenga finali ya ligi ya mabingwa Ulaya (UEFA Champion League)ambayo itaonyeshwa tarehe 25 May.
Heineken® imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na ligi ya UEFA Champions na inaendelea kuwa mdhamini mkuu wa ligi hii.

Dar es Salaam, Tanzania Machi 13 2013: Bidhaa ya bia ya kimataifa Heineken® leo imetangaza uzinduzi wa michuano mipya ambayo itawashirikisha wateja nchini Tanzania, ikielekea kwenye harakati za mwisho wa msimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champion 2012/2013).

Heineken® inalenga kuonyesha jinsi Ligi ya Mabingwa wa Ulaya (UEFA Champions), ambayo ni moja ya mashindano maarufu duniani, na Heineken®, bidhaa ya bia yakimataifa, zikija pamoja kutengeneza kitu kizuri kwa mashabiki wao duniani. Katika michuano hiyo ya mchezo wa Foosball, wateja wakitanzania wanatakiwa kuwa makini katika kuhakikisha wanafikia hatua za mwisho katika mchezo huu.

Foosball, ni mchezo ambao kwa wengine unajulikana kama “mpira wa mezani”: ni mchezo unachezwa duniani kote ingawa mara nyingi zaidi ni kwenye baa na historia yake inaanzia mwaka 1923. Katika mchezo huu wapinzani wanasimama pande zote za meza na wanajaribu kufunga magoli. Wanajaribu kuipiga mipira, ambayo inaanzishwa kutoka ng’ambo nyingine wa meza. Ili uweze kuipiga mipira hii unatumia fimbo iliyotengeneza kwa aluminium iliyounganishwa sanamu za wachezaji wa mpira. Ili upige mpira unahitaji kuzungusha fimbo hiyo ambapo wale sanamu waliounganishwa kwenye hiyo fimbo wanaupiga mpira huo. Mshindi anapatikana kwa kufunga magoli mengi zaidi, kwa kawaida huwa magoli matano, kumi au kumi na moja.
Bia maarufu ya kimataifa ya Heineken® kwa mara ya kwanza itazindua michuano ya foosball ndani ya Afrika Mashariki. Katika michuano hii, Heineken® itawapa wateja wake uzoefu wa Ligi ya Mabingwa ya Ulaya (UEFA Champions). Michuano hii inalenga kuwapa changamoto wateja kuwaonyesha ujuzi katika mchezo huu wa foosball, ambayo inaweza ikachezwa pamoja na marafiki. Kwa mchezo huu wa foosball Heineken® itawapa ‘wanaume wa ulimwengu’ jukwaa yakushindana na kuwaonyesha ‘jinsi inavyochezwa’ hapa Tanzania. Michuano ya foosball ni ya kusisimua na itatengeneza tukio la kihistoria ambapo wale watakaofikia fainali watashindanishwa wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions) ikionyeshwa LIVE siku ya May tarehe 25, Dar es Salaam. Watakaoibuka mabingwa katika michuano hiyo watashinda safari ambayo gharama zote zimelipiwa kwenda Amsterdam, makao makuu ya Heineken®.
Kwa kuongezea kutakuwa na promosheni katika maeneo mbali mbali ya starehe ambayo zinamfurahisha yule mteja wa Heineken® na kuwapa mashabiki wa mpira nafasi yakushinda tiketi ya kwenda kwenye hafla ya kuangalia mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions) Dar es Salaam, tarehe 25 May.
Koen Morshuis, Mkurugenzi Mkuu wa HEINEKEN Afrika Mashariki alisema “Heineken inajitoa kuwapa wateja wetu waafrika mashariki tukio la kipekee kama ilivyokuwa katika ziara ya Kombe la Ligi ya Mabingwa ya Ulaya (UEFA Champions League) 2012. Mwaka huu michuano ya foosball inalenga kuwapa changamoto wateja wetu kuonyesha ujuzi na vipaji vyao. Tunalenga kutengeneza michuano yenye ubunifu ambayo itawapa nafasi kuionyesha vipaji na kupata washindi wa fainali. Washindi watapewa mataji bila kusahau safari ya kuelekea nyumbani kwa Heineken huko Amsterdam.”



NOTES TO EDITORS
About HEINEKEN
HEINEKEN is one of the world’s great brewers and is committed to growth and remaining independent. The brand that bears the founder’s family name - Heineken - is available in almost every country on the globe and is the world’s most valuable international premium beer brand.
The Company’s aim is to be a leading brewer in each of the markets in which it operates and to have the world’s most valuable brand portfolio. The Company is present in over 70 countries and operates 140 breweries with volume of 205 million hectolitres of beer sold on a pro-forma basis. HEINEKEN is Europe’s largest brewer and the world’s third largest by volume.

Heineken®- UEFA Champions league sponsorship
UEFA created the UEFA Champions League back in 1992 from what was previously known as the European Champions Clubs Cup which dates back to 1955. Twenty years later, with a global unique live audience of 1.1 billion, 500 million live viewers in Europe alone, 95,000 hours of total coverage, 20,000 hours of live coverage, and distribution in 200 countries and territories around the world, the UEFA Champions League has become a truly global phenomenon.  A natural fit with the Heineken brand, which is the world's most international premium beer, UEFA Champions League is also available in virtually every country in the world.
In  May  2011,  HEINEKEN  announced  it  was  extending  its  sponsorship  of  the UEFA  Champions League for a further three years.

For all press enquires kindly contact:

Koen Morshuis,
General Manager,
HEINEKEN East Africa
E-mail: koen.morshuis@heineken.com

No comments :

Post a Comment