Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, March 11, 2013

PPF YAONESHA NJIA YA KUSAIDIA KIKUNDI CHA Habari Group


Na Mwanishi Wetu

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki amewataka waandishi wa Habari wa Kike kutumia kalamu zao katika kuandika mambo yanayohamasisha amani na utulivu nchini.

Pia aliwataka kutumia kalamu zao katika kuandika na kuibua vitendo vya unyanyasaji na vya kikatili wanavyofanyiwa wanawake nchini.

Hayo aliyasema hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Lamada , wakati wa uzinduzi wa kikundi cha Habari Group kinachojumuisha waandishi mbalimbali wa habari hapa nchini.

Alisema ni vyema wakatumia fursa zao katika kufichua viashiria mbalimbali vya fujo kwa kuwa endapo itatokea uvunjifu wa amani wanaoathirika zaidi ni wanawake na watoto.

Kikundi cha habari kinajihusisha na ununuaji wa hisa, kukopeshana na kufanya miradi mbalimbali ya kikundi na mmoja mmoja hivyo aliwataka wanakikundi kujibidiisha zaidi na kuongeza wanachama wake.

“Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ni moja ya maadhimio 12 ya ulingo wa Belgin hivyo mnachofanya hapa ni katika kujikwamua wenyewe kiuchumi na kama mnavyofahamu wanawake wanamajukumu mengi katika familia na pia kutingwa na mambo mengi katika tasnia yenu lakini mmethubutu kufanya hivyo hivyo endeleeni,”alisema Kagasheki

Pia alitoa wito kwa wanawake kuhakikisha kuwa majukumu waliyonayo yasiwe kikwazo kwao kushiriki katika kukuza uchumi.

Alisema kinachotakiwa ni kuondoa fikra kuwa haiwezekani na kuhakikisha wanapiga vita mambo yanayomgandamiza mwanamke kwa kuondoa fikra kwamba haiwezekani kujikwamua kiuchumi.

Naye mlezi wa kikundi hiko ambaye pia ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angella Kairuki alisema atakuwa bega kwa bega na wanakikundi hiko katika kuhakikisha kuwa kinasonga mbele.

“Nimefurahishwa sana na wazo la wanahabari hawa na nina ahidi nitakuwa nao bega kwa bega katika kuhakikisha kuwa kikundi kinakua zaidi na kuwatafutia fursa mbalimbali za kukiendeleza pia,”alisema Kairuki.

Naye Meneja Uhusiano wa PPF Lulu Mengele alisema wamekuwa katika mstari wa mbele katika kutoa mikopo kwenye  saccos nchini kwa wanachama wao sehemu za kazi.

Alisema tayari wametoa mikopo kwa wanachama wake kwenye maeneo ya kazi  41 yenye thamani sh bil 48.7 lengo likiwa ni kumsaidia mwanachama akiwa kwenye ajira.

Aliendelea kueleza  kuwa PPF inachukua jukumu la kusomesha watoto wa wanachama ambao wazazi wao wamefariki kuanzia chekechea hadi kidato cha nne ambapo kwa sasa tayari wanasomesha 1333 katika shule mbalimbali.

Alisema PPF inatoa mafao saba ambapo aliyataja kuwa ni pamoja na uzee,ugonjwa,kiinua mgongo,kifo ,elimu,kujitoa, sambamba na kuandikisha wanachama kutoka kwenye sekta mbalimbali na kupata taarifa zaidi kupitia simu ya mkononi.

Naye mratibu wa kikundi cha habari group Rabia Bakari akisoma risala mbele ya mgeni rasmi alisema kikundi kinahitaji zaidi ya milioni 10 ili kila mmoja
aweze kupata mkopo kwa wakati bila kupeana kwa zamu ili kuharakisha shughuli za maendeleo.

”Kwa sasa katika akaunti yetu tumefanikiwa kuwa na milioni mbili na nusu tu, hivyo tunahitaji zaidi ya milioni 23 ili kufanikisha malengo tuliyojiwekea,”alisema Rabia.


Mara baada ya mgeni rasmi kuzindua kikundi kulifanyika harambee ambapo zilichangwa zaidi ya sh mil 6 ambapo mgeni rasmi alitoa mil 2 na mama mlezi wa kikundi alitoa 1.5 mbunge wa Busega Dk.Titus Kamani alitoa laki 2, Jumuia ya kukuza uchumi Ilala laki sita ,TAMADA laki 2 pamoja na wadau wengine

No comments :

Post a Comment