Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, September 21, 2011

Mchezaji bora zaidi wa Uingereza katika mchezo wa tennis na nambari 4 duniani Andy Murray asema kuna uwezekano wa wachezaji wa kulipwa kufanya mgomo i

Andy Murray

Asema kuna uwezekano wa wachezaji tennis kufanya mgomo juu ya malalamiko ya ratiba

Andy Murray amesema wachezaji bora zaidi wa tennis ya kulipwa wangelipenda kuona mabadiliko katika ratiba ya mapambano yao, na kuna uwezekano wa kuyagomea mashindano ikiwa maslahi yao hayatatiliwa maanani.

Amesema wachezaji wengi wamekuwa wakiudhika mno kutokana na ratiba iliyosongamana, na watakutana mjini Shanghai mwezi ujao kujua hatua watakazoweza kuzingatia.

Murray ameielezea BBC kwamba kuna uwezekano wa mgomo kufanyika.

"Kuna uwezekano. Nafahamu hilo, kwani baada ya kuzungumza na baadhi ya wachezaji, wao hawana wasiwasi wa kufanya hivyo [kugoma].

"Tutumaini kwamba hatutafikia hatua hiyo, lakini nina hakika wachezaji wataifikiria."

Alipoulizwa ikiwa suala hilo la mgomo litajadiliwa nchini Uchina, alijibu: "Ndio, nafikiria hivyo".

No comments :

Post a Comment