Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, December 8, 2014

PAMBANO LA MAOKOLA NA MKALAKALA





CHAMA cha Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC),
limeidhinisha pambano la ubingwa wa taifa uzani
wa kilo 69 litakalowakutanisha Ibrahim Maokola
dhidi ya Selemani Mkalakala.
Kwa mujibu wa Rais wa TPBC, Chaurembo Palasa,
pambano hilo limepangwa kufanyika Desemba 19,
mwaka huu kwenye Ukumbi wa Vigae Pub,
Mbagala jijini Dar es Salaam.
Palasa alisema pambano hilo litasindikizwa na
mapambano mengine ya utangulizi kati ya Abdallah
Mohamed dhidi ya Salehe Mkalekwa.
Alisema maandalizi kuelekea kwenye pambano hilo
ni mazuri na kwamba wanategemea mashabiki
wengi watajitokeza kuwaunga mkono vijana hao.
“Tumekuwa tukihamasisha mchezo wa ngumi
sehemu mbalimbali ili kuleta mvuto kwa wakazi wa
jiji na sehemu nyingine ili kuvutia wadhamini,”
alisema Palasa.
Alisema ngumi sio mchezo wa fujo kama baadhi ya
watu wanavyodhani, bali ni mchezo wa
wastaarabu ambao wanapigana kwa kufuata
sheria. Alisema atakayebainika kukiuka sheria
zilizowekwa awe ni bondia au promota
atachukuliwa hatua za kisheria.

No comments :

Post a Comment