Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, March 20, 2013

Z. ANTO KUTOA KAZI MPYA SIKU YA PASAKA




Na Elizabeth John

BAADA ya kuwa kimya kwa muda mrefu, mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ally Mohamed ‘Z. Anto’ usiku wa Pasaka anatarajia kutambulisha kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Tanzania’.
Akizungumza Dar es Salaam, Z.Anto alisema kazi hiyo ataitambulisha katika ukumbi wa Mnyaru nite club uliopo jijini Arusha.
“Nashukuru mungu kwa kupata shoo hii ambayo itanipa nafasi ya kuitambulisha ngoma yangu mpya, tukiwa na kundi zima la Solid Ground Famili kutoka Mabimbo jijini Dar es Salaam,” anasema.
Z.Anto anawaomba wakazi wa Arusha wajitokeze kwa wingi siku hiyo ili waweze kupata burudani iliyoenda shule kutoka kwake na kundi hilo ambalo lililiteka soko la muziki huo kipindi cha nyuma.
Mkali huyo alishawahi kutamba na kibao chake cha ‘Kisiwa cha Malavidavi’ licha ya kuwa na vibao vingi ambavyo vilivyofanya vizuri katika soko la muziki huo.

No comments :

Post a Comment