Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, December 8, 2014

DANNY MRWANDA ASAINI YANGA AWAMWAGA SIMBA USIKU HUU


HABARI zilizotufikia usiku huu, zinasema kuwa Mshambuliaji wa timu ya Polisi Moro, Danny Mrwanda, amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia Klabu ya Yanga ya jijini Dar es salaam, usiku huu.

Imekuwa ni tofauti na mategemeo ya mashabiki walio wengi wa soka kutokana na habari zilizozagaa kuanzia juzi kuwa mchezaji huyo 'eti' alikuwa tayari ameshakamilisha taratibu zote za kujiunga na Klabu ya Simba, ambao walimtaka na kufanya naye mazungumzo.

Kama ambavyo imekuwa kwa timu hizi watani wa jadi kufanyiana 'Kitu Umafia', mara kadhaa kwa kuchukuliana wachezaji na kupandiana dau kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachezaji akiwamo, Mbuyu Twite, na wengineo na ndivyo Yanga walivyofanya tena kwa Mrwanda usiku huu.

Ikumbukwe kuwa Simba, walikuwa wameshatangaza dau la kumsajili mchezaji huyo katika kipindi hichi cha dirisha dogo na tayari taratibu zilikuwa zimekwishaanza.

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Klabu ya Yanga kinasema kuwa,Yanga imeamua kumsajili Mrwanda ili kuchukua nafasi ya Said Bahanuzi aliyetolewa kwa mkopo kwenda Polisi Morogoro wakati Jerry Tegete akiwa ni majeruhi, na mshambuliaji pekee wa ndani aliyebaki tegemeo akiwa ni Hussein Javu.

No comments :

Post a Comment