Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, September 21, 2011

Wenger ataka "miaka mingine" 14 Arsenal

Arsene Wenger amesema wala hasumbuliwi na kelele zinazopigwa dhidi yake na anataka kuendelea kuingoza Arsenal kwa kipindi kirefu zaidi.

Arsene Wenger

Arsene Wenger

Wachambuzi wa soka wamekuwa wakihoji nafasi ya Wenger wakati huu Arsenal ikishikilia nafasi ya 17 ya msimamo wa Ligi Kuu ya England wakiwa wameuza wachezaji muhimu msimu huu.

Lakini baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Shrewsbury kuwania Kombe la Carling, Wenger amesema: "Sijali kabisa kutokana na uvumi uliopo dhid yangu kwamba nitatimuliwa.

"Nimekuwa katika klabu hii kwa miaka 14 na nimefanikiwa kuiweka katika kuwania ubingwa wa Ulaya kwa miaka hiyo 14. Natumai nitaendelea kuwepo miaka mingine 14."

Mtendaji mkuu wa Arsenal Ivan Gazidis ameiambia BBC kwamba kumfukuza Wenger sio jambo wamalofikiria kulitekeleza.

Zaidi anachokiangazia zaidi Wenger ni kuimarisha kikosi chake baada ya nahodha wake Cesc Fabregas kuhamia Barcelona na kiungo mwenzake Samir Nasri kujiunga na Manchester City mwezi wa Aprili.

Katika siku ya mwisho ya usajili, kiungo wa Everton Mikel Arteta, mshambuliaji Park Chu Young, beki wa kushoto Andre Santos na mlinzi wa kati Per Mertesacker walijiunga na Arsenal, wakati Wenger pia alimchukua kwa mkopo Yossi Benayoun kutoka klabu ya Chelsea.

Lakini mabadiliko hayo yamekuwa makubwa kuyazoea uwanjani, wakati Arsenal imeshinda mechi moja tu ya Ligi kati ya mechi tano huku ikiwa imefungwa mabao mengi hadi sasa.

Wenger amesema:"Naelewa watu hawana furaha na wanalaumu, lakini najua mnafahamu kama ninavyofahamu kwamba watu wanakuwa wepesi sana kufikia hatua ya kulaumu".

"Tunapofanya vizuri tunashangiliwa na kupongezwa, kwa hiyo tunawajibika kukubali lawama iwapo mambo yanapokwenda kombo - lakini kwa pande zote mbili pia tunatakiwa kuwa na subira.

No comments :

Post a Comment