Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, April 3, 2011

MO DEWJ ATANGAZA DAU LA MILIONI 50 SIMBA IKISHINDA





Asema Simba ina historia Afrika


Aitambia TP Mazembe



MBUNGE wa Singida Mjini Mohamed Dewji (MO), ametamba kuwa ni lazima Simba, itoke na ushindi mnono dhidi ya mabingwa wa Afrika, TP Mazembe ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC).


Pia, ametangaza dau la sh. milioni 50 kwa Simba iwapo itafanikiwa kuibuka na ushindi mnono, utakaoivua ubingwa TP Mazembe na yenyewe kusonga mbele.


Miamba hiyo inatarajiwa kuminyana (kesho) kwenye mchezo mkali wa kuwania kusonga mbele, ambapo katika mchezo wa kwanza Simba ililala kwa mabao 3-1, mjini Lubumbashi .


Dewji, ambaye alipata kuwa mfadhili wa Simba kwa miaka kadhaa, aliwatambia viongozi na wana habari waliotua na msafara wa TP Mazembe, akiwaeleza watarajie kipigo cha mbwa mwizi.


Alikuwa akizungumza na msafara huo katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski, mjini Dar es Salaam , jana usiku ikiwa ni muda mfupi baada ya kutua nchini.


Alisema Simba ni timu kubwa na ina historia nzuri katika michuano ya klabu bingwa Afrika hivyo, wana kila sababu ya kutoka na ushindi katika mchezo huo na kuiondosha TP Mazembe kwenye mashindano.


“Jiandaeni kwa kipigo kesho, tuna historia nzuri na michuano hii hivyo mstarajie kutoka salama, wapo wenzenu waliumia kama itakavyokuwa kwenu” alisema Dewji, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kusaidia Taifa Stars ishinde.


Dewji aliwapasha wageni hao kuwa watarajie kupata kile kilichowapata Zamalek ya Misri, waliondoshwa na Simba kwenye hatua ya awali ya michuano hiyo.


Zamalek ndiyo walikuwa mabingwa watetezi kama ilivyo kwa TP Mazembe kwa sasa, na kipigo hicho kiliwavua ubingwa huo baada ya kuaga mashindano.


Dewji aliongeza kuwa katika mchezo wa (kesho) leo Simba ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri hasa ikizingatiwa kuwa inacheza nyumbani na mashabiki watakuwa wakiipa nguvu uwanjani.

No comments :

Post a Comment