Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, March 20, 2013

Samsung yazindua Galaxy Camera



 Mpiga Picha Mkuu wa Kampuni ya Free Media inayochapisha magazeti ya Sayari na Tanzania daima, Joseph Senga (kushoto) akiangalia aina mpya ya Samsung Galaxy Camera wakati wa uzinduzi wa camera hiyo jijini Dar es Salaam. 
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Samsung Tanzania, juzi usiku imezindua rasmi bidhaa mpya ya Samsung Galaxy Camera, ambapo kwa kushirikiana na Kampuni ya Simu ya Vodacom wameweka kifurushi cha 1GB kwa muda wa miezi mitatu.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam juzi, Meneja Mkuu wa Samsung Tanzania, Kishor Kumar, alisema kuwa, Samsung Galaxy Camera ni zaidi ya simu yenye kamera kiutendaji na ubora wa huduma zake.
Aliongeza kuwa, Samsung Galaxy Camera, ina CMO sensor, ambayo inawezesha kamera hiyo kuchukua picha zenye ubora wa hali ya juu.
Katika uzinduzi huo wa Galaxy Camera, ambayo ni ya kisasa zaidi, Minhai Patel aliibuka na zawadi ya aina hiyo mpya ya kamera katika droo ndogo iliyoshirikisha waalikwa waliohudhuria uzinduzi.
Kwa upande wake, Meneja Usambazaji na Mauzo wa Samsung Mobile, Sylvester Manyara, alisema kuwa, Galaxy Camera ina tofauti na kamera nyingine, kwa sababu yenyewe inatumia mtandao wa 3G, unaoiwezesha kupata huduma ya Internet ya kasi.
Aliongeza kuwa, Galaxy Camera ina uwezo wa kutuma picha hadi katika mitandao ya kijamii ya Facebook, Twitter, Whatsapp na Instagram na kwamba kamera hizo zinatoa picha za ubora zaidi hata zilizopigwa kutoka umbali mrefu.

No comments :

Post a Comment