Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, March 25, 2013

KITABU CHA KIFO NI HAKI YANGU CHAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR




 
Mtunzi mashuhuri wa vitabu kutoka kampuni ya Mkuki na Nyota, Mzee Walter Bgoya, akikata utepe pamoja na mtunzi wa kitabu cha ‘Kifo ni Haki Yangu’, Eric James Shigongo (kulia) wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika katika duka la vitabu la Tanzania Publishing House lililopo mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam leo.
 
Mtunzi wa kitabu cha ‘Kifo ni Haki Yangu’, Eric James Shigongo, akiongea na wadau (hawapo pichani) waliofika katika uzinduzi wa kitabu chake katika duka la vitabu la Tanzania Publishing House lililopo mtaa wa Samora jijini Dar.
Mtunzi Eric Shigongo akimpatia kitabu mtunzi mwenziye, mzee Walter Bgoya.
Mzee Walter Bgoya akiongea na wanahabari wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Eric Shigongo cha ‘Kifo ni Haki Yangu’.
Afisa wa polisi Patrick Massawe ambaye pia ni mtunzi mashuhuri wa hadithi za magazeti nchini, akisainiwa kitabu na Shigongo wakati wa uzinduzi.
Eric Shigongo (kushoto), akibadilishana mawazo na msomaji wa hadithi zake, Ahmed El Maamry, wakati akimsainia kitabu.
Eric Shigongo akimsainia kitabu mwanaye, Samwel Shigongo.
Eric Shigongo akisaini kitabu kwa ajili ya mwandishi wa Nipashe, Somoe Ng’itu.
 
Shigongo akiwasainia vitabu baadhi ya wasomaji waliohudhuria uzinduzi huo.
Waratibu wa uzinduzi wa kitabu cha ‘Kifo ni Haki Yangu’, Abdallah Mrisho (kulia) na Angela Msangi wakisubiri uzinduzi.
Afisa wa polisi Patrick Massawe na msomaji mwingine wakipitia baadhi ya kurasa za kitabu cha Eric Shigongo aliyesimama kulia.
Baadhi ya wasomaji waliohudhuria uzinduzi huo.
 
Shigongo akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa duka la TPH.
MTUNZI mahiri wa vitabu nchini, Eric James Shigongo, leo amezindua rasmi kitabu chake cha ‘KIFO NI HAKI YANGU’ katika duka la vitabu la Tanzania Publishing House (TPH) lililopo mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam. Katika uzinduzi huo, wasomaji 50 wa mwanzo walipata fursa ya kupata zawadi ya kitabu hicho bure kilichosainiwa na mtunzi. Kujipatia nakala ya kitabu hicho na vinginevyo, wasiliana au fika katika vituo tajwa hapo chini:
 
(PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY / GPL)

No comments :

Post a Comment