Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 5, 2014

ASHATI YAIKOMALIA MBEYA CITY NA KUTOKA YAYO DROO YA BILA BILA



Ashanti United ambaoleo imetoa droo ya bila bila na Mbeya City
 MATOKEO ya 0-0 waliyoyapata Mbeya City leo hii kwenye mchezo mgumu wa ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Ashanti United katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam yamewagharimu na kuwakosha rasmi ubingwa msimu huu.
Ashanti United waliokuwa na lengo la kupata ushindi leo hii mbele ya Mbeya City wameambulia pointi moja muhimu kuliko kupoteza mchezo huo.
City wamefikisha pointi 46 katika nafasi ya tatu sawa na Yanga waliopo nafasi ya pili kwa pointi 46, lakini kikosi cha Pluijm kina wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Hii ilikuwa mechi ya 24 kwa Mbeya City, hivyo wamebakiza mechi mbili nyumbani  dhidi ya Azam fc na Mgambo JKT.
Kama watashinda mechi zote watafikisha pointi 52 ambazo tayari Azam wameshafikisha kileleni.
Kwa maana hiyo, Mbeya City rasmi wamejitoa kuwania ubingwa na kuwaacha wanaume wawili, Yanga sc na Azam fc kuendelea na vita hiyo.
Kilichobaki kwao ni kuisaka nafasi ya pili, kwani wanaweza kuipata kutegemeana na matokeo watakayopata Yanga SC.
Yanga wamebakiza mechi nne kuanzia ya kesho dhidi ya JKT Ruvu ndani ya dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Kama Mbeya City wanataka  kuchukua nafasi ya pili wanatakiwa kuwaombea Yanga mabaya ili wapoteze mchezo mmoja, washinde mmoja na kutoa sare miwili.
Kama matokeo hayo yatatokea, maana yake Yanga atavuna pointi tano pekee na ukijumlisha na pointi 46 walizonazo sasa watafikisha pointi 5I ambazo Mbeya City atazivuka endapo atashinda mechi zote.
Yanga ataanza kazi kesho dhidi ya JKT Ruvu, baada ya hapo atavaana na Kagera Sugar mechi ya kiporo aprili 9, na hatimaye atasafiri kwenda Arusha aprili 13 kuwavaa JKT Oljoro na kurejea Dar es salaam kufunga msimu dhidi ya Simba uwanja wa Taifa aprili 19 mwaka huu.
Kwa mechi alizosaliwa nazo Yanga si rahisi kutabiri matokeo, lolote linaweza kutokeo, lakini kwa Mbeya City biashara imewakata kwasababu mambo ya kusubiri mwenzako apoteze inaweza kutokea au isitokee.
Hata hivo mtandao huu umezungumza na kocha msaidizi wa Mbeya City, Maka Mwalwisyi ambaye amekiri wazi kuwa mchezo wa leo ulikuwa mgumu sana kwa upande wao.
‘Tunamshukuru Mungu mechi imeisha salama na tumeambulia suluhu. Ni matokeo mabaya kwetu, lakini huwezi jua waliopo juu yetu watapata matokeo ya aina gani huko mbeleni. Kimsingi yametuharibia sana, lakini hatukati tamaa kupambana mpaka dakika ya mwisho”.
“Hata kama itakuwa tofauti na malengo yetu sio mbaya. Huu ni msimu wetu wa kwanza. Tumejitahidi kadri ya uwezo wetu na haya ndio mavuno yetu. Tunarudi kujiandaa na mchezo ujao dhidi ya Azam fc”. Alisema Kocha Maka.
Kocha wa Ashanti United, Abdallah Kibadeni aliwahofia Mbeya City kwasababu ya ubora wao, lakini amemaliza mechi kwa kupata pointi moja muhimu.
Kwa matokeo hayo, Ashanti wanafikisha pointi 22 katika nafasi ya 12 baada ya kushuka dimbani mara 24.
Mchezo ujao watashuka dimbani kukabiliana na Simba uwanja wa Taifa na watahitimisha kibarua chao msimu huu dhidi ya Tanzania Prisons uwanja wa sokoine jijini Mbeya.
Kama Ashanti United watashinda michezo hiyo mitatu watafikisha pointi 31 na pengine kujiweka mazingira mazuri ya kubakia ligi kuu.
Wakati huo huo Mgambo JKT wapo nafasi ya 11kwa pointi 22 kama Ashanti, na wamebakiwa na michezo mitatu.
Kama Mgambo watashinda mechi zijazo dhidi ya Coastal Union, Kagera Sugar na Mbeya City watafikisha pointi 31 kama Ashanti, na hapo timu moja italazimika kushuka kwa kuangalia tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Rhino wapo mkiani kwa pointi 13 na wamebakiza mechi tatu. Kama watashinda zote watafikisha pointi 22 ambazo zimefikiwa na Ashanti, Tanzania Prisons na Mgambo, huku timu hizi zikiwa na mechi tatu mkononi.
Oljoro JKT wapo nafasi ya 13 kwa pointi 15 na wakishinda mechi zao tatu zilizosalia watafikisha pointi 24 ambazo zinaweza kupitwa na Ashanti United, Prisons na Mgambo JKT.
Hivyo kwa mazingira haya, Rhino Rangers na JKT Oljoro zina asilimia kubwa ya kushuka daraja, huku Ashanti, Mgambo na Prisons zikipambana kwa nguvu kukwepa kuungana na timu hizi mbili za mwisho.
Mchezo mwingine umepigwa katika dimba la Kaitaba ambapo wenyeji wa uwanja huo wamewakaribisha wekundu wa Msimbazi Simba sc.
Mechi hiyo imemalizika kwa sare ya bao 1-1.
Simba walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 45 kipindi cha kwanza  kupitia kwa Zahor Idd Pazzi akipokea krosi kutoka kwa nahodha wao, Nassor Masoud Cholo.
Kagera walisawazisha  bao hilo dakika ya 51 kipindi cha pili kupitia kwa mshambuliaji wao hatari, Them Felix `Mnyama`.
Kwa matokeo hayo, Simba sc wamefikisha pointi 37 katika nafasi ya 4 baada ya kushuka dimbani mara 24.
Kagera Sugar wamefikisha pointi 34 katika nafasi ya 5 baada ya kushuka dimbani mara 23.
Mechi ya Kaitaba haikuwa na ushindani mkubwa kwani timu zote hazikuwa na cha kupoteza, kwa maana ya kutotafuta ubingwa wala nafasi ya pili.
Timu zote zilikuwa zinashambuliana kwa zamu, lakini Kagera Sugar walipata nafasi nyingi zaidi ya Simba.
Hata hivyo ubutu wa safu za ushambuliaji kwa timu zote ,kumeamuru matokeo yawe 1-1 mpaka dakika 90 zinamalizika.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi kadhaa kupigwa katika miji tafouti.
Jijini Dar es salaam, Yanga watakabiliana na JKT Ruvu na ushindi ni muhimu kwa timu zote.
JKT Oljoro watawakaribisha maafande wa Tanzania Prisons katika dimba la Shk. Amri Amri Abeid Kaluta jijini Dar es salaam.
Rhino Rangers watakuwa dimba la Ali Hassan Mwinyi kuumana na Mtibwa Sugar kutoka Morogoro.
Nao wagosi wa Kaya watawakaribisha ndugu zao, Mgambo JKT katika dimba la CCM Mkwakwani, Jijini Tanga.

No comments :

Post a Comment