Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 29, 2013

UCHAGUZI MIKUU BFT KUFANYIKA JIJINI MWANZA



Viongozi wa sasa BFT, Rasi Joan Minja (kulia) na Katibu Mkuu, Mashaga makore

UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Mchezo wa Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) unatarajiwa kufanyika Mei mwaka huu jijini Mwanza.
Katibu Mkuu wa BFT, Mashaga Makore, aliiambia MICHARAZO asubuhi ya leo kuwa, kuwa uchaguzi huo utafanyika mara baada ya kumalizika kwa michuano ya kimataifa ya Majiji yanayotarajiwa kufanyika jijini humo kati ya Mei 20-25.
Makore alisema mchakato wa kuelekea kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho kitatanguliwa na Mkutano Mkuu wa shirikishi hilo utatangazwa mara baada ya shamrashamra za sikukuu ya Pasaka.
"Uchaguzi Mkuu wa BFT utafanyika mwezi Mei jijini Mwanza mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya kimataifa ya ngumi inayoshiriki miji mikuu ya Afrika Mashariki na Kati, ambapo utatanguliwa na Mkutano Mkuu," alisema Makore.
Makore alisema maamuzi hayo yalifikiwa na Kamati yao ya Utendaji iliyokaa hivi karibuni na kutoa wito kwa wadau wa mchezo huo wenye uwezo na sifa za kuongoza shirikisho hilo kujiandaa kuijitosa kuwania uongozi kwenye uchaguzi huo.

No comments :

Post a Comment