Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, March 26, 2013

SEMINA YA VIONGOZI WA MICHEZO YA COPA COCA COLA YAFUNGULIWA RASMI




Tanzania Football Federation (TFF) President Leodegar Tenga emphases a point as he addresses over 60 delegates from across Tanzania at the opening ceremony of the Copa Coca-Cola Directive Seminar held at the National Stadium in Dar es Salaam Tuesday, March 26, 2013

Coca-Cola Brand Manager Tanzania Maurice Njowoka delivers his speech at the opening ceremony of the Copa Coca-Cola Directive Seminar held at the National Stadium in Dar es Salaam Tuesday, March 26, 2013.

 Washiriki wa semina wakimsikiliza mgeni rasmi Rais wa Tff Tenga akiwaasa kuhusiana na kuwatumia wachezaji waliozindi umri kwani wachezaji wanatakiwa chini ya miaka kumi na tano

Washiriki wa semina kutoka TANZANIA BARA na VISIWANI wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa TFF akiwemo Rais wa Tff pamoja na viongozi wa serikalini semina hiyo imefanyika katika ukumbi uliopo katika uwanja wa Taifa Jijini DSM


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewataka viongozi wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kuhakikisha wanaingiza wachezaji wenye umri sahihi katika michuano ya U15 FIFA Copa Coca-Cola 2013.

Ametoa mwito huo leo (Machi 26 mwaka huu) wakati akifungua semina elekezi ya michuano ya Copa Coca-Cola ambayo kuanzia mwaka huu itakuwa ikishirikisha watoto wenye umri chini ya miaka 15.

Rais Tenga amesema hakuna jambo la kipuuzi kama kuchomekea wachezaji ambao wamezidi umri unaotakiwa kwa vile lengo la michuano ya aina hiyo ni kubaini vipaji na kuwafanya watoto wapende kucheza mpira wa miguu.

“Kwanza nawashukuru kwa kutenga muda wenu na kuhudhuria semina. Lakini ni vizuri pia mkahakikisha mnakuwepo kwenye mashindano ili kutekeleza haya ambayo tutakubaliana katika semina hii. Mkileta mtu mwingine anaweza kutuanzishia mambo mengine badala ya yale tutakayokubaliana,” amesema Tenga.

Pia ameishukuru kampuni ya Coca-Cola ambaye imekuwa ikidhamini michuano hiyo tangu mwaka 2007 ambapo semina hiyo elekezi inayoshirikisha makatibu wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa na waratibu wa mikoa wa michezo ya UMISSETA ni ya saba mfululizo.

Ratiba ya michuano hiyo kuanzia mwaka huu imebadilika ambapo sasa itaanzia ngazi ya wilaya Aprili wakati fainali katika ngazi ya Taifa itachezwa Septemba

No comments :

Post a Comment