Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, April 24, 2014

Mashauzi, Sikinde kuwasindikiza Talent Band



http://4.bp.blogspot.com/-O6fGijIG-Xg/TpazwGlqCXI/AAAAAAAAAIQ/RB1Z12Ke5k8/s320/Hussin+Jumbe
Hussein Jumbe 'Mtumishi'

http://api.ning.com/files/QB639EYNFoD4efIjz*tu6A-tokrUhXrM*zilTmqFjwPaPBf8MRFVKag*kDP98VUlJn2dEoatnVAzlwDEnsygi3UIFRYdWmh1/MITIKISIKOYAPWANIDARLIVE16.JPG?width=650
Ishi Mashauzi atakayemsindikiza Hussein Jumbe na Talent Band
KUNDI maarufu la muziki asilia la Ngoma Afrika na kundi la muziki wa taarab la Mashauzi Classic, yanatarajiwa kupamba uzinduzi wa albamu mpya ya Talent Band utakaofanyika wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO, Mkurugenzi wa Talent Band, Hussein Jumbe alisema kuwa uzinduzi huo utafanyika Aprili 30 kwenye ukumbi maarufu Kisuma Night Park lililopo eneo la Temeke Mwembeyanga na watasindikizwa na makundi hayo mawili.
Jumbe alisema pia bendi yake ya zamani ya Mlimani Park 'Wana Sikinde' watakuwepo ukumbini kumpiga tafu kwenye uzinduzi huo wa aina yake.
"Natarajia kufanya uzinduzi wa albamu ya bendi yetu ya Talent iitwayo 'Kiapo Mara Tatu' na makundi ya Mlimani Park, Mashauzi Classic na Ngoma Afrika watanisindikiza siku hiyo pale Mwembeyanga," alisema.
Jumbe alisema kuwa, maandalizi ya uzinduzi huo unaendelea vyema na kuwataka mashabiki wa muziki wa dansi kujitokeza kupata burudani ambayo wameikosa kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam.

No comments :

Post a Comment