Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, May 15, 2010

SENYONJO ATUA AZAM FC


AZAM FC ya Dar es Salaam imefanikiwa kumsajiri nyota wa kimataifa wa Uganda ambaye ni mshambuliaji hatari wa timu ya ya Polisi ya Uganda, Peter Senyonjo ambaye alikuwa akihusishwa na Yanga kwa misimu miwili mfululizo iliyopita.
Senyonjo ambaye anatisha kwa kuzifumania nyavu za timu pinzani anatarajiwa kutengeneza partnership ya hatari na John Raphael Boko Adebagoals amabye kama siyo kukosa baadhi ya mechi kutokana na kuwa Israel kwa majaribio basi angekuwa mfungaji bora msimu huu.

kwa mujibu wa gazeti la mwanaspoti, Yanga walikuwa wamepania kumsajili mchezaji huyo msimu wa 2007 na 2008 lakini wakashindwa kutokana na kutokuwa makini kwenye ufuatiliaji lakini wikiendi iliyopita timu ya Azam imemshusha Dar es Salaam na kumsainisha mkataba wa mwaka mmoja.

Mchezaji huyo mzoefu na tegemeo kwenye timu ya Taifa ya Uganda, alikuwa jijini Dar es Salaam wikiendi iliyopita kukamilisha uhamisho wake na ameshakwea pipa kurejea Kampala.

Meneja wa Azam, Ibrahim Jeshi amesema kuwa kila kitu kimekwenda vizuri na mchezaji huyo amerejea kwao kukamilisha mambo mengine.

Senyonjo amejijengea umahiri mkubwa akiwa na timu hiyo ya Police kwenye michuano ya kombe la kagame na timu ya Taifa katika chalenji.
Wakati huo huo, beki mahiri wa timu ya Taifa Stars Nadir Haroub Canavaro yupo katika hatua za mwisho za kujiunga za Azam FC, Canavaro mwenyewe ameshatamka wazi kuwa dhamira yake ni kuichezea Azam FC msimu ujao

No comments :

Post a Comment